Facebook Comments Box

Wednesday, August 28, 2013

PICHA: MARAIS WA BURUNDI,UGANDA NA RWANDA WAHUDHURIA UFUNGUZI WA BANDARI YA MOMBASA


Marais wa Burundi, Uganda na Rwanda, wamehudhuria ufunguzi wa Bandari ya Mombasa, Kenya leo wakipokelewa wenyeji wao Rais Kenyatta na William Rutto!

Kenyatta anasema Mombasa ni 'Gateway of East African Business'. Anadai ni manifesto ya serikali yake kuifanya bandari hiyo kuwa 'busy and friendly port in all over East Africa coastline!'

Endelea kusoma zaidi => http://bit.ly/15gV9Aq







Marais wa Burundi, Uganda na Rwanda, wameudhuria ufunguzi wa bandari ya Mombasa, Kenya leo! Wapo pia na wenyeji wao President Kenyatta na Bwana Rutto!
Katika matangazo yao, wamesema bandari hiyo itaunganisha Africa kibiashara hasa ikichagizwa na Ujenzi wa barabara Namanga Arusha. Hii inaashiria nini kwa mustabali wa Uchumi wa Tz ambayo 60% ya makusanyo ya kodi yanategemea bandari ya Dsm



 
Museveni kahudhuria kwa kiti chake cha Uenyekiti wa EAC, ndivyo Kagame alivyomtambulisha. Pia Kagame anasema hiyo ndio faida ya Integrated East Africa Community, pia Miundombinu bora ya Bandari ya Mombasa, itaunganisha nchi zote za East Africa.




Kenyata anasema Mombasa ni Gate way of East African Business. Anasema ni manifesto ya serikali yake kuifanya bandari ya Mombasa kuwa busy and friendly port in all over East Africa coastline



 
Nini hatima ya bandari ya Dsm na siasa zake? Siasa za Kenya hizo wamezindua bandari mpya leo, na wanasema Sudan, Ethiopia na Somalia watatumia bandaria hiyo pia.








YANGA WATOKA SARE NA COASTAL UNION: MWAMUZI ALAUMIWA KWA KUSHINDWA KUMUDU MCHEZO


Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Coastal Union kutoka mkoani Tanga kufuatia bao la kusawazisha la penati ya utata dakika ya 90 ya mchezo la kiungo Jerry Santo baada ya Didier Kavumbagu kuifungia Yanga bao la kwanza.
Coastal Union ambayo katika mchezo wake wa awali dhidi ya JKT Oljoro ilipata  ushindi wa bao 2-0, ilicheza mchezo mbovu tangu mwanzo mwa mchezo hali iliyopelekea mwamuzi Martin Sanya ashindwe kulimudu pambano.
Yanga iliuanza mchezo kwa kasi kwa lengo la kusaka bao la mapema lakini kutokua makini kwa washambuliaji wake Jerson Tegete, Didier Kaumbagu na Simon Msuva kuliifanya ishindwe kupata bao kwa dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Haruna Moshi 'Boban'  na Said Nyosso walionyeshwa kadi za njano katika kipindi cha kwanza kufuatia kuwachezea ndivyo sivyo wachezaji wa Yanga, ambapo wachezaji hao wa Coastal walishindwa kuonyesha soka la uungwana.
Kipindi cha pili cha mchezo kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko kwa kuwaingiza Hussein Javu na Hamis Thabit waliochukua nafasi za Jerson Tegete na Salum Telela aliyeumia katika kipindi cha kwanza.
Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa timu ya Yanga kwani katika dakika ya 69 mshambuliaji Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao la kwanza akimalizia pasi safi ya mlinzi wa pembeni David Luhende aliyewazidi uwezo walinzi wa Coastal Union na kumpasia mfungaji.
Baada ya kupata bao hilo Yanga waliendelea kufanya mashambulizi kupitia kwa washambuliaji wake Hussein Javu na Didier Kavumbagu lakini walinzi wa waliendelea kucheza ndivyo sivyo kwa wachezaji wa Yanga kana kwamba wanacheza mchezo wa mateke na ngumi.
Katika hali iliyowastaabisha wengi mwamuzi alimpatia kadi nyekundu Saimon Msuva baada ya kuchezewa vibaya na mlinzi wa Coastal Abdi Banda, huku watu wakisubiria mwamuzi amuadhibu Banda alimpatia kadi Msuva na kiungo wa Coastal Crispin Odula.
Dakika ya 90 mwamuzi Martin Sanya aliipatia Coastal Union penati ya utata kufuatia kiungo Haruna Moshi 'Boban' kumdanganya mwamuzi kuwa mlinzi Nadir Haroub 'Cannavaro' ameunawa mpira ndani  ya eneo la hatari na penati hiyo ilipigwa na Jerry Santo na kuwapatia bao la kusawzisha.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika Young Africans 1 - 1 Coastal Union.
Mara baada ya mchezo kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amemtupia lawama mwamuzi wa mchezo Martin Sanya kwa kushindwa kuumudu mchezo na kusema katika mchezo wa  amekuwa mchezaji bora baada ya kushindwa kulimudu pambano.
Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro' 5.Mbuyu Twite, 6.Salum TelelaHamis Thabit , 7.Saimon Msuva, 8.Frank Domayo, 9.Didier Kavumbagu, 10.Jerson Tegete/Hussein Javu, 11.Haruna Niyonzima.
Coastal Union: 1.Shaban Hassan 'Kado', 2.Juma Hamada, 3.Abdi Banda, 4.Marcus Ndehele, 5.Juma Nyosso, 6.Jerry Santo, 7.Uhuru Seleman/Seleman Kassim, 8.Haruna Moshi 'Boban', 9.Lutimba Yayo/Kenneth Masumbuko, 10.Crispin Odula, 11.Danny Lyanga/Razack Khalfani


MSIMAMO WA LIGI KUU YA TANZANIA BAADA YA MECHI ZA LEO

Yanga 1 - 1 Coastal Union
Simba 1 - 0 JKT Oljoro
Mtibwa 1 -0 Kagera 0
Rhino Rangers 0 - 2 Azam FC
Mgambo 1 - 0 Ashanti United
 Mbeya City 2  - 1  Ruvu Shooting
JKT Ruvu 3 - 0 Prisons


PICHA YA LEO: WANAWAKE WANAWEZA

Mhandisi wa kike akikagua jengo kwa umakini na ufasaha



VIDEO: KAMA HUKUONA MAGOLI YA ARSENAL WALIVYO ITUNGUA FENERBACHE HAYA HAPA




104.5 RADIO IMAAN FM YARUDI HEWANI ILI KUKUTOA KWENYE GIZA NA KUKUPELEKA KWENYE MWANGA

Ustadh Ally Ajiraan akitoa maelezo baada ya RAdio Imaan kurudi hewani

Sheikh Hamza akiwa na Br Arif Nahdi studio baada ya radio Imaan kurudi hewani








 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU