Facebook Comments Box

Thursday, February 28, 2013

HUYU NDIO MKURUGENZI MPYA WA BENKI YA NBC

NATIONAL BANK OF COMMERCE
PRESS RELEASE


The National Bank of Commerce (NBC) has today announced the appointment of Mizinga Melu as its new Managing Director, subject to regulatory approval. The appointment is with effect from 20th May 2013.

Mizinga is joining NBC from Standard Chartered Bank Zambia where until now she has been Managing Director since 2007. She takes over from Lawrence Mafuru, who left the bank in December, 2012.

Mizinga has previously served in senior roles at Standard Chartered, including as Global Head of Development Organisations in the United Kingdom where she was responsible for strategy development and implementation as well as Africa Regional Head of Financial Institutions in Kenya and South Africa where she led formulation of Standard Chartered’s FI business strategy in Africa. Prior, she served as Head of Treasury at Standard Chartered Bank Tanzania between 2000 and 2003.

Mizinga holds a Masters in Business Administration (MBA) from Henley Management College (UK) and is an Associate of the Chartered Institute of Bankers (A.C.I.B). She holds numerous other banking qualifications.

Commenting on the appointment, Barclays Africa Chief Executive Officer and Head of Africa Group Strategy, Kennedy Bungane said: “The appointment of Mizinga reiterates the importance of NBC to our ‘One Africa Strategy’ and we are excited that she is joining us at a time we are making steady progress towards our goal of becoming the go-to bank in Africa.”

Dr. Mussa Juma Assad, Chairman of NBC commented: “The board welcomes Mizinga to NBC and looks forward to working with her in maintaining the position of NBC as a leading bank in Tanzania.”

Commenting on her appointment, Mizinga said: “NBC has over the years proven to be an important financial services provider in Tanzania. I am privileged to have the opportunity to lead this great bank at this important moment and I am looking forward to working with every colleague in NBC as we continue on our journey of transforming the bank in the market.”

Mizinga will report directly to Kennedy Bungane, Barclays Africa Chief Executive Officer and will be a member of the Barclays Africa Executive Committee.


WAKILI: MAHAKAMA IMUONE PONDA HANA KESI YA KUJIBU



UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi ya Sh. milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imuone Ponda na wenzake wanakesi ya kujibu kwa sababu umeweza kujenga kesi yao.

Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya upande wa Jamhuri unaowakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na Inspekta wa Polisi,  Hamisi Said na upande wa utetezi unaowakilishwa na Juma Nassor na Njama kuwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo ya kuomba mahakama iwaone washitakiwa wanakesi ya kujibu au la.

Kweka ambaye alitumia dakika kumi tu kuwasilisha majumuisho alidai upande wa Jamhuri umeweza kujenga kesi yake kupitia mashahidi wake 16 na vielelezo 13 walivyovileta mahakamani ambapo waamini kisheria vitawafanya washitakiwa wapande kizimbani kujitetea.

Wakili wa utetezi Nassor Juma akiwasilisha majumuisho yake, aliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu na waachiliwe huru kwa sababu upande wa Jamhuri umeshindwa kujenga kesi yao.

Nassor alidai wanachokiona katika kesi hiyo ni kuwa kuna mgogoro wa ardhi ambao ulitakiwa ukatatuliwa kwanza na Mahakama ya Ardhi kwa mujibu wa kifungu cha 167 cha Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, “Sisi upande wa utetezi tunaiomba mahakama hii iwaachilie huru washitakiwa wote na iwaone hawana kesi ya kujibu kwas ababu kesi hii imefunguliwa kwa jazba na polisi na upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao utaweza kuishawishi Mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu,” alidai wakili Nassor.

Hakimu Nongwa aliarisha kesi hiyo hadi Machi 4 mwaka huu, ambapo atakuja kutoa uamuzi wa ama kuwaona washitakiwa wana kesi ya kujibu au la na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe rumande kwa sababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.



KUFELI KIDATO CHA NNE:LAWAMA ZINAPO MFIKIA NYERERE

Picture

UNAAMBIWA HII NDIO HOTELI NDEFU KULIKO ZOTE DUNIANI: ANGALIA NA MANDHARI YAKE

Hivi ndivyo jengo hoteli hiyo inavyo onekana

Hii ni sehemu ya kupumzika na kupata chakula kwenye hoteli hiyo



Hata hapa chakula kinalika






Hoteli hii imefunguliwa Dubai Tarehe 26 baada ya kupata hadhi ya Hoteli ndefu kuliko zote duniani kutoka kwa Guinness World Records ambao ni watunza kumbukumbu wa matukio wa dunia.
Hoteli hii ina mita 355 ambazo ni sawa na futi 1,099. Jengo refu kuliko yote duniani lina mita 828 ambazo ni sawa na mita 2,717

 

 

 

 

 



KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI ASKARI WAWAZUIA WANAHABARI


SAKATA la mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23), limeendelea kuchukua sura mpya baada ya wanahabari kunusurika kupigwa na askari polisi ambao walikuwa wakiwazuia kusogea katika chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo. Askari polisi hao wakiwa zaidi ya 10 walitumia nguvu za ziada katika kuwadhibiti wanahabari wa vyombo mbalimbali waliofika kusikiliza na kuripoti mwenendo wa kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji ya mwanahabari mwenzao, Mwangosi aliyeuwawa Septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi wakati wa polisi walipokuwa wakitumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) aliokuwa katika shughuli za ufunguzi wa matawi ya chama hicho. Hata hivyo moja kati ya mbinu waliyopata kuitumia leo wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani hapo ni kuwafukuza waandishi wa habari eneo hilo la mahakama na kumtoa mtuhumiwa huyo kwa kificho cha hali ya juu kwa kumweka katikati ya watuhumiwa wa makosa mingine zaidi ya 8 huku mtuhumiwa akijificha sura yake kukwepa kamera za waandishi na baadhi ya askari wakimkinga ili kukwepa kupigwa picha. Tukio hilo lilitokea muda wa saa 6.10 mchana wakati mtuhumiwa huyo askari alipokuwa akitolewa na watuhumiwa wengine kutoka chumba cha mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Iringa na kumpeleka katika chumba cha Mahakama ya wazi kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa tena. Hivyo katika hali ya kushangaza ni pale askari hao kuwataka wanahabari hao kusongea umbali wa meta 700 kutoka eneo la Mahakama hiyo wakati mtuhumiwa huyo akiingizwa katika chumba cha Mahakama ya wazi mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa, Gladys Barthy ili kesi hiyo iweze kutajwa kwa zaidi ya mara ya tano sasa bila upelelezi kukamilika. Uamuzi wa askari hao uliwashangaza hata baadhi ya wananchi waliofika kusikiliza kesi na kuwawekea dhamana ndugu zao na kulazimika kuungana na wanahabari kupinga uamuzi huo na kusababisha askari kuwafukuza pia wananchi hao na kuwataka waungane na wanahabari kuondoka eneo hilo la chumba cha mahakama. Hakimu mkazi mkoa wa mkoa wa Iringa mheshimiwa Barthy alisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi hao kuwazuia wanahabari si maagizo ya Mahakama na kuwa wanahabari hao walikuwa huru kuingia kusikiliza kesi hiyo na kuhabarisha umma kwani hakukiwa na siri wala hakuna maagizo ya mahakama ya kuwataka polisi kuwafukuza wanahabari mahakamani hapo. “Kwanza nawapa pore sana kwa misukosuko mlioipata ....ila mimi nilikuwa ndani ya mahakamani sikujua kinachoendelea huko nje ya mahakama ila nawahakikishieni kuwa kesi hii ilikuwa ikisikilizwa katika mahakama ya wazi na mlikuwa huru kusikiliza,” alisema hakimu huyo akiakimhoji mmoja kati ya viongozi wa polisi kuhusu polisi hao kunyanyasa wanahabari na kuwataka kutorudia kufanya hivyo tena. Mwendesha mashitaka wa serikali Blandina Manyanda aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo na kuwa upelelezi bado haujakamilika na mahakama hiyo kupanga tarehe 14 machi ambapo kesi hiyo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.

SOURCE: WAVUTI



BAADA YA KUJAZWA MAHELA MILOVAN AONDOKA BONGO


ALIYEKUWA kocha wa Simba Milovan Cirkovic ameondoka nchini jana alfajili na shirika la ndege ya Uturuki baada ya kufanikiwa kulipwa fedha zake dola 32 alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kocha huyo ambaye alikuja nchini mapema mwezi huu kwa ajili ya kudai fedha zake baada ya kudanganywa na uongozi wa Simba kuwa wanamtamlipa fedha zake bila mafanikio yoyote ndipo aliamua kuja kudai mwenyewe.

Hata hivyo baada ya kusota muda mrefu huku viongozi wakiwa wanampa ahadi kila siku hatimaye jana alfajiri alifanikiwa kuondoka baada ya kulipwa deni lake la Dola 32 kutoka kwa Malkia wa nyuki Rahma Al Kharoos ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na mfadhili wa klabu hiyo.

Kocha huyo ameondoka na rekodi ya ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0 dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
 
Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema kuwa uongozi wake haupaswi kulaumiwa kwa kusajili wachezaji wasio kuwa na uwezo bali anayetakiwa kulaumiwa ni aliyekuwa kocha wao Mserbia Milovan Cirkovic.

Rage alisema kuwa wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni pendekezo la kocha huyo ambaye alitimuliwa raundi ya kwanza baada ya timu kutofanya vizuri katika michezo yake ya mwisho.

Alisema awali waliwaleta wachezaji wawili kutoka Cameroon lakini kocha aliwakataa na kuwasajili wachezaji wake ambao aliwataka yeye.

Aliongeza kuwa haoni sababu ya wao kulaumiwa kwa sababu wao ni uongozi na sio wachezaji na kuongeza kuwa kama watu wanawalaumu wao wanacheza namba ngapi uwanjani.

Rage akiwa anatoa kauli hiyo tayari kocha Milovan kwa upande wake alikwisha sema kuwa katika wachezaji ambao alitaka wasajiliwe aliyesajiliwa ni Mrisho Ngassa pekee na wengine uongozi ulishindwa.

Msimu huu simba iliweza kusajili beki Lino Musombo, Kanu Mbiyavanga (Congo), Patrick Ochierg (Kenya) na Komabil Keita (Mali).

Lakini baadaye waliwaacha wachezaji watatu na kumbakiza mmoja Keita kwa madai ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri katika timu yao.


DOLA 337,000 ZATUMIKA KUNUNUA iPAD BUNGENI

 

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.


BUNGE nchini Uganda limetumia zaidi ya  dola 377,000 kununa kompyuta aina ya iPad kwa ajili ya wabunge wote .
Maofisa wa bunge hilo walisema kuwa mbali na kuwaweka wabunge hao karibu na  ulimwengu wa teknolojia, wanatarajia kuwasaidia kupunguza gharama za fedha zinazotokana na matumizi ya uchapishaji wa nyaraka mbalimbali.
Kamishna wa bunge hilo Elijah Okupa alisema kuwa kompyuta hizo ni bora na zinafaa kwa matumizi hivyo ni vyema zikatumiwa vizuri.
Alisema  iPad hizo zitakuwa ni mali ya wabunge lakini kama mtu atatumia kwa muda wa miaka mitano asitegemee itakuwa na ubora uleule wa kumwezesha mwingine atumie kwa miaka hiyo alisema Okupa
Kwa mujibu wa takwimu kutoka katika bunge hilo zilionyesha Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya dola 12 katika miaka miwili sasa kwa ajili ya mahitaji ya kama kompyuta, uchapishaji wa nyaraka, mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mawasiliano kuwa bora katika bunge.
Kwa mujibu wa mbunge kutoka mashariki, Medard Segona alisema kuwa kutokana na uwepo wa ipad hizo wanategemea kupunguza matumizi ya fedha zilizokuwa zikipotea hapo awali.
‘’Vifaa hivyo vitapunguza sana matumizi ya fedha kwa kuwa hapo awali wizara ya fedha ilikuwa ikichapisha zaidi ya nyaraka 400 kwa kila mbunge na maofisa wengine waliopo ndani ya bunge hilo’’alisema
Aliongeza kuwa komputa hizo ni muhimu kwa utendaji kazi hasa katika kipindi hicho cha kuendeleza matumizi ya teknolojia.
Hata hivyo taarifa zilisema kuwa wabunge hao bado hawana uelewa mzuri juu ya matumizi hayo licha ya kuwa kampuni imeahidi kutoa  mkataba wa mafunzo ambayo pia yatasaidia kupunguza gharama za matumizi.


Wednesday, February 27, 2013

KIWANDA CHA NGUO CHA MAZAVA CHANUSURIKA KUUNGUA KWA MOTO


Picture
Suma na Asha wakiwa hoi baada ya kufikishwa wodi namba 3 hospitali ya mkoa wa Morogoro (picha: Dunstan Shekidele)
Imeripotiwa kuwa Kiwanda cha nguo cha Mazava kinachomilikiwa na wawekezaji kutonga  nje ya nchi, kilichopo Msamvu mkoani Morogoro kimepata hitilafu ya umeme majira ya saa nne wafanyakazi wakiwa ndani wakishona nguo.

Hali ya hewa iliyobadilika kutokana na moshi ndani ya jengo hilo imesababisha baadhi ya wafanyakazi wanaokadiriwa kuwa 30, kuanguka na wengine kupoteza fahamu  na hivyo kupelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Waandishi wa habari, Wafanyakazi wa shirika la umeme - TANESCO na Wafanyakazi wa zima-moto waliofika hapo kwa ajili ya kusaidia uokozi na kupata raarifa, walizuiwa kuingia ndani ya kiwanda hicho na wamiliki ambao ni raia wa China wakidai hakuna tukio lolote kubwa linalohitaji huduma ya uokozi hadi kuingia ndani.
Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele anasema kumbukumbu za matukio zinaonyesha kuwa  hili ni tukio la tatu.

Akiwahoji baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho, amefahamishwa kwamba hali hiyo huenda hali hiyo inatokana na hujuma za baadhi ya wafanyazi wanaolalamika kufanya kazi kwa saa 12 na kulipwa mashahara ya shilingi elfu 80/=.
Picture
(picha: Dunstan Shekidele)
Picture
Bi, Subira Juma Athumani [kushoto] akiwa na majeruhi wenzake. (picha: Dunstan Shekidele)



MUFT SIMBA ATENGUA NAFASI YA SHEIKH MKUU SEMWALI WA MOROGORO


  Sheikh Mkuu na Tanzania, Mufti Issa bin Shaaban Simba, ametengua nafasi ya Shekhe Mkuu mkoani Morogoro, Yahya Semwali akidaiwa kushindwa kusimamia maendeleo ya Waislamu mkoani humo.

Katika barua yake kwa Shekhe Semwali yenye namba MK/BR/UL/03/04/79 ya Februari 19 mwaka huu, Mufti Simba alisema uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha Baraza la Ulamaa Taifa hivyo anatakiwa kukabidhi ofisi.

Kutokana na uamuzi wa baraza hilo, Mufti Simba amemteua Shekhe wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaaban kukaimu nafasi hiyo kwa barua yenye namba MK/BR/UL/03/04/81 ya Februari 20 mwaka huu na kusisitiza kuwa, nafsi hiyo inapaswa kujazwa ndani ya siku 90 kwa kufanya uchaguzi mwingine.

“Waumini wa Kiislamu mkoani Morogoro wapewe fursa ya kuchagua Sheikh mwingine wa Mkoa,” ilisema barua hiyo.

Uamuzi huo umepokelewa kwa hisia tofauti na viongozi mbalimbali wa BAKWATA mkoani humo akiwemo Sheikh
Semwali aliyeondolewa madrakani ambaye alisema madai yaliyotolewa dhidi yake si sahihi na yameegemea upande
mmoja yakisukumwa na hisia zaidi.

Alisema kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kunatokana na hisia za kuunga mkono msimamo wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Issa Ponda jambo ambalohalina ukweli.

Sheikh Semwali alisema:
Hisia nyingine zilizojionesha ni kitendo cha mimi kwenda ibada ya Hijja kupitia taasisi nyingine tofauti na Baraza la Waislamu nchini (BAKWATA), pamoja na uamuzi wangu wa kutengua uchaguzi wa baraza hili ngazi ya kata, wilayani Gairo.

Uchaguzi huu ulifanyika kinyime na utaratibu bila ya ngazi husika kama BAKWATA Wilaya na Mkoa kuwa na taarifa, hili ndio lililomsukuma Mufti Simba kufikia maamuzi haya japo baraza hili Mkoa lina taarifa za ukikukwaji husika lakini bado aliendelea kukaa kimya.
Kuhusu madai ya kushindwa kusimamia maendeleo ya Waislamu, Sheikh Semwali alisema hivi sasa katika Wilaya zote kuna miradi ya maendeleo kama ule wa Wilaya ya Ulanga ambako kuna ujenzi wa vyumba vya maduka 14.

Pia kuna mchakato wa upatikanaji ekari 20 kwa ajili ya upandaji miti ya matunda ambapo hivi sasa walikuwa kwenye hatua za mwisho kupata ekari nyingine 600.

Alisema Wilaya ya Morogoro Vijijini kuna vyumba vitano vya maduka, Mvomero vyumba vinne vya madrasa na Kilombero vyumba vitano vya biashara ambapo maendeleo hayo  yametokana na juhudi zake.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Baraza la Masheikh mkoani humo, ambalo lilikaa hivi karibuni kupitia maamuzi hayo, Sheikh Shaaban Nyoni, alisema uamuzi wa Mufti Simba amekiuka Katiba ya BAKWATA.
Shekhe Semwali alichaguliwa hakuteuliwa hivuyo kama alikuwa na tatizo, wao kama baraza ndio waliopaswa kuwasilisha tatizo lao kwa Mufti Simba si vinginevyo.

Halmashauri ya BAKWATA Mkoa inatarajia kukutana kesho (leo), ili kujadili uamuzi huu na baadaye kikao cha Mashekhe wote wa Wilaya na Mkoa, watakaa kujadili na kutoa msimamo.
Imam wa Msikiti wa Al Aqswaa wa Mazimbu, mkoani humo, Sheikh Mohamed Msoma ambaye ni mjumbe wa Baraza la Masheikh, alisema si sahihi Mufti Simba kumuondoa Sheikh Semwali katika nafasi yake.



KAGERA SUGAR WAPELEKWA PUTA MPAKA WAOMBA POO KWA YANGA: WAMEPIGWA KAMOJA TU

Niyonzima akiwapungia mikono mashabiki baada ya mechi

Na Mahmoud Zubeiry
KWA mara ya pili mfululizo, kiungo Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima leo tena amekuwa shujaa wa timu yake, Yanga SC baada ya kuifungia bao pekee la ushindi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Niyonzima alijikuta akituzwa fedha na mashabiki wa timu yake baada ya mechi hiyo, iliyokuwa ngumu kwa Wana Jangwani, kutokana na kuibeba timu hiyo mara mbili mfululizo kwa kufunga mabao ya juhudi binafsi, ikiwemo mechi iliyopita dhidi ya Azam FC. 
Didier Kavumbangu akipiga shuti langoni mwa Kagera mbele ya mabeki wa Kagera
Ushindi huo unaifanya Yanga ifikishe pointi 42, baada ya kucheza mechi 18, hivyo kujitanua kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi Azam FC kwa pointi sita, ambayo inashika nafasi ya pili kwa pointi zake 36, wakati mabingwa watetezi, Simba SC wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao 31.
Kagera inabaki na pointi zake 28 katika nafasi ya tano, baada ya kucheza mechi 19, chini ya Coastal Union ya Tanga inayoshika nafasi ya nne kwa pointi zake 30.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Simon Mberwa kutoka Pwani, aliyesaidiwa na Milambo Tshikungu wa Mbeya na Said Tibabimale kutoka Mwanza, hadi mapumziko, hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake.
Hata hivyo, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu aliikosesha timu yake bao, baada ya kupiga juu ya lango mkwaju wake wa penalti dakika ya 44.
Refa Mberwa, alitoa penalti hiyo baada ya Kavumbangu mwenyewe kudakwa miguu kwenye eneo la hatari na kipa wa Kagera, Mganda Hannington Kalyesebula.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko, Yanga inayofundishwa na Mholanzi, Ernie Brandts ikiwatoa Kavumbangu na Bahanuzi na kuwaingiza Jerry Tegete na Mganda Hamisi Kiiza, wakati Kagera inayofundishwa na mzalendo, Abdallah Kibadeni, iliwatoa Mnigeria Darlington Enyinna na Julius Mrope na kuwaingiza Paul Ngway na Themi Felix.
Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa kila upande na kuongeza kasi na ladha ya mchezo, lakini bahati hii leo ilikuwa kwa wana Jangwani, kutokana na kupata bao pekee la ushindi lililofungwa na kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Niyonzima.   
Niyonzima alifunga bao hilo dakika ya 65, baada ya kumhadaa kiungo wa Kagera, George Kavilla na kufumua shuti kali akiwa umbali wa mita 25, lililomshinda kipa wa Kagera, Kalyesebula.
Halikuwa na tofauti sana na bao pekee la ushindi alilofunga kwenye mchezo uliopita wa timu yake dhidi ya Azam FC, Uwanja huo huo wa Taifa, Jumamosi iliyopita.   
Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shijja Mkinna alikosa bao la wazi dakika ya 89, baada ya kupewa pasi nzuri na Paul Ngway, lakini akapiga juu ya lango.
Hiyo ilikuwa nafasi pekee ya kujutia kwa Kagera ambao leo iliitoa jasho Yanga.  Jerry Tegete naye alikosa bao la wazi dakika ya 87, akishindwa kuunganisha krosi ya Simon Msuva. 
Kwa ushindi huo, Yanga imelipa kisasi cha kufungwa 1-0 na Kagera katika mchezo wa kwanza wa ligi hiyo, mwishoni mwa mwaka jana mjini Bukoba.
Katika mchezo huo, kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbangu/Hamisi Kiiza dk67, Said Bahanuzi/Jerry Tegete dk 67 na Haruna Niyonzima.
Kagera Sugar; Hannington Kalyesebula, Benjamin Asukile, Martin Muganyizi, Malegesi Mwangwa, Amandus Nesta, Gaorge Kavilla, Julius Mrope/Paul Ngway dk 62, Juma Nade, Darlington Enyinna/Themi Felix dk 69, Shijja Mkinna na Daudi Jumanne.    

SOURCE: BIN ZUBEIRY

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI KENYA SAMWEL KIVUITU AMEAGA DUNIA


336544_319369068086667_163569676999941_1031123_336563521_o

Wakili aliyekuwa mwenyekiti  wa tume ya uchaguzi ya Kenya,  ECK ndugu Samuel Kivuitu ameaga dunia
Taarifa zilizotolewa na familia ya Kivuitu zinasema kuwa marehemu aliaga dunia jana usiku mwendo wa saa nne katika hospitali ya MP Shah iliyopo jijini Nairobi, alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya saratani.
Kivuitu alikuwa akisumbuliwa na saratani ya  koo ambapo alikuwa akipelekwa katika hospitali hiyo mara kwa mara kwa muda wa miaka miwili.

Marehemu Kivuitu alivuma sana mwaka 2007 baada ya matokeo ya uchaguzi wa Rais nchini Kenya yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya wakati huo ECK yeye akiwa Mwenyekiti, matokeo ambayo yalipokelewa kwa hisia tofauti na kuwa sababu hasa ya kuchochea machafuko makubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Kenya ambapo watu 1,133 waliuawa na wengine laki sita na nusu kuachwa bila ya makazi.


Monday, February 25, 2013

ANGALIA LIVE HAPA MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA URAIS WA KENYA

Live Video streaming by Ustream

MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA URAIS KENYA UMEANZA



Mdahalo wa mwisho wa wagombea wa uchaguzi nchini Kwenya unafanyika jioni ya leo.
Awali kulikuwa na taarifa kuwa mgombea wa Urais Uhuru Kenyatta alikuwa amesusia mdahalo huo akidai kuwa mdahalo wa kwanza waliokuwa wanauendesha mjadala wenyewe waliangazia sana swala la ICC na kuwafanya wagombea wengine kumlemea.
Duru zilisema kuwa Uhuru alisitisha kampeini zake leo ili kuweza kujiandaa vilivyo kwa mjadala huo.
Wagombea wengine akiwemo waziri mkuu Raila Odinga wanajiandaa kwa mjadala huo ambaop hii leo utalipa kipao mbele mbele swala la ardhi, sera za kigeni, na uchumi.
Kura za maoni zinaonyesha kuwa asilimia tisini ya wapiga kura wanaona mjadala huu una manufaa kwa wakenya. Asilimia themanini na tano walisema wako trayari kutazama mjadala huo.
Asilimia robaini ya wapiga kura waliohojiwa punde baada ya mjadala wa kwanza walisema wangempigia kura Uhuru Kenyatta wakati asilimia 33 walisema wangempigia kura Raila Odinga.Wawili hao ndio wagombea wakuu katika uchaguzi huu.



RAGE AKATAA KUJIUZURU ILA ASEMA MAAMUZI YATAKAYOFUATA NI MAGUMU

Mh Aden Rage akiwa amependeza katika rangi za kijani na njano
Na Dina Ismail
KAMATI ya utendaji ya klabu ya Simba inatarajiwa kutoa uamuzi mgumu kuhusiana na mwenendo mbaya ulionayo timu hiyo katika ligi kuu ya Vodacom.
Aidha, Rage amekanusha taarifa za kujiuzulu kwake kufuatia mwenendo mbaya wa timu hiyo kwenye ligi hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mwenyekiti wa Simba Alhaj Ismail Aden Rage alisema kwamba kamati ya utendaji ya Simba ilitarajiwa kukutana jana kwa ajili ya kujadili mustakabali wa timu yao.
Alisema kikao hicho kitajadili kwa kina hali iliyopo sasa ambayo imesabababisha timu yao kupoteza hata matumaini ya kutetea ubingwa wao.
“Tutakuna baadaye leo na kujadili hali hii maana tukiiacha hivi hivi inaweza kutuletea madhara makubwa sana…pia tutatoa maamuzi mazito baada ya kikao chetu,”alisema.
Kuhusu na taarifa za kujiuzulu kwake, Rage alisema anashangazwa na taarifa hizo zinapotoka kwani kama atafikia uamuzi huo ataitisha mkutano na waandishi wa habari na kuzungumzia hatua hiyo.
“Mimi sijasema nitajiuzulu jamani hata hiyo taarifa yenyewe ukiisoma haileweki, hivyo nawaomba wanasimba kutulia kuona kipi kitakachofuata,”aliongeza Rage
Simba imeonekana kusuasua sua katika ligi hiyo baada ya kutokuwa na matokeo ya kuridhisha sambamba na kuamulia vipigo katika mechi zake.
Hali hiyo ilianza kujitokeza tangu mwishoni mwa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ambao ulipelekea kutoka kileleni hadi kushika nafasi ya tatu.
Aidha, tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo, Simba imeshinda mechi mbili dhidi ya African Lyon 3-1 na Tanzania Prisons 1-0, huku ikitoka sare mbili dhidi ya JKT Ruvu na JKT Oljoro kwa bao 1-1 kabla ya kufungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar juzi. 

SOURCE:  BIN ZUBEIRY 

SERIKALI YAITOA KATIBA YA TFF YA MWAKA 2012 YAAGIZA UCHAGUZI UTUMIE KATIBA YA 2006

Serikali imeingilia kati sakata la uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuamuru kufutwa kwa katiba ya sasa ya shirikisho hilo na badala yake kuamuru itumike katiba ya zamani (mwaka 2006) baada ya kubaini kuwa iliyopo ina kasoro nyingi.

Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari leo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo imeeleza kuwa katiba ya sasa ya TFF si halali. Imeelezwa vilevile kuwa msajili wa vyama vya michezo aliyedaiwa kuipitisha katiba hiyo ameondolewa.

Mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF umesimamishwa kutokana na mgogoro mzito uliotokana na kuenguliwa kiutata kwa wagombea kadhaa, wakiwamo Jamal Malinzi anayewania urais na Michael Wambura anayetaka kugombea nafasi ya makamu wa rais.

Kamati ya rufani ya TFF inayoongozwa na Iddi Mtiginjola ndiyo iliyozua balaa lote la sasa baada ya kuwaengua kina Malinzi na mwishowe kumuacha makamu wa sasa wa rais, Athumani Nyamlani abaki kuwa mgombea pekee.


Hata hivyo, tayari mchakato wa uchaguzi huo uliozua mabishano makali umeshasimamishwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na maafisa wa chombo hicho cha juu cha mchezo wa soka duniani wameshaanza kuwasili kufuatilia kinachotokea nchini.

Uamuzi wa serikali wa kufuta katiba ya sasa na kutaka itumike ya 2006 unampa ahueni kubwa Wambura ambaye alishasema hadharani kuwa  ataiburuza TFF mahakamani kama isipoachana na katiba mpya na kufuata ya zamani; huku akitoa sababu kadhaa za kupinga matumizi ya katiba mpya, mojawapo ikiwa ni kupitishwa kwake kwa njia ya waraka wa barua pepe (e-mail) kwenda kwa wajumbe badala ya kufuata maelekezo ya katiba yanayotaka mabadiliko kufanywa na wajumbe kupitia mkutano mkuu.

Hata hivyo, kwa mujibu wa taratibu za FIFA, ni marufuku kwa shughuli za soka kuingiliwa na serikali au mahakama na nchi yoyote inayokwenda kinyume na taratibu hizo hujikuta ikifungiwa kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya.


HUYU NDIO MTOTO WA MIAKA NANE ALIE MUOA MWANAMKE WA MIAKA 61

Zaidi ya watu mia moja walikusanyika katika nchi ya Zimbabwe kushuhudia mtoto wa miaka nane (8) akimuoa mwanamke mwenye umri wa miaka (61) ambae anaweza akafaa kabisa kuwa bibi yake. Cha kushangaza zaidi familia zote mbili za wanandoa hao pamoja na watoto watano wa mwanamke huyo walikuwepo.
Shangazi wa mtoto huyo mwenye miaka (46) alitoa sababu za kutokea ndoa hiyo alisema "Huyu kijana alipewa jina la bibi yake ambae hakuwahi kufunga ndoa, mizimu imemuamuru afunge ndoa na Hellen (Mmama huyo) ndio imekuwa chaguo lake.
Wanafamilia walichukulia matamanio ya huyo kijana kufunga ndoa kwa umakini sana na kuamua kumruhusu kufunga ndoa na kulipia kila kitu. Na bibi huyo alieolewa na kijana huyo pamoja na kuwa na mume alikubali kuolewa kwa kuwa alijua ndio mizimu ya mababu waliokufa inavyo waamuru na kutaka.
Mtoto huyo alimuambia mama yake "Nataka kuoa kwa kuwa nataka kufanya hivyo na nimemchagua mwanamke huyu kwa kuwa nampenda na baada ya ndoa hii nitasoma kwa bidii sana na nikiwa mkubwa nitamuoa mwanamke ninalingana nae"
Mume wa mwanamke huyo alisema yeye hana shida wala wivu na kijana huyo kwa kuwa ni mdogo na ni mizimu iliyoyataka hayo. "watoto wangu na mimi hatuna shida na hili na tumefurahi sana"
Baadhi ya wanafamilia walioneshwa kushitushwa na ndoa hiyo na wanafamilia wenzao kuchukulia swala la mizimu kwa umakini wa kiasi hicho.
Wanandoa hao walimaliza harusi yao kwa mabusu moto moto.




TAASISI YA AL JAZIRA ISLAMIC CENTRE KULIBURUZA GAZETI LA MTANZANIA MAHAKAMANI


Shekh Jabir Katula ambaye ni mmoja kati ya waasisi wa kituo cha Aljazira Islamic akizungumza na waandishi wa habari huku akishuhudiwa na baadhi ya waalikwa kutoka taasisi mbalimbali.
Uongozi wa Taasisis ya Al Jazira Aslamic Centre umekanusha habari ilizotaja kuwa ni za uongo, uzushi na ufitini zilizochapishwa na gazeti la Mtanzania toleo la tarehe 13 februari 2013 na toleo la tarehe 20 februari 2013 zikikitaja kituo hicho kufadhiliwa na makundi ya Al-Qaeda na Al-Shabab yanayoaminika kuwa na mtandao mkubwa wa ugaidi duniani.

Aidha kituo hicho kimesikitishwa na taarifa hizo na kutia mkazo kulitaka gazeti hilo (Mtanzania) kuomba radhi kabla ya siku saba kutokana na demand note waliyoitoa, kinyume na hapo taasisi hiyo imesema kuwa itachukuwa hatua zaidi za kisheria.
Kusanyiko lililofika kushuhudia tamko.

Shekhe Mohamed Salum Mbala Katibu wa BAKWATA mkoa wa Mwanza.
"Habari iliyotangazwa imetustusha sana imetudhalilisha, imetuudhi ni taarifa ambayo haikufanyiwa utafiti, imevunja heshima ya waislamu sio wa Mwanza Tanzania pekee bali dunia nzima, tunasema wazi kuwa sisi waislamu tunapenda amani na tuko kwa ajili ya kuitangaza amani na hatuko tayari kuvurugwa kuipoteza amani ya nchi hii"

"Kwa kweli tunalaani sana udhalilishaji huu tunaomba mwandishi wa habari hizo atoe ushahidi na hatutokubali kama hatotoa ushahidi"
Shekhe Musa Kunenge ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa Chuo cha Aljazira Islamic Centre Ukerewe amesema kuwa chuo chake kilipata idhini ya waislamu kwenye msikiti, kisha kikafuata njia zote za kisheria ikiwa ni pamoja na kupata kiwanja hatimaye usajili na shughuli zote zinatendeka kwa haki na uhalali na wala kituo hicho hakijihusishi na yale yanayotajwa kwenye magazeti kukichafua chuo hicho. 


HIZI NDIO PICHA ZINAZOSEMEKANA ZA TIMBULO BAADA YA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA BURUNDI




TCRA YAIFUNGIA TV IMAAN

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imeifungia Televisheni pekee ya Kiislam ambayo inamilikiwa na Taasisi ya The Islamic Foundation ya Mjini Morogoro. Hiyo ndio Televisheni pekee ya Kisslam ambayo imekuwa ikimilikiwa na kuupasha habari umma wa Kiislam nchini Tanzania. 
Sababu za kuifungia Televishni hiyo bado hazijawekwa wazi. Televisheni hiyo imefungiwa tokea jumamosi.
Baadhi ya wananchi walioongea na Blog hii wamekuwa wakihisi labda ni katika mchakato wa kuendelea kuwashughulisha ili wasikae sawa katika malengo yao. Wenfgi wa wakazi wa Morogoro wamekuwa wakiitambua Taasisi ya The Islamic Foundation kama msaada mkubwa kwao na kwa jamii bila kujali hata rangi, kabila wala dini.
Kufungwa kwa Televisheni hii kumekuja huku serikali ya Morogoro ikiwa imekitambua kwa kuitunuku cheti maalumu Taasisi hiyo ya The Islamic Foundation kwa msaada wake mkubwa inaotoa kwa jamii. Wengi wamekuwa wakilaumu mamlaka hiyo ya mawasiliano kwa kitendo hicho tena kuifungia jumamosi wakati ofisi za kiserikali zikiwa zimefungwa.
Chini ni baadhi ya habari zilizowekwa na mmoja wa waandamizi waliokuwa wakishughulika na Televisheni hiyo ikitanabaisha kufungwa kwa Televisheni hiyo na kuwaomba Waislam Tanzania kuwa na Subra na kuongeza moambi katika ukuta wa mtandao wa jamii. Muhusika huyo anajulikana kwa jina la Ahmed Bawazir ambae jina lake limekuwa likisomeka hivyo kwa kiarabu

www.kitongoni.blogspot.com
 




Sunday, February 24, 2013

AJALI MBAYA IMETOKEA MKOANI IRINGA




Ajali hii iliyohusisha magari mawili,Toyota Rav 4 na Toyota Cresta imetokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la jirani na Maktaba ya mkoa, mjini Iringa,ambapo gari hiyo aina ya RAV 4  iliruka ukingo wa barabara  uliojengwa kwa sementi na kutua juu ya Gari hiyo aina ya Toyota Cresta (Taxi) na kushindwa kuendelea na safari.inasemekana kuwa isingesimama gari hiyo aina ya Toyota Cresta,basi dereva wa gari hiyo aina ya Rav 4 labda angekuwa katika wakati mgumu zaidi au kupoteza maisha kabisa. hakuna aliepoteza maisha kwenye ajali hiyo. 
(Picha na Meshack Maganga-Iringa)
HABARI ZAIDI INGIA HAPA 



MNYIKA: MH. SHUKURU KAWAMBWA AMEBAKIZA SIKU KUMI TU


KAULI ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kwamba hawezi kujiuzulu, imeamsha hasira ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kimesisitiza kwamba maandamano ya kumng’oa yako pale pale na sasa amebakiza siku kumi tu.

Kauli hiyo ilitolewa  na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika wakati alipotakiwa kueleza msimamo wa chama chao, hasa baada ya kauli ya Waziri Kawambwa  kwamba hawezi kujiuzulu.

Akizungumza na mdau wa Kitongoni Blog, Mnyika ambaye ni Mbunge wa Ubungo, alisema kauli aliyoitoa Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe kwamba anampa siku 14 Waziri Kawambwa ajiuzulu, vinginevyo atang’olewa kwa maandamano bado ipo pale pale.

Alisema majibu ya Waziri Kawambwa yameonesha dharau kwa Watanzania, hasa walalahoi ambao ndio watoto wao wengi wamepata ziro katika mitihani yao ya kidato cha nne.

“CHADEMA tunaendelea kusisitiza kwamba Waziri Kawambwa ang’oke, awajibike, ameshindwa kazi na hili tunamaanisha,” alisisitiza Mnyika.

Alisema CHADEMA inaangalia namna ya kuitisha maandamano hayo kwa kuwashirikisha vijana waliofeli kwani wanaamini wamehujumiwa.

Mnyika aliwataka Watanzania na wengine wenye uchungu na udhaifu wa elimu ya Tanzania, hasa wazazi wajitokeze kwani fedha walizowekeza kwa watoto wao kwa ajili ya elimu, zimeteketea bure.


WAZIRI MKUU AUNDA TUME KUCHUNGUZA MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA NNE

wpid-Prime-Minister-Mizengo-PindaWAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameunda Tume maalum itakayofanya uchunguzi wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ambayo yalitangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa Februari 18, mwaka huu.
Katika matokeo hayo yaliyotangazwa Jumatatu wiki hii, asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne Oktoba, 2012 walifeli.
 
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Peniel Lyimo amesema Tume hiyo ambayo inatarajiwa kuanza kazi wakati wowote wiki ijayo inajumuisha wadau kutoka Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi (Tanzania Association of Managers and Owners of Non-Government Schools/Colleges (TAMONGSCO), Taasisi za Dini zinazotoa huduma ya elimu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Asasi zisizo za Kiserikali (NGOs) zinazoshughulikia masuala ya elimu.



Picture

MWAKYEMBE AFANIKIWA KUPANDISHA MAPATO BANDARI YA DAR ES SALAAM.




Meli zinapakua makontena katika bandari ya Dar es Salaam tarehe 29 Disemba, 2012. [Deodatus Balile/Sabahi]

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imeongeza ukusanyaji wa mapato katika bandari ya Dar es Salaam kutoka shilingi bilioni 28 mwezi Novemba hadi shilingi bilioni 50 (dola milioni 18 hadi dola milioni 31) katika mwezi wa Disemba, kufuatia kusimamishwa kwa muda maofisa 16 wa bandari wanaotuhumiwa kwa mwenendo usiofaa.
 
Maofisa hao wa bandari, wakiwemo wakurugenzi wa ngazi za juu, walisimamishwa kwa muda mwezi Disemba baada ya Wizara ya Usafirishaji kuanzisha uchunguzi wa ndani kwa lengo la kutoa mwitikio wa malalamiko ya wateja kuhusu kucheleweshwa katika bandari hiyo, kwa mujibu wa Waziri wa Usafirishaji Harrison Mwakyembe.
Maofisa wa bandari wengine wasiopungua sita. Uchunguzi huo, ambao bado unaendelea, uligundua kuwa waajiriwa wa bandari walibadilisha mwelekeo wa biashara kutoka katika bandari kwenda kwa kampuni ndogo za usafirishaji na utoaji mizigo wanazomiliki, ukiukaji wa moja kwa moja wa mkataba wao wa ajira.
"Wateja wanakimbia bandari yetu kwa sababu ya ucheleshaji wa kukusudia unaofanywa na waajiriwa wasio na maadili ambao wanaongeza gharama za kufanya biashara," Mwakyembe aliiambia Sabahi. "Hii ni kinyume na mikataba yao ya ajira na wana mgongano wa maslahi na mwajiri wao ambae ni Serikali."
 
Miongoni mwa viongozi wa bandari wa ngazi ya juu waliosimamishwa ni Mkurugenzi Mkuu wa TPA Ephraim Mgawe, Mkurugenzi wa Mipango Florence Nkya, Mkurugenzi wa Uhandisi Bakari Kilo, Mkurugenzi wa Mifumo ya Utawala Maimuna Mrisho, Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Ayub Kamili, Naibu Mkurugenzi Mkuu Hamad Koshyuma, Naibu Mkurugenzi Mkuu Julius Fuko, na Meneja wa Bandari Cassian Ng'amilo.
Mashtaka rasmi bado hayajatolewa dhidi ya viongozi waliosimamishwa na bado hawajajibu tuhuma zozote hadharani. Mwakyembe alisema Bodi ya Wakurugenzi ya TPA itakutana hivi karibuni kutoa uamuzi wa mwisho kuhusiana na ajira yao.


IMAM APIGWA MAPANGA NA KUFA ZANZIBAR



Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema (kulia) Waziri wa Mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi na Kamnda wa Pilisi Zanzibar Ally Mussa kwenye moja ya mikutano na waandishi wa habari.          

SIKU chache baada ya kutokea kifo cha Padri Evarist Gabriel Mushi kupigwa risasi na watu wasiojulikana kichwani eneo la Beit el Raas, Jana Imamu wa Msikiti wa Mwakaje ameuawa baada ya kupigwa mapanga hadi kufa. Kwa mujibu wa maelezo ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ahmada Khamis amethibitisha kutokea kwa tukio hilo hapo jana mchana majira ya saa 8 na kumtaja aliyefariki kuwa ni Sheikh Ali Khamis ambaye ameuawa na watu wasiojulikana.
  Kamanda Ahmada alisema Sheikh Khamis mbali ya kuwa ni Imamu wa Msikiti lakini pia ni mkulima na ameuliwa wakati akiwa katika mazingira ya kazi zake ndani ya shamba lake huko Kidoti Mkoa wa Kaskazini Unguja. Akielezea mazingira ya tukio hilo Kamanda Ahmada alisema tukio hilo limetokea baada ya Sheikh Khamis kwenda shambani kwake katika shmba la minazi Kidoti ambapo wakati akiwa shambani hapo ndipo walipotokea watu kadhaa na kumpiga mapanga sehemu za shingoni mwake na kusababisha kifo chake muda mfupi baada ya kipigo hicho.
  Alisema baada ya tukio hilo, watu walimchukua na kumkimbiza hospitali lakini kutokana na kupoteza damu nyingi alifariki dunia wakati akiwa njiani na hivyo harakati za mazishi zinafanyika baada ya kuchukuliwa vipimo na wataalamu wa afya. Kamanda Ahmada ametoa wito kwa wananchi kutopuuzia taarifa za watu ambao wanawashuku na wenye kuleta maafa yakiwemo mauaji hapa nchini, kwani kuwaficha wahalifu ni kuendeleza utamaduni usiofaa katika jamii ambayo imeanza kuharibika kutokana na mauaji hayo yanayoendelea kila kukicha. Hili ni tukio la nne kwa viongozi wa dini kuhujumiwa ambapo tukio la kwanza Sheikh Fadhil Suleiman Soraga kumwagiwa tindi kali na watu wasiojulikana na kujeruhiwa vibaya wakati akifanya mazoezi nyakati za asubuhi karibu na nyumbani kwake Magomeni, tukio la pili ni lile la Padri Ambrose Mkenda aliyepigwa mapanga shingoni na kurejuhiwa vibaya na watu wasiojulikana wakati akitaka kuingia nyumbani kwake huko Tomondo Mjini Unguja. matukio hayo mawili yalitokea mwaka jana. Katika mwaka huu nako kumetokea matukio mawili kwa kuuawa kwa Pardi Evarist Mushi huko Beit El Raas wakati akitaka kuingia Kanisani na pia kuuawa kwa Sheikh Ali Khamis huko Kidoti shambani kwake Mkoa wa Kaskanizini Unguja.  Inna lillahi wainna ilayhi rajiiun.


Friday, February 22, 2013

MBUNGE WA CHADEMA AINGIZWA MJINI KWA KUIBIWA MILION SITA BENK

SAKATA la wizi wa fedha katika akaunti za wateja wa benki, sasa limeingia katika sura mpya baada ya Mbunge wa Biharamulo Magharibi, Dk Gervas Mbasa (Chadema) naye kuibuka na kudai kuwa ameibiwa Sh6 milioni kutoka kwenye akaunti yake. Akizungumzia wizi huo, mbunge huyo alisema fedha zake ziliibwa kwa nyakati tofauti kati ya Desemba 20 mwaka jana na Januari 3, mwaka huu. 
Alisema kitendo hicho kilifanywa na mtu mmoja aliyempigia simu na mtu mmoja aliyejitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa Makao Makuu ya Kampuni ya Airtel na kwamba alikuwa katika zoezi la kuhakiki namba zote za zamani.
“Alinieleza kwamba kwa niaba ya Airtel yupo katika zoezi la kuhakiki namba zote zilizosajiliwa zamani na yangu ilikuwa ni ya miaka 10 na akaniuliza namba ya mwisho kuwasiliana na mtu kupitia simu yangu. Nilimtajia namba ya mke wangu na baada ya maelezo hayo aliniomba nisizime simu yangu wakati wakiwa wanashughulika na kuisajili na kwamba muda wowote nitapatiwa maelekezo,” alieleza mbunge huyo.


JCB AFUNGA PINGU ZA MAISHA NA MZUNGU

JCB afunga ndoa na girlfriend wake wa kitambo,Diana
Jorgensen 
ambae kwa sasa wanamtoto mmoja pamoja, huko jijini Arusha


 
Jcb akipitia makaratasi huku mke wake akicheza na pete na maua na mwanae
 
 


Baada ya kufunga ndoa, kinachofata huwa ni picha na hapa ni akiwa na ndugu jamaa na marafiki


PSPF WAONESHA NYUMBA ZAO ZA MKOPO ZILIZOPO BUYUNI - CHANIKA




Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) umekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba 641 katika mikoa mitano ambazo zilianza kuuzwa tangu Novemba mwaka 2012. Mradi huo unalenga kutatua tatizo la makazi kwa wanachama wake na jamii kwa ujumla.

Mikoa iliyojengwa nyumba hizo na idadi ya nyumba katika mabano ni Dar es salaam – Buyuni (491), Morogoro – Lukobe (25), Shinyanga – Ibadakuli (50), Tabora – Usule (25) na Mkoa wa Mtwara – Mang’amba (50).

Aidha kwa Mujibu wa maelezo ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bwana Adam Mayingu amewaambia wanandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliotembelea eneo la mradi huo Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Shirika lake limejenga nyumba za aina nne ambazo ni za nyumba viwili, Vyumba vitatu, Nyumba za vyumba vitatu kimoja ikiwa ni Master na Nyumba ya vymba vine kimoja kikiwa ni Master.

Gharama ya ununuzi wa nyumba hizo ambazo zinauzwa kwa wanachama wa Mfuko huo ni kati ya Shilingi Milioni 64 hadi milioni 94 gharama zikijumlishwa na Kodi ya ongezejo la Thamani.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (katikati) akiwaonesha maofisa wa Jeshi la Polisi moja ya nyumba 491 zilizopo katika mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ambazo zitkopeshwa kwa wanachgama wa mfuko huo. Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara hiyo ya kuakagua makazi hayo. Kulia ni  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Hery Mohamed Kessy Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.
 Wadau mbalimbali wakitembelea nyumba hizo hii leo.

 Ziara ikiendelea katika nyumba hizo zipatazo 491




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU