Facebook Comments Box

Tuesday, September 25, 2012

ZIMWI LA YANGA LAIKUTA COAST UNION. KOCHA WAO KIBARUA CHAOTA NYASI

Juma Mgunda akiokolewa na polisi kuondoka uwanjani kwa amani baada ya mechi ya Bandari
Baada ya kunusurika kupigwa na mashabiki katika mechi ya kirafiki dhidi Bandari ya Mombasa, na kuendelea kupewa presha kubwa na mashabiki wa timu yake ya Coastal Union hatimaye kocha wa klabu hiyo yenye maskani yake jijini Tanga Juma Mgunda ametangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo baada kuiongoza timu kwenye mechi zisizozidi nne kwenye ligi kuu ya Tanzania bara.

Mgunda ambaye alipewa kibarua cha kuifundisha Coastal Union kipindic ha kiangazi kilichopita amesema ameamua kujiuzulu kutokana na presha kubwa anayopewa mashabiki kiasi cha wengine kutishia usalama wake.

Mgunda ameiongoza Coastal katika mechi 3 za ligi, akishinda moja na wakitoa suluhu mechi mbili.



MCHUNGAJI MTIKILA ASHINDA KESI

Picture
Mchungaji Christopher Mtikila akifurahia ushindi baada ya kushinda kesi dhidi yake.
MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.

Akizungumza baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema, "Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu".

Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa kumtia nguvuni.

Picture
Mtikila amkimsikiliza Koplo wa Polisi mwenye RB Namba : KMR/RB/10482 yenye maelezo ya kutishia kuuwa kwa maneno na wizi wa viwanja iliyofunguliwa na bwana Gotta Ndungulu.
* "Hukumu dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila, iliyoahirishwa mara mbili kwa sababu ya hakimu kuwa na dharura, ilisomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu a Hakimu Mkazi Mfawidhi, Illivin Mugeta aliyeisikiliza kesi hiyo ya kutoa maneno ya uchochezi.

Mtikila alikuwa akikabiliwa na mashitaka ya kusambaza waraka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete, kwamba anataka kuuangamiza Ukristo.

Mshitakiwa Mtikila alifunga ushahidi kwa kuwa na mashahidi wawili wa utetezi, akihofia kupoteza fedha za Serikali kwa kuwaleta mashahidi wengi ambao hawana kitu tofauti na mashahidi wengine waliokuwa wamewasilisha ushahidi wao mahakamani hapo.

Mtikila, anadaiwa kwamba, Aprili, 2010 Dar es Salaam, alisambaza waraka aliokuwa akidai ni wa kuunusuru Ukristo wenye lengo la kuangamizwa na Jihad ya Rais Jakaya Kikwete na kwamba Wakristo wajitoe mhanga kukomesha ugaidi, “Kikwete anaangamiza Ukristo, amekuwa jasiri wa kuingiza Uislamu katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alidai Mtikila katika waraka wake huo.

Alidai waraka uliosambazwa alisaini akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunusuru Ukristo na walichapisha nakala 100,000, lakini aligoma kutaja mahali walipochapishia nakala hizo. Maelezo yote hayo yalitolewa mahakamani kama kielelezo na ofisa wa polisi, SSP, Ibeleze Mrema aliyemuhoji Mtikila Aprili 14, 2010."



HAKIMU KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA

 

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala Pamela Kalala (kushoto),akitoka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana,baada ya kusomewa shitaka la kuomba rushwa ya Shilingi milioni tatu. 
HAKIMU Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Pamela Kalala amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, kujibu mashitaka ya kuomba rushwa Sh milioni 3 na kupokea Sh 900,000.

Kalala alipandishwa kizimbani jana mbele ya Hakimu Aloyce Katemana na kusomewa mashitaka yanayomkabili. Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Allen Kasamala alidai kuwa mshitakiwa anakabiliwa na mashitaka matatu.

Kwa mujibu wa Kasamala katika tarehe tofauti Februari mwaka huu mshitakiwa akiwa katika Manispaa ya Ilala aliomba rushwa ya Sh milioni 3 kutoka kwa Josephine Wage. Wage ni mke wa mshitakiwa katika kesi namba 703 ya mwaka 2008, dhidi ya Aboubakar Hamis na wenzake, na alitaka kumshawishi ili atoe uamuzi wa kumpendelea mumewe katika kesi inayomkabili.

Katika mashitaka la pili, Kalala anatuhumiwa kupokea rushwa ya Sh 800,000 kutoka kwa Wage, ikiwa ni ushawishi wa kutoa uamuzi wa kumpendelea mume wake huyo.

Hata hivyo, Kasamala alidai kuwa katika mashitaka ya tatu, hakimu huyo anatuhumiwa kupokea rushwa ya Sh 100,000 kutoka kwa Wage Februari 6, ukiwa ni ushawishi wa kutoa uamuzi wa upendeleo.

Mshitakiwa alikana mashitaka yote na Kasamala kudai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na upande wa Jamhuri hauna pingamizi juu ya dhamana.

Katemana alisema ili mshitakiwa aweze kuwa nje kwa dhamana, anatakiwa asaini hati ya dhamana ya Sh milioni moja na mdhamini mmoja wa kuaminika atakayesaini hati ya dhamana ya kiasi hicho cha fedha.

Mshitakiwa alikidhi masharti ya dhamana na kuwa nje hadi Oktoba 23 kesi hiyo itakapotajwa.

Baada ya kutimiza mashati hayo, Kalala akifuatana na mtu anayedaiwa kuwa mumewe, walitoka mahakamani hapo kwa kupitia mlango wa nyuma kwa lengo la kukwepa wapigapicha waliokuwa wakisubiri picha yake. Hata hivyo, wapigapicha hao walimwona na kumkimbilia ili kumpiga picha, hata hivyo waliendelea kupata ugumu baada ya mumewe kumkumbatia huku akicheka kwa dharau na kuwataka wapige picha kadri wawezavyo.


WIZI WA VIFURUSHI VYA ABIRIA NA WATEJA JK NYERERE AIR PORT




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU