Facebook Comments Box

Monday, October 29, 2012

DR SLAA ACHEMKA TABORA

Habari ifuatayo imetumwa na Abunuwasi Alinacha (email: a...a...@gmail.com):
---

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Wilbroad Slaa majuzi, Ijumaa, kule Sikonge, Tabora amezua na kutunga jipya.

Amedai kuwa Julai 2, mwaka huu, 2012, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alisafiri kwenda Hong Kong kumwokoa mtoto wake wa kiume, Ridhiwani Kikwete ambaye anadaiwa kuwa alikuwa amekamatwa na mihadarati siku moja kabla, yaani Julai Mosi.

Huu ni uongo wa dhahiri kwa sababu ratiba ya Mhe. Rais Kikwete katika siku hizo anazozitaja Slaa iko wazi.

Julai Mosi, akitumia Ndege ya Rais, alisafiri kwenda Rwanda ambako alihudhuria Sherehe za Miaka 50 ya nchi hiyo na akalala mjini Kigali. Julai 2 alisafiri kwenda Bujumbura kuhudhuria Sherehe za Miaka 50 ya Burundi.  Alirejea Dar es Salaam Julai 3 na Julai 4 alikutana na ujumbe wa Kampuni ya IBM na Mjumbe Maalum kutoka Zimbabwe. Julai 5, alikwenda Dodoma ambako aliendesha Kikao cha Baraza la Mawaziri na kurejea Dar es Salaam siku hiyo hiyo. Sasa alikwenda Hong Kong lini? Ama alikuwa Burundi na Hong Kong siku hiyo hiyo? Slaa anadai pia kuwa alipowasili Hong Kong, Mheshimiwa Rais Kikwete alipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini China, Mheshimiwa Philip Marmo ambaye alimpeleka kwenye mkutano na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mheshimiwa Hu Jintao. Huu ni uongo mwingine wa dhahiri na ambayo sijui unamsaidia nini Slaa. Slaa anasema uongo kuhusu Balozi Marmo kwa sababu ratiba ya Mheshimiwa Marmo kwa siku sita za mwezi Julai nayo iko wazi na siyo kificho.

Kwanza, Ubalozi wa Tanzania katika China hauko Hong Kong bali uko mjini Beijing na Mheshimiwa Marmo hajawahi hata kufika Hong Kong. Taarifa kutoka Hong Kong amekuwa anazipata kutoka kwa Balozi Mdogo wa heshima wa Tanzania Mheshimiwa Clement Chan. Hata juzi, Ijumaa, Oktoba 26, Balozi Marmo alikutana na Bwana Clement Chan. Balozi Marmo anapanga kutembelea Hong Kong kwa mara ya kwanza mwishoni mwa mwezi ujao, Novemba, 2012. Angalia ratiba ya Mheshimiwa Marmo katika wiki ya kwanza ya mwezi Julai mwaka huu:

Julai Mosi, Balozi Mamro alikuwa ofisini Beijing. Julai 2, Balozi alihudhuria Sherehe za Siku ya Mongolia mchana na usiku alihudhuria Sherehe za Siku ya Djibouti kwenye Hoteli ya Lengedane mjini Beijing. Siku nzima ya Julai 3 alishiriki katika warsha ya Kampuni ya China Chemicals Techonologies Group ambayo inataka  kufungua viwanda cha madawa na mbolea nchini Tanzania. Asubuhi ya Julai 4, Balozi Marmo alikutana na ujumbe wa Kampuni ya Sichaun Honda Group inayowekeza katika miradi ya Mchuchuma na Liganga na jioni ya siku hiyo alikutana na ujumbe wa Kampuni ya Mawasiliano ya ZTE. Julai 5, Balozi  alihudhuria Sherehe za Siku ya Venezuala Day na Julai 6 alijiunga na Mabalozi wa Nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki katika mkutano wa Forum on Trade na Cooperation na jioni alihudhuria Sherehe za Rwanda Day. Sasa, Balozi Marmo alikwenda lini Hong Kong kumpokea Mheshimiwa Rais kama siyo uongo?

Katika siku zinazotajwa, Bwana Ridhiwan alikuwa Dar es salaam muda wote.  Kwa hakika, Ridhiwan hajapata kufika Hong Kong ama China katika maisha yake yote. Nchi pekee inayokaribia China ambayo amewahi kuitembelea ni Dubai kwa sababu hata India hajapata kufika. Ratiba hizi za Mhe. Rais na Mheshimiwa Marmo na ukweli kuwa Ridhiwan hajapata hata kufika China ama Hong Kong ni ushahidi usiopingika kuwa Mzee Slaa kwa mara nyingine ametunga, yeye amekuwa bingwa wa goofing. Huyu ni mtu anayezeeka vibaya. Tunaamini kuwa ameanza kuchanganyikiwa pengine kwa kuzidiwa na jukumu ya kulea mtoto-mjukuu na kumtunza mchumba Bi Josephine ambaye wanaishi kama vimanda kwa sababu huyo mama bado anayo ndoa halali. Pole sana Mzee Slaa kama Josephine na mwanae amekushinda



TFDA INAFAA KUSHITAKIWA

 
MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imewekwa matatani ikielezwa kuwa nayo inastahiki kuchukuliwa hatua kutokana na kuzembea katika ukaguzi wa dawa na hivyo kusababisha dawa bandia za kupunguza makali ya ukimwi (ARV’s) kusambazwa.

Sakata hilo linakuja wiki chache tangu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Hussein Mwinyi, kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Joseph Mgaya, na viongozi wengine kupisha uchunguzi wa tuhuma za kusambaza dawa hizo.

Wengine waliosimamishwa kazi ni mkuu wa kitengo cha udhibiti ubora na ofisa uthibiti ubora huku kiwanda cha dawa cha Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd (TPI) kikisitishiwa uzalishaji na usambazaji wa dawa zilizokwishatengenezwa.

Taarifa za ndani ya TFDA ambazo Tanzania Daima imedokezwa na mmoja wa maofisa wake ambaye aliomba kuhifadhiwa jina kwa vile si msemaji, zilisema kuwa mamlaka hiyo nayo ilizembea katika sakata zima la dawa bandia za ARV’s kusambazwa.

Kiwanda chochote kabla ya kuzalisha dawa au chakula ni lazima kipate kibali cha TFDA baada ya kukaguliwa na kukidhi viwango husika.

“Hata dawa ingekuwa inaingizwa kutoka nje ya nchi, vilevile TFDA inapaswa kukikagua kiwanda husika kuona kama kina ubora wa kutengeneza dawa na kukidhi viwango,” kilisema chanzo chetu.

Gazeti hili pia limefanikiwa kupata nakala ya waraka wa TFDA kuhusu hali ya viwanda vya dawa nchini, ambayo inabainisha kuwa Tanzania ina viwanda saba vya dawa vilivyosajiliwa katika mwaka 2011/2012.

Viwanda hivyo ni Shelys Pharmaceuticals Ltd, Zenufa Laboratories Ltd, Mansoor Daya Chemicals Ltd, Keko Pharmaceuticals (1997) Ltd, Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd, A.A. Pharmaceuticals Ltd na Tanzansino United Pharmaceuticals (T) Ltd.

Waraka huo unabainisha kuwa kiwanda cha Tanzansino United Pharmaceuticals (T) Ltd, ambacho serikali kupitia Jeshi la Kujenga Taifa ni mmbia mmojawapo kimesimamisha utengenezaji dawa tangu Agosti 2010 kutokana na mwekezaji wa nje kujiondoa.

“Ukaguzi uliofanywa na TFDA katika miaka ya fedha ya 2010/11 na 2011/12 umeonyesha kuwa hakuna kiwanda kilichokidhi viwango vya utengenezaji wa dawa,” alisema ripoti yao.

TFDA katika taarifa yake hiyo inakiri kuwa viwanda vya dawa hapa nchini katika kipindi cha miaka miwili iliyopita vimeshindwa kukidhi vigezo vya usajili wa dawa.

Kutokana na hali hiyo dawa za viwanda hivyo zimekuwa zikiruhusiwa na mamlaka hiyo kuwepo sokoni kwa kuzingatia utaratibu maalumu ambao hauzingatii vigezo vyote vya usajili wa dawa.

“Utaratibu huu ulikuwa wa muda mfupi uliokuwa na nia ya kutoa muda kwa kiwanda husika kurekebisha mapungufu ili dawa zao zisajiliwe. Baadhi ya dawa zinazotengenezwa na viwanda vya ndani ni za tiba za ugonjwa wa malaria na vijiua sumu,” iliongeza taarifa.

Pia inafafanua kuwa katika siku za karibuni, sampuli za matoleo (batches) kadhaa za dawa za viwanda hivyo zilizochukuliwa katika soko na kuchunguzwa zimeonekana kuwa na ubora duni na hivyo kuondolewa.

Ni katika mtiririko huo, mtoa habari wetu anasema TFDA haijawahi kutoa kibali kwa kiwanda cha TPI kuzalisha dawa za ARV’s kinachoonyesha kuwa kiwanda hicho kimekidhi vigezo tajwa.

Lakini katika hali inayoonyesha kutokuwepo umakini, TFDA ilizisajili dawa hizo za ARV’s kutoka TPI wakati katika ripoti yake wanakiri kuwa kiwanda hicho hakina sifa za kuzizalisha.

“Dawa inaweza kuwa moja lakini ikawa na matoleo tofauti, hivyo hata toleo hilo la dawa bandia zinazolalamikiwa halikuletwa TFDA kwa ukaguzi maana ingebainika haraka kabla ya kuingia sokoni,” kiliongeza chanzo hicho.

Ofisa huyo anashauri kuwa TFDA ilipaswa kuwa na mkaguzi wake ndani ya MSD ambaye angekuwa anasaidia kukagua na kuhakikisha dawa hizo hazizalishwi na kusambazwa.

“Hapa utaona kuwa haikuwa sahihi kumwajibisha mkurugenzi wa MSD pekee na kutuacha TFDA ambao hatukutimiza wajibu wetu. MSD hawana utaalamu wa kuchunguza dawa bandia hiyo ni kazi ya TFDA,” alisisitiza ofisa huyo.

Dawa hiyo bandia aina ya TT-VIR 30 toleo namba OC.01.85 iliyotengenezwa Machi 2011 na kuisha matumizi Februari 2013, nyaraka zake zilionyesha kiwanda cha TPI kiliwauzia MSD.

Waziri Mwinyi alieleza kuwa vidonge vilivyokutwa kwenye vifungashio vya dawa husika vilikuwa vimesajiliwa na TFDA.

Mkurugenzi Mkuu wa TFDA jana alipotafutwa kwa njia ya simu, alisema atatoa ufafanuzi wake leo akiwa ofisini.



Sunday, October 28, 2012

PICHA ZA UTENGENEZAJI WA COVER YA SINGLE YA DIAMONDS


Hizi ni picha alizoziweka mwimbaji Diamond kwenye website yake, picha za utengenezaji wa cover la single yake mpya ya ‘nataka kulewa’.

.

.

.

.

.

Mkali Raqey akiwa kwenye kazi yake kama kawaida.

.

.
Baada ya kazi ya kupiga hizo picha… Cover lenyewe liko tayari, ndio hili hapa chini.




Thursday, October 25, 2012

TIMU YA PRISON YA MBEYA YAPATA AJALI

Timu ya prison ya Mbeya imepata ajali eneo la Hare mkoani Tanga,wachezaji Issa Mwantika,Lugano Mwangama,Khalidi Fungabreki,Daudi Masungwe wamepoteza fahamu na kukimbizwa hospitali ya Tanga, Kiungo wa Prisons Diego Magai akiongea na blog hii kutoka eneo la tukio amesema chanzo cha ajali iyo ni baada gari aina ya COaSter kuacha njia na kupinduka baada kupigwa na mwanga mkali wa taa za gari walilokua wanapishana nalo usiku huu,hadi saa tano na dk hamsini usiku huu majeruhi walikuwa wakikimbizwa hospitali teule ya Muheza.

POLISI WADAIWA KUTOROSHA MTUHUMIWA

MKAZI mmoja wa Kijiji cha Kogaja kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara Bw. Hamisi Omenda (33) amedaiwa kumuua kikatili mke wake Bi. Levina Hamisi (27) kwa kumkatakata kwa panga na kisha kutoroka, huku Polisi wakidaiwa kushiriki katika utoro huo kwa kuandaa mazingira ya kutoroka. Polisi wa kituo cha Kogaja wanadaiwa kuhusika na utoro huo kwa kile kilichodaiwa kuwa hawakumkamata mtuhumiwa licha kufika kituoni hapo kuchukua PF3 baada ya kufanya kitendo hicho. Hata hivyo, taarifa kutoka Kituo cha Polisi Kogaja zimedai kuwa Mtuhumiwa alitoa maelezo kuwa mkewe alikatwakatwa mapanga na watu wasiofahamika hivyo aliomba PF3 kwa ajili ya kumpeleka marehemu katika Hospitali ya Tarime mjini Tarime. Utetezi huo unadaiwa kuwa ni njama ya Polisi kwa kuwa wanayo mahusiano wa kibiashara na mtuhumiwa huyo. Akizungumza na waandishi wa habari, Mtendaji wa Kijiji cha Kogaja, Bw. Lukas Ambonya alikiri Bw. Omenda kuhusika katika tukio hilo na kwamba wakiwa njiani kwenda hospitalini mke wake alifariki na yeye kutokomea kusikojulikana hivyo hakuwepo hata wakati wa maziko. Kitendo hicho kiliwakasirisha ndugu wa marehemu ambapo juzi wakati wa maziko walitishia kuvamia kituo cha Polisi na kutaka kuchoma baadhi ya nyumba za ndugu wa mtuhumiwa kijijini hapo. Alisema chanzo cha mauaji hayo ni marehemu kutofautiana na Mumewe siku ya Jumamosi asubuhi, tarehe 20 Oktoba, 2012, (tofauti ambayo haijawekwa bayana), na marehemu baada ya kuhisi hali ya hatari alikimbia kutoka nyumbani hapo. Hata hivyo mume wake Bw. Omenda aliwatuma baadhi ya vijana kwa pikipiki waolifanikiwa kumkamata na kumrudidha nyumbani ambapo majira ya saa 4 asubuhi siku hiyo alimfungia ndani na kuanza kumkatakata kwa panga. “Sisi tunasema haya kwa sababu tunaishi kijijini hapa na Bwana huyu ana mahusiano makubwa na polisi hawa , ndio maana hawakutaka kumtia ndani badala yake walisaidia kuandaa njama za kutoroka kwake ..yeye alipeleka mke wake hospitalini akiwa marehemu” alisema mkazi mmoja ambaye hakutaka kutaja jina. Marehemu hajaacha watoto. Polisi inawashikilia baadhi ya ndugu wa mtuhumiwa kwa mahojiano zaidi.

WALIOGOMEA SHAHADA ZA ARDHI UNIVERSITY KUPEWA ZA UDSM


Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kitakuwa na mahafali ya 42 tarehe 27 Oktoba 2012 na Novemba 3, 3012.

 Jumla ya wahitimu 3,643 watatunukiwa shahada na stashahada wakati wahitimu 902 wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi (UCLAS) watatunukiwa shahada.

UCLAS kwa sasa ni sehemu ya UDSM.

Hayo yalisemwa na Makamu Mkuu wa wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala akitoa taarifa kwa umma kupitia waandishi wa habari.

“Tunapenda kuufahamisha umma pia kuwa, katika mahafali ya sasa wanafunzi wa UCLAS na wao watatunukiwa shahada kama wanafunzi wa UDSM, uamuzi huu umefuatia kumalizika kwa kesi Lello & Others Vs Ardhi University, University of Dar es Salaam and Attornry General, Misc.Civil Cause No. 69 of 2008, iliyofunguliwa na wanafunzi wa UCLAS wakipinga kupata shahada za UCLAS kwa madai kuwa udahili wao ulibaki wa UDSM, hivyo UDSM kinakubalina kwa dhati na uamuzi wa Mahakama Kuu,” alisema Prof Mukandala.

UDSM imekubali kuwatunuku shahada mbalimbali wahitimu hao 902 waliomaliza masomo yao UCLAS ambao awali waligoma kutunukiwa shahada zao na chuo hicho (UCLAS) katika Mahafali ya 42 kutokana na madai kuwa walipata udahili chini ya UDSM wakati UCLAS kilipopata hadhi ya kuwa chuo kikuu kinachojitegemea mwaka 2007 hivyo walistahili kutunukiwa shahada na chuo kilichowadahili. Wanafunzi hao ni wale waliohitimu masomo katika miaka ya 2007 hadi 2010.

Wanafunzi hao kwa kupinga suala hilo walifungua kesi mahakamani dhidi ya Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Sisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tumekubaliana kwa dhati na uamuzi huu wa mahakama na tumeamua kuwatunuku shahada wanafunzi hao kwa vile hakuna rufaa iliyokatwa dhidi ya uamuzi huo,” alisema Profesa Mukandala.

Kati ya watakaotunukiwa shahada mbalimbali, 28 watatunukiwa Shahada za Uzamivu, 671 Shahada ya Uzamili; 153 Stashahada za Uzamili na 2, 790 Shahada ya Kwanza.

Licha ya mahafali hayo, Profesa Mukandala alisema chuo hicho kitahitimisha maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa kwake kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwamo kufanya mkutano na wahitimu waliowahi kusoma chuoni hapo shughuli ambayo itafanyika Alhamisi.

Profesa Mukandala alisema wakati wa kuhitimisha sherehe hizo, shughuli zitakazofanyika ni kuweka jiwe la msingi la jengo la kituo cha wanafunzi, kuzindua Dira ya Chuo hicho (UDSM Vision 2061) na kutoa tuzo mbalimbali kwa watu na vikundi vilivyotoa mchango uliotukuka kwa chuo kikuu katika miaka 50 iliyopita.

Akizungumzia dira hiyo, alisema itakuwa ni ya nusu karne ijayo na malengo yake ni kufikia mwaka 2061 chuo kitakuwa katika nafasi za juu za viwango vya ubora vya kimataifa.



MAADHIMISHO YA MIAKA 67 YA UN

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Raphael Muhuga aliyemwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Tanzania katika sherehe za maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa tangu kuzaliwa kwake.
Mgeni rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta akiwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo katika Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa Tanzania kusheherekea miaka 67 tangu uanzishwe.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akimlaki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaa leo.
Pichani Juu na Chini ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou (katikati) akimtambulisha Mh. Samwel Sitta kwa baadhi ya Wakurugenzi wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa hapa nchini.
Waziri wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta akipokea heshima ya wimbo wa Taifa baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo kuhudhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa baada ya kutimiza miaka 67 ya UN tangu kuanzishwa.
Mh. Samuel Sitta akikagua gwaride maalum katika kilele cha wiki ya maadhimisho ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Afrika Mashariki akishuhudia upandishwaji wa bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni ishara ya kusheherekea miaka 67 ya Umoja huo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar leo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou, Mgeni rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meha Jenerali Raphael Muhuga wakiwa Meza kuu.
Pichani Juu na Chini ni viongozi wa Madhehebu ya Dini nchini wakiomba Dua kwa ajili ya kubariki sherehe za kutimiza miaka 67 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta akizungumza katika sherehe za kutimiza miaka 67 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa (UN) katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Sitta aliipongeza Umoja wa Mataifa kwa kuisaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali za maendeleo ili kutokomeza umaskini.Waziri Sitta alisisitiza kwamba bado Umoja wa Mataifa unakabiliwa na changamoto nchini kama vile amani na usalama, tatizo la njaa, mabadiliko ya tabia nchi na uwepo wa silaha za maangamizi.Mh. Sitta alifafanua katika kilele cha sherehe hizo umuhimu wa kupitia na kusaidia nchi zinazoendelea kufikia malengo ya millennia.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akitoa nasaha zake wakati wa maadhimisho ya umoja huo katika viwanja vya Karimjee alisema matatizo ya njaa, kupanda kwa bei za mafuta na mtikisiko wa uchumi duniani ni kati ya changamoto kubwa ambazo Umoja wa Mataifa inakabiliana navyo katika dunia ya leo. Dtk Kacou pia aliipongeza Tanzania katika juhudi zake za kupunguza vifo vya wakinamama wakati wa kujifungua na watoto ili waweze kufikia malengo ya millennia itakapofika 2015.Mratibu Mkazi wa UN alisema Tanzania imepunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi mapya ya ugonjwa wa Ukimwi.
Katibu wa UNA Tanzania Fancy Nkuhi akizungumza kwenye hafla hiyo alisema umoja wa mataifa imefanya kazi kubwa katika kuwaunganisha vijana wa bara la Afrika. Nkuhi alisema kupitia YUNA walitoa elimu ya afya ya uzazi na ugonjwa wa Ukimwi kwa vijana katika mikoa kumi hapa nchini Tanzania katika harakati ya kuelimisha vijana madhara ya ugonjwa huo na afya ya uzazi kwa vijana.
Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium Schools) ambao walikuwa kivutio wakati wa maadhimisho ya miaka 67 ya wiki ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania wakiwa katika gwaride maalum kupamba sherehe hiyo.
Meza kuu ikifurahia jambo wakati wa gwaride la watoto wa shule ya Heritage baada ya kuonyesha mbwembwe katika kupamba sherehe hiyo.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Azania wakitoa burudani ya Wimbo maalum wa kuipongeza UN kutimiza miaka 67 ya kuzaliwa.
Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium Schools) wakiimba wimbo maalum uliobeba ujumbe wa kuhimiza utunzaji wa amani miongoni mwa mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa.
Pichani Juu na Chini ni baadhi ya Mabalozi, Wakurugenzi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Wafanyakazi wa UN na wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo.
Pichani ni baadhi ya maafisa wa Jeshi waliohudhuria sherehe hizo.
Waziri Sitta akiwa ameambatana na Mwenyeji wake Mratibu Mkazi wa UN Tanzania Dkt. Alberic Kacou (kushoto) wakisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa Kitengo cha maafa UN Bw. Mdathiru Abubakar (wa pili kushoto) akielezea namna ya shirika la Umoja wa Mataifa linavyoshiriki pindi inapotokea maafa nchini. Kulia ni Judith Bihondwa wa UNICEF.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu (kulia) akifafanua utendaji wa kazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake 21 yanavyofanya kazi kwa ukaribu na Serikali ya Tanzania kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta (wa pili kushoto) aliyeambata na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou.
Mwenyekiti wa Shirikisho la vijana la Umoja wa Mataifa nchini (YUNA) Bw. Lwidiko Edward akisalimiana na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta kwenye banda la maonyesho la Umoja wa Mataifa katika viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Waziri Sitta katika banda la maonyesho la shirika linalohudumia wakimbizi nchini (UNHCR). Katikati ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou na kushoto ni Afisa Habari kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Stella Vuzo.
Afisa Itifaki na Uhusiano wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) Bw. Rodney Thadeus akimweleza Waziri Sitta jinsi ya kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) kinavyojipambanua kwa kupokea wageni mbalimbali wanaofanya mikutano katika kituo hicho na kutmia mwanya huo kutangaza Utalii na vivutio vya nchi.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dkt. Alberic Kacou katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye banda la maonyesho katika wiki ya Umoja wa Mataifa.


POLISI AGOMBEA UONGOZI UVCCM-NEC

WAKATI Mkutano Mkuu wa Nane wa Uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM) ukimalizika, mmoja wa wagombea wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho nafasi sita Tanzania Bara, Stanley Mdoe, ametiwa mbaroni na Polisi akibainika kuwa askari Polisi.

Askari huyo mwenye namba F 7961 wa cheo cha Konstebo, anatoka kituo cha Polisi Mvomero, Morogoro ambaye alibainika jana akijihusisha na siasa hata kuingia kinyang’anyiro cha kuwania ujumbe wa NEC kupitia Vijana.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana Morogoro, askari huyo alijitambulisha kwa baadhi ya wajumbe kuwa yeye ni mtoto wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, akijiita Stanley Bendera.

Wapambe waliofuatana naye kutoka Morogoro wakiwa Dodoma waliarifu kuwa mgombea huyo alikamatwa juzi jioni akiwa amevalia sare za chama hicho akiomba kura kwa wajumbe ili wamchague kwa nafasi hiyo.

Hata hivyo, ilielezwa na baadhi ya wanachama waliofuatana naye na wengine wanaotambua kazi yake uaskari, waliwajulisha maofisa usalama waliokuwa eneo hilo nao kufikisha taarifa hizo Polisi na kukamatwa.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, askari huyo alikuwa ameomba likizo isiyo na malipo, wakati wengine wakidai kuwa ameacha kazi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile akizungumzia tukio hilo alisema alipata taarifa ya kukamatwa kwa askari huyo Dodoma na kwamba wakati huo alikuwa akimtafuta kwa siku mbili kwa ajili ya shughuli za kikazi bila mafanikio.

“Sina uhakika kama askari huyu amejiingiza katika siasa ... nimetuma askari wengine kwenda Dodoma kufanya uchunguzi wa suala hilo,” alisema Kamanda Shilogile na kuongeza:

“Iwapo itabainika kuwa kweli, atachukuliwa hatua stahiki na kinidhamu kulingana na taratibu za kijeshi. Hata hivyo siwezi kuzungumzia suala la ugombeaji wake, sijathibitisha ukweli wake, isipokuwa hakuwa kazini kwa siku mbili na ni utovu wa nidhamu kwa Jeshi letu kutoonekana eneo la kazi,” alisema Kamanda Shilogile.

Kwa mujibu wa Kamanda, sheria za nchi na Katiba kuna vifungu vinavyohusu majeshi ya ulinzi na usalama vikitamka kuzuia na kupiga marufuku mwanajeshi kujihusisha na siasa.

Alisema iwapo jambo hilo litabainika, litakuwa limefanyika kinyume na kanuni na taratibu za kazi ya uaskari. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Bendera, hakupatikana ofisini kwake wala kwa njia ya simu ya mkononi ili kufafanua kadhia hiyo.

Hata hivyo wasaidizi wake walidai kuwa yuko nje ya nchi kwa shughuli za kikazi.





KESI YA DECI: MCH MTARES AKIRI BOT WALIWAKATAZA KUPOKEA HELA

 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kusimamia na Kuendesha Upatu (DECI), Mchungaji Jackson Mtares amekiri kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) iliwakataza kupokea fedha kutoka kwa mwanachama yeyote wa taaasisi hiyo.

Mtares alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kuendesha shughuli za upatu bila kibali inayomkabili pamoja na wakurugenzi wenzake wanne.

Akihojiwa na Wakili wa Serikali Prosper Mwangamila, Mtares alidai katika barua ya majibu ya kuomba leseni ya kufanya shughuli za taasisi hiyo, BOT iliwatakaza kupokea fedha kutoka kwa mwanachama yeyote iwe kwa hiari au kwa lazima.

Hata hivyo alipoendelea kuhojiwa na kupewa barua hiyo ambayo imepokelewa mahakamani hapo kama kielelezo cha upande wa mashitaka, Mtares alidai kuwa Mkurugenzi mwenziye ambaye pia ni mshitakiwa ndiye atakayetoa maelezo zaidi.

Awali Mtares aliwasilisha kielelezo ambacho ni barua ya maombi waliyoandika kwa Gavana wa Benki Kuu (BOT) kuomba leseni ya kufanya shughuli za taasisi ambazo ni kusaidia watu wenye kipato cha chini kujikimu kimaisha.

Akiongozwa na Wakili wake wa utetezi Hudson Ndusyepo, Mtares alidai hakuhusika kupokea fedha wala kutoa risiti kwa wanachama na hata katika ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa mashitaka hakuna shahidi aliyedai yeye alipokea fedha.

Mtares aliendelea kudai kuwa,  Benki ya Afrika (BOA) ilikataa kuhifadhi fedha za taasisi hiyo hivyo walizihamishia katika akaunti ya kanisa lake la Jesus Christ  deliverance iliyopo katika Benki ya Wananchi Dar es salaam (DCB) ambayo ilikutwa na zaidi ya Sh bilioni 1.3 baada ya shughuli za Deci kusimama.

Alipoulizwa sababu za benki hiyo kukataa kuhifadhi fedha hizo alidai hajui bali walipewa taarifa kuwa wanatakiwa watoe fedha hizo haraka ndipo bodi ya wakurugenzi ilipoamua fedha hizo ziwekwe kwenye akaunti ya kanisa lake.

Aliendelea kudai kuwa wanachama walikuwa wanalipa kiingilio cha Sh 30,000 na baadaye wanaweka fedha na kupata uwezeshwaji (riba) ya asilimia 150 ya fedha ambayo mwanachama ameweka.

Alipobanwa kwa maswali na upande wa mashitaka, Mtares alidai fedha za riba  zilitokana na fedha walizokuwa wanaweka wanachama kwasababu Deci ilikuwa haijishughulishi na biashara yeyote zaidi ya kuwasaidia watu wenye kipato cha chini.

Hakimu Stewart Sanga aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 8 mwaka huu, wakatakapoendelea kusikiliza ushahidi wa upande wa utetezi.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Wachungaji wa makanisa tofauti ya Pentecoste ni, Dominic Kigendi, Samuel Mtares, Timotheo Ole Loitingye na  Arbogast Francis.

Wanadaiwa katika tarehe tofauti mwaka  2007 na  Machi 2009 katika Makao Makuu ya Deci, Mabibo Dar es Salaam walikusanya fedha kutoka kwa wananchi  wakiwaahidi kuwa watapata faida ya riba kubwa, katika mpango huo waliouita kupanda na kuvuna pia walifanya shughuli hiyo bila leseni.


KIBONZO CHA LEO

Picture

Thursday, October 18, 2012

Wanafunzi MUHAS wapinga kufukuzwa, waiomba Mahakama iingilie

ALIYEKUWA Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba cha Muhimbili (MUHAS), Gervas Shayo na mwenzake Charles Jackson, wameomba Mahakama Kuu Dar es Salaam, iingigilie kati sakata la kufukuzwa kwao. Shayo na wenzake walifukuzwa chuoni hapo Juni 21, mwaka jana kufuatia mgomo wa wanafunzi wa udaktari chuoni hapo, wakituhumiwa kuwa ndiyo walioandaa, kuratibu na kutekeleza mpango wa vitendo vya ukiukaji wa kisheria katika maeneo ya mlalamikiwa (Chuo). Hata hivyo, juzi Shayo na Jackson kupitia kwa Wakili Peter Kibatala wamefungua maombi mahakamani hapo, chini ya hati ya dharura, wakiomba kibali cha amri ya mahakama kufuta uamuzi wa chuo kuwafukuza masomo. Katika maelezo ya maombi yao waliyoyawasilisha mahakamani hapo, walalamikaji hao wamedai kuwa, uamuzi wa chuo hicho kuwafukuza haukuwa sahihi. “Hatukuridhishwa na uamuzi wa majibu, maombi na taratibu zilizotumika kufikia uamuzi huo.”, wanadai walalamikaji hao katika hati yao ya maelezo na kubainisha sababu nne za za kutokulidhika na uamuzi huo. Kwanza, wanadai kuwa wakati wa usikilizaji wa mashtaka yao chuoni hapo, walinyimwa haki ya kuwakilishwa na taasisi yao na sababu ya pili wanadai kuwa, walitiwa hatiani kwa kosa ambalo hawakuwa wameshtakiwa nalo. Katika sababu ya tatu, wanadai kuwa adhabu waliyopewa haikuwa halali na kwamba, ilikuwa ni kubwa zaidi kulinganisha na adhabu waliyopewa wenzao wengine ambao nao walitiwa hatiani kwa makosa hayo. Katika sababu ya nne, wanadai kuwa taratibu zilizotumika kuwaadhibu zilikuwa kinyume kabisa na kanuni za haki asili. Wakifafanua zaidi, wanadai kuwa Aprili 16, mwaka huu walipewa na mlalamikaji taarifa na maelezo ya mashtaka na kwamba, nao wakatoa maelezo yao ya utetezi. Wanaongeza kuwa Mei 8, mwaka huu wote walipewa taarifa ya kuhudhuria kikao cha nidhamu ili kusikiliza mashtka yao na kwamba, baada ya hapo Juni 21, mwaka huu walipewa uamuzi wa kufukuzwa masomo. Katika hati ya kiapo chao, walalamikaji hao wanadai kuwa kabla ya kuwafukuza, Desemba 15 walisimamishwa masomo kwa tuhuma za kupanga, kuratibu na kutekeleza vitendo hivyo vya uvunjaji sheria chuoni hapo. Walalamikaji hao wanatetewa na Kibatala, ambaye ni Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), katika utaratibu wa chama kutoa msaada wa kisheria kwa watu mbalimbali wanaohitaji msaada huo.

University of Dar es Salaam Student hangs himself to death

A first-year University of Dar es Salaam (UDSM) student has committed suicide by hanging himself with his shirt in a guest house in the city. Kinondoni Regional Police Commander Charles Kenyela told The Citizen yesterday that Joseph Lugemalila, 21, killed himself at Rombo Guest House in Manzese last Saturday, just six days after reporting at the university. He said Lugemalila, who hailed from Ukerewe District, Mwanza Region, had on Friday checked into the guest house, where he registered himself as Dickson John. Police found in the room an envelope containing a suicide note, medical documents, school certificates, identity cards and various other documents. According to Mr Kenyela, Lugemalila said in the suicide note dated October 12: “I have decided to end my life because of a number of difficulties. I won’t succeed even if I decide to continue with my studies.” One of the documents found in the room showed that Lugemalila underwent a medical examination at the UDSM Dispensary on October 7, and the next day he received results showing that he was HIV-positive. “It’s possible he killed himself because of shock and a sense of hopelessness after he was diagnosed with HIV… a preliminary investigation has established that he killed himself on Saturday night and the body was discovered the following morning,” Mr Kenyela said. UDSM spokesperson Jackson Isidory confirmed that Lugemalila was a student at the university, but declined to give details and referred this reporter to the police. The student’s father, Mr Pastory Lugemalila, who had travelled to Dar es Salaam to collect the body, said: “My son called me about a week before his death, and told me that he was fine and happy to get accommodation at the main campus. His sudden death has shocked me.” The body was flown to Mwanza yesterday for burial in Ukerewe tomorrow.

TBC YAPATA MABOSI WAPYA



 


Wednesday, October 17, 2012

KILICHOMUUWA KAMANDA BARLOW CHAHUSISHWA NA KISASI CHA MAPENZI

MWELEKEO wa upelelezi wa mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow umebadilika na sasa tukio hilo linahusishwa na kisasi cha mapenzi na tayari mtu mmoja anayedaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi Mwalimu Dorothy Moses kutiwa mbaroni na polisi.Awali, ilidaiwa kwamba Kamanda Barlow ambaye aliuawa kwa risasi usiku wa kuamkia Jumamosi muda mfupi baada ya kumfikisha mwalimu huyo nyumbani kwake, alivamiwa na majambazi. Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, DCI, Robert Manumba alithibitisha jana kukamatwa kwa mtu huyo (jina tulihifadhi) akisema: “Ni kweli mtu mmoja amekamatwa, lakini kwa sasa siwezi kuzungumzia kwa kina kuhusu suala hilo kwa sababu bado tunamhoji na tunaendelea na uchunguzi. Tutakapokamilisha, tutatoa taarifa.” Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Lily Matola pia alithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo. Hata hivyo, alisema amesikia habari hizo kwa kuwa yuko safarini kwenda mkoani Kilimanjaro kwenye mazishi ya kamanda huyo... “Hayo nimesikia, lakini kwa sasa sipo Mwanza hivyo siwezi kuzungumzia lolote.” Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi, zinaeleza kwamba upelelezi wa mauaji hayo umefanikiwa kwa hatua kubwa na kwamba mtu huyo alikamatwa Dar es Salaam baada ya kuwekewa mtego na makachero waliopo katika timu ya uchunguzi na alisafirishwa hadi Mwanza ambako anashikiliwa na jeshi hilo. Ilielezwa kuwa mtu huyo alikamatwa kutokana na kuwapo kwa taarifa za siri za kiitelejensia kutoka kwa watu mbalimbali. “Kuna hali imefunguka na imesaidia sana. Inaonyesha kwamba Dorothy alikuwa na uhusiano na mtu huyu ambaye alikuwa akifika nyumbani kwake, kama mumewe na watu wanajua jambo hili,” alieleza mmoja wa askari polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Alisema kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba uamuzi wa mwalimu huyo kusitisha uhusiano wa mapenzi na mtu huyo huenda ndicho chanzo cha mauaji hayo lengo likiwa ni kumshawishi Dorothy kurejesha uhusiano. “Mimi natambua kwamba huyu jamaa na Dorothy walikuwa na uhusiano na inajulikana mjini kuwa hata mke wa mtuhumiwa anatambua jambo hilo kwani walishagombana siku moja mjini na hata katika msiba nyumbani kwao na mtuhumiwa,” alisema mama mmoja (jina tunalo), aliyejitambulisha kama mmoja wa marafiki wa karibu wa Dorothy. Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Kitangiri (jina tunalo), anasema amekuwa akimfahamu mtuhumiwa aliyekamatwa kama baba mwenye nyumba hiyo na kila mara amekuwa akimkuta hapo nyumbani wakati wa kujisomea na wanafunzi wenzake. “Mimi ninamfahamu kama baba wa rafiki yangu na nimewahi kumkuta wakati wa kujisomea hapo nyumbani na watoto wa nyumba hiyo.” Dorothy ambaye ametajwa kuwa mjane, ni Mwalimu katika Shule ya Msingi Nyamagana na tangu kufariki kwa mumewe Ofisa wa zamani wa TRA, Modest Lyimo mwaka 1997. “Watu wote wanajua kwamba mtuhumiwa alikuwa akitembea na huyo mwalimu, wameonekana mara nyingi wakiwa muziki,” alieleza mmoja wa ndugu wa karibu wa mke wa mtuhumiwa. Hili ni tukio la tatu mkoani Mwanza kutokea kwa ofisa wa polisi kuuawa. Katika tukio la awali lililotokea mwaka 1987, askari aliyetambulika kwa jina la Inspekta Gamba aliuawa kwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi eneo la Nyakato na katika tukio la pili mwaka 1997, aliyekuwa Mkuu wa Kituo cha Kati ASP Mahende aliuawa kwa kupigwa risasi eneo la Bugando saa nne usiku alipokuwa akifuatilia majambazi waliokuwa wakijitayarisha kuvamia. Dar wamuaga Kamanda Barlow Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal aliongoza waombolezaji waliofika kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Barlow nyumbani kwake, Ukonga Dar es Salaam jana. Mwili wa Kamanda Barlow ambao unasafirishwa leo kwenda mkoani Kilimanjaro kwa mazishi, uliwasili nyumbani kwake saa 6.45 kabla ya kupelekwa katika Kanisa la Mtakatifu Agustino, Ukonga kwa ajili ya ibada na kutoa heshima za mwisho. Akitoa salamu za Serikali, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima alisema kifo cha Kamanda Barlow ni pengo kwa taifa... “Tutahakikisha watuhumiwa wanapatikana kwa mikono yote miwili na hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yao.” Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema alisema juhudi za kuwasaka watuhumiwa zinaendelea kwa ushirikianao wa wananchi. “Kifo cha Kamanda Barlow kimeacha pengo kwani hivi sasa askari mmoja analinda watu 1,300 hivyo kwa kifo chake unaweza kuona ni pengo la aina gani na ukilinganisha yeye alikuwa kamanda wa mkoa mzima,” alisema IGP Mwema. Alisema jeshi lake litaendelea kulinda amani ya wananchi na kifo cha Kamanda Barlow kinalifanya liongeze nguvu. Akitoa mahubiri, Padri Veri Urio alisema kila jambo hutokea kwa wakati na kifo cha Kamanda Barlow kimesababishwa na watu. Alisema mwenye mamlaka ya kuondoa uhai wa mtu ni Mungu pekee hivyo waliosababisha kifo chake siku ikifika, watajibu kwa nini walifanya hivyo. IGP Mstaafu, Omary Mahita alisema atamkumbuka Kamanda Barlow kwa uchapaji wake kazi tangu akiwa polisi Interpol (polisi kimataifa)alifanya kazi kwa weledi uliotukuka. “Daima nitamkumbuka kwani nimefanya naye kazi sehemu tofauti na askari waliobaki waige mfano wake wa uwajibikaji” alisema Mahita. Mbali ya Dk Bilal, viongozi wengine walioshiriki katika ibada hiyo jana ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), makamanda wa polisi, viongozi wa Serikali na vyama vya siasa na wananchi.

Saturday, October 13, 2012

MNYAMA AANZA KUSUASUA




DK: Mpira unamalizika hapa uwanja wa Mkwakwani kwa matokeo ya sare tasa.

DK 85: Simba  0 - 0 Coastal

DK 78: Atupele Green anakosa bao la wazi 

DK 75: Coastal wanafanya mabadiliko anaingia Danny lyanga anatoka Soud.

DK 68: Simba wanafanya mabadiliko anatoka Daniel Akuffoer anaingia Salim Kinje.

DK 65: Nsa Job anapewa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi ya pili ya njano.

DK 63: Nsa Job anapiga shuti kali linaokolewa kwa ustadi mkubwa na Juma Kaseja.

DK 60: Mwamuzi anawapa kadi za njano Nsa Job na Amir Maftah.

DK 55: Coastal wanakosa bao la wazi huku Simba wakifanya mabadiliko anatoka kinda Haruni Chanongo anaingia Uhuru Suleimani.

DK 47: Anaingia Lameck Dayton kuchukua nafasi ya Razack Khalfan aliyeumia.

DK 46: Kipindi cha pili kinaanza na ghafla Razack Khalfan anakaa chini akionekana kuwa na maumivu, machela zinambeba na kumtoa nje ya uwanja kwa jinsi inavyoonekana sidhani kama atarudi dimbani.

Mpira ni mapumziko hapa Mkwakwani Simba 0 - 0 Coastal.

DK 45: Coastal wanaendelea kuishika nafasi ya kiungo kwa sababu Selembe, Razack na Santo wanaelewana sana pia udhaifu wa Boban katika kukata unawapa wakati mgumu Kiemba na Kazimoto katika kuweza kumiliki dimba.

DK 40: Nsa Job anakosa bao la wazi bada ya kazi nzuri iliyofanywa na Selemani Kassim.

DK 35: Timu zote zinafanikiwa kufika kwenye lango la wapinzani lakini wanashindwa kuzitumia nafasi zao vizuri.

DK 30: Coastal 0 - Simba

DK 26: Simba wanapata kona yao ya kwanza lakini haizai matunda.

DK 25: Coastal wanaonekana kutawala sehemu ya kati ya kiungo inayochezwa na Jerry Santo na Razack Khalfan.

DK 20: Coastal 0 - 0 Simba

DK 15: Kichwa kizuri cha Felix Sunzu kinatoka nje.


DK 13: Haroun Chanongwa anapiga bonge la shuti linagonga mtambaa wa panya kipa wa Coastal Chove anashindwa kuzuia.


DK 10: Simba 0 - 0 Coastal


DK 9: Coastal wanafanya shambulizi la kushtukiza na mpira unatoka juu ya lango.


DK 1: Mpira unaanza hapa mkwakwani - Simba wamevaa jezi nyeupe na bukta nyekundu, Coastal wamevaa jezi nyekundu juu nyeupe chini.
endelea kufuatilia mtandao huuu tutakuletea picha zote za mchezo huu wa leo. 


PICHA YA JOE MAKINI YAVUJA

Picha ikimuonesha mwamba wa kaskazini a.k.a mweusi Joe makini akiwa na mrembo warda. picha hii imevuja. samahani lakini.....

KWA HERI KAMANDA LIBERATUS BALLOW

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza RPC Liberatus Ballow ameuwa usiku wa kuamkia leo na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi katika eneo la Kitangiri karibu na Hotel ya Tai Five majira ya kati ya saa saba hadi nane. Haya yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza Injinia Everest Ndikillo wakati akitoa taarifa za tukio la kuuawa kwa Kamanda Ballow. Tukio hilo ambalo limeacha simanzi kubwa kwa wakazi wa jiji la Mwanza pamoja na familia yake huku watu wa kijiuliza kuhusiana aliyehusika na mauuaji hayo ya kikatili. Taarifa ya Mkuu wa Mkoa zinasema kuwa Kamanda Ballow alikiuwa anatoka katika kikao cha harusi na ndugu yake aitwaye Sembeli Maleto kilichokuwa kinafanyika katika Hotel y a Florida na kish akumpelek amwanamke aitwaye Dorcas Moses Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Nyamagana maeneo ya barabara ya Kona ya Bwiru kwenda Kitangiri. Walipofika getini kwa Mama Dorcas mara waliwaona watu wawili wakiwa wamevaa makoti ya PolisiJamii, Mama Dorcas alimuuliza Kamanda Ballow kama anawafahamu Kamanda akasema kuwa hawa na watu wa ulinzi wa Jamii wako doria. Mara wale watu waliongezeka na kuwa sita wakaanza kama kuzozana wao kwa wao na ndipo Kamanda alipowauuliza kuna nini, Mmoja wao akajibu hakuna kitu na ikapelekea Kamanda kutaka kutoka nje ila wale watu watatu wakaizingira gari ya Kamanda Ballow aina ya Rav 4. Kamanda Ballow alipoona kama hali hewa inabadilika alichukua redio call ili aweze kuwa taarifu askari na ndipo wale jamaa walipompiga risasi kichwani nakupelekea kifo chake. Taratibu za mazishi ya Kijeshi bado zinaendelea na nyumbani kwa marehemu ambapo mwandishi wa blogu hii amefika na kukuta watu mbalimbali wakiwa katika hali ya majonzi sana. Mke wa Kamanda Ballow yuko Dar es Salaam na anatarajia kufika Mwanza. Mpaka sasa Polisi wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Dorcas kwa ajili ya Mahojiano huku uchunguzi mkali ukiendelea kuhusiana na kifo cha kamanda Liberetus Ballow.

Wednesday, October 10, 2012

NANI NI CCM-B? CHADEMA AU CUF?


Madhumuni ya Chama cha wananchi CUF kama yalivyo katika Katiba  yake ni, “Kuwaunganisha watanzania wakatae uonevu,kudhalilishwa,kunyanyaswa,kubaguliwa au maovu mengine yanayoweza kufanywa dhidi ya heshima ya utu wa binaadama, yawe yanayotendwa na Serikali, kikundi cha watu walio na uwezo kwa ajili ya mabavu yao au kwa ajili ya kujinufaisha kwao kiuchumi au kisiasa na kiitikadi au kwa kujali dini, kabila jinsia au rangi zao”. (Kifungu cha, 6[1] Katiba ya CUF uk.12)

Na, JUMA DUNI HAJI


Kwa kiasi miaka miwili sasa ndugu zetu wa CHADEMA wamekuwa wafanikiwa wakisambaza na kufanya siasa nyepesi nyepepi za maji taka kwa watanzania bara kwamba eti CUF ni “CCM-B” kwa sababu ya kuunda Serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar (Government of National Unity Zanzibar) Dhamiri yangu leo ni kufanya uchambuzi na kuweka wazi kwamba hoja ni “U-CCM-B” au choyo na Kuchukizwa kwa CHADEMA kwa wazanzibari kusikilizana? au ni ukosefu wa dira na agenda sahihi ya kisiasa? Hoja hii ya “U-CCM–B” imerejewa tena na viongozi wa CHADEMA pale Mheshimiwa. James Mbatia alipokubali uteuzi wa Rais Kikwete wa kumteua kuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Watanzania wanapaswa kufahamu kwamba kilichopo pale Zanzibar ni SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA SIYO VYAMA VYA UMOJA WA KITAIFA. Hakuna chama cha CUF wala CCM ambacho kimeungana na kufanya viwili hivyo kufanya umoja unaoitwa CCM-CUF Taifa au vinginevyo. Serikali ya umoja wa kitaifa ilipatikana baada ya kura ya maoni ya Tarehe 31 Julai, 2010 kupigwa na asilimia 66.3 ya wazanzibari bila kujali ni chama gani walikubali kuundwa Serikali hiyo ya GNU. Ni wananchi wa Zanzibar siyo wanachama wa vyama waliopiga kura ya maoni. Tunapokutana katika baraza la mawaziri hatukutani viongozi wa vyama , bali ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi (Siyo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi) wanaokutana na kujadili masuala ya maendeleo ya nchi yao na wala si maendeleo ya vyama vyao, wakati wowote chama cha Mapinduzi wanapokutana huwa wanazungumza masuala ya chama chao, na CUF huzungumza chama chao. Kwenye baraza la mawaziri tunazungumza nyaraka za  wizara za Serikali siyo za idara ya chama chochote kati ya hivyo viwili. Sasa huu “U-CCM-B au A” unatoka wapi.

Kama hoja ni chama kuingia Serikalini! Hebu tuone  “UCCM-B” upo wapi?

Madhumuni ya Chama cha wananchi CUF kama yalivyo katika Katiba  yake kifungu cha, 6[8] Katiba ya CUF uk.13) ni “kushika hatamu za dola ili dola au serikali itekeleze vizuri itikadi na sera za chama na ustawi wa Taifa letu” Chama cha siasa ambacho hakina malengo ya kuunda serikali na au kuingia serikalini kuweza kusimamia utekelezaji mzuri wa sera na itikadi na badala yake inajielekeza katika kazi ya kulipua “MABOMU” na kung’ang’ania kupiga kelele za ufisadi hali chama chenyewe na watendaji wake wakiamini kuwa ufisadi ni sehemu ya njia ya kupata manufaa ya kisiasa na kiuchumi, tunavishukuru vyombo vya habari kwa kutujulisha kuhusu hali hii. Hebu tujikumbushe tuone “UCCM-B” upo wapi? Mwaka 1991 Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi Rais wa CCM alimteua Mabere Marando (NCCR) kuwa mjumbe wa Tume ya kuratibu maoni ya wananchi juu kuanzishwa mfumo wa Chama kimoja au vyama vingi chini ya Mwenyekiti Jaji Nyalali, Mwaka 2001, Mabere Marando huyu huyu alichaguliwa na bunge  kuwa Mbunge wa Bunge la EAC akiwa NCCR na kumshida marehemu Bob Makani aliyesimamishwa na CHADEMA, CHADEMA wakarudia, lugha hii wanaowaambia wazanzibari kwamba NCCR Mageuzi ni CCM-B. Leo Mheshimiwa. Marando ni CHADEMA, U-CCM–B wake umeyayuka maana kaingia katika chama kitakatifu kinachopokea maono kutoka kwa Mungu?

Mwaka 2008 Mheshimiwa Rais  Jakaya Kikwete alimteua Zitto Kabwe kuwa mjumbe wa Kamati ya Madini chini ya Mzee Jaji Mark Bomani. Iliandikwa kuwa Mheshimiwa Mbowe amekatisha masomoni yake kutoka nchini ujerumani alikuja kwenye kikao kuthibitisha uteuzi huo, Si Zitto Kabwe wala  chama cha CHADEMA kilichojitangaza kuwa wao ni CCM-B ! , Mwaka huu Rais Kikwete amemteua Prof. Mwesiga Baregu kuwa mjumbe wa Kamati ya kuratibu maoni ya uandikwaji wa katiba ya Jamhuri ya Muungano. Viongozi wa CHADEMA Mr. Slaa na Tundu Lissu wakampongeza Rais na Prof. Baregu, lakini muasisi wa CHADEMA akasema uteuzi huo wa Mheshimiwa Kikwete una “UDINI” akimaanisha WAISLAMU WAMO KATIKA HUO UTEUZI WA KIKWETE!!! HATA hivyo CHADEMA haijawa CCM-B.

John Mnyika na Tundu Lissu walikua na kesi za uchaguzi dhidi ya CCM kule Singida na pale Ubungo. Kesi hizi wameshinda zote chini ya utetezi wa mwanasheria Mkuu wa Serikali ya CCM. Hawasemwi kwamba wametetewa na mwanasheria  wa serikali ya CCM na hivyo ni CCM-B!, April 17, 2012 umefanyika uchaguzi mwengine wa EAC pale bungeni na CHADEMA walikua na wabunge 43 kati ya 48 wa chama hicho wakati kura zikipigwa. Antony Komu mgombea wa CHADEMA alipata  kura 93, kura 50 kati ya hizo zilikua za  wabunge wa CCM. CHADEMA wakaenda mahakamani ili uchaguzi urudiwe ili wapate nafasi ya kuwapata wabunge zaidi kumchagua Komu. Hapa UCCM-B. haukuwepo? Tarehe 22/08/2012 Mahakama kuu kanda ya Tabora imetengua matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Igunga na kuwapa ushindi wa kesi hiyo CHADEMA. Uchaguzi utarudiwa. Jee CHADEMA wamesaidiwa na Jaji wa Serikali ya CCM na hivyo na wao ni CCM-B?  Mheshimiwa, James Mbatia alikua na kesi ya uchaguzi ya Jimbo la Kawe lakini akashindwa na Halima Mdee (CHADEMA). Mbatia akaenda Mahakamani kisheria. Viongozi wa CHADEMA wakatafuta njia za kiungwana kumaliza tatizo hilo nje ya Mahakama. Tarehe 6 Februari 2012 makatibu wakuu wa NCCR-Mageuzi Samwel Ruhuza na Wilbroad Slaa walikubaliana kufutwa kwa kesi hiyo No.101/2010 na kumuacha Halima Mdee abaki kuwa Mbunge. Jee Halima nae ni NCCR-B au Mbatia CHADEMA-B?

Mwaka 2001 Rais Mkapa alimteua Mh. Hamad Rashid kuwa Mbunge, wakati huo siasa za ushabiki na mapambano zilikua kubwa mno na CHADEMA kilikuwepo- hoja ya CCM-B hawakuisema. Mwaka 2009 Mheshimiwa Rais Kikwete alimteuwa Mheshimiwa, Ismail Jusa kuwa Mbunge Hoja za “UCCM-B” haikuwepo! Mwalimu Nyerere aliwahi kumpigia kura Paulo Ndorobo wa NCCR-Mageuzi jimbo la Musoma  na Mheshimiwa Ndorobo akashinda Nyerere alikuwa NCCR?

Kuna lugha ya kiswahili ya kuonewa bata kwa sababu ya umbo na sifa zake. Bata akitembea huambiwa anakata viuno kama mrembo wa Tanzania. Hivyo ndivyo alivyoumbwa, hakuchagua kukata viuno anapotembea na wala hajui kwamba anafanya hivyo. Bata huyu huyu anapotafuta chakula kwenye tope huambiwa anakula uchafu sina hakika kwamba CHADEMA wanapokubali uteuzi wa Rais huyu huyu ikawa ni sahihi chakula chao safi, lakini wengine wanapoteuliwa na Rais, kwa CHADEMA hua sawa na kula tope za choo. Kwa  CHADEMA  kuku anapokwenda haja kubwa hua anakunya, lakini bata huambiwa kahara, hakunya: wote wamekunya mmoja amekunya kutu ngumu mwengine kanya kutu laini, wote wamekunya mavi ya kuku na yote yananuka.Vipi CHADEMA wao wajione watakatifu wanapopata uteuzi kwa Rais wengine wawe wamekufuru, huu ni unafiki na uzandiki wa viongozi wanaotaka eti wapewe dhamana ya kuongoza nchi kwa akili kama za Panzi. Kule Kigoma CCM na CHADEMA walikubaliana na CCM kuunda Serikali ya Halmashauri ya Kigoma nusu kwa nusu ya madiwani kwa miaka mitano. Hoja ya CCM kuioa CHADEMA CCM-B haikutajwa, yaani yale kwa CHADEMA  yalikua na mavi ya kuku CUF na CCM Zanzibar ni uharo wa bata. Kule Arusha kulikua na Serikali ya aina hiyo, mpaka yalipotokea malumbano na upuuzi wa wawakilishi wa wananchi [madiwani] walipozuiliwa na chama chao CHADEMA kuwawakilisha barazani.

Wengi tumezoweshwa kwamba siasa ni uongo na mchezo mchafu, Hapana, Moja ya suala ambalo CUF na viongozi wake tunalisimamia na kutaka watanzania waamini kuwa Siasa si uongo wala si mchezo mchafu bali baadhi ya wafanya siasa[wanasiasa] ndio waongo na wachafu. Kama viongozi wanaweza kusema uongo wa kiwango cha uharo wa bata wakiwa nje ya Ikulu watakunya nini hawa wakiingia ikulu? Kama kuna viongozi wanaweza kuiba wake za watu na kuja jukwaani kujisifu kwamba wao ni wezi wa wake za watu, jee wakiwa ikulu watafanyaje hawa?, watawapanga foleni wanawake wote waliopo pale kwa uwezo wa  madaraka yao ya urais na kuwalazimisha kufanya nao ngono. Hivyo tunategemea hawa wakajenge nyumba ya umalaya pale ikulu, je nyie ndiyo munashangilia hayo? Eti kunja ngumi, ngumi gani ya wizi wa wake za watu? Eti kunja ngumi, ngumi ya kutengeneza vifo vya watanzania wenzetu? Watanzania muna kila sababu za kutafakari na kuchukua maamuzi sahihi juu ya hatma na mustakbali wa maisha yenu ya sasa na kizazi kijacho, wapi pa kuunganisha nguvu zenu ili mabadiliko ya kweli kiuchumi na kisiasa yaweze kupatikana. Siasa za milipuko na mihemuko za leo linasemwa hili na kesho linasemwa vinginevyo jambo hilohilo hazina nafasi kwa CUF ya DIRA YA MABADILIKO.

SUALA LA U-A na U-B unatoka wapi na unakujaje katika mahusiano ya chama kimoja na kingine wakati kilichojenga umoja ni ridhaa ya wazanzibari. Mwaka 2005 hadi 2010, wabunge wa Chama cha wananchi CUF kiliunda kambi ya upinzani na wabunge wa CHADEMA bungeni kwa miaka mitano, na Dk. Slaa akawa Naibu kiongozi wa kambi hiyo kwa muda wote wa miaka mitano. MheshimiwaZitto na wabunge wengine wa chama hiki wakishika nyadhifa za uwaziri kivuli wa Kambi hiyo. Ilikua ni Serikali kamili nje ya Serikali ya Muungano. Vyama viwili hivi viliendelea kubaki na shughuli zake ndani na nje ya Bunge. Mbona hoja ya CHADEMA kujiita CUF-B haikuja wala hawakujigamba hivyo kuwa wao ni CUF-B? Chama cha wananchi CUF kilifanya hivyo kwa sababu madhumuni yake ni: “Kuwaunganisha watanzania wakatae uonevu,kudhalilishwa,kunyanyaswa,kubaguliwa au maovu mengine yanayoweza kufanywa dhidi ya heshima ya utu wa binaadama, yawe yanayotendwa na Serikali, kikundi cha watu walio na uwezo kwa ajili ya mabavu yao au kwa ajili ya kujinufaish kwao kiuchumi au kisiasa na kiitikadi au kwa kujali dini, kabila jinsia su rangi zao”.

Muda wote huu vyama vya upinzani tumeshindwa kuungana na kukiondoa chama cha CCM kwa sababu ya udhaifu huu wa CHADEMA kujikubalisha kujigawa mafungu huku CCM ikichekelea na kutuona wajinga. Ujinga na upumbavu huu umezidi tulipogundua kwamba Viongozi wa CHADEMA wanaonesha udhaifu wao kwa kukosa furaha kuwaona wazanzibari wanasikilizana na nyinyi wananchi munafurahia hilo kwamba tuaachwe wazanzibari tuuwane na kwamba eti hicho ndiyo chama munachokitaka eti kiingie Ikulu. Msimamo huu wa CHADEMA ni kuthibitisha kwamba Wazanzibari kugombana ndiyo furaha ya viongozi wa Chama hicho, maana furaha na agenda ya muda mrefu ya baadhi ya viongozi watanganyika wawe wa CCM au CHADEMA ni kuhakikisha WAZANZIBARI tunawagawa ili tuwatawale (divide and rule them) Kama hivyo ndivyo wazanzibari hatuna sababu ya kushangaa ya jinsi viongozi wenzetu wa Tanganyika munavyotuona, maana sisi wazanzibari ambao wazee wetu akina mzee Karume na Mzee Thabit Kombo walimuamini mwalimu Nyerere kwa kuunganisha nchi mbili hizi kwa faida ya pande mbili, leo vijana wake waliorithi siasa zake wanaziendeleza kwa kutuambia eti Zanzibar siyo nchi. Wakati viongozi (Tundu Lissu) wanafurahia na kushikilia kwamba Zanzibar siyo nchi, chama hicho hicho kinashikilia hadharani kupitia kwa Joshua Nassari mbunge wa CHADEMA wa Arumeru Maashariki, anapendekeza na kusisitiza kuwa mikoa ya kaskazini ya Tanganyika kujitenga na kua taifa pekee. CUF hatuamini katika siasa za kikabila na kuigawa nchi mapande pande kwa siasa za itikadi za kimajimbo. Maana kama Arusha ijitenge na wasukuma wa Mwanza na Shinyanga ambao ni wengi na ni mikoa miwili tajiri kuliko mikoa yote nao  pia watajitenga na wale wa Mbeya watajitenga na wale kusini kwa wamakonde nao watajitenga. Kwa hivyo hata hiyo Tanganyika pia haitokuwepo. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema mara kadhaa kwamba Tanzania ipo kwa sababu ya Zanzibar. Msimamo wetu ni kuwa wazanzibari hawako tayari tena kufanywa koloni la Tanganyika. Kinachohitajika sasa ni kurekebisha makosa yaliyofanywa miaka 50 iliyopita yaliyoasisiwa na mwalimu Nyerere mwaka 1964.

Ninachotaka kuwakumbusha watanzania na Machadema, ni kwamba Mimi binafsi na wenzangu wengi ni wahanga wakubwa wa siasa mbovu za zamani za Zanzibar, tuliathirika sana kwa kubambikiwa kesi za uhaini na kesi za mauaji, leo ni waziri wa Serikali ya umoja wa kitaifa siyo umoja wa vyama vya CCM na CUF. Wazanzibar tumemaliza matatizo yetu ya ndani wenyewe, tumeamua kujenga nchi yetu, wakati nyinyi yenu munaitayarisha ibomoke, sisi huko tumeshatoka. Fursa ya kujenga siasa za kistaarabu, siasa za heshima, siasa zenye lengo la kuwasaidia watu wetu kuondokana na lindi la umasikini, maradhi na ujinga ipo, HATUJACHELEWA! Tuutumie vyema mchakato wa uratibu wa ukusanyaji maoni ya katiba, ipendekezwe uwepo wa UUNDWAJI WA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA, CUF katika manifesto yetu ya mwaka 2010 tuliieleza hili. CUF chini ya dira ya mabadiliko[vision for change] inaamini katika mazungumzo [dialogue],

Kwa hivyo CHADEMA angalieni siasa zenu kama mnataka kuendelea na siasa za kuonja umwagaji wa damu kisha ndo muamini juu ya ‘diablogue’ endeleeni kujaribu, kama munaamini kuwa njia siasa hizo mnazozitaka zisizo na ushirikiano na wenzenu, siasa za nchi isitawalike, siasa za maandamano, siasa za propaganda chafu, siasa za kubaka wake za watu, siasa za kutaja mafisadi wazuri na mafisadi wabaya, kama mnaamini kufanya hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo kutoka kwa Mungu. Namaliza kwa kuwaambia Zanzibar kuna Serikali ya umoja wa kitaifa , hakuna muungano wa vyama vya kitaifa, wala hakuna CCM-B wala CUF –G. Kilichopo ni Serikali siyo vyama kuunganisha nguvu kujenga taifa letu. Na ndugu zangu watanganyika hamtaweza katu kumaliza migogoro yenu ya kisiasa na kidini kama hamukuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Mungu Ibariki Tanzania!

Mungu Ibariki Zanzibar!

 

Muandishi wa makala hii ni waziri wa Afya wa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar na mjumbe wa baraza kuu la uongozi CUF Taifa. Harakati za kisiasa zilimuweka ndani bila kuhukumiwa miaka mine[4]




Tuesday, October 9, 2012

MAJAMBAZI YAKAMATWA KWA CCTV BAADA YA KUIBA KWENYE M-PESA




JANET JACKSON NDANI YA HIJJAB



Pop star Janet Jackson mwenye umri wa miaka 46 ambae ni mpenzi wa zamani wa producer Jermain Dupri anaolewa mwaka 2013 na tajiri bilionea wa kiarabu Wissam Al Mana na inaaminika kwamba Janet itabidi abadili dini na kuwa muislam

YANGA WALALA TENA MZUNGU WA NNE

HISTORIA ya wachezaji wa Yanga kulala mzungu wa nne imejirudia tena Bukoba, baada ya kulala kwa kubanana katika kitanda kimoja kama ilivyokuwa Mbeya, licha ya kufikia katika Hoteli ya Smart, yenye hadhi kubwa.

Hali kama hiyo ilijitokeza wakati timu hiyo ikijiandaa kucheza na Prisons, Mbeya, huku aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Tom Saintfiet akianika ukweli ambao baadaye ulimponza na kufukuzwa.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa wachezaji alisema, mambo ni yale yale kama ilivyokuwa Mbeya.

“Mambo kama ya Mbeya, hoteli ni nzuri, lakini wachezaji tumelala wawili wawili katika hoteli, pamoja na kupata huduma nzuri lakini tatizo lilikuwa ni hilo,” alisema mmoja wa wachezaji hao.

Hata hivyo wachezaji wanatarajiwa kurejea kwa usafiri wa basi, badala ya ndege maalumu ya kukodi ya Kampuni ya Precision Air, iliyotumika kwenda Kagera kwa ajili ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, dhidi ya Kagera, uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Habari zilizopatikana kutoka kwa kiongozi mmoja, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, zinasema wachezaji hao watarejea kwa usafiri huo baada ya mchezo wao dhidi ya Toto African, ambao utachezwa keshokutwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Wachezaji hao wanatarajiwa kuondoka mjini Mwanza Ijumaa, baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Toto African, kwa basi maalumu walilopewa na wadhamini wao, Kampuni ya Bia Tanzania TBL kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro.

Hata hivyo, gazeti hili liliweza kuongea na mkuu wa msafara, Mussa Katabaro, ambaye alisema anachojua yeye ni kwamba timu yao itarejea kwa ndege kama ilivyokuja.

Wakati huo huo, uongozi wa Kagera Sugar uliondoa mabango ya wadhamini wa Yanga, Kampuni ya Bia Tanzania, kutokana na kuwa wenyeji wa mchezo huo.

Kagera Sugar ambao ndio wenyeji wa uwanja huo kupitia kwa mratibu wake Mohamed Hussein, ilikataa katu katu mabango hayo kuwekwa katika uwanja huo, kwa kuwa wao ndio wa miliki wake.

MATUMLA NDANI YA MKASI NA SALAMA JABR





VURUGU ZA UVCCM MARA NDIO HIZI




UDA KULITEKA SOKO LA TANZANIA BAADA YA KUPATA MUWEKEZAJI

 
Picture
Viongozi wa Kampuni ya Simon Group na wengine Wakielekea kuzindua mabasi15 waliyowekeza UDA.
KAMPUNI ya Usafiri jijini Dar es Salaam (UDA) imejipanga kuteka soko la usafiri nchini ifikapo mwezi Machi mwaka 2013.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena alipokuwa akipokea mabasi 15 kutoka kampuni ya Tata Africa ya India ikiwa ni sehemu ya mabasi 30 yanayotarajiwa kuingizwa nchini ifikapo Desemba mwaka huu.

Kisena alisema kampuni ya Simon Group iliyowekeza katika shirika la UDA imejipanga kuwa kampuni kubwa barani Afrika kwa mtaji wa Dola25 milioni (sawa na Sh375 bilioni)  utakaowezesha kupatikana kwa mabasi 300 ifikapo mwezi Machi mwakani, “Simon Group imejipanga kuwa kampuni kubwa Afrika ifikapo Machi mwakani na tuna mpango wa kununua mabasi 300 kwa mtaji wa Dola25 milioni,” alisema Kisena.

Aliongeza kuwa kati ya mabasi hayo kutakuwa na mabasi ya wanawake, mabasi ya wanafunzi, mabasi ya binafsi, mabasi ya mikoani na mabasi yatakayosafiri barani Afrika, “Mazingira mabovu ya sasa ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam mara kwa mara yamekuwa yakisababisha udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake, bila shaka wengi wenu mtakumbuka vizuri kisa cha Maumba. Tunataka kukomesha udhalilishaji huo kwa wanawake ili wasafiri kwa uhuru na raha mstarehe,” alisema Kisena.

Kuhusu mabasi ya wanafunzi, alisema yatakuwa matano kila barabara kuu jijini Dar es Salaam na yatafanya kazi hiyo tu.

Kuhusu mabasi ya binafsi (Executive class), alisema yatakuwa na nauli ya juu lakini yatatoa huduma kama vile televisheni, vinywaji, magazeti na kiyoyozi, “Tunataka tuwahamasishe watu wasitumie tena magari yao binafsi. Unajua kwa mwezi mtu hutumia katiya Sh800,000 hadi Sh1milioni kununua mafuta ya gari, hela ambayo ni nyingi mno. Lakini kwa kutumia usafiri huu, inawezekana kubana matumizi,” alisema.

Akizungumzia mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) alisema kuwa wanatarajia kushinda zabuni ya kuuendesha kwa kuwa kampuni hiyo haina mshindani katika usafirishaji nchini, “Kwa sasa Dart inajengwa barabara ya Morogoro na barabara itakamilika mwaka 2014. Kwa sasa tutaendesha mradi huo kabla Dart haijaanza na kwa barabara nyingine baada ya hapo. Kwa kuwa sasa UDA haina mpinzani katika sekta ya usafirishaji nchini, naamini tutashinda zabuni ya kuendesha,” alisema. Aliongeza kuwa mradi huo unatarajia kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 1,500.
Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group,Robert Kisena (wa pili kulia) Wawekezaji wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA akipokea mfano wa funguo kutoka kwa Meneja wa Biashara wa TATA Afrika Holding Tanzania Ltd,Srinivas Nemalapuri (wa pili kushoto) kulia ni Mkurugenzi wa Simon Group, Leonard Rubuye na kushoto Kaimu Meneja Biashara,Sarvan Keshri. ikiwa ishara makabidhiano ya mabasi 15 katika awamu ya kwanza, hafla hiyo ilifanyika kwenye Ofisi za UDA Dar es Salaam.
Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Simon Group,Robert Kisena (wa nne kushoto) akiwaongoza viongozi wengine ndani ya Basi la UDA.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU