Facebook Comments Box

Friday, July 11, 2014

DIAMOND PLATNUMZ APOKELEWA KWA SHANGWE NA BASHASHA AKITOKEA MAREKANI

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya hapa Tanzania maarufu kama Bongo Fleva Naseeb Abdulmalik a.k.a Diamond Platnumz aliwasili jana tarehe 10/07/2014 akitokea Marekani alikokwenda kwa ajili ya kushiriki katika tuzo za BET ambazo hufanyika kila mwaka.

Diamond alikua katika kategori ya Best African Act ambayo ilichukuliwa na Davido kutoka Nigeria na yeye kuishia kupata cheti cha ushiriki ambapo kwake sio vibaya maana anaamini huo ni mwanzo mzuri kwake wa kuelekea katika mafanikio.


Baada ya kuwasili Diamond aliwashukuru wote waliofika kumpokea na kusema kuwa safari yake ilikuwa nzuri na amejifunza mambo mengi sana pia amekutana na watu wengi na tutarajie mengi mazuri katika muziki wetu.

Na kwa upande mwingine alitoa shukran za dhati kabisa kwa watanzania kuipokea vema video yake mpya ya mdogomdogo, ambayo inafanya vema kwenye vituo vya luninga hapa nchini kwa sasa.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU