Facebook Comments Box

Wednesday, July 24, 2013

VIDEO: ARSENAL WATOA POUND MILIONI 42 KWA AJILI YA SUAREZ




VIDEO: H BABA AKIWAAMBIA WASANII WAACHE ULIMBUKENI WA KUFUTURISHA




GONZALO HIGUAIN NA PEPE REINA WANAFANYA VIPIMO VYA AFYA NAPOLI SASA HIVI

Inaonekana Arsenal imepoteza nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa kiargentina Gonzalo Higuain ambaye imemuwania kwa muda mrefu baada ya mshambuliaji kukaribia kujiunga na klabu ya Napoli ya Italia.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.


Real Madrid na Napoli zimekubalina ada ya uhamisho wa Higuain kuwa kiasi cha £32million na kukubaliana na mchezaji mwenyewe mkataba wa miaka mitano kwa mshahara wa paundi 140,000 kwa wiki.




KIBONZO: HII NDIO I PHONE 20




AZAM FC KUFANYA ZIARA KAMA YA MANCHESTER CITY

935239_563553203685040_41751076_n 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Wana lambalamba Azam fc wanatarajiwa kuondoka  Agosti 2 mwaka huu kuelekea nchini Afrika kusini kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa mwakani ambapo watakaa kwa wiki mbili.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema wameamua kufanya ziara bondeni kwani wao wameendelea zaidi kisoka kwa maana ya kuwa na ligi bora, timu bora na mfumo wa kisasa wa kuendesha soka, hivyo watajifunza mambo mengi kutoka kwao.
Jafar alisema ziara hiyo itakuwa na manufaa makubwa sana kwani watacheza na klabu kubwa za huko wakiwemo Supersport United na Orland Pirates.
“Malengo yetu ni kufanya makubwa katika michuano ya kimataifa, lakini Ubingwa wa ligi kuu ni muhimu sana kwetu. Na ndio maana tunaenda Afrika kusini kuweka kambi ya wiki mbili”. Alisema Jafar.
Kuhusu usajili, Jafar alisema wao hawajasajili mchezaji yeyote mpaka sasa na hawana mpango wa kufanya hivyo kwani kikosi chao kipo kamili gado.
“Timu yetu ni nzuri sana, kusajili mara kwa mara kunaharibu timu, sisi tuna wachezaji wengi wakiwemo vijana wetu na ndio maana hatuhangaiki na usajili”. Alisema Jafar.
Wakati huo huo shirikisho la soka Tanzania, TFF, limethibitsha kupokea barua kutoka klabu ya Azam fc kuwa wanatarajia kuondoka nchini kuelekea Afrika kusini.
Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema Azam wamefanya vziuri kuwataarifu wao ili waende kwa kibali sahihi.


VIDEO MAWAIDHA: SHEIKH KIPOZEO - WANAWAKE WANAVYOHARIBU SWAUMU




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU