Facebook Comments Box

Sunday, March 3, 2013

OMMY DIMPOZ FT VANESSA MDEE - ME AND YOU




MBATIA, ULUOCH WAKATAA KUSHIRIKI KWENYE TUME YA KUCHUNGUZA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Mh Mbatia

WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka hadharani majina ya wajumbe wa Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya mwaka 2012 ya Kidato cha Nne jana, baadhi ya wajumbe waliopewa heshima hiyo ya kusaidia kutafuta sababu za matatizo ya elimu na jinsi ya kuyatatua, Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiel Oluoch, wamekataa uteuzi huo. Mbatia katika hoja yake kwa waandishi wa habari jana, alisema kwa kuwa hadi jana hakuwa amepata taarifa ya maandishi kuhusu uteuzi wake, asingeweza kutamka kama amekubali au la, hadi atakapokuwa amepata maandishi hayo akisema atakapoyapata ndipo, “nitafanya uamuzi kwa maslahi ya pamoja ya Watanzania.” Hata hivyo, habari za uhakika kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, zilisema Mbatia alifahamishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo kwa njia ya simu afike Ofisi ya Waziri Mkuu achukue barua yake ya uteuzi kama walivyofanya wajumbe wengine. Oluoch alipotafutwa azungumzie uamuzi wake wa kujitoa kwa mujibu wa barua aliyoiwasilisha Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema yuko mkutanoni akaomba apigiwe baada ya nusu saa na ilivyofanyika hivyo, alikata simu kila alipopigiwa. Ikiwa nia yetu ni thabiti ya na kweli ya kutaka kubadili mwenendo wa mambo yasiyo sahihi katika nchi ya Tanzania, hatuna budi kutii na kufuata sheria tulizojiwekea sisi wenyewe. Kama siyo kasuku, kila leo tunaimbiana misemo maarufu tunayonukuu kutoka kwa watu mahiri, mfano, “insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results. ~Albert Einsten” na “walk the walk, talk the talk” (ingawaje hii tumeibadili tunavyojua kwa akili yetu ati, ‘walk the talk’ -- hakuna msemo kama huo! How do you walk the talk? Kupinda tu misemo ya wenyewe). Sasa ikiwa Waziri Mkuu aliripotiwa na Ofisi yake kuwa alikutana na Wajumbe wa Tume aliyoiteua, bila ya kupata hakika ya kila mteuliwa --iwe ni kwa njia ya kumpigia simu kuthibitisha, kutuma ujumbe mfupi wa simu, kutuma barua, nukushi, barua pepe n.k-- kuwa (1) Amepata taarifa rasmi ya uteuzi huo na (2) Ameridhia uteuzi huo; Waziri Mkuu akaitisha kikao ijapokuwa baadhi ya wajumbe hawakuwemo kikaoni bila ya kuwa na hakika kama wanaopelea wametoa taarifa rasmi ya udhuru wa kutokuhudhuria kikao hicho, sioni ni kwa namna gani Mbatia analaumiwa kususia Tume il hali anaifuata sheria. Kuongoza ni mfano na Kiongozi ni mfano. Kwa wasiojali sheria au wanaojiona wapo juu ya sheria ama wenye adabu za woga, hili litakuwa jambo la kipuuzi kwao. Kwao wao amri ya mkubwa inatiiwa bila kuhojiwa hata kama imekiuka sheria, hata kama nchi ni ya utawala wa kiraia na haiendeshwi kijeshi. Kwao kuvunja sheria mama si jambo la ajabu. Ndiyo wale kila leo wanaimba misemo kama kasuku bila kutafsiri wala kujua maana yake. Na hao hawakawii kusema kwa kuwa huyu ni mmoja wa wanachama wa upinzani, basi lolote lile hata liwe jema atapata pa kupinga tu. Na utawasikia majuha hao wakijitapa kwa bezo la kejeli, “sheria Bongo?” Utakuwa na kasoro ukithubutu kusema Mbatia hana nia ya kusaidia nchi kuondokana na tatizo kwa kuhoji utaratibu uliotumika kumfikishia taarifa. Angekuwa hana nia angetumia miaka inayokaribia kumi kutafiti kuhusu elimu na kisha kukusanya vielelezo na kuwasilisha hoja Bungeni kuhusu uozo wa elimu? Kama anaweza kuunda hoja yenye nguvu hivyo kwa maslahi binafsi, je atakapounda hoja inayolihusu Taifa?

SOURCE: WAVUTI

YALIYOJIRI KWENYE KILIMANJARO MARATHON LEO: WAKENYA WAENDELEA KUTAMBA


Washiriki wa Kilimanjaro Marathon wakiwa tayari kabisa kwa ajili ya kukimbia
Vituko hafikukosekana wazungu hawa wao hawakukimbia marathon ila wametembea mpaka wamemaliza

Afisa ujasiliamali watu wa Kilimanjaro Christian Medical University College Victor Selengia katikati akiwa na mwanafunzi wa mwaka wa udakitari Carl Jacob(Kulia) na mwanafunzi wa udakitari mwaka wa nne Nico (kushoto) wakifurahia medali zao baada ya kumaliza kilometa 21
Dr Fransis akifurahia medali na |Carl baada ya kumaliza kilomita 21
Dr Sudai (kulia) akiwa na Dr Joseph (katikati) wakifurahia medali zao

Mwanafunzi wa udakitari David Majule akishuka kumalizia kwa kasi sana. Ameiambia KITONGONI kuwa mwaka huu ameweza kuvunja rekodi yake kwa kupunguza zaidi ya dakika 32 kutoka muda alio utumia mwaka jana. Amekuwa akishangazwa na watanzania kufanya vibaya katika haya mashindano na kuaacha kila mwaka mshindi akitokea Kenya na wakati mashindano yanafanyika Tanzania. Ameomba viongozi wa chama cha riadha wajiangalie upya na ikiwezekana wawajibike kwa hili

Principal Investigator wa MEPI Tanzania kutokea marekani akifurahia medali yake baada ya kumaliza kilomita 21 na Carl Jacob

Motta, Carl na Kimario baada ya kumaliza mbio. \Wanafunzi wengi wa KCMUCo wameshiriki kwenye mashindano haya na kufanya vyema. Japo ushindi umeenda kwa wakenya

Wenye medali zao wakishuka kwa kasi




Wanariadha kutoka Nchini Kenya wameendeleza Umwambawao katika mbio za Nyika za Kilimanjaro ‘Kilimanjaro Marathon 2013’ zilizofanyika leo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakenya walidhihirisha umwamba katika Mbio za Kilometa 42 baada ya Mkimbiaji wao Kipsang Kipkemoi kunyakua nafasi ya kwanza katika mbio hizo za mwaka huu upande wa wanaume na Wanawake ilinyakuliwa na Mwana dada Edna Joseph alebeba Medali ya Dhahabu.

Nafasi ya pili hadi ya tano kwa wanaume ni Julius Kilimo, Dominick Kiagor, Onesmo Maithiya Loshile Moikari ambapo upande wa wanawake ni Eunice Muchiri, Frida Too, Rosaline David na Jane Kenyara.
Jumla ya wakimbiaji 65000 walishiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.
Kocha wa Taifa Stars Kim Poulsen akiwa na Dr Josephine



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU