Facebook Comments Box

Saturday, February 14, 2015

HUU NDIO UKWELI KWA YANAYO ENDELEA AMBONI TANGA

Kamishna wa Polisi Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja ametoa maelezo ya kile kinachoendelea Tanga. Kumekuwa na maneno mengi katika mitandao ya kijamii kuhusu yanayo endelea huko Tanga. Hii imepelekea Kamishna huyo kutoa taarifa

Katika taarifa yake ameelezea kuwa manamo tarehe 26 mwezi wa kwanza mwaka huu majira ya saa tano usiku polisi wakiwa katika doria walivamiwa na majambazi na kuporwa silaha na kujeruhiwa.Polisi wakishirikiana na Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) walifanya upelelezi na kugundua zilipofichwa silaha walipofika eneo la tukio ndio yakatokea majibizano ya risasi kati ya majambazi na polisi. Majibizano hayo ya risasi yamewajeruhi askari sita na mpaka sasa msako unaendelea.

Hapa chini ni taarifa ya Kamishna Chagonja





TAMBWE WA KIMATAIFA: APIGA MBILI ZILIZOIPA YANGA USHINDI DHIDI YA BDF YA BOTSWANA

Amis Joselyn Tambwe akishangilia goli lake pamoja na Simon Happygod Msuva
YANGA Leo ndani ya Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam imeichapa Klabu ya Botswana BDF XI Bao 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Awali ya Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho.
 
Bao zote za Yanga zilifungwa na Straika wao Amisi Tambwe anaetoka Burundi moja katika kila Kipindi.
Tambwe akishangilia goli lake na Mrisho Ngassa na Msuva ambao ndio wapishi wa magoli yake.

Tambwe alifunga Bao la Kwanza Dakika ya Kwanza tu ya Mchezo alipounganisha kwa Kichwa Krosi ya Simon Msuva na kupiga Bao la Pili katika Dakika ya 55 pia kwa Kichwa baada ya Krosi safi ya Mrisho Ngassa.
Mrisho Ngassa akichanja mbuga


Timu hizi zitarudiana huko Botswana Wiki mbili baadae na Mshindi wake atatinga Raundi ya Kwanza kucheza na Mshindi kati ya Sofapaka ya Kenya na FC Platinum ya Zimbabwe.
Hapo Kesho Jumapili, Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC, watakuwa kwao Azam Complex huko Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kuivaa El Merreikh ya Sudan katika Mechi ya Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONZ LIGI.
Timu nyingine mbili za Tanzania ambazo pia zimo michuano ya CAF Barani Afrika ni KMKM na Polisi, zote za toka Zanzibar, Wikiendi hii zinaanzia Ugenini kwa KMKM kucheza Sudan na Al Hilal kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI  na Polisi kucheza Nchini Gabon na CF Mounana kwenye Kombe la Shirikisho
Mchezaji wa BDF akimfanyia rafu Haruna Niyonzima



APPLE SASA WAJA NA GARI LISILOTUMIA MAFUTA

Gazeti la Wall Street Journal linayo ripoti kuwa watengenezaji wa simu maarufu ya iPhone na kifaa cha iPad, Apple wanajishughulisha kutengeneza gari litakalotumia umeme ikiwa ni changamoto kwa kampuni ya Telsa inayotawala soko hilo kwa sasa.

Taarifa hiyo ya WSJ haijamtaja mtoboa siri hiyo zaidi tu ya kusema kuwa ni mwajiriwa wa Apple anayefanya kazi katika mradi huo.

Mtoa habari huyo ametanabahisha kuwa wapo watu mamia kadhaa wanaofanya kazi kwa siri kutengeneza gari hilo la mradi uliopewa jina la "Titan" na tayari wameshaunda muonekano unaoelekea kabisa kufanana na 'minivan'. 

Msemaji rasmi wa kampuni ya Apple alipoulizwa kuhusu hilo alikataa kuthibitisha au kukanusha taarifa hizo.

Nalo gazeti la Financial Times lina habari ambayo chanzo chake ni mtu ambaye hakutaka kutajwa, akisema kuwa wafanyakazi wa Apple wamekuwa wakitafiti kuhusu vipuri vya magari katika eneo moja huko Silicon Valley.

Waajiriwa wa hivi karibuni katika kampuni ya Apple ni pamoja na mkuu wa kitengo cha utafiti cha Mercedes-Benz katika tawi la Silicon Valley.


BREAKING NEWS: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA

Baraza la mitihani la taifa (NECTA) wameweka matokeo ya kidato cha nne kwa wanafunzi walio maliza kidato cha nne mwaka 2014.
Haya ni baadhi ya matokeo ya shule ya Mivumoni Islamic Secondary ambao imeshika nafasi ya 20 kitaifa. Wanafunzi wa shule hiyo wamepata Distinction 18 na Merit 21. matokeo mengine ingia kwenye link hapo chini.
BONYEZA HAPA KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

PIKIPIKI YAO YACHOMWA BAADA YA KUKWAPUA SIMU YA MWANADADA MMOJA

 Pikipiki hiyo ikiteketea kwa moto.
 Wananchi wakishuhudia pikipiki hiyo ikiteketea.
Wananchi wakipiga picha pikipiki hiyo.

Kamera yetu mtaani:

Wizi wa kukwapua kwa kutumia Pikipiki umeshamiri sana Jijini Dar es Salaam kwa watumiaji hao wa pikipiki kukwapua vifaa kama simu za mikononi, mabegi ya wanawake maarufu kama "vipima joto", laptop na vitu kama hivyo.

Kuna vijana wawili waliwahi kuchomwa moto baada ya kutimiza siku zao arubaini kama msemo usemavyo kuwa "Za Mwizi arubaini" katika maeneo ya Tabata-Liwiti.

Hali hiyo ilitokea tena katika maeneo ya Hospitali ya Ocean Road ambapo wataalamu hao wa kuiba kwa pikipiki walipokutwa na zahma hiyo baada ya kumkwapulia simu mwanadada mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja na wao kukimbia ndipo msamaria mmoja akawakimbiza kwa gari lake na watu hao kuzidiwa ujanja na kukamatwa katika eneo hilo na pikipiki yao kuchomwa moto kama inavyoonekana pichani.






 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU