Facebook Comments Box

Monday, July 15, 2013

MAWAIDHA: UMUHIMU WA TAWBA - SHEIKH NURDIN KISHK




THIAGO ALCANTARA AITOSA MAN UNITED NA KUJIUNGA NA BAYERN MUNICH



Hatimaye kiungo wa kimataifa wa Spain na FC Barcelona Thiago Alcantara ameuzwa rasmi kwenda kujiunga na mabingwa wa ulaya na Ujerumani Bayern Munich.

Thiago ambaye alikuwa akihusishwa mno na kujiunga na Manchester United ingawa juzi kocha David Moyes alisema hawakuwahi kusema wanamhitaji mchezaji, amejiunga rasmi ya Bayern Munich kwa ada ya uhamisho wa 25 million euros.

Mapema wiki iliyopita kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola alikaririwa akisema kwamba anamhitaji Thiago kwenye timu yake na amewaomba viongozi wake kumsajili mchezaji huyo tu msimu huu.

Thiago amesaini mkataba wa miaka minne kuichezea Bayern Munich.


PICHA: HALI ILIVYOKUWA JANA KATIKA UPIGAJI KURA ARUSHA

 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.
 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.
 Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu. 
Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu. 
 Polisi wakiimarisha ulinzi katika lango kuu la kuingilia  kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu katika uchaguzi ulifanyika leo mjini Arusha. 
 Mkazi wa kata ya kimandolu akichomvya wino mara baada ya kukamilisha zoezi  la kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika jana katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata.
 Mkazi wa Kata ya Kimandolu akitumbukiza kura yake wakati wa uchaguzi wa madiwani uliofanyika mjini Arusha.
 Mkazi wa kimandolu,Juliana Mosha akitumbukiza kura yake katika sanduku la kura katika uchaguzi wa madiwani uliofanyika jana kuziba nafasi  ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo,zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
 Dina Naftal Mkazi wa kata ya kimandolu akitumbukiza kura yake katika sanduku la kura katika uchaguzi wa madiwani uliofanyika jana kuziba nafasi  ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo,zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata.
 Wakala wa chama cha siasa akihakiki kitambulisho cha mpiga kura kabla ya kuruhusiwa kupiga kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo ya Kimandolu,zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika jana katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika jana katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika jana katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata 
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika jana katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
Polisi akiwasogeza wananchi waliokuwa karibu na kituo cha kupigia kura cha Shule ya msingi Kimandolu ambapo walitakiwa kukaa umbali wa mita 200 na sio mia 100 kama ilivyozoeleka.(Picha zote na Ferdinand Shayo)


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU