Facebook Comments Box

Sunday, January 20, 2013

BARABARA YA LINDI MTWARA SI SHWARI

Barabara ikifanyiwa matengenezo na mvua zimekuwa zikinyesha kipindi hiki



Magari yamekuwa yakipata dhahama kubwa kama hizi




NSSF YAANZA KUUZA NYUMBA ZAKE ZA KIBADA KIGAMBONI


Mkurugenzi  wa Mipango Uwekezaji na Miradi wa  Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),  Yacoub Kidula (kulia) akimkabidhi funguo ya nyumba, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Hamid Mahmoud Hamid baada ya kununua nyumba ya shirika hilo iliyopo katika eneo la mradi wa nyumba za bei nafuu huko Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mahfoudha Alley Hamid.

Mkurugenzi  wa Mipango Uwekezaji na Miradi wa  Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),  Yacoub Kidula akiangali akikagua nyumba ya shirika hilo kabla ya kuikabidhi kwa mnunuzi wa nyumba hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Hamid Mahmoud Hamid. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mahfoudha Alley Hamid.
Baadhi ya nyumba za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizopo katika eneo la mradi wa nyumba za bei nafuu huko Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam.






POLISI LINDI YAZUIA MAANDAMANO YA GESI YALIOANDALIWA NA VYAMA VYA SIASA




JESHI la Polisi mkoani Lindi,limezuia kufanyika kwa maandamano ya
kuunga mkono majirani zao wa Mtwara,kupinga kusafirishwa kwa njia ya
bomba la gesi asilia,kutoka mkoani humo kupelekwa Jijini Dar es salaam
kwa ajili ya kufufua umeme utokanao kwa rasilimali hiyo.

Kwa mujibu wa barua kutoka Ofisi ya Jeshi hilo,ambayo inaonyesha
kukosewa kwa mwezi na mwaka,yenye kumbukumbu LND/271/VOL.1/17 ya
Decemba 17/2012,na mwandishi wa habari hizi kupata nakala yake,na
kusainiwa na Kamanda George Mwakajinga,imepelekwa kwa vyama vinne vya
siasa.

Vyama vilivyopelekewa barua za zuio la maandamano hayo ni pamoja na
Chama cha mapinduzi (CCM), (CUF), CHADEMA na NCCR-MAGEUZI.

Kwa mujibu wa barua hiyo,inawataka viongozi wa vyama hivyo vinne vya
siasa kuchukua hatua mapema ya kuwasihi na kuwaelimisha wanachama wao
kwanza, kwa ujumbe wa gesi kama ulivyotolewa na wananchi wa mkoa wa
Mtwara.

“Napenda kuchukuwa nafasi hii kuwaandikia kuwakumbusha tarehe kuwa 04/01/2013,siku ya Ijumaa mkuu wa mkoa wa Lindi,Ludovick Mwananzila
alipata fursa ya kuwaalika wadau wote,wazee wa mji wa Lindi,viongozi
wa madhehebu ya dini na vyama vya siasa,alizungumzia na
kufafanua mwelekeo na msimamo wa Serikali katika suala la gesi na jinsi
mkoa unavyochangia pato la Taifa kwa gesi ya Songosongo na jinsi
anavyojiandaa kwa ugunduzi mpya kwenye kina kirefu cha bahari ya Hindi
wilaya ya Kilwa”Imeeleza sehemu ya barua hiyo.

Aidha,barua hiyo imeeleza kwamba Jeshi hilo la Polisi,lisingependa
kukwaruzana na jamii katika maandamano hayo ya barabarani kwa hoja za
kisera za kiuchumi ambazo ni za ki-Taifa, zinazoweza kuzungumzika
katika mifumo mingine ya kiutawala kama vile katika vikao vya Bunge.

“Tunaomba ushirikiano na ushirikishwaji wa Jamii katika utii wa
sheria bila Shuruti katika kudumisha amani na utulivu ndani ya mkoa wa
Lindi”Imeeleza barua hiyo.

Baadhi ya viongozi na wanachama wa vyama vilivyopelekewa barua
hizo,wamemuomba kamanda huyo wa Polisi mkoani hapa,George
Mwakajinga,kutoupotosha umma juu kauli yake,kwani maandamano
yanayotarajiwa kufanywa ni kuunga mkono jirani zao wa Mtwara katika
kutetea gesi iliyogunduliwa huko kutopelekwa nje ya mkoa huo kwa njia
ya Bomba,na sio kupinga kauli ya mkuu wa mkoa wa Lindi.

“Sisi tunawaunga mkono jirani zetu wa Mtwara, juu ya kuondolewa gesi
kupelekwa Dar es salaam,kwani huo ni uonevu na unyang’anyi mkubwa
unaofanywa na hawa viongozi wetu waliopo madarakani”

“Kwani sisi watu wa mikoa ya kusini tumeikosea nini hii Serikali,kama
ni gesi tumewapa kutoka Songosongo Kilwa,licha ya wenzetu kuizuia kwa
njia ya kiustaarabu,yaani kuifikisha mahakamani,lakini
tuliwaachia na Kilwa kukosa kiwanda cha mbolea kama ilivyokuwa
imepangwa,sasa leo wanataka kuihamisha ya Mtwara tuendelee kuwa
masikini”Walisema viongozi na wanachama hao.
Januari 04 mwaka huu,viongozi wa Chama cha wananchi (CUF) mkoani
Lindi, wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja vya
Sera,Manispaa ya Lindi,Walitoa wito kwa wananchi kushiriki katika
maandamano yatakayofanyika Februari 23 mwaka huu,ili kuwaunga mkono
jirani zao wa mkoa wa Mtwara,kupinga uamuzi wa Serikali kusafirisha
gesi kwa njia ya bomba na kuipeleka Jijini Dar es salaam kwa ajili
ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme.

Mambo mengine yaliyotajwa na viongozi hao ni pamoja na kuwepo kwa
mfumo wa ununuzi wa mazao kwa utaratibu wa mfumo wa Stakabadhi
ghalani, kwa maelezo kwamba umekuwa hauwasaidii walengwa (wakulima) na
badala yake umekuwa ukiwasaidia wachache



ANGALIA PICHA ZA MAANDALIZI YA KUAPISHWA RAIS OBAMA WA MAREKANI


Maandalizi makubwa yafanyika jijini Washington DC kwa Sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Marekani Barack Obama yameanza kukamilika.

Vyombo vya Habari mbali mbali hapa nchini Marekani vimekuwa katika kukamilisha matayarisho ya kupata matukio ya kuapishwa Rais Barak Obama kwa muhula wa Pili Ikiwa Mmarekani wa kwanza mwenye asili ya Kiafrika kuchaguliwa kwa mara ya pili na hivyo kuifanya sherehe hiyo kuwa ya Kihistoria.

Sherehe hizo zitafanyika katika viwanja vya National Mall na Memorial Parks zitahudhuriwa na mamilioni ya Raia wa marekani na wageni kutoka nchi mbali mbali kote ulimwenguni.

Rais Obama wa Marekani alichaguliwa kwa kura nyingi baada ya kumshinda mgombea wa kiti cha chama cha Republican Mitt Romney na kuingia awamu ya pili ya Urais ya Urais wa Marekani

Karibia mwenzi mzima ufundi wa maandalizi ya Obama inauguration 2013 yaliokua yakifanyika katika maeneo mbali mbali ya Jijini Washington DC yaaza kutia Sura, hapa ni Jengo la Congress ya Marekani Jijini Washington DC.
Baadhi ya ufundi uliokamilika katika jingo la Capitol Hill liliopo washington DC na viti vilivyopangwa rasmi kwa ajili ya wageni wanunuzi watikiti za 2013 Inauguration History ndio makazi yao yatakapokua hapa kwa siku ya Jumatatu Jan. 21, 2013 
Cheif wa swahilivilla blog Abou Shatry akipata picha ya 2013 katika jingo la Congress ya Marekani liliopo washington DC katika jingo la Capitol Hill liliopo down town Washington DC Nchini Marekani.
Picha 2008 Inauguration History: Hivi ndivyo itakavyokua Siku ya Jumatatu Januwari 21, 2012 kwenye Jumba la Congress ya MarekaniDown Town Washington DC.
Sehemu kubwa ya sherehe ya kuapishwa kwa rais Obama ikifanyiwa ukarabati wamuda.
Rubber floor tiles zikitandazwa maeneo ya sakafu zilizokua na mchanga kwaajili ya kuhifadhi tope tope zisitimke na kuharibu eneo hilo kubwa la National Mall,
Kukanyaga mchanga Marekani ni kosa kubwa na ndio maana wameweka Rubber floor tiles kwaajili ya kukanyagia ili kunusuru michimbuko ya tope tope na kutoshafua barabara kwa msongamano wa watu watakaomiminika kutoka Nchi mbali mbali kuja kushuhudia kuapishwa kwa Obama
Sehemu iliotandikwa Rubber floor tiles: Hivi ndivyo Rubber floor tiles zinavyotandikwa kwenye michanga ili kunusuru topetote raia wasichafuwe maeneo ambayo bado yanafanyiwa ukarabati sehemu ya National Mall Jijini hapa.
Hivi ni baadhi ya yyoo vya Potty shortage vinavyotumika kwa haja ndogo na kubwa viko tayari kwaajili ya raia na wa geni watakao miminika kuanzia kesho Jumapili na Jumatatu siku ya Obama's inauguration
Fundi mitambo wa NBC NEWS akianda mpango mzima wa kuahabarisha sherehe za kuapishwa kwa rais wa Marekani Barack Obama Live
Banda la CBS NEWS lilijengwa kwa muda vile vile wako tayari kwa kutoa huduma za kuhabarisha matangazo ya moja kwa moja kwenye kumbukumbu za 2013 Inauguration
Channel marufu ya CNN wakia kwenye uwanja wa National Mall na wao pia wapo tayari kwa kutoa huduma za kuhabarisha na matangazo ya moja kwa moja kwenye sherehe ya kuapishwa kwa Obama 2013 Inauguration 
Basi lililowakilisha baadhi ya wafanyakazi wa CNN kumbukumbu ya 2013 Inauguration ndani ya Jiji la Washington DC 
Basi jengine lililowakilisha wafanyakazi wa C-SPAN kumbukumbu ya 2013 Inauguration ndani ya Jiji la Washington DC 
Kamera iliopo mbele ya Presidential Inaugural Review Stands, in front White House Washington, D.C. baada ya kuapishwa kwa Obama. hii ni moja itakayo tumika kwenye Inaugural Review Stands
Cheif wa swahilivilla akia mbele ya White House na mmoja wa wafanya kazi wa Super Control Camera ambayo kwa jina wanaita Gym Camera inauwezo wa kunyanyuka juu umbali wa futi 16 na kuhabarisha Live.
Sony Camera ipo tayari kwa kuhabarisha mbele ya Presidential Inaugural Review Stands, mbele ya White House Jijini Washington DC.
Nyuma ya Presidential Inaugural Review Stands ni White House kuna ujia mrefu wa Red carpet ndio atakaotumia kuingilia kwenye Review Stands.
Cheif wa swahilivilla blog Abou Shatry akiwa mbele ya Presidential Inaugural Review Stands ambayo kutumika kwa ajili ya uzinduzi wa Rais Barack Obama baada ya kuapishwa.
Mjengo wa Matangazo pamoja na Camera LIVE uliojengwa kwa moda mbele ya White House
Benchi nyingi zilizojengwa kwa ahili ya wageni na rais kutoka sehemu mbali mbali watatumia kukalia wakati wa Parade


HII NDIO SHEHENA YA MIHADARATI ILIYOKAMATWA ARUSHA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP),Liberatus Sabas (kulia) akiongea na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya jinai Mkoa wa Arusha Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP),Camirius Wambura aliyeshika madawa ya kulevya aina ya mirungi nje ya jengo la Makao Makuu ya jeshi hilo Jijini Arusha mara baada ya kukamata shehena hiyo.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP),Liberatus Sabas (wa pili kushoto) akiongea na baadhi ya Waheshimiwa Madiwani na Waandishi wa habari nje ya jengo la makao makuu ya jeshi la Polisi Jijini Arusha.
Gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T. 284 AGL ambalo lilikuwa na shehena ya mirungi viroba vipatavyo 173 vyenye jumla ya uzito wa kilogramu 1800.(Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha).

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU