Facebook Comments Box

Tuesday, January 29, 2013

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA




MAFURIKO YALETA BALAA MORO JIONI YA LEO


 Mvua kubwa iliyonyesha morogoro jioni ya leo imesababisha mafuriko katika mtaa wa morogoro.Mvua hiyo iliyoanza kunyesha kuanzia saa tisa alasiri imenyesha takribani kwa masaaa mawili imesababisha mafuriko katika barabara ya msamvu kuingia katikati ya mji hali iliyosababisha msongamano mkubwa wa magari.
 Maji yakiwa yamejaa eneo la mtawala baada ya mvua kubwa kunyesha jioni hii mkoani morogoro
 Mafuriko hayo yaliingia katika makazi ya watu na hapa ni mashine za kukoboa mpunga wakiwa wamesimamisha kazi zao baada ya maji kuingia ndani.





VILIO VYATAWALA BAADA YA LULU KUACHIWA LEO KWA DHAMANA


Lulu na mama yake mzazi wakilia baada ya kukutana nje ya Mahakama, Lulu amechiwa huru na Mahakama leo january 29 2013 mchana, pembeni ni mwigizaji Dr. Cheni ambae amekua karibu na familia ya Lulu kwa muda mrefu sana.

Ama kwa hakika nnje ya mahaka pamegeuka kilio mara muigizaji elizabeth michael kuachiwa kwa dhamana leo tarehe 29 lulu amepewa dhama kutokana na kesi inayomkabili ya kumuuwa bila kukusudia aliyekuwa star wa bongo movie marehemu steven kanumba.

Mara baada ya lulu kumuona mama yake wamejikuta wakiangua kilio hadi watu wakaribu wakawa wanashangaa.kazi ilikuwa kwa muigizaji dk cheni ambaye kiukweli katika watu wakupongezwa katika hili anachukuwa nafasi ya kwanza kwa binadamu ,cheni amekuwa mstari wa mbele kumsimamia lulu hadi amepata dhamana.
Lulu akiingia kwenye gari huku akisaidiwa na Dk cheni kwa nyuma yake
Mama yake lulu aliwahi kukaririwa akisema kwa sasa anamuona cheni ni zaidi ya binadamu wa kawaida kwani bila yeye hajui kama ataweza kumuokowa mwanae mama huyo amejikuta akilia kwa furaha baada ya kumuona tena mwanae huyo.

Dk chen amezungumza na thesuperstarstz na kutuambia anashukuru mungu kwakumpa moyo wa ujasiri wa kumsaidia binti huyo kwani wengi walimsusa lakini tukumbuke mungu ndiye mlipaji wa yote hatupaswi kumuhukumu mtu kwani hata mahakama bado haijamuhukumu lulu sasa sikuona sababu ya baadhi ya wasanii kujitenga na lulu na ndio maana nikajitolea kumsaidia hadi nijue mwisho wake.
Lulu akilia kwa furaha na kushindwa hata kuongea chochote alipokuwa anahojiwa jambo lililofanya cheni amuongelee
Cheni ambaye ni mmoja kati ya wadhamini waliotoa milioni 20 za kitanzania cheni amekuwa masaada mkubwa sana kwa lulu jambO ambalo limefanya lulu kumuona cheni ni zaidi ya baba yake kwa sasa na ndio maana mara nyingi hata kabla ya tukio la lulu na kanumba kutokea  bado lulu alikuwa anamuita cheni baba japo  haikujulikana kwanini na cheni katika familia ya kina lulu anaheshimika sana na ndio maana haikuwa rahisi kwake kutojitolea kwa hilo.


WAZIRI MKUU AENDESHA KIKAO CHA KUTAFUTA SULUHU MTWARA




Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya siasa na viongozi wa Asasi mbalimbali kuhusu mgogoro wa gesi kwenye ukumbi wa VETA mjini Mtwara Januari 27, 2013

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda yupo Mkoani Mtwara akikutana na makundi ya wadau mbalimbali wa mkoa huo ili kusikia kutoka kwao mawazo, michango na dukuduku zao kuhusu mradi wa gesi asilia.

Imeripotiwa kuwa Waziri Mkuu angekutana na wanahabari baadaye leo saa 9 alasiri ili kutoa mjumuisho wa maongezi yake...
 Taarifa mpya zitawekwa hapa punde zitakazopatikana. Kwa sasa, tafadhali sikiliza rekodi ya kipindi cha Amka na PRIDE FM radio, kilichozungumzia muhtasari wa yaliyojiri katika kikao cha jana kati ya Waziri Mkuu na Wadau.

TAARIFA MPYA ZA ZIARA YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu alikuwa akutane na Waandishi leo saa tisa alasiri. Kutokana na kikao kirefu cha madiwani wa Manispaa ya Mtwara/Mikindani na Mtwara vijijini pamoja na kikao cha wafanyabiashara, majumuisho ya ziara ya Mtwara atayatolea ufafanuzi kesho.

Dondoo muhimu:
  • Kwa ufupi wajumbe wengi wamekataa bomba la gesi lisiende Dar
  • Wamemkataa Mkuu wa Mkoa na kumtaka Waziri Mkuu aondoke naye
  • Wajumbe (Madiwani ) kumpinga kwa kauli moja  Hawa Ghasia kwa kile kilichosemwa kutumia mamlaka  kutoa kauli za uongo kuhusu Mtwara Vijijini kuunga mkono suala la gesi iende Dar madiwani waMtwara vijijini. Wamesema hawakushirikishwa.
  • Mzozo wa viwanja baina ya Madiwani na Mkuu wa Wilaya
  • Waziri Mkuu ametumia mbinu ya kisiasa kuwashawishi Wadau kuwa bomba liende Dar
  • Wajumbe wameondoka kwa shingo upande kwa kukubali kutokubaliana na Waziri Mkuu
  • Kikao kinafanyika chini ya ulinzi Mkali wa FFU, JWTZ na UwT (Usalama wa Taifa)
  • Hawa Ghasia arudishwa Uwanja wa Ndege, JKNIA asije Mtwara kwani anaweza kuchafua hali ya hewa
  • Polisi wanadai Meya anataka kuwachonganisha na jamii/wananchi kutokana na kauli yake ya kusema wao ndio chanzo cha vurugu


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU