Facebook Comments Box

Wednesday, May 8, 2013

MANCHESTER UNITED WATHIBITISHA KUWA ALEX FURGESON ANASTAAFU BAADA YA MECHI YA WEST BROMWICH ALBION

Alex Ferguson quits as Man Utd manager
Baada ya miaka mingi ya kuifundisha manchester United kocha Alex furgeson anatarajiwa kustaafu mwaka huu na uamuzi wake huo utatangazwa na kupewa heshima ya mwisho pale Manchester United itakapo pambana na West Bromwich Albion. Alex Furgeson ameifundisha timu hiyo kwa miaka 26 na kuipa makombe ya ligi takribani 13.
Kocha huyo alisema nampongeza mkewe Cathy kwa kuwa nae bega kwa bega katika muda wote huo pamoja na binti yake

Isome habari hapo chini iliyonukuliwa kutoka website halali ya Manchester United:



Sir Alex retires

• Thirteenth league title in 26 years will be his last
• Most successful manager in English football history to become a director of Manchester United FC

NYSE: MANU.  Manchester, UK. Sir Alex Ferguson will retire at the end of the season, Manchester United announced today.
The most successful manager in English football history will bow out after the West Bromwich Albion game on 19 May and join the football club board.
Announcing his decision to retire, Sir Alex Ferguson said:
“The decision to retire is one that I have thought a great deal about and one that I have not taken lightly. It is the right time.
“It was important to me to leave an organisation in the strongest possible shape and I believe I have done so. The quality of this league winning squad, and the balance of ages within it, bodes well for continued success at the highest level whilst the structure of the youth set-up will ensure that the long-term future of the club remains a bright one.
“Our training facilities are amongst the finest in global sport and our home Old Trafford is rightfully regarded as one of the leading venues in the world.
“Going forward, I am delighted to take on the roles of both Director and Ambassador for the club. With these activities, along with my many other interests, I am looking forward to the future.
“I must pay tribute to my family, their love and support has been essential. My wife Cathy has been the key figure throughout my career,


RUGE AKIZUNGUMZIA SAKATA LA LADY JAY DEE




HII NDIO HABARI MPYA KUHUSU KESI YA LWAKATARE WA CHADEMA

 
Mahakama Kuu ya Tanzania imefuta mashtaka yote ya ugaidi yaliyokuwa yanamkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Wilfed Lwakatare. Taarifa kutoka Mahakama Kuu zinasema Mahakama Kuu imebakiza shitaka moja tu, la utekaji ambalo lina dhamana.


KINANA AJISAFISHA KUHUSU MENO YA TEMBO

 


Katibu Mkuu wa CCM ndg Abdulrahman Kinana amesema kinga ya Bunge isiwe sababu ya baadhi ya wabunge kutumia fursa hiyo kuchafua watu wasio na nafasi ya kujitetea ndani ya mhimili huo wa Dola.

Amehadharisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari  mjini Dodoma juzi kukanusha tuhuma zilizoelekezwa kwake binafsi na chama chake na Kambi ya Upinzani Bungeni.

Tuhuma hizo zilihusu shehena ya pembe za ndovu iliyokamatwa Vietnam mwaka 2009 ambazo aliziita za kupika na za uongo. "Tuhuma hizo hazina ukweli wowote, zina nia mbaya dhidi yangu na zimelenga kuniharibia taswira yangu na ya chama changu," alisema Kinana.

Alisema hahusiki vyovyote na tuhuma hizo na kutuhumu Kambi ya Upinzani Bungeni kwa kushindwa kujadili hoja za maana za maendeleo na badala yake kujihusisha na siasa za kuchafua heshima za watu.

"Bado nina nguvu na sijayumba kwa namna yoyote. Nina jukumu la kuilinda CCM na kutekeleza ahadi tulizozitoa kwa wananchi kupitia ilani ya uchaguzi," alisisitiza na kushangaa suala hilo la tangu mwaka 2009, kujitokeza sasa.

"Jibu ni jepesi, lengo ni kumvunja moyo Katibu Mkuu wa CCM ambaye CHADEMA inamwona tishio kwao," alisema Kinana na kusisitiza kuwa tuhuma dhidi yake hazina msingi na hata kambi ya upinzani inatambua kuwa mamlaka zote za ulinzi na usalama za ndani na nje zilimsafisha.

Kinana alisema baada ya shehena hiyo kukamatwa, Mamlaka ya Kimataifa ya Kudhibiti Wanyama Walio Hatarini Kutoweka (CITES) na Polisi wa Kimataifa (INTERPOL) walifuatilia na wakabaini kuwa hakuhusika.

Watuhumiwa walikamatwa na kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, akiwataja kuwa ni Eladius Colonerio (Mkurugenzi wa Team Freight (T) Ltd), Gabriel Balua (Meneja wa TEA Freight (T) Ltd) na Shaban Yabula (Mkurugenzi Mtendaji wa Kigoma M.N. Enterprises (T) Ltd).

Wengine ni Erick Morand (Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania katika bandari ya Dar es Salaam) Issa Lweno, Norbert Kiwale na Abubakari Omar Hassan.

Kinana alikana kumiliki meli yoyote na wala kujihusisha na usafirishaji wa nyara hizo za Serikali. Katika mkutano huo, alimtuhumu Msigwa kuwa na ajenda ya siri na kswamba aliamua kumtuhumu huku akijilinda kwa kinga za Bunge na akijua kuwa kufanya hivyo ni kutumia vibaya kinga hiyo.

Kinana amesema anaamini chanzo cha kuchafuliwa kwake na wapinzani ni wadhifa wake.

Kinana alisema anaamini kuwa kama asingekuwa na wadhifa huo, asingesakamwa kwa tuhuma alizoziita za uzushi.

“Hivi vitu havinisumbui. Hapa tatizo ni kuwa Katibu Mkuu wa CCM. ‘I am a senior officer’ (Ofisa Mwandamizi) sasa katika chama changu kama ningekuwa nimekaa nyumbani nafanya biashara zangu yasingetokea haya.

“Nataka kuwaambia tu, waelewe kuwa hawawezi kunitoa katika ajenda yangu ya msingi. Hii ni sawa na mwanajeshi anayekwenda kupigana vita na adui halafu akawa na vikundi vidogo vinakushambulia kutoka kila upande kukutoa katika lengo la msingi... ni lazima mtu ukomae na ili ufanikiwe,” alisema Kinana.

Alisema Msigwa alikuwa katika Kamati ya Ardhi na Maliasili ya Bunge tangu mwaka 2010 na ukweli wa mambo hayo anaujua... “Msigwa anajua kabisa nikiwa kama ‘shipping agent’ (wakala wa meli), sihusiki na kujua kilichopo ndani ya kontena. Wale wanaopaswa kujua ni meneja wa bandari, mamlaka ya mapato, walinzi na wakala wa kupakia na kupakua mizigo, kwa kuwa wao ndiyo wanafanya ukaguzi na kuweka seal (lakiri) …siyo kazi yetu,” alisema.

Alipoulizwa kwa nini hajachukua hatua za kisheria kama anaona amechafuliwa na kama tuhuma hizo hazina ukweli? Kinana alijibu kuwa anajua kuna njia tatu za kuchukua kuhusiana na tatizo hilo lakini bado anazifanyia kazi.

“Kwanza unaweza kujieleza kwenye vyombo vya habari. Pia unaweza kukata rufaa kwa Spika na kesi yako kusikilizwa lakini pia unaweza kwenda mahakamani. Bado natafakari cha kufanya.”

---
Taarifa hi imenukuliwa kutoka kwenye magazeti ya HabariLeo na Mwananchi.



KIBONZO: KIPANYA KUHUSU YANAYOJIRI SASA TANZANIA



MLIPUKO WA BOMU KANISANI: PENGO AFICHUA SIRI

 
Kadinali Pengo alisema amepata taarifa kutoka kwa watu ambao hana na shaka nao.
“Jana (juzi), niliongelea kwamba suala zima la tukio la Arusha halihusiani na imani yoyote ya kidini. Tamko hilo nilitamka kutokana na taarifa nilizofikishiwa na watu ambao sikuweza kuwa na shaka kwamba wanaoniambia ni kweli na sidhani kama ningekuwa na sababu ya kusema wamefika kwa kunidanganya kwa hiyo tamko litakuwa limesimama juu ya msimamo huo,” alisema Kadinali Pengo na kuongeza:
“Lengo la msingi kabisa, langu na la kanisa ni kwamba tukio lolote lile liwe kwa nia mbaya au nzuri kwa upande wetu isiwe ni sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu wa amani katika nchi yetu,” alisema Pengo.
Alisema kuwa kila anayehusika ajue amani ya kweli ya taifa lolote haiwezi ikapatikana isipokuwa ikijengwa juu ya ukweli na ukweli kabisa bila kufuta au kujaribu kupotosha ukweli kwa namna yoyote ile.
“Tusipojua kusema ukweli ulivyo hatuwezi kufaulu kuleta amani katika taifa letu. Kwa hiyo pamoja na kuendelea kuwaomba waumini wa Katoliki pamoja na watu wenye mapenzi mema kuendelea kumwomba Mwenyezi Mungu arehemu taifa letu na mapambano ya aina yoyote ile. Tuendeleze nia yetu njema ya kusema ukweli, haidhuru ukweli huu unamgusa nani,” alisema Pengo.
Alisema kujaribu kuficha ukweli na kupotosha ni njia sahihi kwa ibilisi kuleta vurugu katika jumuiya ya watu na ieleweke hivyo.
“Naomba kila mtu akubaliane na tamko langu haidhuru pana kosa, amani ya taifa letu ni jambo la msingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusema ukweli kama ulivyo,” alisema.
Mwingine afariki, 20 wakutwa na vipande vya chuma miilini
Katika hatua nyingine, majeruhi mmoja katika shambulio hilo lililotokea Jumapili iliyopita, amefariki dunia juzi jioni na kufikisha idadi ya waliopoteza maisha kufikia watatu.
Aliyefariki ni mtoto wa miaka tisa, Patricia Joachim ambaye alikuwa amehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi. Wengine waliofariki katika tukio hilo ni Regina Losyoki (45) na James Gabriel (16).
Mazishi ya watu hao watatu yamepangwa kufanyika katika eneo la kanisa hilo Ijumaa.
Katika hatua nyingine, majeruhi 20 wamebainika kuwa na chembechembe za vyuma walivyopata katika shambulio hilo. Hao ni miongoni mwa majeruhi 42 waliolazwa hadi sasa kwenye hospitali mbalimbali za Arusha.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk Thomas Kway alisema majeruhi hao 20 wamedhuriwa na chembechembe za vyuma vya mabomu na baada ya miili yao kubainika kuwa na vyuma vyenye urefu hadi wa sentimita tisa.
Dk Kway alisema hayo wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipofika katika hospitali hiyo kuwafariji majeruhi hao.

SOURSE: MWANANCHI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU