Facebook Comments Box

Monday, August 12, 2013

VIDEO: HATUNA IMANI NA UCHUNGUZI KUHUSU SHEIKH PONDA - MTANDAO WA HAKI ZA BINADAMU




KIONGOZI WA SHIA TANZANIA AKEMEA VIKALI KITENDO ALICHO FANYIWA SHEIKH PONDA

Sheikh Hemedi Jalala

Kiongozi wa Shia Tanzania Sheikh Hemedi Jalala ameungana na Masheikh na wanazuoni wengine wa kiislam kupitia ukurasa wake wa facebook kukemea kitendo alichofanyiwa Sheikh kipenzi cha waislam wengi na mpigania haki Sheikh Ponda Issa Ponda na kusema kuwa busara haikutumika na jeshi la polisi katika tukio hilo. Pamoja na kuto kukubaliana na mbinu anazotumia Sheikh Ponda bado Sheikh Hemedi Jalala amekubali kuwa Sheikh Ponda anapigania haki za Waislam wa Tanzania. Hapo chini ni maelezo aliyoyaweka Sheikh Jalala katika ukurasa wake huo



POLISI WAMUWEKEA ULINZI SHEIKH PONDA MUHIMBILI



Dar es Salaam/Moro. Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda yupo chini ya ulinzi huku akitibiwa majeraha katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Sheikh Ponda alisafirishwa usiku wa manane kutoka Morogoro baada ya juzi kupigwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni mtutu wa bomu saa 12:25 jioni alipokuwa akisindikizwa na wafuasi wake kwenda katika Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja mara baada ya kumaliza kutoa mhadhara katika kongamano mjini hapo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Sheikh Idd Mussa Msema, alidai kuwa Sheikh Ponda alipigwa risasi tatu begani.
Taarifa kutoka ndani ya familia ya Ponda zilisema kwamba baada ya kupata taarifa za kupigwa risasi, baadhi ya masheikh walifunga safari kwenda Morogoro na kumrejesha Dar es Salaam usiku huohuo. Kabla ya kurudishwa Dar es Salaam, imeelezwa kuwa Sheikh Ponda alipelekwa katika Zahanati ya Islamic Foundation.
Mmoja wa wanafamilia alidokeza kwamba Sheikh Ponda alifichwa na alikuwa chini ya ulinzi mkali wa wafuasi wake na hakuna aliyeruhusiwa kumsogelea.
Muhimbili
Hata hivyo, habari zilizopatikana baadaye jana zilisema kuwa alifikishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Sheikh Ponda alifikishwa Muhimbili jana saa 7:18 mchana na alipelekwa kwenye chumba cha wagonjwa wa dharura na baadaye alitolewa na kupelekwa kwenye chumba cha x-ray kwa ajili ya vipimo. Baadaye alipelekwa chumba cha upasuaji.
Eneo kubwa la hospitali hiyo lilikuwa na idadi kubwa ya askari na mmoja wa askari waliokuwa doria hospitalini hapo alisema walitawanywa kwenye hospitali mbalimbali za Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kuwa angeletwa kwa matibabu.
“Nakuambia tuko hapa tangu saa kumi na moja asubuhi, tumetawanywa hospitali mbalimbali baada ya kupata taarifa kuwa analetwa Dar. Bahati nzuri kaletwa hapa Muhimbili... tunasubiri apate matibabu na tutamtia mbaroni,” alisema askari huyo.
Taarifa ya polisi
Msemaji wa Polisi, Advera Senso alisema jana katika taarifa yake kuwa Sheikh Ponda yuko Hospitali ya Muhimbili akitibiwa baada ya kupata majeraha yaliyotokana na purukushani na polisi wakati wafuasi wake walipokuwa wanataka kumtorosha
 
 
SOURSE:MWANANCHI


SAKATA LA ZAM TV: TENGA AOMBA KAMATI IMPE MAELEZO AZAM ILISHINDA VIPI ZABUNI YAKE

Sakata la klabu ya Yanga kugomea kukubaliana na mkataba wa kati ya kamati ya Ligi na Azam Media wa kuipa haki za matangazo ya televisheni ya mechi za ligi kuu kituo cha Azam TV limechukua sura mpya baada ya Raisi wa shirikisho la soka la nchini TFF Leogdar Tenga  kuingilia kati.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi mtandao huu ulizozipata ni kwamba Tenga amewaandikia barua Yanga akiwaambia kwamba amepata malalamiko yao dhidi ya mkataba wa urushwaji wa matangazo ya mechi za ligi kupitia Azam TV.

Pia Tenga amewaambia Yanga kwamba ameiomba kamati ya ligi kumpatia maelezo namna mchakato mzima wa ugawaji wa tenda hiyo ulivyofanywa mpaka kufikia maamuzi ya kuingia makubaliano na Azam TV.

Tenga amewaomba Yanga kuwa wavumilivu ili kushughulikia malalamiko yao kuhakikisha muafaka unafikiwa kwa ajili ya manufaa ya soka la Tanzania.
 
SOURSE: SHAFFIH DAUDA


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU