Facebook Comments Box

Sunday, December 16, 2012

YANGA KUPAA DESEMBA 28, KULA MWAKA MPYA ULAYA



Kocha Brandts na wachezaji wake

MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Yanga SC wanatarajiwa kuondoka Desemba 28, mwaka huu mjini Dar es Salaam, kwenda Uturuki kuweka kambi ya wiki mbili kujiandaa kwenda kutetea taji lao hilo mjini Kigali, Rwanda.
Habari kutoka ndani ya Yanga, zimesema kwamba wiki hii mwalimu, Ernie Brandts ataamua idadi na wachezaji wa kwenda ziara hiyo, ambayo ni maalum pia kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.
Kocha huyo Mholanzi, kwa wiki zaidi ya mbili amekuwa akikinoa kikosi chake kwenye Uwanja wa sekondari ya Loyola, Dar es Salaam baada ya kumaliza likizo fupi ya baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu.
Yanga, chini ya Mwenyekiti wake, Alhaj Yussuf Manji imepania kurejesha utawala wake katika soka ya Tanzania na kwa kuanzia inataka kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu kwa kishindo mwishoni mwa msimu.
Yanga inataka pia kutetea Kombe la Kagame Januari mwakani mjini Kigali, katika michuano ambayo watakwenda na wapinzani wao wa jadi, Simba SC.
Yanga ilimaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ikiwa inaongoza kwa pointi zake 29, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 24, wakati Simba ni ya tatu kwa pointi zake 23.     


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU