Facebook Comments Box

Friday, May 30, 2014

MWANAFUNZI WA UDSM AFARIKI USINGIZINI LEO

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam amefariki jioni hii.
Alitoka lecture akaenda kulala,akamwambia mwenzake amuamshe ndio akalala moja kwa moja.




KIBONZO: USTAADH NA MASHARTI YA KUOA YA SIKU HIZI




ZITTO KABWE ATOA UFAFANUZI JUU YA TUHUMA ZA KUOKOTEZA ZA SUGU


"Maelezo yangu kuhusu kazi za Kigoma AllStars/LEKADUTIGITE kwa NSSF na TANAPA.

Leo tarehe 29 Mei, 2014 Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Habari, Michezo, Vijana na Utamaduni amenituhumu kuhusika na kinachoitwa ufisadi katika Shirika la TANAPA na NSSF.
Nasikitika kwamba katika hali niliyonayo ya kumwuguza mama yangu naingizwa kwenye siasa za majitaka. Kwa sasa nitatoa maelezo kwa ufupi ili kuondoa upotoshaji.
Kampuni ya LekaDutigite inamilikiwa na wasanii 15 ambapo kila mmoja ana hisa 5% ambazo niliwalipia ili waweze kushirikiana katika kazi zao. Hisa 25% zilizobakia zinamilikiwa na kampuni ya Gombe Advisors ambayo ni kampuni isiyofanya faida (Company limited by guarantee) na haina maslahi yeyote ya kibiashara (not for profit company). Hivyo Mimi binafsi sina maslahi yeyote ya kifedha zaidi ya kuwasaidia wasanii hawa katika kazi zao mbalimbali.
Wasanii wa Kigoma AllStars wamefanya kazi na TANAPA na NSSF, kazi ambazo zinajulikana na zipo. Kwa upande wa TANAPA wasanii hawa waliandaa kazi ya kuitangaza Hifadhi ya Saadani na walilipwa. Kwa upande wa NSSF wasanii hao walitunga wimbo na video yake ( http://m.youtube.com/watch?v=sMl8T-RkIdM ) na wimbo huo unatumika katika Shirika hilo.
Vile vile walifanya matamasha mbalimbali ya kuhamasisha watu kujiunga na NSSF. Wasanii wa Kigoma All Stars wote ni wanachama wa Mfuko huo.
Katika kazi zote hizi Mimi binafsi sijafaidika kwa namna yeyote ile kifedha. Kauli yeyote ya kujaribu kuonyesha kazi hizi za wasanii ni ufisadi ni kauli za kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mtu ambaye anajaribu kusaidia wasanii kufaidika na kazi zao za sanaa.
Toka mwaka 2012 nilipoanza kujitokeza kusemea wasanii watu kadhaa wenye maslahi na tasnia hii wamekuwa wakinikatisha tamaa na hata wengine kuona nimewaingilia kazi zao.
Hivi sasa wasanii wa Kigoma AllStars ni wanahisa katika kampuni ya PERA Africa limited ili kufaidika na biashara ya miito ya simu. Yote haya nilifanya kwa uchungu nilionao kwa vijana wetu na sio kwa kutaka kufaidika kifedha. Nimeumizwa sana na tuhuma hizi za kuokoteza okoteza.
Inaniumiza zaidi kutokana na ukweli kwamba ninamwuguza mama yangu mzazi, kipindi ninachohitaji kutiwa moyo na kuombewa hata na maadui zangu kisiasa. Kipindi ambacho mama yangu yupo mahututi, tena mjumbe wa kamati kuu ya chama ambacho watoa tuhuma wanatoka, pole ninayopewa ndio hiyo. Hakuna namna ya kukosa ubinaadamu zaidi ya hivi.
Najua wajibu wangu ni kusimamia Mashirika ya Umma na nikiwa mpigania uwajibikaji nipo makini sana kuhakikisha sina mgongano wa maslahi katika mambo yangu. Ndio maana sina biashara yeyote ile ili kuhakikisha natimiza wajibu wangu kwa uadilifu mkubwa. Napata 'moral authority' ya kutaka uwajibikaji kwa sababu nafanya kazi zangu kwa misingi hiyo 'at arms length'.
Hivyo ninataka mara moja CAG afanye ukaguzi wa kazi za wasanii hao kwenye NSSF na TANAPA. Pia achunguze kama Gombe Advisors ( company limited by guarantee) ina maslahi yeyote ya kifedha katika kazi hizo za wasanii. Nataka pia Shirika la NSSF na TANAPA waweke wazi mchakato wa kazi zao na wasanii hawa kupitia LEKADUTIGITE Limited.
Zitto Kabwe
Mei 29, 2014
Dar Es Salaam.


MZUNGU AMLAZIMISHA MSICHANA KUFANYA MAPENZI NA MBWA JIJINI DAR




Mzungu huyo ambaye jina tunalihifadhi, alidaiwa kufanya tukio hilo la kinyama Mei 26, mwaka huu na inadaiwa Aneth alipomkatalia, alimtimua nyumbani hapo kwa kumtupia virago.
Chanzo makini kilidai kuwa, baada ya kutupiwa virago bila kupewa mshahara wake sambamba na kipigo, Aneth aliripoti tukio hilo katika Kituo Kidogo cha Polisi cha Tabata, Dar na muda mfupi polisi walifika nyumbani hapo lakini Mzungu huyo hakutoka ndani, akakataa kuzungumza chochote
Taarifa zilidai kuwa, baada ya polisi kukutana na kizingiti hicho, walimpigia simu kiongozi wao ambaye aliwaamuru warudi kituoni wajipange upya.
Akisimulia zaidi ishu hiyo, Aneth alisema polisi walipoondoka eneo hilo, umati uliochukizwa na kitendo hicho ulikusanyika nje ya nyumba ili kumdhibiti ‘mtasha’ huyo kwa lolote.
    Kuna jirani mmoja alipiga simu tena kituo cha polisi alipoona hali ya hewa imechafuka ndipo polisi wakafika kwa mara nyingine na difenda na kufanikiwa kuingia ndani kwa kutumia geti kubwa, walipofika walikuta milango imefungwa lakini ilisemekana aliruka ukuta na kutimkia kusikojulikana.
    Polisi waliniambia nimpigie simu ajisalimishe lakini nilipompigia alisema hayupo na kama tunamhitaji tukutane sehemu huku na yeye akiwa na polisi wake
kilisema chanzo.



Mmiliki wa nyumba hiyo anayeishi Kigamboni, Mr. Cris alipoulizwa kuhusiana na ishu hiyo, alikiri kupokea malalamiko na manyanyaso kutoka kwa Aneth.
Akisimulia zaidi maisha anayoishi na Mzungu huyo, Aneth alisema:
     Alikuwa akinitafutia sababu za kunitimua kwani hivi karibuni kwa bahati mbaya nilipoteza ufunguo wa ndani, akanipiga mateke na kunisababishia maumivu makali mwilini kiasi cha kushindwa kutembea.

    Lakini lililoniuma zaidi ni hili la kunilazimisha eti nifanye mapenzi na mbwa wake, amekuwa akifanya hivyo mara kwa mara mimi nikaona siyo sawa na nilipokataa ndipo yakanikuta hayo.
Aneth aliripoti matukio hayo katika Kituo Kidogo cha Polisi Tabata na kupewa fomu ya matibabu (PF-3) sambamba na kufunguliwa jalada la kesi namba TBT/RB/3132/2014/ SHAMBULIO na jalada la uchunguzi lenye namba TBT/IR/1829/2014/UCHUNGUZI.



Thursday, May 29, 2014

MTOTO WA MFALME WA SAUDIA RABIA AMENUNUA NDEGE YA KIFAHARI 'AIR BUS A380' KWA $500 MILIONI

Mtoto wa Mfalme wa Saudia Rabia ameonesha jeuri ya pesa pale aliponunua ndege ya kifahari aina ya AIR BUS A-380 kwa dola za kimarekani 500 Milioni. Ndege hiyo ya kifahari ina vyumba ambavyo ndani yake vina malu malu na kila aina ya Nakshi nakshi kama uonavyo hapo pichani:-



Monday, May 26, 2014

HAWA NDIO VIJANA WA PANYA ROAD NA MBWA MWITU WALIO KAMATWA

Hawa ndio viongozi wa panya road na mbwa mwitu ambao tayari
wameshakamatwa
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanya msako
wa nyumba kwa nyumba, mtaa na maeneo yaliyoathirika kwa
hofu ya vijana ambao ni vibaka maarufu kama Mbwa mwitu au
Panya Road.  Msako huu uliofanyika ndani ya masaa 24 hadi
alfajiri ya tarehe 26/5/2014 kwa lengo la kuwaondolea hofu na
uhalifu dhidi ya makundi ya vijana wadogo wasio na ajira ambao
uliibuka hivi karibuni.
Maeneo yaliyoathirika ni Kigogo, Magomeni, Tabata, maeneo
yote yanayozunguka mto Msimbazi, maeneo ya Mbagala nk.
Msako huu unaendelea kufanywa na askari wa vikosi maalum
ambao wamepewa kazi ya kuhakikisha kuwa vikundi hivyo
haviibuki tena na vinatokomezwaa kabisa kwa  kuwakamata wale
wote wanaojihusisha na vitendo vya kuvamia kwa mkundi
wananchi ambao hawana hatia

Kamishna kova ambaye amezungumza na wanahabari muda
mfupi uliopita
Kati ya watuhumiwa 149 waliokamatwa mmoja amegundulika
kuwa ni kiongozi aitwaye ATHUMANI SAIDI miaka 20, Mkazi wa
Kigogo na amekiri anaongoza kundi la watu zaidi ya 15 ambao
baadhi yao ni kati ya waliokamatwa.
Imegundulika pia kwamba vijana hawa wanatumia dawa za
kulevya aina ya bangi na wengine hujichoma sindano na
kuwafanya iwe rahisi kujihusisha na matukio ya uhalifu.  Vijana
hao hupenda kushiriki katika ngoma kama Mnanda, Mchiriku,
Kigodoro, Kanga moja nk. ambazo kwa kawaida huchezwa hadi
usiku wa manane.
Wakitoka katika ngoma hizo hujikusanya pamoja na kufanya
matukio ya uporaji kwa mtu wanayekutana naye, kufanya uvunjaji
katika majumba na wakati mwingine wana mtindo wa kugema
mafuta ya diesel au petrol katika matanki ya malori
yanayosafirisha mafuta.
Operesheni kali inafanyika katika maficho ya wahalifu hao
ikiwa ni pamoja na daraja la River side, Kigogo darajani, Manzese,
maeneo ya Tandale pamoja na maeneo mengine ya maficho mkoa
wa Kipolisi Temeke.
Tunawasiliana na Maafisa utamaduni wa Wilaya zote za Mkoa
wa D’Salaam kusimamisha utoaji wa vibali wa ngoma za usiku
ambazo hazina tija.  Pia Jeshi la Polisi linafuatilia na kuwavizia
vijana wanaopora  watu wanaotoka katika sherehe za usiku kama
vile Harusi na wanaotoka katika mikesha ya Ibada na sehemu
zozote zenye mikusanyiko.
Aidha Jeshi la Polisi wanapambana na vijana wanaowavizia
watu katika vituo vya mabasi pindi wanapotoka alfajiri kwenda
katika shughuli zao za kila siku.
Zipo taarifa kwamba baadhi ya wazazi wasio waaminifu
wamewasafirisha watoto wao wahalifu katika makundi haya
kwenda mikoani ili kukwepa wasinaswe na msako huu mkali.
Hata hivyo Jeshi la Polisi lina mtandao wa kutosha kati yake na
mikoa mingine na nchi jirani hivyo litawatafuta popote walipo na
kuwakamata.
Oparesheni hii ni endelevu na ya kudumu hadi kero hii ya
vibaka itakavyokwisha kabisa. Baadhi ya majina waliokamatwa ni
kama ifuatavyo:-
1. DANIEL PETER @ MALUNDE, miaka 25, mkazi wa Yombo
Kigunga
2.    MWISHEHE ADAM, miaka 35, mkazi wa Mtoni mashine ya
maji
3. MOHAMED SAID, miaka 32, mkazi wa Mtoni
4.    JAKAMA ALPHONCE, miaka 23, mkazi wa Mtoni Kilakala
5.    HAMADI MDUDU, miaka 25, mkazi wa Mbagala
6.    SALUM MUSA, miaka 25, mkazi wa Kiwalani
7.    ANTHONY DANIEL, miaka 20, mkazi wa Mashine ya maji
8.    FIDELIN ANTHONY, miaka 18, mkazi wa Kigogo
9. HAMZA MAZUMA, miaka 19, mkazi wa Kigogo
10.           MGANGA ABEID, miaka 20, mkazi wa Kigogo
11. SAID ABEID, miaka 19, mkazi wa Kigogo
12.           SALUM NYENJE, miaka 36, mkazi wa Chamazi
13.           DOMINICK PETER miaka 22, Mkazi wa Kigogo
14.           KULWA ABEID, miaka 20, mkazi wa Mabibo
15.           MUSA IBTRAHIM, Miaka 20, mkazi wa Magomeni
16.           HUSSEIN SHABAN, miaka 22, Mkazi wa Magomeni
S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM


VIONGOZI WA MBWA MWITU NA PANYA ROAD WATIWA MBARONI.

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limefanikiwa
kuwakamata viongozi sita wa makundi ya uhalifu maarufu kwa
majina ya Mbwa Mwitu na Panya Road.Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi wa kanda
hiyo, Suleiman Kova, aliwataja viongozi hao kuwa ni Athumani Said
(20), Joseph Ponela, Clement Petter (25) na Romans Vitus (18)
wakazi wa Kigogo.Wengine ni Mwinshehe Adamu (37) mkazi wa
Temeke na Daniel Petter (25) mkazi wa Yombo, huku kamanda
huyo akibainisha kwamba maeneo yenye vijana hao wahalifu ni
Kigogo,
Magomeni, Tabata, Manzese na Mbagala ambapo askari wa
kutosha wapo kwa lengo la kuwadhibiti. aliwaonya wanaoeneza
uzushi kwamba makundi hayo ya wahalifu yamevamia maeneo
hayo jambo alilodai kuwakosesha wananchi amani huku akisisitiza
kuwa si kweli.Alisema uchunguzi wa jeshi hilo umebaini kwamba
chanzo cha uvumi huo ni baada ya mauaji ya vibaka wawili
walihusishwa na makundi hayo yaliyotokea Mei 18 na Mei 20
mwaka huu eneo la Kigogo Sambusa.
CHANZO:FREEMEDIA


Sunday, May 25, 2014

MAXIMO KUJA KUINOA YANGA?

Kuna habari za kurejea tena kwenye soka la Bongo kwa aliyekuwa
kocha wa timu ya Taifa Mbrazil Marcio Maximo lakini safari hii sio
kuinoa Taifa Stars, ni watoto wa Jangwani timu ya Dar es salaam
Young Africans maarufa kama Yanga.
Maximo ni kocha ambaye atakumbukwa kwa mambo mengi kwenye
soka la Bongo na machache kati ya hayo, ni namna alivyokuwa na
msimamo kwa wachezaji waliokuwa na utovu wa nidhamu,
kuhamasisha watanzania kuipenda timu yao ya taifa na kubwa
kuliko yote, ni kuipeleka Taifa Stars kwenye michuano ya kombe la
Afrika kwa wachezaji wa ndani maarufu kama CHAN.
Baada ya mkataba wa aliyekuwa kocha wa timu ya Yanga Hans Ven
Der Pluijm kumalizika mwishoni mwa msimu uliomalizika hivi
majuzi, kumekuwa na habari za wanajangwani hao, kumsaka mtu
ambaye atakuja kuungana na kocha msaidizi wa timu hiyo Boniface
Mkwasa ili kuirejesha timu hiyo kwenye makali yake baada ya
msimu huu, kujikuta wakipoteza ubingwa wao mbele ya watoto wa
mjini timu ya Azam dakika za lala salama.
Kama Mbrazil huyo atafikia makubaliano na kuja kuinoa timu hiyo,
ni wazi kuwa atakuwa na faida kutokana na kuyafahamu vema
mazingira na utamaduni wa watanzania. Maximo anajua kiwango
cha wachezaji wa kibongo na umuhimu wa mechi kubwa kama
“Kariakoo Derby” ambayo huwakutanisha timu za Simba na Yanga.
Kwa siku za hivi karibuni, Yanga ni mahali ambapo makocha
wamekuwa hawakai muda mrefu kutokana pengine na sababu
mbalimbali kama vile, maslahi na kutofikia malengo ya timu.
Mashabiki wa timu hiyo kwa muda mfupi, wamemuona kocha
Mbelgiji Thom Saintfiet na waholanzi Ernie Brands na Hans Van Der
Pluijm ambaye amemaliza mkataba wake wa miezi sita.
Pamoja na kufanya mawasiliano na kocha Maximo, bado Yanga
wanaendelea kusaka kocha mwingine ambaye atakuja kuwaletea
mafanikio endapo makubaliano na Mbrazil huyo hayatofikiwa.Huu
ni muda ambao mashabiki wa Jangwani wana hamu ya kujua
mwalimu wao mpya kuelekea kuanza kwa ligi kuu ambayo
inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu.
CHANZO: TANZANIA SPORTS


Wednesday, May 21, 2014

MAMA AMFUNGIA MTOTO KWENYE BOX MIAKA MINNE

Mtoto huyu ana miaka minne alikuwa amefungiwa ndani tangu akiwa na miezi mitatu na  mama yake mdogo, mama yake mzazi alifariki Kwa kipindi chote hicho alikuwa anamfungia kwenye box anamtupia chakula humohumo Mara ya mwisho kumuogesha ilikuwa mwaka jana mwezi wa tisa
Alikuwa anajinyea na kujikojolea hiyo rangi nyeusi ni taka hajawahi kukatwa kucha wala nywele.
Amepata ulemavu wa mikono na miguu Kwa sababu ya kukaa kwenye box. Inadaiwa mama wa Mtoto huyo alikufa Kwa ugonjwa unao ambukiza ndio maana huyo mama yake mdogo alikuwa anaogopa kuambukizwa.
Hajawahi kupewa chanjo yoyote tangu azaliwe




Tuesday, May 20, 2014

BALOZI AFA AKIWA NA KIMADA

Balozi wa Togo nchini Nigeria amefariki akiwa na kimada. Balozi huyo inasemekana walikuwa wametoka klabu ya usiku na binti huyo na bahati mbaya ndio wakadumbukia baharini na mauti yakawafika.
Wapasha habari wanasema walikuta wawili hao wakiwa wamesema ndani ya maji






MUUGUZI MWENYE HIV AFUNGWA JELA UGANDA

Nchini Uganda mahakama imempata na hatia muuguzi mwenye HIV,
aliyeshitakiwa kwa kumdunga mtoto mchanga sindano, ambayo
awali ilimchoma yeye mwenyewe.
Muunguzi huyo, Rosemary Namubiru, mwenye umri wa miaka 64,
mwathiriwa wa virusi vya HIV, amefungwa miaka mitatu jela, kwa
kile hakimu amekiita, 'uzembe wa weledi'.
Hukumu hio imetolewa wiki moja baada ya bunge la Uganda
kupitisha muswada, unaomtia hatiani mtu yeyote ambaye kusudi
anamuambukiza mtu mwengine virusi vya ukimwi.
Mtoto huyo hata hivyo hakuambukizwa virusi vya HIV na
wanaharakati wamekosoa mahakama kwa kumfunga jela
mwanamke huyo.
Babake mtoto huyo hata hivyo alielezea kufurahishwa na uamuzi wa
mahakama.
Baba huyo, Daniel Mushabe, amesema kuwa anatumai kesi hiyo
itampa motisha Rais Museveni kuidhinisha mswada uliopitishwa na
wabunge wa kuwachukulia hatua za kisheria watu
wanaowaambukiza wengine HIV kusudi.
Adhabu ya kosa hilo ni faini ya dola 1,900 au miaka kumi jela.
Sheria hiyo ikiwa itapitishwa itawaadhibu wanaotenda uhalifu huo
kwa maksudi.
Wananchi bila shaka walionyesha kuudhiwa na kitendo cha muuguzi
huyo ingawa wanaharakati wamemtetea mama muuguzi.
Hakimu aliyetoa hukumu alisema kuwa Namubiru alikosa
kuonekana kama aiyesikitishwa na kosa lake.
Namubiru, muuguzi mwenye uzoefu wa kazi wa miaka 30, alisisitiza
kwamba hana hatia na kuwa mtoto huyo hakuambukizwa HIV.
Namubiru aliamua kumdunga sindano mtoto huyo kutafuta mshipa
lakini kapata ugumu na hivyo kujidunga mwenye kwa bahati mbaya
lakini amesisitiza kuwa hakuwa na nia yoyote ya kumuambukiza
mtoto huyo virusi vya HIV.
CHANZO: BBC SWAHILI


Wednesday, May 14, 2014

TV IMAAN NDANI YA STARTIMES DAR ES SALAAM LEO.

TV Imaan kituo cha televisheni chini ya Islamic Foundation,
Morogoro hii leo In Sha Allah kitaanza kurusha matangazo
yake kupitia Startimes kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Fuatilia kipindi ''Walioacha Alama Katika Historia ya
Tanzania,'' ambamo Mohamed Said atafanya mahojiano na
wale waliosukuma gurudumu la historia ya Tanzania.
Patakuwa na vipindi vingine vingi vya kuuelewa Uislam
kwa watazamaji wa kila rika vipindi ambavyo vinaelimisha,
kuburudisha, kutuliza akili ya mja na kumjengea uwezo
mkubwa wa kuijua dini yake kwa wepesi na kumjua Allah
Subhana wa Taala.


Monday, May 12, 2014

CHRISS BROWN AONGEZEWA MUDA WA KUKAA JELA

Brown alifungwa jela baada ya kumchapa aliyekuwa mpenzi wake
Rihana
Mwanamuziki wa Marekani Chris Brown atasalia jela kwa siku
nyingine 131 baada ya kukiri kukiuka amri ya mahakama kuhusu
kifungo cha nje alichokuwa amepewa na mahakama.
Muimbaji huyo wa muziki wa mtindo wa R&B alikiri mahakamani
mjini Los Angeles mnamo siku ya Ijumaa kuwa alitenda uhalifu mjini
Washington Oktoba mwaka jana.
Jaji alimuhukumu kifungo cha siku 365 jela ingawa alimpongeza
kwa kuhudumia siku 234 katika kituo cha kupata ushauri nasaha.
Brown amekuwa chini ya aungalizi wa mahakama tangu mwaka
2009 alipokiri kumpiga mwanamuziki mwenza na ambaye alikuwa
mpenzi wake wakati huo,Rihanna.
Mshindi huyo wa tuzo la Grammy amekuwa kizuizini tangu mwezi
Machi alipokamatwa kwa kukiuka amri ya mahakama iliyomweka
ndani ya kituo cha ushauri nasaha pamoja na jela.
Kifungo alichopata kuongezewa siku kinahusiana na kisa cha
ugomvi kilichotokea mjini DC mwaka jana.
Brown anakabiliwa na mashitaka ya kumchapa mwanamume
mmoja nje ya hoteli moja mjini Washington



Wednesday, May 7, 2014

Tuesday, May 6, 2014

MSIBA WA USTAADH ILUNGA WAINGIA KATIKA HISTORIA YA TANZANIA

Katikati ni Sheikh Ilunga na pembeni ni.Salum Ally Mkangwa na nyuma ni Mohamed Said picha ilipingwa CBE mwaka 1988.
Sheikh Ilunga Hassan Kapungu kaingia katika historia ya Dar es
Salaam katika kifo chake. Bahari ya watu walijazana Msikiti wa
Kichangani kuja kuswalia jeneza lake na kisha kulifata nyuma jeneza
hilo hadi Makaburi ya Mwinyimkuu, Magomeni Mapipa. Sheikh
Ilunga ni mgeni katika mji wa Dar es Salaam kwa maana ya kuwa
hakuzaliwa Dar es Salaam wala hakuwahi kuishi Dar es Salaam.
Alikuwa akija na kuondoka zamani akirejea kwao Tabora na baadae
baada ya kuhamia Mwanza, akija Dar es Salaam na kurejea
Mwanza. Iweje leo mji mzima wa Dar es Salaam usimame na utoke
kuja kumzika Sheikh Ilunga Hassan Kapungu? Hakika hili ni swali
linalotaka majibu ya kuridhisha. Jibu ni dogo na rahisi sana. Hivi
ndivyo Waislam wa Dar es Salaam wanavyofanya kila wanapofiwa
na kipenzi chao. Labda linaweza kuja swali jingine, ''kipenzi?''
Sheikh Ilunga kawaje kuwa kipenzi cha Waislam? Naam Sheikh
Ilunga Hassan Kapungu juu ya udogo wake wa umri alikuwa kipenzi
cha Waislam si Waislam wa Dar es Salaam peke yake. Sheikh Ilunga
Hassan Kapungu alikuwa kipenzi cha Waislam wa Tanzania nzima.
Kibla cha kila msikiti wa Waislam katika Tanzania kilikuwa
kinamkaribisha kama si kuwaidhi basi angalau asimame awasalimie
nduguze Waislam. Sheikh Ilinga Hassan Kapunga hakuwa katika lile
kundi la mesheikh ambao wao wenyewe kwa hofu tu kuna baadhi ya
misikiti wanaogopa si kuingia kuswali, bali hata kupita nje. Sheikh
Ilunga hakuwa katika lile kundi la masheikh wenyeji katika futari za
serikali ''misikiti ya wakubwa'' na shughuli zinazohusiana na mambo
kama hayo lakini wageni katika misikiti ya ndugu zao Waislam.
Kubwa Sheikh Ilunga hakukosa usingizi kwa kukosa kualikwa futari
Ikulu au kualikwa katika dhifa za serikali akapigwa picha na
waheshiwa na kutokea katika runinga na magazeti siku ya pili
ukurasa wa mbele. Sheikh Ilunga Hassan Kapungu
hakushughuliswa na hayo. Yeye alishughulishwa na kuliweka juu
jina la Allah Subhana Wataala. Hili ndilo lililokuwa likimshughulisha
mpaka siku Allah alipomfisha. Sheikh Ilunga kaweka historia katika
historia ya mazishi makubwa Dar es Salaam, historia inayokwenda
nyuma kiasi miaka takriban 100 ukianzia mazishi ya Sheikh
Mwinyikheri Akida sheikh aliyeasisi Msikiti wa Mwinyikheri Akida,
Kitumbini unakuja kwa Sheikh Idrissa bin Saad Khalifa wa Tariqa
Askariyya, kisha Sheikh Kaluta Amri Abeid, halafu Abdulwahid
Sykes, kisha Sheikh Kassim bin Juma, halafu Prof. Kighoma Ali
Malima unaishia kwa Mzee Kitwana Dau baba yake Dk. Ramadhani
Dau. Iweje Ilunga kijana mdogo mno aungane na majina ya watu
maarufu kama hawa na katika hao wote walikuwa katika umri
mkubwa ukimtoa Abdul Sykes? Kitu kimoja ndicho
kilichompandisha daraja Ilunga katika jamii ya Kiislam Tanzania.
Ilunga alikuwa mtumishi wa Waislam. Wakimtuma Ilunga kila kazi
na akiifanya kwa moyo mkunjufu, kuanzia kujenga madras na shule
kisha akawasomeshea na watoto wao hadi siku aliposimama
Ukumbi wa Diamond kuitahadharisha serikali kuwa kuna
''Mfumokrsisto'' nchini unaotawala na kudhulumu haki za Waislam.
Hii ilikuwa mwaka 2012. Nilikuwa mmojawapo wa Waislam
waliokuwa pale ukumbini kushuhudia kitendo kile cha kihistoria.
Kwa nini nakiita kitendo cha kihistoria kwa kuwa kwa takriban miaka
40 Waislam walikuwa wanasemea pembeni. Wakati ulikuwa umefika
Waislam wakasimama kuitahadharisha serikali kuhusu kujiachia dini
moja ikahodhi fursa zote za nchi kwa hila na Radio Imaan na TV
yake vilikuwapo na Radio Imaan ilirusha hafla ile na mubashara,
yaani ''live.'' Kote Radio Imaan ilikosikika Waislam walimsikia Sheikh
Ilunga akieleza nini Waislam walifanya katika Tanganyika wakati wa
kupigania uhuru kuuondoa dhulma na kuleta haki kwa kila
mwananchi. Hili lilikuwa jambo kubwa na zito kwa serikali yoyote ile
kuwa inashutumiwa kwa kulea udini ndani ya serikali. nchi nyingi
Afrika zimeangamia kwa ugonjwa huu. Vyombo vyote vya habari
ukitoa vile vya Kiislam viligoma kabisa kuitaarifu jamii kuhusu
kongamano hili la Waislam. Ikawa kama vile hapajapatapo kutokea
kitu chochote. Kuanzia siku ile Sheikh Ilunga alitembea nchi nzima
na kufanya mikutano ya hadhara kuitahadharisha kwanza serikali
kuhusu Mfumokristo na pili Waislam ili wajue nini kilikuwa
kinawatafuna.

Profesa Lipumba akisali nje baada ya kukosa sehemu ya kusali ndani ya msikiti
Mohamed Said anaelezea alivyomjua Ustaadh Ilunga
Nilimfahamu vipi Sheikh Ilunga Hassan Kapungu? Nilianza kuzisikia
sifa zake katika miaka ya 1980 kabla sijauona uso wake. Wkati ule
Sheikh Ilunga alikuwa kijana mdogo sana na mdogo kwangu kwa
miaka kadhaa. Wakati naingia kusoma Chuo Kikuu Cha Dar es
Salaam Ilunga alikuwa maarufu pale chuoni msikiti wa Muslim
Students Association of the University of Dar es Salaam (MSAUD)
kiasi unaweza ukadhani kuwa na yeye ni mwanafunzi. Ilikuwa Ilunga
na wenzake ndiyo walioleta ''documents'' za Mzee Bilali Rehani
Waikela MSAUD. Hizi ''documents'' zilikuwa zimefichwa Tabora kwa
karibu miaka 20. Katika ''documents hizi,'' kulikuwa na kisa kizima
cha kile kilichokuja kujulikana kama ''Mgogoro wa East African
Muslim Welfare Society (EAMWS),'' Ndani ya jalada lililofikishwa
MSAUD kulikuwa na ''minutes,'' za mikutano ya EAMWS, taarifa ya
Kamati ya Upatanishi iliyokuwa inajaribu kupatanisha kati ya kundi
la Adam Nasibu na wenzake waliokuwa wanaipiga vita EAMWS,
kulikuwa na ''cuttings'' ya magazeti ya ''Uhuru,'' ''Nationalists'' na
''Tanganyika Standard,'' magazeti makubwa ya zama zile yaliyokuwa
yakifuatilia kwa karibu sana mgogoro ule. Nyaraka hizi za Mzee Bilal
Rehani Waikela zilikuwa hazina kubwa. Kutokana na nyaraka hizi
ndipo ukweli wa nini na nani alikuwa nyuma ya kuvunjwa EAMWS na
kuundwa kwa BAKWATA. Lakini kubwa zaidi waliokabidhiwa
Nyaraka za Waikela walizileta zikiwa na maelezo ili maelezo yale
yaenda na kile kitakachosomwa ndani ya jalada. Ilunga alikuwa
kijana wa Mzee Waikela. Katika hali ya unyonge sana walikuwa
wakiendesha shule ya Nujum katika juhudi za Waislam kujitoa katika
dhulma ya elimu. Mzee Waikela alimsomesha vyema Ilunga kuhusu
fitna na chuki ya Nyerere kwa Uislam na Waislam na mbinu
zinazotumika kuudhalilisha Uislam. Bilali Rehani Waikela alikuwa
mmoja wa waasisi wa TANU Western Province mwaka wa 1955 na
ni yeye na wenzake ndiyo waliomleta Nyerere Nyerere na Bi. Titi
Mohamed kuja kuitia nguvu TANU Western Province. Mzee Waikela
vilevile alikuwa Katibu wa EAMWS Western Province. Mzee Waikela
alikuwa mfano na kigezo kikubwa kwa Ilunga katika maisha yake ya
kuwatumikia Waislam.
msikiti ulijaa hadi nje wakati wa Sala ya jeneza




Monday, May 5, 2014

MAELFU NA KIONGOZI WA SERIKALI WAMZIKA SHEIKH ILUNGA.

Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif akikaribishwa katika msikiti wa kichangani
Maelfu ya waumini wa dini ya kiislam akiwemo makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif wamehudhuria mazishi ya mwanaharakati na mpiganiaji haki wa kiislam Ustaadh Ilunga Hassan Kapungu.
Chini ni gari la Maalim Seif likiingia viwanja vya msikiti wa kichangani magomeni Dar es salaam

waumini wakizika mwili wa sheikh Ilunga Hassan Kapungu
Jeneza lililombeba sheikh Ilunga likiingizwa msikitini kwa ajili ya Sala ya mwisho


HUU NDIO MSHAHARA WA SENETA MIKE SONKO.



USTAADH ILUNGA HASSAN KAPUNGU AFARIKI DUNIA

Nchi ya Tanzania imezizima kwa huzuni baada ya mwanaharakati wa kiislam Ustaadh Ilunga Hassan Kapungu kuaga dunia jana kwenye saa tano usiku.

Mwili wa marehemu utaswaliwa leo Alasir katika msikiti wa kichangani magomeni. Mwili utazikwa kwenye makuburi ya Mwinyi mkuu

Inna lilayh wa inna ilayhi rajiuun.

Allahuma ghfirlahu warhamhu waskanahu filjannah




Saturday, May 3, 2014

WARIOBA NI "BWANA KERO" KWA SERIKALI TOKEA ZAMANI

Kama alivyoandikika Edson Kamukana katika makala yake moja
"ukiachilia mbali wasomi kadhaa walioamua kulamba matapishi
yao na kumtusi Jaji Warioba na wana-CCM wengi wanaotukana
bila kujua wanamtusi nani, katikati yake utaona wanaosalia si bure
wana jambo na sababu za kufanya hivyo, hawa bila shaka
wanalipa kisasi."
Mnamo tarehe Julai 17, 1997, Rais Mkapa alimteua Jaji Warioba
kuongoza Tume ya Rais (Warioba Commission) kuchunguza na
kubainisha mianya na vyanzo vikuu vya rushwa nchini. Baada ya
kufanya mapitio ya sheria, kanuni na taratibu ndani ya serikali na
kuonyesha mianya ya kukua na kuongezeka kwa rushwa nchini,
Tume ya Warioba ilichapisha ripoti yake (Ripoti ya Warioba) tarehe
7 December 1997.
Baadhi ya mambo ambayo Tume ya Warioba iliyakuta ni pamoja
na baadhi ya wafanyakazi wa umma kuchukua rushwa kama
sehemu ya kujazia mishahara yao (petty corruption) midogo.
Lakini pia Tume ya Warioba ilikuta kuwa kulikuwa na rushwa
nyingine (grand corruption) aka ufisadi iliyohusisha maafisa wa
ngazi za juu na baadhi ya wafanyakazi wa serikali walio na ulafi wa
kujilimbikizia mali.
Tume ya Warioba ilitoa mapendekezo ya hali ya juu yaliyogusa
wizara na idara zote za serikali. Ripoti ya Warioba iligusa mioyo ya
walalahoi na wengi waliotoa maoni ya kumtaka Rais Mkapa
awafikishe mahakamani wale wote waliohusishwa na ufisadi
kwenye Ripoti ya Warioba. Hata hivyo, ripotii hiyo iliwekwa
kabatini na kutiwa kofuli. Ripoti ya Warioba ni imekuwa adimu
sana kupatika ilivyokuwa kwa Hati ya Muungano.
Japokuwa ripoti hiyo iliwekwa kabatini, iliwagusa moja kwa moja
vigogo kadhaa hasa wa CCM na wengi wao au watoto, ndugu na
jamaa zao ndio wanaoshika madaraka leo. Kama mnakumbuka
baada ya ile ripoti, ndipo vyombo vya habari vilianza kuripoti
masuala ya rushwa, ikiwemo ile skendo ya IPTL iliyomfanya
Mwalimu Nyerere aseme kuwa "kama huu ndiyo ushirikiano wa
nchi za kusini, basi bora ukoloni urudi." Waliounga mkono au
kuipinga IPTL wanajulikana. Wengine mtakuwa mnawakumbuka
hata watawala wa miaka hiyo na wizara/idara walizokuwa
wanaziongoza.
Akihojiwa na gazeti la Raia Mwema Mei 13, 2008, Jaji Warioba
alisema kuwa "Baadhi yetu tumepiga kelele muda mrefu kuhusu
hali ya rushwa nchini mpaka ikafika mahali ikawa watu wanatoa
dhihaka tu. Kuna rafiki yangu mmoja, yeye alinipachika jina la
‘Bwana Kero’ kwa sababu ya taarifa ile ya Tume ya Kero ya
Rushwa. Alisema mimi nimegeuka kuwa kero kwa kuzungumzia
rushwa kila wakati." Bado anaendelelea kuwa "Bwana kero" kwa
kutetea Rasimu ya Katiba Mpya.
Kama alivyouliza Edson Kamukana, inawezekana kweli hao vigogo
au watoto wao, ndugu na jamaa zao walioguzwa moja kwa moja
na ile ripoti wakamsifu "Bwana Kero" wakati alishawaharibia
kitumbua chao? Hatuoni vigogo hao wanautumia mchakato
mzima wa Katiba mpya kama mwanya pekee was kumdhoofisha
"Bwana Kero" na kujaribu kuendelea kuficha madhambi yao
yaliyoyafichuliwa na "Bwana Kero" kwenye ile ripoti yake ya kero
za rushwa 1997?
Kwa wale ambao hawakuwahi kuisoma Ripoti ya "Bwana Kero"
itafuteni muisome halafu muone "kero" ambazo "Bwana Kero"
aliziodhoresha kwenye ripoti yake. Halafu muunganishe the dots
kwa kujiuliza ni kwa nini kigogo A na B au mtoto/ndugu/jamaa wa
Kigogo C "anakereka" sana mpaka kumtusi "Bwana Kero"? Mara
ya mwisho nilisoma muhtasari wa ripoti kwenye maktaba ya
HakiElimu. Ilikuwa imejaa vumbi kweli kweli. Inaitwa " The Report
of the Presidential Commission of Inquiry Against Corruption",
kwa kifupi "The Warioba Report".
CHANZO: JAMII FORUM


Thursday, May 1, 2014

MBUYU TWITE NAE KUJIUNGA NA AZAM?

Uongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha
wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa
taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank
Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni
mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi
kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi
kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na
kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu
zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel
Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa
TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya
kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji
hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa
muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa
ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa
mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi
wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia
Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa
kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa
kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo
linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa
mwongozo wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji
wa kimataifa kwa msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo
kuelekeza msimu huu kila timu inapasa kuwa na wachezaji watatu
wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga haujapata majibu juu ya
utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite
na uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya
kanuni zipi zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa
wachezaji wa kigeni na katika hali ya kushangaza Kavumbagu
akaonekana tayari ameshasaini kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia
alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai
2013, alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na
kilichobakia ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini
Domayo alisema hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba
wake ambaye ndie wakala wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda
wa mwaka mzima kabla ya jana kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua wapenzi, wanachama na washabiki wa
Young Africans lakini ukweli ni kuwa wachezaji wenyewe walisindwa
kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku walikua na mipango
yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya uwezo wake lakini
wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea kuichezea Yanga
SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa msimu ujao pamoja na
ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la Ufundi
zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi kukaa
kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake,
wapenzi na washabiki wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa
wachezaji hao kwani Yanga bado ina nafasi wachezaji wengi wenye
vipaji na itaendelea kuboresha kikosi chake kwa kuzingatia
maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu ujao.
Kwa maelezo hayo hapo juu inaonesha Mbuyu twite hana nafasi tena maana azimio la Bagamoyo limetiliwa mkazo sana na TFF.
Na kuna habari kocha wa Azam ameuambia uongozi uhakikishe imemsajili 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU