Facebook Comments Box

Wednesday, December 31, 2014

TAHADHARI KWA PICHA: MTU MMOJA AMEKUFA NA KUNING'INIA GETINI HEBU JIONEE MWENYEWE

 Mtu huyo anaitwa Abdul Koroma ni raia wa Siera Leone akiwa amening'inia getini akiwa amekufa, kwa kile inachosemekana kuwa ni mtuhumiwa wa dawa za kulevya na alikuwa anatoroka mahakamani kabla ya kupigwa risasi na kufa juu ya geti ambapo alitaka aruke na kukimbia.
 Hapa askari Magereza wakijaribu kumuondoa mahali alipokuwa amenasa juu ya geti la mahakama ya kisutu
 Mtu huyo hapa baada ya kushushwa chini toka juu ya geti.



Picha na Camera yetu mtaani:

FUNGA MWAKA NA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 31-12-2014 HAPA


















PICHA: BASI LA ABOUD LAPATA AJALI MLANDIZI ASUBUHI HII

Picha chini basi la Aboud likiwa limeanguka baada ya kupata ajali mlandizi asubuhi hii.  Haijajulikana idadi ya majeruhi na waliopoteza maisha.



HAKIMU AJITOA KESI YA UAMSHO




 Sheikh Farid Katikati ya Askari Magereza.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hellen Liwa amejitoa kusikiliza kesi ya ugaidi inayowakabili viongozi 23 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI).
 
Hakimu huyo amefikia uwamuzi huo baada ya wakili wa washtakiwa hao wa ugaidi, Abubakar Salim kumtaka ajitoe kuisikiliza kesi hiyo ili iweze kupangiwa hakimu mwingine ambaye atatoa uamuzi juu ya hoja zao walizozitoa mahakamani hapo Septemba 19,2014.

Salim aliiambia mahakama kuwa baada ya kushauriana na wateja wao na uamuzi uliotolewa na Jaji wa Mahakama Kuu, Dk Fauzi Twaib wakaona kuwa ni ukweli kuwa Hakimu Liwa alikwisha toa uamuzi wake juu ya hoja zao Oktoba Mosi, 2014 kuwa mahakama hiyo ya kisutu haina mamlaka ya kusikiliza hoja hizo. 

Alidai Mahakama Kuu katika uamuzi wake uliotolewa na Jaji Twaib umeelekeza kuwa Mahakama ya Kisutu inayo mamlaka ya kuzisikiliza hoja za washtakiwa hao wa ugaidi na hata kuzitolea uamuzi.

"Mahakama Kuu imeelekeza mawakili wa upande wa utetezi kama tutakuwa na hoja mpya ama  zile za awali tuzitoe kwenye mahakama hii ya Kisutu ili ziweze kutolewa maamuzi hivyo naona ni bora ujitoe tupate neno kutoka kwa hakimu mwingine."Alisisitiza kusema wakili huyo mahakamani hapo.

Wakili wa Serikali Mkuu, Benard Kongola alimuomba Hakimu Liwa asijitoe katika kuisikiliza kesi kwa madai sababu zilizotolewa na upande wa utetezi za kumtaka ajitoe hazina msingi.

Kongola alieleza kuwa uamuzi uliotolewa na Jaji Twaib aliamuru utekelezaji wa hoja za upande wa utetezi katika kesi hii ya ugaidi zisikilizwe na kutolewa uamuzi katika Mahakama ya Kisutu.

"Tukiendekeza hii tabia tutamaliza mahakimu wote wa mahakama hii tunasisitiza upande wa utetezi utoe sababu za msingi za wewe kujitoa."Alisema Kongola.
Akijibu hoja hizo, Wakili Salim alieleza kuwa ili haki ionekane inatendeka wewe Hakimu Liwa ujitoe ili hakimu mwingine atoe maamuzi wa hoja zetu.

Hakimu Liwa alisema ni kweli nilikwisha toa uamuzi wangu juu ya maombi ya washtakiwa lakini Mahakama Kuu imeona kivingine kuwa sijatumia mamlaka yangu vizuri nakubaliana na uamuzi huo.
Lakini uamuzi huo wa Jaji Twaib haukufafanua nini kifanyike, umetuacha hoi, ila alitoa angalizo kuwa ushahidi wa kesi hauwezi kutoka hewani na kwamba maelezo yaliyomo katika hati ya mashtaka ya kesi hiyo yapo sahihi.

"Kitu ambacho hata mimi nilikuwa nakishangaa ni hii hati ya mashtaka kuletwa Tanzania Bara badala ya Visiwani, lakini nilipoisoma sheria ya ugaidi nikabaini mtu anaweza kushtakiwa mahali popote." Alisema Hakimu Liwa.Alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria Mahakama Kuu ndiyo yenye uwezo wa kuisikiliza kesi hii na siyo mahakama ya Kisutu hivyo yeye hawezi kusema kitu labda kesi ingekuwa imefikia kwenye mwenendo wa uhamishaji shauri (Committal Preceding).

Hatua hiyo inafikiwa baada ya upelelezi wa kesi kukamilika inahamishwa kutoka mahakama ya Kisutu kwenda Mahakama Kuu ambayo inamlaka ya kusikiliza kesi hizo.

"Mimi nimejifunza kitu hapa, kuwa mimi najua nini na wenzangu wanajua nini hivyo siwezi kuendelea na kesii haitakuwa haki najitoa."Aliongeza kusema Hakimu Liwa na akajitoa na kuiahirisha hadi Januari 13,2015 ili ipangwe kwa hakimu mwingine.


Tuesday, December 23, 2014

KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI ASIMAMISHWA KAZI

Kutokana na hotuba ya Mh Rais Prof Jakaya Mrisho Kikwete kutaka uchunguzi ufanyike ili ajiridhishe kuhusu sakata la Escrow katibu mkuu kiongozi amemsimamisha katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini ili uchunguzi ufanyike.

Chini ni tangazo lililoelezea kuzimamishwa kazi kwa katibu mkuu huyo.





HII NDIO CV YA KATIBU MKUU MPYA WA YANGA

Dr. Jonas B. Tiboroha (Ph. D)
Personal Particulars
• Date of Birth: 25th September 1969.
• Place of Birth:  Kasulu.
• Marital status: Married
• Nationality: Tanzanian.
• Employer: University of Dar es salaam (UDSM)
Education Background
• PhD (Education), Malmo University, Sweden Sept
2010 – August 2013, Awarded at the University of
Dar es Salaam, November, 2013.
• MSc. Exercise and Sports Sciences (Training
Methods); Norwegian University of Sport and
Physical Education – Oslo, Norway, August 2002 –
Feb 2004
• BSc Exercise and Sport Sciences: Norwegian
University of Sport and Physical Education- Oslo,
Norway, August 1999 - June, 2002
• Norwegian Language Certificate for Foreigners:
University of Oslo, Norway; September 1998 – May
1999.
• BEd. Physical Education Sport and Culture;
University of Dar es Salaam- Tanzania – Sept 1994
– May 1998.
Professional Experiences and Community Services
• Technical Development Officer at the Tanzania
Football Federation, October 2014 – Now.
• Part time Lecturer Saint Augustine University
College, Tabora campus, 2013 – Now.
• Part time Lecturer University of Gaborone –
Botswana, 2013 –Now.
• U-15 Manager, Malmo Football Club, Malmo
Sweden; October 2010 - 2013
• Lecture: School of Education, Department of
Physical Education and Sport Science, University
of Dar es salaam – since Jan, 2008 – Now.
• Assistant Lecturer; The School of Education,
Department of Physical Education and Sport
Science, University of Dar es salaam – since Jan,
2005 – 2008
• Lecturer in Sports Biomechanics, Exercise
physiology, Theories and Methods of Sports
Training, Measurement and evaluation of Higher
Performance Athletes and Research Methodology
in Physical Education and Sports Science, 2005 -
Now.
• Reporteur TAFCA Conference on Key Aspects of
Football Development in Tanzania. Held at the
Waterfront Conference Center from 18th – 22th
September 2008. Report Submitted.
• Founder and Director of Talent Identification,
Mobilization and Development Organization
(TIMaD); A Community Based Organization for
Promoting Football Talents in Youth – since
December 2004 - Now.
• Chief Coach Wakati Ujao Football Academy; An
academy led by TIMaD for Promotion of Youth
football Talents, 2004 – Now.
Professional Courses, Seminar and Conferences
Attended.
• Conference of Sports Management held at UDSM
November, 2013
• European Conference of Sports Science held at
Malmo, Feb 2012.
• CAF License C  in September 2011
• Conference on Coach Education on Analysis of
Global Issues and Challenges held in Amsterdam,
Netherland, 10th – 15th January 2011.
• FIFA Comm-Unity Seminar on Women Football
Development Held at PPF Tower Dar es Salaam,
Tanzania from 25th – 28th October 2011.
• Symposium on Women and Sport for
Empowerment held in Stockholm, Sweden, from
8th – 12th Feb 2011.
• MRC/UCT Conference on Sports Medicine Held at
the University of Cape Town, South Africa from
16th – 19th September, 2009.
• TAFCA Conference on Key Aspects of Football
Development in Tanzania. Held at the Waterfront
Conference Center in Dar es salaam, Tanzania,
from 18th – 22th September 2008, Report
Submitted.
• DFB Advanced Football Coaching Course for
Youth Football Development, held at the
Department of Physical Education and Sports
Science University of Dar es salaam, Tanzania
from 14th – 18th September, 2007.
• KNVB Course for Coaching Youth Football held at
the International School of Tanganyika Dar es
salaam, Tanzania in 2002.
• The FIFA Course on Coaching Youth Football,
Held at the National Stadium in 2007.
• The TFF/TAFCA Course on Youth Football and
Grassroots Development held at the TFF
Conference Hall, Dar es salaam, Tanzania, 2006.
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway November 2004
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2003
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2002
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2001
• Intermediate Course in Coaching Football in Dar
es salaam, Tanzania in 2001.
• Preliminary Course in Coaching Football in Dar es
salaam, Tanzania in 1996.
Sports Activities and Youth Development
Programs Participated as a Coach
• The EDUSPORT Regional Football Tournaments
for Youth in Lusaka, Zambia 2010 and 2011 with
Wakati Ujao.
• The Rollingstone Youth Tournaments in Arusha,
2009, 2010 and 2011 with Wakati Ujao.
• Taysa Tournaments in Dar es salaam 2005, 2006,
2007 and 2008 With Wakati Ujao.
• Gorthia Cup in Gotenberg, 2000, 2001, 2002 and
2004 with Staeback youth team of Oslo.
• Norway Cup; 1999, 2000, 2001, 2002, 2003 and
2004 with Staeback youth team of Oslo.
• Tivoli Cup; 2000, 2001, 2002 and 2004 with
Staeback youth team of Oslo.
• Gorthia Cup 2006 with Wakati Ujao of Dar es
salaam, Tanzania
• Tivoli Cup 2006 with Wakati Ujao of Dar es
salaam, Tanzania.
• Norway Cup 2006 with Wakati Ujao Dar es
salaam, Tanzania.
Sports Related Publications, Reports and Papers
Presented
• Tiboroha, J (2014). The development dilemma
facing youth football coaches: A case of Managing
and engaging volunteer academy coaches.
Submitted at the International Journal of Sports
and Coaching.
• Tiboroha, J. (2014) Adoption of FIFA Youth
Football Coach Education: A rhetoric or reality. In
for publication, Scandinavian Journal of Sports
Studies
• Tiboroha, J. (2013). Transnational Coaching
Education Courses in Tanzania: An investigation
on the Adoption Process and Barriers for Coaches
to Participate. A Thesis Submitted in Fulfilment of
the Doctoral Degree in Sports Science at the
University of Dar es Salaam.
• Tiboroha, J. (2005). The Influence of Strength
and Endurance on Elite football players’ Jumping
and Sprinting Abilities: A comparative Study on
Tanzanian and Norwegian Elite football Players,
ActaScandinavia Journal, 5(2) 14-16.
• Tiboroha, J. Physiological Demands of Young
Amateur football Players: A study on Dar es
salaam UMISETA, Team-Manuscript, Idrotts forum
journal, October 2009.
• Tiboroha, J. The Implementation of Health School
Programs in Tanzania: A Critique to the
Implementation of the MDGs in Tanzanian
Education System. A paper presented at the
EdQUAL Doctoral Conference held at the University
Bouya, Cameroon, 8th – 15th December, 2010.
• The Physical Status of Tanzanian Olympic
Swimmers one Year after Beijing: What do we learn
on the demands and levels of competitiveness? A
paper presented at the Tanzanian Swimmers
Association Seminar, Held at the Millennium
Towers Hotel 12 – 14 December, 2009.
• Tiboroha, J. The Making of Professionals in the
Development of Quality Physical Education. Paper
presented in the Annual analysis of Physical
Education status in Sub Saharan African
Countries, Bulawayo, Zimbabwe, March, 2007
• Tiboroha, J. Challenges and Prospect of Fitness
and Health promotion in Tanzanian Primary
Schools, Papers in Education and Development
Journal, May 2006.
• Tiboroha, J. Mainstreaming Physical Education in
Primary and Secondary schools for Promotion of
Sports, Tanzania Institute of Education Quarterly,
May 2009.
• Tiboroha, J. Challenges in Organizing Physical
Activities to promote Health in People with special
needs – Paper presented to the Eastern African
conference for Fitness and Health to People with
Special Needs – October 2005
Academic Visits and Scholarships Received
• The World Bank’s “Quick Wins Project”,
Scholarship for PhD Study on The Transnational
Youth Football coaching courses in Tanzania: An
investigation on the adoption process and barriers
for coaches to participate, August 2010 – May
2013
• The SIDA-SAREC research fund on the desk-
review of the eliciting factors for poor youth socio-
economic development in Tandale: What can youth
football do to avail the situation? August, 2009 –
February, 2010
• The SIDA-Linnaeus Palme Scholarship, Academic
Visit to Malmo Sweden, Jan 2009 – June 2009.
• EdQUAL Prospective Doctoral Students’
Workshop on Qualitative Research Method held at
The University of Bouya, Limbe, Cameroon, 2nd –
12th December, 2008
• Norwegian State Educational Fund (NSEF), MSc
Studies, September 2002 - February 2004.
• Norwegian State Educational Fund (NSEF), BSc
Studies in Exercise and Health Sciences,
September 1999 – June 2002
• Norwegian State Education Fund (NSEF),
Norwegian Language Course for Foreign Students
at the University of Oslo Norway, August 1998 –
June 1999.
Referees
1. Dr Hamad Said Ndee
Head of Department
Department of Physical Education and Sports
Sciences
hndee@yahoo.com
2. Rune Hansen
Director of Youth Football Development
Staebeck Football Club
Oslo, Norway
E-Mail: rune.hansen@staebeckfk.no
3. Peter Tape Kristiansen,
Development Executive Director
Malmo Football Club
Malmo, Sweden
E-mail: peter.taper@mff.se
4 Prof. Susanna Hadenberg
Malmo University,
20506 Malmo, Sweden.
E-mail; sussana@mah.se
I Jonas B. Tiboroha, hereby certify that the above
given are my true personal information. Signed on
17th November, 2011.


Friday, December 19, 2014

HII NDIO HABARI MPYA KUTOKA YANGA

Mwenyekiti wa Yanga amefanya mabadiliko katika Safu za uongozi wa klabu hiyo huku akiweka vijana ili waweze kuitumikia klabu kwa muda mrefu. Mmoja wa vijana aliepata bahati hiyo ni Jerry Muro ambae amekuwa msemaji wa timu. Katibu Mkuu atakuwa Dr Jonas B Tiboroha.

Pamoja na hayo mwenyekiti Manji amelibadilisha benchi la ufundi kwa kumuondoa kocha Maximo na kumleta Kocha mpya mdachi Bw Hans van Pluijm akiwa anasaidiwa na mzawa Bw CharlesMkwasa.  




SSERUNKUMA MAJANGA SIMBA: HUENDA ASICHEZE MECHI YOYOTE YA LIGI

Wakati Simba SC ikidai kumalizana na mshambuliaji Mganda Simon Sserunkuma na kupata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC), klabu yake ya Express imesema imechezewa rafu na itavunja uhamisho huo sanjari na kuipeleka
Simba mahakamani kwa kughushi nyaraka.

Baada ya kufanya vizuri katika mechi yao ya kwanza ya majaribio Tanzania wakiisaidia Simba kuifunga Yanga mabao 2-0 Jumamosi, Sserunkuma na beki wa kati Juuko Murshid (Mganda pia),walisaini mikataba ya kuitumikia
klabu hiyo ya Msimbazi. Sserunkuma alisaini mkataba wa miaka miwili wakati Murshid alisaini miaka mitatu.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Express SC Francis Ntalazzi amekaririwa na mtandao wa Kawowo Sports leo akilia kufanyiwa rafu na Simba katika kukamilisha usajili wa Sserunkuma uliofanyika Jumapili, siku moja baada ya mechi ya ‘ndondo’
ya ‘Nani Mtani Jembe 2′.

Akielezea faulo iliyofanywa na Simba kufanikiwa usajili wa Sserunkuma, Ntalazzi anahoji juu namna saini yake ilivyoghushiwa kwenye mkataba wa mchezaji huyo.

“Binafsi, sikusaini nyaraka yoyote kuthibitisha uhamisho wa mchezaji husika (Sserunkuma) hivyo saini ilighushiwa,” kiongozi huyo wa juu
amesema huku akiweka wazi kusudio la kuipeleka Simba mahakamani kwa udanganyifu na amejipanga kuhakikisha anavunja uhamisho wa mchezaji huyo.

Ingawa uongozi wa Simba haukuwa tayari kuweka wazi fungu ambao nyota huyo amepewa kabla ya kukubali kumwaga wimo, ilielezwa jana kuwa ilimpatia dola la Marekani 40,000 (Sh. milioni 67).

Baada ya kusaini dili hiyo, (Sserunkuma) alirejea kwao Uganda na katika hali ya kushtusha Jumanne alikuwa miongoni mwa nyota wa Express, timu hiyo ilipochapwa mabao 2-1 dhidi ya Kikosi cha Bul F.C katika mechi ya Ligi Kuu ya
Uganda msimu huu.

Kabla na baada ya mechi hiyo, Sserunkuma alionekana akigawa pesa kwa wachezaji wenzake na viongozi wa Express kama ishara ya kuagana.
Sserunkuma, ambaye aliwahi kukipiga na klabu za Kyegenra Happy Boys F.C, Victors, SC Villa, Vipers na Express alisema; “Nimefurahi kuhamia Simba na ninawashauri wachezaji wenzangu kujifua kwa bidii, kuwa na nidhamu, kila mmoja na muda wake maalum katika maisha.”

SIMBA WANASEMAJE
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope, baada ya kutafutwa na mtandao huu kuzungumzia suala hilo, amesema Sserunkuma hana mkataba na klabu, bali wakala wake ndiye amekuwa akiingia mikataba na klabu zinazomsajili.

“Mkataba wa Sserunkuma na Express ulionesha kwamba hamzuii kujiunga na timu yoyote muda wowote. Sisi tumeingia mkataba na wakala wake kama ilivyokuwa kwa Express,” amesema
Hanspope. Ameongeza kuwa walipata ITC ya mchezaji huyo kutoka Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) siku mbili baada ya kumsainisha mkataba (Jumanne).

Kuhusu kucheza mechi ya Ligi Kuu ya Uganda akiwa na Kikosi cha Express ilhali amejiunga na Simba, Hanspope amedai hawana taarifa hizo huku akiahidi kufuatilia suala hilo.


Tuesday, December 16, 2014

KOCHA WA YANGA PRUIJM ATUA DAR

Van Der Pruijm alipotua usiku wa saa nane na nusu
Kocha wa zamani wa Yanga mdachi Hans Van Der Pruijm amesema amerudi tena kwenye timu yake ya zamani kuendeleza pale alipoishia,

‘Falsafa yangu ipo pale pale ya kucheza soka la kushambulia, kwasababu naamini ili ushinde mchezo ni lazima ufunge mabao ya kutosha’.

akiwasili jijini Dar
Kocha huyo amesema bado hajasaini mkataba ila ana matumaini makubwa atamalizana na wakurugenzi wa klabu pale watakapokutana, Van Pruijm anakuja kuziba pengo la kocha aliye timuliwa Mbrazil Marcio Maximo .

 Ahsante: Shaffih Dauda


RASMI: YANGA WAMTIMUA MAXIMO

Pita hivi: askari akimuelekeza maxio Maximo uwanja wa ndege
Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,

Baada ya kuchapwa mabao 2-0 na mahasimu wao wa soka Simba SC katika mchezo wa ‘ Hisani Nani Mtani Jembe’ siku ya Jumamosi iliyopita, klabu ya Yanga SC imeamua kufikia maamuzi magumu ya kumfuta kazi kocha Marcio Maximo na ni wazi Mholanzi, Hans Van De Pluijm atachukua nafasi hiyo. 

Hii ni mara ya pili kwa Yanga kumfukuza kazi kocha wao mara baada ya kufungwa na Simba. Ikumbukwe mwaka uliopita, Mholanzi, Ernie Brandts aliondoshwa baada ya kufungwa mabao 3-1 katika Mtani Jembe.

Tofauti na ilivyokuwa kwa Brandts ambaye aliifundisha Yanga kwa mwaka mmoja na kuisaidia kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2012/13, Maximo yeye amefukuzwa baada ya kuiongoza timu hiyo katika michezo tisa ndani ya miezi mitatu. 

Yanga imepoteza michezo miwili kati ya saba ya ligi kuu msimu huu, Maximo ambaye alianza vizuri klabuni hapo kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Jamii, alipoteza mchezo wa kwanza tu wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Yanga imeshinda michezo minne msimu huu, lakini hadi l,igi inasimama katika raundi ya saba hakuna mtu alikuwa na shaka kuhusu uwezo wa Maximo. Kocha huyo wa zamani wa timu ya Taifa
ya Tanzania, Taifa Stars amechokwa haraka sana na mashabiki, wapenzi, wanachama na viongozi wa klabu yake kutokana na kiwango kidogo cha uchezaji. Mifumo yake ya ufundishaji imekosa mvuto, lakini kitendo cha kufungwa kidhaifu na Simba kimeshindwa kuvumilika.

COUTINHO, JAJA, EMERSON WAMPONZA?

Ndiyo sababu kubwa, ukitoa mbinu zake, Maximo alikuwa akiwakumbatia zaidi wachezaji raia wa Brazil, Andrey Coutinho, Geilson Santos ( ambaye aliomba mwenyewe kuachwa baada ya michezo saba), kwa Emerson Oliveira siwezi kuzungumzia kwa sababu mchezaji huyo wa nafasi ya kiungo alicheza katika kiwango cha kawaida wakati alipoichezea Yanga kwa mara ya kwanza.

Jaja alifunga mara mbili dhidi ya Azam, ila alikosa makali katika ligi kuu kiasi cha kufunga bao moja tu katika michezo saba ya ligi kuu. Alishindwa kumudu presha ya mashabiki wa Yanga ambao hawakuwa wakipendezwa na kiwango chake huku uchezaji wake wa taratibu ukiwaboa wengi.

Maximo aliwanyima nafasi washambuaji kama Said Bahanunzi, Jerry Tegete, Saimon Msuva, Hussein Javu na Hamis Kizza hata pale wachezaji hao wa Kibrazil waliposhindwa kufanya vizuri.
Kuwang’ang’ania wachezaji hao na kuwanyima nafasi wale wenye uwezo kumewakera . Brandts aliondolewa baada ya kufungwa 3-1 licha ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili zaidi, yeye aliondolewa kwa kuwa alipingana na uamuzi wa viongozi kuwasajili baadhi ya wachezaji ambao hakuwataka wakati ule.
Brandts ndiye mwalimu aliyeifanya Yanga kucheza mchezo mzuri wa kupasiana na ndiye aliyeimarisha kiwango cha wachezaji kama, Saimon Msuva, Frank Domayo ( yuko Azam FC kwa sasa), Juma Abdul, Oscar Joshua na wengineo lakini kwa Maximo imekuwa ni tofauti,
wachezaji wengi wameshuka viwango na
ameshindwa kuwaimarisha wachezaji ambao ‘ wanasua-sua’. 

Yanga wamefanya uamuzi sahihi kwa kumuondoa Maximo na Coutinho.

Ahsante: Shaffih Dauda


Monday, December 15, 2014

BREAKING NEWS: HAMIS TAMBWE ASAJILIWA NA YANGA

Hamis Tambwe akisaini

 Akihojiwa na kipindi cha sports bar cha clouds tv Hamis Tambwe amekubali kuwa amesaini Yanga



MWANAMUZIKI MKONGWE WA BENDI YA TABORA JAZZ AFARIKI DUNIA


 Shem Karenga wapili kutoka kushoto waliosimama.

 Shem Ibrahim Karenga, mkongwe wa muziki wa dansi Alizaliwa mwaka 1950, Bangwe, Kigoma na kupata elimu ya msingi katika shule ya kimishionari ya Kihezya kuanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1964.

“Kiukweli, nilianza kujifunza muziki tangu nikiwa shuleni kwa sababu mimi nimesoma shule ya Wamishionari, sasa kule tulikuwa tukifundishwa fani hiyo,” ndivyo anavyoanza kusema Karenga.

Karenga anasema kuwa, baada ya kumaliza shule huku shetani muziki akiwa kampanda kichwani, mwaka 1964 alijiunga na bendi ya Lake Tanganyika Jazz ambayo maskani yake yalikuwa mjini Kigoma.
 
Anakumbuka kuwa, aliingia Lake Tanganyika akiwa mwimbaji na mcharazaji wa gitaa la besi, ambako pia alikuwa na ujuzi wa kutengeneza gitaa kwa kutumia vifaa vya kuokoteza. Akiwa na Lake Tanganyika Jazz, aliyodumu nayo kwa miaka minane, alianza pia kujifunza vyombo vingine vya muziki kama vile; Drums, Kinanda, gitaa la Rithym na la Solo’.
 
“Mwaka 1972, aliitwa kwenye bendi ya Tabora Jazz kama mwanamuziki mwenye kipaji cha utunzi, mwimbaji na mpigaji wa gitaa la Solo, alijiunga na Tabora Jazz akiwa na vibao vyake Dada Asha na Lemmy alivyovitungia Lake Tanganyika, ambavyo vilimpa umaarufu mkubwa alipo vipakua hapo Tabora Jazz'.
 
 Anasema, Tabora jazz walimchukua akiwa Mtaalam wa muziki, ambako hata hivyo alipokuwa na bendi hiyo alikuwa akijiendeleza zaidi kwa masomo ya jioni kwenye shule ya Sekondari ya Milambo, Tabora pamoja na kusoma vitabu mbalimbali vya muziki.

Katika bendi ya Tabora Jazz ambako alikuwa pia kama Kiongozi wa bendi, Karenga alikutana na wakali wengine wa muziki kama vile Kassim Kaluona na Athuman Tembo ambao kwa sasa ni marehemu pamoja na Salum Muzila.

Kutokana na sababu binafsi ambazo hakutaka kuziweka wazi, mwaka 1983 alijiengua kutoka Tabora Jazz na kusimama kabisa kujihusisha na muziki, ambako kilichofuatia ilikuwa ni kifo cha bendi hiyo.

“Mwaka 1990 aliondoka Tabora na kutua jijini Dar es Salaam alipokutana na Baraka Msilwa katika mwaka huohuo na kuniomba nijiunge na MK Beats ili kuiongezea nguvu,” anasema Kalenga.

Ndani ya MK Beats iliyokuwa ndugu na bendi nyingine iliyotamba vilivyo enzi hizo, MK Group, Karenga alikutana na wakali kama Malik Star, Sisko Lulanga, Fungo Shomari na Bwami Fanfan.

Baada ya kujiunga na MK Beats iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Tukunyema’, Karenga aliisuka vema na kuinyanyua vilivyo hasa kwa vibao moto wa kuotea mbali vilivyozitetemesha vikali bendi nyingine
zote za wakati huo.

Mwaka 1995, MK Beats ilisambaratika, ambako mwaka uliofuata, yaani 1996 alianzisha bendi ya Tabora Jazz Star kwa kushirikiana na mtu aliyemtaja kwa jina la Ibrahim Didi.

“Bendi ya Tabora Jazz Star ndio niliyo nayo hadi sasa nikiwa Mkurugenzi Msaidizi, ambako nafasi ya Mkurugenzi Mkuu imeshikiliwa na Didi mwenyewe,” alisema Karenga.

Akizungumzia anavyouona ushindani wa kimuziki akiwa na bendi yake hiyo ya Tabora Jazz Star, Karenga alisema kwa upande wake mambo si mazito sana kwa kuwa ana mashabiki wake wa tangu huko nyuma.

Kwa upande wa mafanikio, Karenga anasema ukiondoa nyumba nzuri aliyoiporomosha nyumbani kwao Kigoma, anashukuru kuona ana marafiki wengi na anaishi atakavyo akiwa anamudu vema kuitunza familia yake.

Ushauri alioutoa kwa wanamuziki na mashabiki wa dansi ni kuwa, wasibabaike kwani muziki huo ni wa kudumu, ambako hata hivyo alisikitika kuona kuna uhaba mkubwa wa vijana warithi wa miondoko hiyo
kwa sasa.

“Unajua, sisi tulirithi dansi kutoka kwa baba, kaka na wakubwa zetu wengine, lakini ni masikitiko makubwa kuona vijana wetu wa sasa wanarithi muziki hewa wa Bongo Fleva,” alisema.

Alisema, sababu ya kuuita muziki wa Bongo Fleva kuwa hewa ni namna wasanii wake wanavyopora midundo na ala kutoka nje huku wakijidai kuwa ni mtindo mpya wa muziki hapa nchini.

Mkongwe huyo aliyebainisha siri yake ya kukubalika katika muziki kuwa ni bidii na juhudi za dhati kwenye fani hiyo, alisema anavutiwa na wasanii wote wanaofanya vema katika sanaa.

Kama ilivyo kwa wakongwe wengine wengi wa muziki, Karenga alifaulu kuwarithisha muziki watoto wake wawili wa kiume ambao ni Ramadhan na Mussa waliowahi kuwika vilivyo katika bendi ya TOT Plus.

“Mussa ni mwimbaji na rapa mahiri, ambako kaka yake, Ramadhan ni mcharazaji wa gitaa kiongozi, Solo,” anasema Karenga, baba wa watoto sita.

Watoto wengine wa Karenga ambao hawakubahatika kurithi kazi yake ya muziki ni Tausi, Biata pamoja na Rehana.




BREAKING NEWS: PRUIJM KUREJEA KUINOA YANGA

kocha Mdachi Hans Van Der Pruijm huenda akarejea nchini kuifundisha tena YANGA,kutoka chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo kinasema kocha huyo wa zamani wa klabu hiyo huenda akawasili usiku wa leo kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya awali.

Mwishoni mwa juma hili kwenye mchezo wa NANI MTANI JEMBE Yanga ilifungwa na mtani wake wa jadi Simba mabao 2-0 huku timu hiyo inayonolewa na Mbrazil Marcio Maximo ikionyesha kiwango cha kawaida kwenye mchezo huo ikilinganishwa na kipindi cha mdachi huyo.
AHSANTE: SHAFFIH DAUDA


Friday, December 12, 2014

KIIZA ATUPWA NJE YANGA

Hamisi Kiiza "Diego "
Taarifa za kuaminika ambazo tumezipa hivi punde, klabu ya Yanga ipo mbioni kukatisha mkataba na mshambuliaji Hamis Kiiza raia wa Uganda.

Mmoja wa watu ambao wanashughulika na usajili wakati akiongea na mtandao huu amesema

‘’Tutakaa chini kuzungumza na Kiiza ili kuangalia namna ya kuachana kwa amani,baada ya Mliberia kufuzu vipimo vya afya hatuna jinsi lazima tuliondoe jina la Kiiza kwenye usajili wetu,kilisema chanzo hicho ‘’

Yanga inalazimika kupunguza mchezaji mmoja wa kigeni hasa baada ya mshambuliaji Kpah Sean Sherman kufuzu vipimo vya afya na kuwa mbioni kusaini mkataba na klabu hiyo.

Hivi karibuni Yanga ilimsainisha kiungo Emerson toka nchini Brazil mkataba wa mwaka mmoja, ukiachana na Kiiza wachezaji wengine wa kigeni ndani ya klabu ya Yanga ni Mbuyu Twite,Haruna Niyonzima, Kpah Sean Sherman na wabrazil Courtinho na Emerson.

Ikumbukwe Idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa na timu ni watano.


Thursday, December 11, 2014

DAVIDO AMWAMBIA DIAMOND AWE NA SHUKRANI

DAVIDO AND DIAMOND
Huhitaji kujifikiria mara mbili kuamini kuwa Davido na Diamond haziivi tena kwa sasa!

Yote yalianza baada ya Davido kutweet ‘N they cheat again, Lol’ baada ya Idris kutangazwa mshindi wa Big Brother Hotshots. Tweet hiyo ikimfanya Davido atukanwe matusi ya kila aina kutoka kwa Watanzania.

Usiku huo huo, Diamond alishinda tuzo za TFA (The Future Awards) za Nigeria na kuandika:

Thanks God, we have cheated another one on The.Future Awards Africa in Lagos Nigeria… #SameDay.#SameNight Thank you Allah.”

Ujumbe huo moja kwa moja ukaashiria kuwa jibu kwa.Davido ambaye matusi kutoka Tanzania yaliendelea kumsakama.

Baadaye, Davido anayeaminika (na huo ndio ukweli) kuwa msanii aliyesaidia kumtambulisha Diamond kimataifa, aliandika ujumbe kwenye Twitter. unaoshiria kumlenga Diamond.

An ungrateful stone will eventually fall… I will always be grateful to pple that have helped me climb this tall ladder of success,” alitweet Davido.

Tweet hiyo ilimaanisha: Jiwe lisilo na shukrani hatimaye huanguka… Nitakuwa mwenye shukrani siku zote kwa watu walionisaidia kuipanda ngazi ya mafanikio.”

Hata hivyo naye Diamond alitumia siku ya Uhuru wa Tanganyika jana kutoa nasaha zake kuhusiana na mikwaruzano baina ya wasanii wa Afrika kwa kuandika:

Badala ya wasanii kuwa ndio mfano bora wa kuweka karibu nchi zao na kujenga Afrika yenye upendo na amani…eti wao ndio wanakua chanzo cha kutenganisha nchi zao. Namna hii kweli tutajenga Afrika? Anyway, Happy Independence day Tanzania.”

 Thanks: BongoClan


Tuesday, December 9, 2014

BREAKING NEWS: KUNA MAPIGANO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI DUMILA

Abiria wakishirikiana na polisi kuzima moto uliowashwa barabarani

Polisi wa kutuliza ghasia wakielekea kwenye tukio
Yametokea mapigano kati ya wakulima na wafugaji dumila mkoani morogoro. Magari yamesimama hayaendi morogoro na wala ya morogoro hayaendi dodoma.

Polisi wa kutuliza ghasia (FFU)  wameelekea huko kutuliza ghasia hizo.

kwenye moshi ndio eneo la mapigano

Foleni ya magari iliyosababishwa na mapigano hayo

 



DANNY MRWANDA ASAINI YANGA KWA MKATABA WA MWAKA MMOJA

Mchezaji Danny Mrwanda amesaini kuitumikia klabu ya Yanga kwa mkataba wa mwaka mmoja. Mkataba huo umesainiwa jana usiku.
Danny Mrwanda akiweka saini katika mkataba



Friday, December 5, 2014

MWANAFUNZI KCMC ATUPA KICHANGA KWENYE PIPA LA TAKA

MWANAFUNZI wa mwaka wa kwanza shule ya viungo KCMC mjini Moshi  mkoani Kilimanjaro, Rachel Malima (22), amewekwa chini ya uangalizi maalumu wa madaktari baada ya kujifungua na kumtelekeza mtoto kwenye pipa la kuhifadhia takataka katika vyoo vya hospitali hiyo.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Ofisa Uhusiano wa hospitali ya KCMC, Gabriel Chiseo, alikiri kutokea kwa tukio hilo juzi baada ya mwanafunzi huyo kushikwa uchungu wa kujifungua.

Alibainisha kuwa, Malima alifika hospitalini hapo akiwa na wenzake na kupokelewa na wahudumu wa mapokezi na kuwekwa mapumziko wodini kabla ya muda mfupi kuomba kwenda msalani kujisaidia na kuruhusiwa.

Alieza kuwa, baada ya kufika msalani ndipo alipojifungua mtoto huyo na kumweka katika pipa la takataka na kutokomea kusikojulikana.

Inaelezwa kuwa, mara baada ya kuondoka mmoja wa wafanya usafi hospitalini hapo, aliingia msalani kwa ajili ya kuhakiki usafi na ndipo alipokuta choo kikiwa kimetapakaa damu na alipofungua pipa la takataka alikuta kichanga kikiwa na mfuko wa uzazi (Placenta), kinatupa tupa mikono na miguu na mdomoni kimesokomezwa taulo ya kike (Pad), ili sauti isisikike.

Chiseo, alisema jitihada za kumtafuta na kumkamata zilifanyika na hivi sasa yupo chini ya uangalizi maalum wa madakatari wa hospitali hiyo kwa ajili ya kumjenga kisaikolojia ili aweze kuhojiwa sababu ya kufanya hivyo.

“Hivi sasa Malima yupo chini ya uangalizi maalum, mtoto anaendelea vizuri  lakini pia bado tukio hilo halijaripotiwa polisi ila lipo chini ya kitengo cha uastawi wa jamii wa hospitali ambao watajua ni nini kitafuata baada ya Malima kupata nafuu,” alisisitiza Ofisa Habari huyo.

Kukamatwa kwa mwanafunzi huyo, kulitokana na jitihada za mashuhuda wa tukio hilo na uongozi wa KCMC, ambao walimwona Malima akiingia hospitalini hapo akiwa na baibui na alitoka akiwa anachechemea huku akiwa amesaidiwa mkoba na mtu ambaye hadi sasa hajafahamika.

CHANZO: TANZANIA DAIMA



Saturday, November 29, 2014

HAYA NDIO MAAZIMIO YA BUNGE JUU YA ESCROW

MAAZIMIO YA BUNGE KUHUSU HOJA YA TAARIFA MAALUM YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU TAARIFA YA UKAGUZI 

MAALUM KUHUSIANA NA MIAMALA ILIYOFANYIKA KATIKA AKAUNTI YA ‘ESCROW’ YA TEGETA

PAMOJA NA UMILIKI WA KAMPUNI YA IPTL

_____________________________________

 

1.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuhusu Ukaguzi Maalum wa Malipo yaliyofanyika katika Akaunti ya Escrow ya Tegeta uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (‘CAG’) pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (‘TAKUKURU’) imeonesha kwamba kwamba Harbinder Singh Sethi, James Rugemalira (VIP), Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Waziri wa Nishati na Madini, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (‘TANESCO’) walihusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha kufanyika miamala haramu ya fedha za Akaunti ya Escrow ya Tegeta kwenda kwa makampuni ya Pan African Power Solutions Ltd. (‘PAP’), na VIP Engineering & Marketing (‘VIP’);

KWA KUWA, kwa sababu ya kuhusika kwa watu hao na miamala iliyofanyika kwenye Akaunti ya Escrow imeliingizia Taifa hasara ya mabilioni ya fedha za umma zinazotokana na kutokulipwa kwa kodi mbali mbali za Serikali na kushindwa kwa TANESCO kukokotoa upya kiwango cha malipo ya gharama za uwekezaji (‘capacity charges’) wa IPTL;

KWA KUWA, mabilioni ya fedha yaliyotolewa kwenye Akaunti ya Escrow yametumika kuwapa kile kinachoonekana kuwa ni rushwa baadhi ya viongozi na maafisa wa serikali kama vile Mawaziri, Majaji, Wabunge, Wenyeviti wa Kamati za Bunge, wakuu wa taasisi za umma, viongozi wa dini, mawakili wa kujitegemea na watu binafsi.

NA KWA KUWA, vitendo vilivyofanywa na watu hawa vinaashiria makosa mbali mbali ya jinai kama vile uzembe, wizi, ubadhirifu, kutakatisha fedha haramu, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa na kupokea mali ya wizi;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, TAKUKURU, Jeshi la Polisi na vyombo vingine husika vya ulinzi na usalama viwachukulie hatua stahiki za kisheria, kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, watu wote waliotajwa na Taarifa Maalum ya Kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusiana na miamala ya Akaunti ya Escrow, na watu wengine watakaogundulika kuhusika katika vitendo hivyo vya jinai kufuatia uchunguzi mbali mbali unaoendelea;

2.    KWA KUWA, vitendo vya kijinai wanavyhohusishwa navyo viongozi wa umma na maafisa wa ngazi za juu serikalini vinakiuka pia maadili ya viongozi wa umma na kuwanyima viongozi na maafisa hao uhalali wa kuendelea kushikilia nafasi za mamlaka katika uongozi wa umma;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO wawajibishwe, kwa kuishauri mamlaka yao ya uteuzi kutengua uteuzi wao;

3.    KWA KUWA, katika watu walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kashfa ya miamala ya Akaunti ya Escrow wapo pia viongozi wa Kamati za Kudumu za Bunge kama vile Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO;

NA KWA KUWA, Bunge na/au Kamati zake za Kudumu zina uwezo na mamlaka, kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, ya kuwawajibisha viongozi hawa wa Kamati kwa kuwavua nyadhifa zao;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Kamati husika za Kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka, na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge, kuwavua nyadhifa zao Wenyeviti tajwa wa Kamati husika za Kudumu za Bunge;

4.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba katika watu waliotajwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kashfa ya miamala ya Akaunti ya Escrow wapo pia Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania;

KWA KUWA, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (‘Katiba’) imeweka utaratibu mahsusi wa kushughulikia nidhamu ya Majaji;

KWA KUWA, utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji kwa mujibu wa Katiba unamtaka Rais kuunda Tume ya Uchunguzi ya Kijaji kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Majaji;

NA KWA KUWA, utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji kwa mujibu wa Katiba unamruhusu Rais kumsimamisha kazi Jaji au Majaji husika wakati uchunguzi wa tuhuma dhidi yake unaendelea;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aunde Tume ya Kijaji ya Uchunguzi kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania;

5.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba Stanbic Bank (Tanzania) Ltd. ilishiriki kupokea na kutakatisha fedha zilizotolewa kwa njia haramu kutoka katika Akaunti ya Escrow na kupelekwa katika akaunti zilizofunguliwa na PAP katika benki hiyo;

KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba akaunti za PAP  katika Stanbic Bank Tanzania Ltd. zimekwishafungwa baada ya fedha zote zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow kumalizika na Akaunti ya ya VIP katika Mkombozi Commercial Bank imebakiza kiasi fulani cha fedha;

NA KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati inaonesha kwamba kuna uwezekano fedha zilizotolewa kutoka kwenye akaunti za PAP na VIP zilipelekwa katika benki nyingine;

NA KWA KUWA, vitendo vya Stanbic Bank (Tanzania) Ltd., na benki nyingine kupokea na kutakatisha fedha zilizotolewa kwenye Akaunti ya Escrow ni vitendo vya jinai kwa mujibu wa Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, mamlaka husika za kifedha na za kiuchunguzi ziitaje Stanbic Bank (Tanzania) Ltd. na benki nyingine yoyote itakayogundulika, kufuatia uchunguzi wa mamlaka za kiuchunguzi, kujihusisha na utakatishaji wa fedha zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow, kuwa ni taasisi zenye shaka ya utakatishaji wa fedha haramu (institutions of money laundering concern);

6.    KWA KUWA, vitendo vya wizi, ubadhirifu wa mali ya umma, hujuma ya uchumi na ufisadi vimeongezeka, kushamiri na kushirikisha viongozi wa kisiasa na maafisa wa serikali pamoja na wafanya biashara wakubwa;

KWA KUWA, kwa mujibu wa sheria iliyoiunda, TAKUKURU inashughulikia vitendo vya aina zote za rushwa zikiwemo rushwa ndogo ndogo (petty corruption) na rushwa kubwa na ufisadi (grand corruption) na matumizi mabaya ya madaraka;

NA KWA KUWA, kwa sababu ya majukumu yake mapana kisheria, TAKUKURU inaelekea kuelemewa katika vita ya kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa letu kiuchumi, kijamii na kisiasa;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Serikali iandae na kuwasilisha Muswada wa marekebisho ya Sheria iliyoiunda TAKUKURU kwa lengo la kuanzisha taasisi mahsusi itakayoshughulikia, kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa;

7.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha jinsi ambavyo TANESCO imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kulipa gharama za umeme unaozalishwa na IPTL na hivyo kuathiri hali ya kifedha ya Shirika hilo;

KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati inaonesha kwamba TANESCO itaendelea kulipa fedha nyingi kwa ajili ya gharama za umeme huo wa IPTL;

HIVYO BASI, Bunge linaazimia kwamba Serikali iangalie uwezekano wa kununua mitambo ya kufua umeme ya IPTL na kuimilikisha kwa TANESCO kwa lengo la kuokoa fedha za Shirika hilo.

8.    KWA KUWA, kwa miaka mingi mikataba mibovu ya kuzalisha umeme kati ya TANESCO na makampuni binafsi ya kufua umeme imeisababishia TANESCO hasara ya mabilioni ya fedha na hivyo kutishia uhai wake wa kifedha;

KWA KUWA, Bunge lilikwishaazimia kwamba serikali iwasilishe mikataba husika Bungeni au kwenye Kamati zake kwa lengo la kuliwezesha Bunge kutekeleza vyema wajibu wake wa kuisimamia na kuishauri serikali;

NA KWA KUWA, Serikali haijatekeleza Azimio hilo la Bunge hadi sasa;

HIVYO BASI, Bunge linaazimia kwamba Serikali itekeleze Azimio husika la Bunge mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile kabla ya kumalizika kwa Mkutano wa Bunge la Bajeti Serikali iwasilishe taarifa ya utekelezaji wa mapitio ya mikataba ya umeme.

Imewasilishwa leo hii tarehe 28 Novemba, 2014.

------------------------------------------------------

ZITTO ZUBERI KABWE (MB)

MWENYEKITI

KAMATI YA PAC



HELKOPTA YA MALI ASILI YAANGUKA UKONGA MOMBASA

Wananchi wakiangalia helkopta hiyo
Helicopter mali ya serikali wizara ya mali asili yaanguka maeneo ya moshi bar mombasa Dar na kuua wote walio kuwemo na kuangukia nyumba za wananchi.

Polisi wameshafika eneo la tukio
Wananchi wenye nyumba hizo bado haijajulikana kama wamekufa ama hawakuwemo. Rubani na capt wa ndege hiyo inasemekana walikuwa na uzoefu mdogo sana(masaa machache sana) kutoka chuo cha 44 cha huko south African.





 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU