Facebook Comments Box

Monday, September 17, 2012

iPHONE 5 ZAUZWA MILIONI 2 NDANI YA MASAA 24

Kampuni ya Apple imesema imeuza simu yake mpya aina ya iPHONE 5 milioni 2 ndani ya masaa 24 baada ya kuizindua duniani kote. Mauzo hayo ni oda zilizotolewa kabla ya simu hiyo kuzinduliwa (pre oder). Vilevile kampuni hiyo imesema haitabadili siku ya kuitoa rasmi kwa wateja wake hao. Imebainisha kuwa itapeleka kwa wateja hao tarehe 21 septemba mwaka huu.




MWAKYEMBE AENDA KUINGIA MKATABA BERLIN

Waziri wa uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe na ujumbe wake wapo Berlin kuanzia tarehe 15 hadi 19 septemba kwa ziara ya kikazi. Moja ya tukio muhimu atakalo lifanya huko ni kusaini mkataba wa ushirikiano wa usafiri wa anga (Bilateral Air Service Agreement- BASA) baina ya nchi ya Tanzania na Berlin tarehe 17 septemba 2012. Tarehe 16 septemba Mheshimiwa alitembelea maonesho ya kimataifa ya sekta ya usafiri wa anga yaliyofanyika Berlin.
Mh Mwakyembe akiwa ndani ya moja ya ndege zilizokuwa kwenye maonesho hayo

Mh akipata maelezo kutoka kwa wataalam wa ndege za Airbus

Mh Mwakyembe akipiga picha na Balozi wa Tanzania Berlin Mh Ahmada (kushoto) na Afisa wa wizara ya uchuzi Ndg Ubwa (kulia)


Mh waziri akifanya mazungumzo na viongozi wa sekta ya anga wa Berlin



NYUMBU WARUDI SERENGETI KUTOKA MAPUMZIKONI






Msafara maarufu kwa jina la "Annual Animal Migration" unaohusisha wanyama aina ya Nyumbu wakiwa wanarudi katika mbuga ya Serengeti ya Tanzania wakiwa wanatoka katika mbuga ya Masai mara ya Kenya. Nyumbu hao walisafiri umbali wa zaidi ya kilometa 1000 katika mapumziko yao hayo. Msafara huo ambao ni maarufu zaidi duniani umevuta watalii wengi. Mwaka huu Nyumbu hao wamewahi kurudi kutokana na mvua zilizowahi kunyesha nchini Tanzania ambazo zimewawekea mazingira mazuri ya chakula. Nyumbu hao hukutana na mikasa na mazingira magumu wakati wa safari yao hiyo ambapo huwabidi kukatiza katika mto ambao una mamba na viboko ambao nao huwafanya msosi. Nyumbu hao waliorudi wanakaribia kuwa zaidi ya milioni moja na laki tano na huu ni msafara wa awali.

PICHA ZA UCHAGUZI MDOGO BUBUBU

Polisi wa kutuliza ghasia akimzuia mwananchi

Waangalizi wa usalama wakiwa kazini


Mawakala wa vyama wakifuatilia zoezi zima la upigaji kura

Mmoja ya wanasiasa akiongea na waandishi wa habari



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU