Facebook Comments Box

Thursday, September 12, 2013

WAGENI WOTE WATAKAO INGIA ZANZIBAR KUPIMWA MALARIA

KITENGO cha kupambana na Malaria Zanzibar (ZMPC) kimesema kinatarajia kuanza kampeni ya kuchunguza malaria kwa wageni wote watakaoingia nchini kupitia uwanja wa ndege na bandari ya Malindi.

Ofisa mwandamizi wa kitengo wa ZMPC, Mwinyi Mselem akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mikakati ya kupambana na malaria nchini, alisema kitengo kimepanga kutekeleza mikakati hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha kwamba ugonjwa wa malaria unatokomezwa na hakuna njia za kuambukizwa kwa wananchi.

“Tunakusudia kuanzisha zoezi la kupima afya za wageni wote wanaoingia nchini kupitia njia za uwanja wa 
ndege pamoja na bandarini ili kujuwa afya za wageni wanaoingia nchini,” alisema.

Alisema mikakati ya kitengo cha kupambana na malaria ifikapo mwaka 2017 ni kuhakikisha ugonjwa huo umetokomezwa na siyo tishio tena kwa afya za wananchi. Kwa sasa Zanzibar imefanikiwa kushusha maambukizi ya ugonjwa huo kutoka asilimia 32 hadi kufikia asilimia moja na kupunguza vifo vya akinamama na watoto.

Hata hivyo, Mselem alisema katika kipindi cha miaka miwili sasa kumejitokeza maambukizi mapya ya malaria kutokana na kuongezeka kwa uchafuzi wa mazingira na hivyo kupelekea mbu kuzaliana zaidi.

Alisema kitengo cha kupambana na malaria kinatarajia kuanza kazi ya kupiga dawa majumbani pamoja na sehemu za mazalia ya mbu. Mselem alisema kazi hiyo inatarajiwa kuanza katika kipindi cha msimu wa mvua za vuli, ambazo huibuka kwa mazalia mengi ya mbu yanayosababisha ugonjwa wa malaria.

Zanzibar inatajwa mfano wa kupambana na ugonjwa wa malaria, ambapo hivi karibuni Rais mstaafu wa Marekani, Bill Clinton alizindua mradi wa kupambana na ugonjwa huo wa kupima damu hapo katika uwanja wa Amaan mjini hapa.

Khatib Suleiman
HabariLeo, Zanzibar


JWTZ YAKANA TAARIFA YA JAMII FORUM, TWITTER NA FACEBOOK

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO
Telex : 41051                                                      
Tele Fax  : 2153426
Barua pepe : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Makao Makuu ya Jeshi,                
Simu ya Upepo  : “N G O M E”      
Simu ya Mdomo  : DSM  22150463
 Sanduku la Posta  9203,              
DAR ES SALAAM,                           

           12 Septemba, 2013. 
Taarifa kwa vyombo vya Habari

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limepata habari kupitia mtandao wa Jamii Forumna Gumzo la Jiji  na mingineyo kuwa likizo zimesitishwa Jeshini  na waliokuwa  likizo wameitwa kurudi kazini.

          Taarifa hizo pia zimeeleza kwamba Brigedi za Tembo na Kifaru zimepewa maagizo ya kuwa katika hali 
ya utayari endapo watahitajika kusonga mbele.

          JWTZ  linapenda kuwaeleza wananchi pamoja na watumiaji wa mitandao hiyo kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji mtupu na hazina ukweli wowote.  Aidha, taarifa hizo ni zenye nia ya kuzorotesha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu (Tanzania) na majirani zake. 

Sambamba na taarifa hii, pia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa taarifa za kutohusika na viunganishi vya JWTZ kwenye mitandao ya  ‘Facebook‘ – (Facebook/JWTZ) na  ‘Twitter‘  (Twitter/ JWTZ).

Mitandao hiyo yenye viunganishi vya JWTZ imekuwa ikijihusisha na kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikichangiwa na watu mbalimbali, ambapo baadhi yao wamekuwa wakitoa taarifa za upotoshaji  na zisizo sahihi.  Tunapenda kutaarifu kwamba akaunti za facebook na twitter zilizotajwa siyo za JWTZ.

Hatua zimechukuliwa za kuwatambua wahusika na kuwachukulia hatua za kisheria.

         Aidha inasisitizwa kwamba JWTZ lina taratibu za zake zinazotumika kufanya mawasiliano na Vyombo vya Habari, Taasisi, au mtu binafsi kuhusu utoaji wa taarifa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi
Dar es salaam, Tanzania



AKAMATWA MUDA MCHACHE KABLA YA KUTIMIZA AZMA YAKE YA KUCHOMA QUR`AN

Kiongozi mmoja wa Kanisa nchini Marekani anayeishi jimboni Florida, Terry Jones alitiwa mikononi mwa polisi jana muda mchache tu kabla ya kutimiza azimio lake la kuchoma Quran takriban elfu tatu, katika siku ambayo taifa hilo lililkuwa likiadhimisha miaka 12 tangu Marekani ishambuliwe kigaidi Septemba 11.

Magazeti kadhaa ya jimboni Florida yaliandika ifuatavyo:

The Tampa Tribune: "When he and another pastor were pulled over by Polk County sheriff's deputies near the small town of Mulberry, their pickup bed was full of kerosene-soaked Qurans - and they were towing a 
large, barbeque-style grill behind the truck. The arrest happened shortly before 5 p.m., when Jones was scheduled to burn the Qurans - one for every victim of the terrorist attacks - at a public park just outside Mulberry."

The Polk County Ledger:  County officials had previously denied a permit for the event. The paper reports that in a press conference Sheriff Grady Judd said Jones had been stopped because his trailer did not have a license plate and he has been charged with "unlawful conveyance of fuel and unlawful carry of a firearm."
Essentially, Judd said, Jones was driving a "bomb" down the road.
"We couldn't allow that vehicle to continue down that road," Judd alinukuliwa na gazeti kusema hayo.

The AP: "Jones is the pastor of a small evangelical Christian church. His congregation burned a Koran in March 2011, and last year he promoted an anti-Muslim film. His actions have sparked violence in the Middle East and Afghanistan. The U.S. Central Command, based at MacDill Air Force Base in Tampa, earlier this week had urged him not to go through with Wednesday's event."

Hii si mara ya kwanza kwa Jones kufanya jaribio la kuchoma Quran kwani miaka mitatu iliyopita, alipigiwa simu na Robert Gates, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi wa wakati huo, akimtaka aachane na mpango wake wa kuchoma kitabu hicho kitakatifu cha Waisalam, kwa sababu kufanya hivyo kungehatarisha maisha ya askari wa Marekani waliopo ng'ambo, duniani kote.

Pamoja na kuwa alitii wito huo, mwaka 2012 mwezi Aprili alitimiza azma yake hiyo
.


MESUT OZIL KUANZA KUITUMIKIA TIMU YAKE MPYA YA ARSENAL JUMAMOSI NA SUNDERLAND



KIUNGO Mesut Ozil amewasili katika klabu yake mpya, Arsenal tayari kuanza kumtumikia Arsene Wenger anayekabiliwa na tatizo la wachezaji wengi majeruhi.

Mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa Pauni Milioni 42 ataanza mazoezi leo makao makuu ya klabu, Colney London kwa mara ya kwanza tangu ahamie akitokea Real Madrid.
 
Na Wenger anajiandaa kumtumia mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerumani katika mchezo dhidi ya Sunderland Jumamosi hii baada ya Tomas Rosicky kurejea kwenye mechi ya timu yake ya taifa akiwa majeruhi.
 
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech aliumia wakati timu yake ikilala 2-1 dhidi ya Italia na yuko shakani kucheza Uwanja wa Light.
 
Hiyo inaacha milango wazi mno kwa Ozil kuanza kazi Arsenal, licha ya kwanza atakuwa na siku mbili tu kamili za kufanya mazoezi na wenzake kabla ya mechi hiyo.
 
Licha ya msimu kuwa umekwishaanza kwa karibu mwezi mzima, Arsenal tayari ina idadi kubwa ya majeruhi. 


FAMILIA YA MATUMLA: TUNASHANGAZWA NA TAARIFA YA NDUGU ZETU KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA

TAARIFA za kukamatwa na unga kwa mabondia wawili Mbwana na Mkwinda wa familia maarufu ya mchezo wa ngumi nchini ya Matumla, zimeishangaza familia na jamii nzima ya Tanzania.

Bondia Rashid ‘Snake man’ Matumla ambaye ni kaka wa Mbwana na Mkwanda, amedai endapo itathibitika wadoeo zake wanajihusisha kusafirisha dawa za kulevya, watakuwa ameipa fedheha familia yao.

Mbwana Matumla ambaye ni mkubwa, ameelezwa kukamatwa mpakani mwa Uswisi na Ujerumani wakati Mkwanda Matumla amekamatwa Addis Ababa nchini Ethiopia.

Akikaririwa kuzungumza na wanahabari kadhaa, Rashid, bingwa wa zamani wa dunia wa WBU amesema:

    Tumesikia Mkwanda hadi ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia umethibitisha, lakini Mbwana bado hatuna uhakika ingawa hakuna anayeweza kumpata kwa sasa.

    Ni mwezi sasa umepita sina taarifa naye na hata wakati anaondoka hakuniaga, nimesikia kupitia

    vyombo vya habari. Kitendo cha mdogo wangu kukamatwa kimenisikitisha mno, siyo siri nimekwazika na ninarudia kusema hii ni fedheha kwenye familia yetu.
    
    Mimi mwenyewe nashangaa ni lini amejiingiza kwenye kazi hiyo, hata wakati anaondoka hakuniaga, mimi kaka yao na familia hatuelewi chochote.

    Unajua Mbwana hakumuaga hata mkewe, kweli inatusikitisha sana na tunasikia maumivu makubwa. Kama kweli itakuwa ni hivyo, basi watakuwa wameiangusha sana familia ambayo ilipigana kujenga jina. Lakini hatuwezi kuwatenga kwa kuwa ni ndugu zetu, tutawapigania.

Maisha:
Mkwanda alikuwa akiishi nchini Sweden ambako alikuwa na mpenzi wake aliyejaaliwa naye kupata mtoto mmoja aitwaye Liam aliyezaliwa mwaka 2010. Mpenzi wake huyo raia wa Sweden alikuwa mwanafunzi katika chuo kimoja mjini Norrkoping wakati Mkwanda alikuwa mwanafunzi katika chuo kingine akisomea Lugha ya Kiswidi. Alisema mdogo wake huyo alikuwa amebadilisha uraia na kuchukua uraia wa Sweden licha ya kwamba hapa Tanzania alikuwa amepanga Mbagala, Dar es Salaam na alikuwa anakuja na kukaa kwa muda na kisha kuondoka.

Kurejea:
Hivi karibuni inaelezwa alirejea jijini Dar es Salaam na alionekana ni mtu mwenye furaha na mishemishe kibao. Alikuwa anamiliki gari aina ya Toyota Vitz ambalo pia aliliuza lakini kuna taarifa kuwa, alinunua kiwanja katika moja ya maeneo ya Jiji la Dar.

Ngumi:
Katika familia ya Matumla, Mkwanda ndiye alikuwa bondia mdogo kuliko wote baada ya wengine sita. Kwa mujibu wa Rashid alipumzika kucheza ngumi miaka kadhaa iliyopita kutokana na kusumbuliwa na maradhi. Rekodi zinaonyesha kabla ya kupumzika kwa muda kucheza ngumi, Mkwanda alishinda mapambano manane (sita kwa KO) alipigwa mara tatu zote kwa KO alitoka sare mara moja tangu 2004. Mkubwa ni Ally ambaye ni marehemu, anafuatiwa na Rashid Matumla aliyewahi kuwa bingwa wa dunia mara mbili, bingwa wa mabara, Afrika mara moja na ndiye anaaminika kuwa bondia mkali zaidi ya wengine. Anafuatia Hassan, Mbwana ambaye anaelezwa ‘kudakwa’ Ulaya, Kareem na Mkwanda. 

--- Habari kwa mujibu wa magazeti ya MWANANCHI na GPL



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU