Facebook Comments Box

Sunday, February 22, 2015

CHELSEA YATOKA SARE NA TIMU AMBAYO HUWA INAISUMBUA KATIKA LIGI BURNLEY

 Mshambuliaji wa Burnley akisawazisha bao na kufanya sare ya 1-1


Ivanovic akiifungia timu yake bao la kwanza katika mechi hiyo likiwa ni goli la 4 katika michezo 6 aliyocheza.
Mchezaji wa Chelsea Matic alipewa kadi nyekundu na kutolewa katika mchezaji huo baada ya kumsukuma mchezaji wa Burnley mpaka kumdondosha chini baada ya awali kumchezea rafu.
Wachezaji wa Burnley wakipongezana baada ya kufanikiwa kusawazisha wakiwa ugenini na kufanya mpambano huo kumalizika kwa kufungana 1-1.


ARSENAL YAICHAPA CRISTAL PALACE UGENINI

 Wachezaji wa Arsenal wakishangilia bao la kwanza lililofungwa katika dakika ya 8 na Sant Carzola
 Sant Carzola akishangilia baada ya kuipatia timu yake bao la kwanza likiwa ni bao lake la 7 katika msimu huu.
Straiker Force Giroud akiwatoka walinzi wa Cristal Palace na kufunga bao la pili na la ushindi kwa Arsenal lakini likiwa ni bao lake la 5 katika michezo saba aliyocheza.
Hapa Beki na kipa wa Cristal Palace wakiokoa michomo ya Monreal na Kosienly wa Arsenal


LEO NDIYO LEO FAINALI YA LIGI DARAJA LA KWANZA KATI YA MWADUI FC NA AFRICAN SPORTS YA TANGA NDANI YA AZAM COMPLEX CHAMAZI


Mwadui FC

African Sports

Fainali ya kumsaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), inatarajiwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika leo kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TTF imelazimika kuhamishia mchezo huo Chamazi.

Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.

Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia. Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Lakini pia katika uwanja huo wa Azam Cmplex kutakuwa na mpambano mwingine wa wenyeji Azam watakao cheza na Tanzania Prisons ambapo mchezo huo utaanza majira ya saa mbili kamili usiku.

Mjini Shinyanga wenyeji timu ya Stand United wataikaribisha Simba SC kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku wagonga nyundo wa jiji la Mbeya, timu ya Mbeya City wakicheza na timu ya Young Africans kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA

MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


WATAKA KUWA NA LADY JAY DEE COMMANDO, MAMAA SOME FOOD? ONA SIFA ZA MWANAUME AMTAKAE

 Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee hapa akiwa na aliyekuwa mumewe ambae wameachana Gardner G Habash ambae kwa sasa ni Mtangazaji wa kituo cha E-FM kilichopo Dar es Salaam.
Lady Jay Dee akiwa amesimama nyuma ya gari lake Range Rover.


Kama wewe ni Mwanaume mwenye ndoto za kuwa na Nyota huyu wa Muziki wa Tanzania angalia sifa alizo orodhesha katika mtandao wa Instagram huenda ukawa wewe.

Jide ambae ameachana na aliyekuwa mumewe kwa sasa yupo single na ameonekana kutaka kuwa na mtu mwingine ambae atakuwa na sifa ambazo amezitaja kuwa ni Anaejali na kujiheshimu, Mwenye roho ya upendo na huruma, Anaeweza kum take care financially, Asiechepuka hovyo, Asiwe tegemezi, Hata kama sio tajiri lakini asimtegemee yeye, Asiwe mlevi kupindukia wa kulala bar au kulala nje kwa "machangu" wa kinondoni au wa sehemu yoyote.

Lakini pia Jide amesema kuwa kwa sasa ana marafiki wengi lakini wengi wao ni wa kiume ambao walio wengi ni wa kutoka nje ya nchi na huwa anakutana nao kwenye mikusanyiko ya watu wengi na urafiki wao ni wa kubadilishana mawazo, kwenda dinner, na kualikana majumbani kufungua shampeni na kuchoma nyama. "Kama mmeniona nao huko We were just having fun", nothing serious alisisitiza Jide.

Amesema kwa sasa anae mpenzi wa miaka mingi sana ambae amekuwa akimpa karibia kila anachotaka kama vile, Amemjengea nyumba, amemnunulia viwanja, magari, anamlisha na kumvisha pia anamsomeshea ndugu zake, Amemfungulia Restaurant na ameahidi kumnunulia Beach House na Land Rover model ya 2015 ila hizo ni ahadi bado hajazitimiza.

Kila akitaka kwenda holiday anagharamia kila kitu, akitaka kwenda kwa Fans wa Paris analipa tena anmlipia ndege Business Class. "Sasahivi ameahidi kunilipia Trip ya Italy nikawaone kina Kayumba, Shopping na n.k tena hajawahi kunisaliti. JE WAMJUA HUYU MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI?, ANAITWA "MUZIKI".

Ila akasema maswali kuhusu mambo ya ndoa yake atayajibu siku nyingine ili aongelee maswala hayo tu hataki kuchanganya na mambo mengine maana yamesemwa mengi.


Wednesday, February 18, 2015

RAIS KIKWETE ATEUWA WAKUU WA WILAYA WAPYA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA WAPYA 27
 
Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Wakuu wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya kazi vya zamani.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa OWM TAMISEMI leo mchana (Jumatano, Februari 18, 2015) Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais  Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.

Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni:- 

Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilayaya Wanging’ombe.

Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Shaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).

Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).

Wakuu wa Wilaya saba ambao uteuzi wao umetenguliwa lakini watapangiwa kazi nyingine ni:- 

Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).

Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa ni:-

 James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015


Monday, February 16, 2015

MWADUI FC NA TOTO AFRICAN ZAKAMILISHA IDADI YA TIMU NNE ZILIZOPANDA LIGI KUU


MWADUI FC

Timu ya Mwadui yenye maskani yake Mwadui - Shinyanga imefanikiwa kurudi ligi kuu baada ya miaka 27 tangu iliposhuka daraja hilo. 

Timu hiyo inayofundishwa na Kocha JAMHURI KIWELU "JULIO ALBERTO" Imerudi ligi kuu baada ya kuichapa timu ya Bukinafaso kwa mabao 4-1 na kuongoza katika kundi lao kwa kufikisha point 46 kileleni huku Mshindi wa pili wakiwa wana kishamapanda Toto Africans wa Jijini Mwanza ambao nao walishinda mechi yao iliyopigwa katika uwanja wa CCM - KIRUMBA kwa kuwafunga Rhino Rangers mabao 2-0 na kufikisha point 45 baada ya kuongezwa point 3 za mechi iliyokwisha kwa vurugu ya Geita.

Kwa ujumla timu zilizopanda ligi kuu ni nne ambazo ni AFRICAN SPORTS(TANGA), MAJIMAJI(SONGEA), MWADUI FC(SHINYANGA) na TOTO AFRICANS(MWANZA). Ligi ya msimu ujao itakuwa na timu 16 baada ya kupanda hizo nne na kushuka timu mbili.




Saturday, February 14, 2015

HUU NDIO UKWELI KWA YANAYO ENDELEA AMBONI TANGA

Kamishna wa Polisi Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja ametoa maelezo ya kile kinachoendelea Tanga. Kumekuwa na maneno mengi katika mitandao ya kijamii kuhusu yanayo endelea huko Tanga. Hii imepelekea Kamishna huyo kutoa taarifa

Katika taarifa yake ameelezea kuwa manamo tarehe 26 mwezi wa kwanza mwaka huu majira ya saa tano usiku polisi wakiwa katika doria walivamiwa na majambazi na kuporwa silaha na kujeruhiwa.Polisi wakishirikiana na Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) walifanya upelelezi na kugundua zilipofichwa silaha walipofika eneo la tukio ndio yakatokea majibizano ya risasi kati ya majambazi na polisi. Majibizano hayo ya risasi yamewajeruhi askari sita na mpaka sasa msako unaendelea.

Hapa chini ni taarifa ya Kamishna Chagonja





TAMBWE WA KIMATAIFA: APIGA MBILI ZILIZOIPA YANGA USHINDI DHIDI YA BDF YA BOTSWANA

Amis Joselyn Tambwe akishangilia goli lake pamoja na Simon Happygod Msuva
YANGA Leo ndani ya Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam imeichapa Klabu ya Botswana BDF XI Bao 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Awali ya Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho.
 
Bao zote za Yanga zilifungwa na Straika wao Amisi Tambwe anaetoka Burundi moja katika kila Kipindi.
Tambwe akishangilia goli lake na Mrisho Ngassa na Msuva ambao ndio wapishi wa magoli yake.

Tambwe alifunga Bao la Kwanza Dakika ya Kwanza tu ya Mchezo alipounganisha kwa Kichwa Krosi ya Simon Msuva na kupiga Bao la Pili katika Dakika ya 55 pia kwa Kichwa baada ya Krosi safi ya Mrisho Ngassa.
Mrisho Ngassa akichanja mbuga


Timu hizi zitarudiana huko Botswana Wiki mbili baadae na Mshindi wake atatinga Raundi ya Kwanza kucheza na Mshindi kati ya Sofapaka ya Kenya na FC Platinum ya Zimbabwe.
Hapo Kesho Jumapili, Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC, watakuwa kwao Azam Complex huko Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kuivaa El Merreikh ya Sudan katika Mechi ya Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONZ LIGI.
Timu nyingine mbili za Tanzania ambazo pia zimo michuano ya CAF Barani Afrika ni KMKM na Polisi, zote za toka Zanzibar, Wikiendi hii zinaanzia Ugenini kwa KMKM kucheza Sudan na Al Hilal kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI  na Polisi kucheza Nchini Gabon na CF Mounana kwenye Kombe la Shirikisho
Mchezaji wa BDF akimfanyia rafu Haruna Niyonzima



APPLE SASA WAJA NA GARI LISILOTUMIA MAFUTA

Gazeti la Wall Street Journal linayo ripoti kuwa watengenezaji wa simu maarufu ya iPhone na kifaa cha iPad, Apple wanajishughulisha kutengeneza gari litakalotumia umeme ikiwa ni changamoto kwa kampuni ya Telsa inayotawala soko hilo kwa sasa.

Taarifa hiyo ya WSJ haijamtaja mtoboa siri hiyo zaidi tu ya kusema kuwa ni mwajiriwa wa Apple anayefanya kazi katika mradi huo.

Mtoa habari huyo ametanabahisha kuwa wapo watu mamia kadhaa wanaofanya kazi kwa siri kutengeneza gari hilo la mradi uliopewa jina la "Titan" na tayari wameshaunda muonekano unaoelekea kabisa kufanana na 'minivan'. 

Msemaji rasmi wa kampuni ya Apple alipoulizwa kuhusu hilo alikataa kuthibitisha au kukanusha taarifa hizo.

Nalo gazeti la Financial Times lina habari ambayo chanzo chake ni mtu ambaye hakutaka kutajwa, akisema kuwa wafanyakazi wa Apple wamekuwa wakitafiti kuhusu vipuri vya magari katika eneo moja huko Silicon Valley.

Waajiriwa wa hivi karibuni katika kampuni ya Apple ni pamoja na mkuu wa kitengo cha utafiti cha Mercedes-Benz katika tawi la Silicon Valley.


BREAKING NEWS: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA

Baraza la mitihani la taifa (NECTA) wameweka matokeo ya kidato cha nne kwa wanafunzi walio maliza kidato cha nne mwaka 2014.
Haya ni baadhi ya matokeo ya shule ya Mivumoni Islamic Secondary ambao imeshika nafasi ya 20 kitaifa. Wanafunzi wa shule hiyo wamepata Distinction 18 na Merit 21. matokeo mengine ingia kwenye link hapo chini.
BONYEZA HAPA KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

PIKIPIKI YAO YACHOMWA BAADA YA KUKWAPUA SIMU YA MWANADADA MMOJA

 Pikipiki hiyo ikiteketea kwa moto.
 Wananchi wakishuhudia pikipiki hiyo ikiteketea.
Wananchi wakipiga picha pikipiki hiyo.

Kamera yetu mtaani:

Wizi wa kukwapua kwa kutumia Pikipiki umeshamiri sana Jijini Dar es Salaam kwa watumiaji hao wa pikipiki kukwapua vifaa kama simu za mikononi, mabegi ya wanawake maarufu kama "vipima joto", laptop na vitu kama hivyo.

Kuna vijana wawili waliwahi kuchomwa moto baada ya kutimiza siku zao arubaini kama msemo usemavyo kuwa "Za Mwizi arubaini" katika maeneo ya Tabata-Liwiti.

Hali hiyo ilitokea tena katika maeneo ya Hospitali ya Ocean Road ambapo wataalamu hao wa kuiba kwa pikipiki walipokutwa na zahma hiyo baada ya kumkwapulia simu mwanadada mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja na wao kukimbia ndipo msamaria mmoja akawakimbiza kwa gari lake na watu hao kuzidiwa ujanja na kukamatwa katika eneo hilo na pikipiki yao kuchomwa moto kama inavyoonekana pichani.






Friday, February 13, 2015

TFF YAIPA MATUMAINI MAKUBWA TOTO KURUDI LIGI KUU KWA KUIPA USHINDI DHIDI YA GEITA

Baraka-Kizuguto_3a74e.jpg
Afisa Habari wa TFF Baraka Kizuguto

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imethibitisha ushindi wa pointi 3 na mabao matatu kwa timu za Majimaji na Toto Africans baada ya mechi zao za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuvurugika kutokana na sababu mbalimbali.

Toto Africans imepewa ushindi huo kwa mujibu wa Kanuni ya 41(3) ya FDL baada ya vurugu za washabiki wa Geita Gold kusababisha mechi hiyo iliyochezwa Februari 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita kuvunjika dakika ya 12.

Pia Kamati hiyo iliyokutana Dar es Salaam jana (Februari 12 mwaka huu) imezuia mechi za FDL kuchezwa kwenye uwanja huo ambao hauna uzio wa kutenganisha wachezaji na washabiki kwa sababu za kiusalama.

Naye mchezaji Venance Joseph wa Geita Gold ambaye alimpiga kichwa refa akipinga adhabu ya penati iliyotolewa dhidi ya timu yake kwenye mechi hiyo amesimamishwa wakati akisubiri kosa lake kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Malalamiko ya Friends Rangers kwenye mechi dhidi ya Majimaji yametupwa na kupigwa faini ya sh. 500,000 kwa kusababisha mchezo huo uliochezwa Januari 29 mwaka huu Uwanja wa Majimaji mjini Songea kuvunjika dakika ya 39. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(4) ya FDL.

Friends Rangers imepoteza mechi hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 28(1) ya FDL, Majimaji kama ilivyo Toto Africans imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu.

Naye Kocha wa Friends Rangers, Herry Chibakasa (Mzozo) suala lake limepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF ili aweze kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni ya 39(8) ya FDL kwa kuhamamisha vurugu kwenye mechi dhidi ya Majimaji.

Mwamuzi John Mafuru wa Mbeya aliyechezesha mechi ya Majimaji na Friends Rangers amefungiwa miezi 12 (kumi na mbili) kwa kutozingatia sheria kiasi cha kuvuruga mchezo. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 37(1) ya FDL.

Pia Kamishna wa mechi hiyo Kim Rajab wa Dodoma amefungiwa miezi 12 (kumi na mbili) kwa mujibu wa Kanuni ya 38(1) ya FDL kwa kutoa taarifa zisizo sahihi.

Lipuli ya Iringa imepewa ushindi wa mabao matatu na pointi tatu baada ya timu ya KMC (Tessema) kumchezesha mchezaji Morris Paulo Katumbo aliyekuwa na kadi tatu za njano kinyume na Kanuni ya 41(12) ya FDL. Katumbo ambaye alipata kadi hizo kwenye mechi namba 85, 100 na 112 alicheza mchezo huo uliomalizika kwa timu ya KMC kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


Tuesday, February 10, 2015

RAIS KIKWETE ALIPOFANYA MAZOEZI YA KUTEMBEA ASUBUHI





RAIS KIKWETE ZIARANI KILIMANJARO LEO

Jengo jipya la kisasa la kitega Uchumi la Mfuko wa Hifadhi ya Jami NSSF mkoani Kilimanjaro

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete leo anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro ambapo miongoni mwa shughuli anazotazamiwa kufanya ni pamoja na
kufungua jengo la kitega uchumi la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mbali na ufunguzi huo Rais Kikwete pia anatarajia kufungua jengo la Upasuaji na kuweka jiwe la msingi katika jengo la wodi ya wazazi na watoto katika hosptali ya rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro ,Mawenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ,mkuu wa mkoa huo Leonidas Gama alisema Rais Kikwete atawasili mkoani humo leo jioni majira ya saa 11:00 jioni ambapo atapokelewa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kuelekea Ikulu ndogo kwa ajili ya kupokea taarifa ya Mkoa.

Alisema Kesho (February 10) Rais Kikiwete atafanya shughuli katika Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi ikiwemo ufunguzi wa jengo la Upasuaji (Theater) ambalo limekuwa tatizo la muda mrefu katika hosptali hiyo.

“Kwanza kama mnavyo fahamu tumekuwa na tatizo la muda mrefu ya wodi ya upasuaji katika hospitali yetu ya Mawenzi,lakini kwa juhudi zilizofanywa na serikali na ushirikiano wa wadau mbalimbali lile jengo

la Upasuaji limekamilika na liko katika kiwango kizuri kwa hiyo shughuli ya kwanza atakuja kulifungua rasmi jengo la upasuaji.”alisema Gama.

Gama alisema pia Serikali tayari imefanya juhudi za kujenga jengo jipya la Wodi kwa ajili ya Wazazi na Watoto katika hosptali hiyo na kwamba Rais Kikwete ataweka rasmi jiwe la msingi kwa ajili ya muendelezo wa ujenzi wa jengo hilo.

Alisema kwa mujibu wa ratiba shughuli ya mwisho anayotazamia kufanya Rais Kikwete ni ufunguzi rasmi wa jengo la kitega Uchumi la NSSF, jengo ambalo litatumika kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi .

“Ufunguzi rasmi wa jengo hili utabadilisha taswira ya mji wetu,ni jengo la kisasa lenye Hotel,Maofisi mbalimbali,Kumbi za mikutano na maduka mbalimbali makubwa kwa madogo ambayo yatahudumia wananchi wote”alisema Gama.

Gama alitoa wito kwa viongozi na wananchi wote wa mkoa wa Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi katika ufunguzi wa jengo hilo la NSSF majira ya saa 2:00 asubuhi ambapo rais Kikwete pia atapata nafasi ya kuzungumza na wananchi.

“Lengo la Rais Kikwete kuja ni kutuunga mkono sisi wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro katika miradi yetu ya maendeleo hivyo basi tufike mapema katika maeneo hayo ili tumsubiri na tumuone rais na kumshangilia”alisema Gama.
  • Dixon Busagaga, Moshi via Michuzi Blog


TEKNOLOJIA YATUMIKA KATIKA KESI YA SHEIKH PONDA

UPANDE wa Mashikata kesi inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shehe Ponda Issa Ponda umewasilisha ushahidi muhimu wa mkanda wa video unaodaiwa kuonesha uhalisia wa tukio zima la kesi yake inayomkabili ya kutoa maneno ya uchochezi.

Mkanda huo wa video uliletwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, Mary Moyo na kuoneshwa na shahidi wa tano wa kesi hiyo ambaye ni askari kutoka makao makuu ya Jeshi la Polisi kitengo maalumu cha uchunguzi wa picha,

Aristides alieleza vigezo alivyovitumia kuitambua uhalisia wa video hiyo iliyochukuliwa Agosti 10 mwaka 2013.
Shahidi huyo akiongozwa na Wakili wa Serikali, Benard Kongola alieleza mahakamani hapo kuwa video aliichunguza na kugundua kuwa ilichukuliwa katika eneo la tukio kupitia kamera ndogo aina ya JVC na kwamba baada ya kuichunguza aliandika hati na taarifa iliyoeleza vigezo alivyovitumia
katika uchunguzi huo na yale aliyoyaona na kuyasikia katika video hiyo ambayo aliitoa mahakamani kama kielelezo.
Pamoja na ushahidi wake, lakini pia aliionesha video hiyo mahakamani hapo ambapo ilionesha tukio zima pamoja na maneno aliyoyatoa Shehe Ponda ambayo yanadaiwa kuwa yalikuwa ya uchochezi na yaliyoumiza imani ya dini nyingine.
Shahidi huyo pia alitoa kamera, DVD, hati na taarifa ya uchunguzi wa video hiyo kama kielelezo na kupokewa na mahakama hiyo.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna msaidizi wa Polisi, Faustine Shilogile alikuwa shahidi wa nne katika kesi hiyo ambaye alieleza kuwa baada ya kupata taarifa za kutafutwa kwa Shehe Ponda kufuatia tuhuma mbalimbali zilizomkabili yeye kama kiongozi wa jeshi la polisi
mkoa aliandaa askari kwa ajili ya kumkamata baada ya kufika mkoani Morogoro.

Shahidi huyo alidai kuwa taarifa hizo za kiintelijensia zilimhusisha Ponda na tuhuma za kumwagia tindikali wasichana wawili raia wa Uingereza huko Zanzibar na tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi jijini Dar es Salaam na kwamba tuhuma hizo alizipata wakati akiwa kwenye adhabu ya kifungo cha nje cha mwaka mmoja ambapo pia alitakiwa kutofanya kosa lolote katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Juma Nasoro ulimuuliza maswali shahidi huyo, hata hivyo baadhi ya watu waliokuwepo mahakamani hapo walishindwa kuzuia vicheko vyao kutokana na aina ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa pamoja na majibu yaliyokuwa yakitolewa.

Wakili wa utetezi: “Je wewe ulijuaje kama Shehe Ponda alitoa maneno ya uchochezi?”

Shahidi: “Niliambiwa na OCD wangu kupitia radio call (simu ya upepo) kwani alikuwepo eneo la tukio.”

Wakili: “Je, unayajua mashitaka yanayomkabili Shehe Ponda?”

Shahidi: ”Siyafahamu kwa kuwa mimi sio muandaaji wa hati ya mashitaka.”

Wakili: “Ni askari wangapi uliwaandaa kumkamata Shehe Ponda?”

Shahidi: “Sikumbuki”

Wakili: “Je, hukuandaa askari 25 hadi 30 kwa ajili ya kumkamata Shehe Ponda? “

Shahidi: “Wewe ndio utakuwa umeeleza hiyo idadi”

Wakili: ”Je, askari wako walikuwa na silaha na kama walikuwa nazo tunaweza kuamini kuwa wao ndio waliomjeruhi Shehe Ponda?”

 Shahidi: “Ndiyo baadhi ya askari wangu walikuwa na silaha lakini siwezi kufahamu Shehe Ponda
alijeruhiwa na nini.”

Wakili: “Je, unajua kama Msemaji wa Polisi, Advera Senso alitoa taarifa kuwa kuna askari alisimamishwa kazi kupisha uchunguzi?”

Shahidi: “Sina taarifa na kama alitoa taarifa hizo basi ni yeye na sio mimi.”

Wakili: “Je, kibali cha kufanya kongamano kilitolewa na nani na je uliambiwa kama Shehe Ponda ni mzungumzaji katika kongamano hilo?”

Shahidi: “Kibali kilitolewa kwa OCD na sikuwa na taarifa kama Shehe Ponda atakuwa mzungumzaji.”

Awali, upande wa mashtaka ulipanga kusikiliza mashahidi watano hata hivyo mahakama ilishindwa kuendelea kusikiliza mashahidi wengine watatu kutokana na muda kuwa umekwisha hivyo mashahidi hao watatu wataendelea kusikilizwa leo Februari 10 katika mahakama hiyo.

Hata hivyo, kesi imeendelea kuvuta hisia za wakazi wengi wa mkoa wa Morogoro na maeneo mengine huku hali ya ulinzi katika viwanja vya mahakama hiyo ikiwa imaimarishwa na kufikia hatua ya kuweka vifaa maalumu vya kuwakagua watu wanaoingia katika mahakama hiyo.

Monday, February 2, 2015

SOMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 02 FEBRUARI, 2015 HAPA



















FRANCIS CHEKA AFUNGWA MIAKA MITATU JELA

Bondia maarufu nchini wa ngumi za kulipwa Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha miaka 3 jela na kutakiwa kulipa fidia ya shilingi millioni 1 kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi meneja wa baa yake iliyopo huko Morogoro.

Meneja huyo ajulikanaye kwa jina la Bahati inaelezwa alienda kudai fedha zake alizokuwa hajalipwa na bondia huyo wakati akifanya kazi ya umeneja katika baa yake hiyo ndipo Bondia huyo alikataa kumlipa na kumshushia kipigo.
 Francis Cheka akiwa amevaa mkanda wa ubingwa katika moja ya mapambano yake aliyo wahi kucheza na kushinda.
 Francis Cheka hapa akiwa anafanya mazoezi kabla ya mpambano.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU