Facebook Comments Box

Monday, February 16, 2015

MWADUI FC NA TOTO AFRICAN ZAKAMILISHA IDADI YA TIMU NNE ZILIZOPANDA LIGI KUU


MWADUI FC

Timu ya Mwadui yenye maskani yake Mwadui - Shinyanga imefanikiwa kurudi ligi kuu baada ya miaka 27 tangu iliposhuka daraja hilo. 

Timu hiyo inayofundishwa na Kocha JAMHURI KIWELU "JULIO ALBERTO" Imerudi ligi kuu baada ya kuichapa timu ya Bukinafaso kwa mabao 4-1 na kuongoza katika kundi lao kwa kufikisha point 46 kileleni huku Mshindi wa pili wakiwa wana kishamapanda Toto Africans wa Jijini Mwanza ambao nao walishinda mechi yao iliyopigwa katika uwanja wa CCM - KIRUMBA kwa kuwafunga Rhino Rangers mabao 2-0 na kufikisha point 45 baada ya kuongezwa point 3 za mechi iliyokwisha kwa vurugu ya Geita.

Kwa ujumla timu zilizopanda ligi kuu ni nne ambazo ni AFRICAN SPORTS(TANGA), MAJIMAJI(SONGEA), MWADUI FC(SHINYANGA) na TOTO AFRICANS(MWANZA). Ligi ya msimu ujao itakuwa na timu 16 baada ya kupanda hizo nne na kushuka timu mbili.




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU