Facebook Comments Box

Sunday, September 1, 2013

KIBONZO: HIKI KIMETENGENEZWA BAADA YA TOTTENHAM KUFUNGWA NA ARSENAL




PICHA: LIVERPOOL WATOA KIPIGO KWA MANCHESTER UNITED; ARSENAL WATOA KIPIGO KWA TOTTENHAM

David Beckham na watoto wake Cruz, Romeo na Brooklyn wakiangalia Arsenal wakitoa kipondo


Olivier Giroud akishangilia baada ya kutupia goli la kwanza dakika ya 22

Wojciech Szczesny akishangilia goli

Olivier Giloud akifunga goli mbele ya walinzi wa Tottenham

Santi Cazorla akimtoka  Paulinho



Kocha wa Tottenham Andre Villas-Boas akitoa maelekezo kwa wachezaji wake

Etienne Capoue akitolewa nje baada ya kuumia kifundo cha mguu. Mechi hiyo iliisha kwa Tottenham kufungwa goli moja na Arsenal
 
BAO pekee la Daniel Sturridge limeipa Liverpool ushindi wa tatu mfululizo katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuwalaza wapinzani wao wa jadi, Manchester United 1-0 jioni hii Uwanja wa Anfield.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alikuwa katika sehemu mwafaka na kwa wakati mwafaka wakati anaunganishia nyavuni mpira wa kona dakika ya nne.
Hilo lilikuwa bao la tatu kwa Sturridge katika msimu huu na linaipa ushindi wa tatu mfululizo wa 1-0 timu ya Brendan Rodgers kuendeleza redeki ya ushindi asilimia 100 katika mbio za ubingwa.
Philippe Coutinho wa Liverpool alikuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Kikosi cha Liverpool kilikuwa: Mignolet; Johnson/Wisdom dk78, Agger, Skrtel, Enrique, Henderson, Lucas, Gerrard, Aspas/Sterling dk60, Sturridge na Coutinho/Alberto dk84. 
Man United: De Gea, Jones/Valencia dk37, Ferdinand, Vidic, Evra, Carrick, Cleverley/Young/Nani dk62, Welbeck, Giggs/Hernandez dk75 na Van Persie. 
Liverpool's Daniel Sturridge
Tatu: Liverpool imepata ushindi wa tatu mfululizo katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuifunga Manchester United 1-0 Anfield
Flying start: Daniel Sturridge gave Liverpool the lead with a header in the fourth minute
Ameanza na moto: Daniel Sturridge ameipa Liverpool ushindi kwa bao pekee dakika ya nne
Right place: Sturridge flicked home Daniel Agger's header from two yards
Sehemu mwafaka: Sturridge akiunanisha pasi ya Daniel Agger
On form: Sturridge has scored in all four of Liverpool's matches this season
Yuko moto: Sturridge ameifungia Liverpool katika mechi zote tatu msimu huu
Embrace: Sturridge hugs manager Brendan Rodgers after giving Liverpool the lead
Shangwe: Sturridge akimkumbatia kocha wake Brendan Rodgers baada ya kufungaStunning: Liverpool fans at the Kop End made a stunning mosaic in honour of Bill Shankly before kick-off
Imependeza: Mashabiki wa Liverpool katika Kop End wakitoa heshima kwa Bill Shankly kabla ya mechi
Birthday: Players and fans took part in a minute's applause for Shankly a day before he would have turned 100
Kuzaliwa: Wachezaji na mashabiki walitumia dakika moja kwa ajili ya Shankly kabla ya mechi
Fiesty: Steven Gerrard and Robin van Persie share their thoughts with each other
Mkwara: Steven Gerrard na Robin van Persie wakichimbiana mikwara
Physical: Martin Skrtel, who replaced the injured Kolo Toure, rises high to win a header
Kazi: Martin Skrtel, aliyechukua nafasi ya majeruhi Kolo Toure, akiruka juu kupiga mpira kichwa
Effort: Gerrard attempts a shot on goal from a free-kick, which was saved by David de Gea
Jatibio: Gerrard akipiga shuti la mpira wa adhabu ambalo liliokolewa na kipa David de Gea
Fall: Danny Welbeck takes a tumble after pressure from Lucas and Iago Aspas
Rafu: Danny Welbeck akienda chini baada ya kuchezewa rafu na Lucas na Iago Aspas
Spectator: England manager Roy Hodgson was in the stands for the clash at Anfield
Alikuwepo: Kocha wa England, Roy Hodgson alikuwapo jukwaani Anfield kushuhudia mechi hiyo
Sidelined: Liverpool's suspended striker watches the action at Anfield on Sunday
Jukwaani: Mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez anayetumikia adhabu alikuwepo uwanjani leo
In the dugout: Liverpool manager Rodgers (right) and Manchester United boss David Moyes
Makocha: Kocha wa Liverpool, Rodgers (kulia) na wa Manchester United, David Moyes wakiwa kazin

MAJAMBAZI YAJERUHI NA KUIBA FEDHA MBEZI AFRIKANA

Difenda la Polisi likiondoka eneo la tukio na mmoja wa viongozi wa kampuni hiyo aliyejeruhiwa.
Geti la kampuni ya Diab Furniture Manufacturing iliyovamiwa na majambazi.


Mke wa mlinzi aliyejerujiwa na majambazi akiwa getini na mwanaye. Kundi la majambazi waliokuwa na silaha za moto wakiwa na magari mawili Landcruiser na Noah wamevamia kampuni inayojishughulisha na utengenezaji na uuzaji wa fenicha ya Diab Furniture Manufacturing Company iliyopo Mbezi Afrikana jijini Dar es Salaam. Majambazi hayo baada ya kuvamia eneo hilo yalifanikiwa kupora sefu iliyokuwa na fedha pamoja na kuwajeruhi mmoja wa viongozi wa kampuni hiyo na mlinzi. (Picha / Habari: Haruni Sanchawa / GPL)


KUMBUKUMBU: BOMU LAUA WANNE BUKOBA

Mmoja wa majeruhi wa bomu la shule ya msingi Tumaini Mwaka 1994, Datius Kalokola hospitalini na baada ya kurudi nyumbani


Ni kichwa cha habari iliyotoka kwenye gazeti flani siku ya alhamisi tarehe 1 Septemba 1994, siku moja  baada ya kutokea mripuko wa bomu katika shule ya msingi Tumaini iliyoko Manispaa ya mji wa Bukoba. Ilikuwa  Jumatano  31 Agosti  1994 majira ya saa mbili asubuhi tarehe kama ya leo, tulipowapoteza wanafunzi  wanne huku 85 wakiwa wamejeruhiwa kutokana na ajari hiyo. Nianze kwa kuwakumbuka wenzetu waliotutoka siku hiyo. Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi Ibrahim Mebu, Salehe Abdalah, Yusuph Bahati na Emmanuel Joseph.

Tukiwa tumejipanga mistari “parade” tayari kukaguliwa ili tuanze gwaride  kuelekea madarasani, mara nikasikia kishindo kikubwa kilichoambatana na hali ya mtikisiko. Hali iliyomfanya kila mwanafunzi akimbie pasipo kujua jambo gani limetokea. Baada ya kukimbia umbali wa takribani mita 15 kutoka eneo la tukio ghafra nikahisi kuishiwa nguvu mguu wangu wa kushoto, niliposimama na kugeuka nyuma nikaona idadi ya wanafunzi wasiopungua sita wakiwa wamedondoka chini eneo la tukio.Nilipotizama mguu wangu ulikuwa ukitokwa na damu nyingi.Nilipata mshtuko na mshangao mkubwa  huku nikiwaona wanafunzi wengine pia wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao. Walimu walitahamaki wasijue wafanye nini zaidi ya kutuambia wanafunzi tuliokuwa bado tuko ndani ya mazingira ya shule tulale chini. Wakati huo wengi wetu wakiwa hawaonekani kabisa katika mazingira hayo ndani ya muda mfupi wengine pasipokujua kama wamepatwa na majeraha na wengine wakikimbia kuelekea nyumbani kwao huku wakilia sana na damu zikiwatoka.

Nikiwa kwenye gari l a Msalaba Mwekundu na  majeruhi wengine kuelekea hospitali, tulikutana na baadhi ya wanafunzi wakirudi shuleni baada ya kufika nyumbani na kugundua hawako pamoja na ndugu zao ambao walikuwa nao shule moja. Hali ya utulivu ilipotea ghafla ndani ya mji wa Bukoba na hasa kutokana na taarifa zilizowafikia wazazi  wa wanafunzi ambao walikuwa wakijiandaa kwenda kazini na wengine wakiwa tayari wamefika maeneo yao ya kazi. Hakuna mwanafunzi wa shule ya jirani aliyesubiri kupewa ruhusa ya kwenda nyumbani na mwalimu wake hasa pale wanafunzi wa shule ya msingi Tumaini walipoonekana wakipita karibu na shule hizo wakibubujikwa  machozi huku wakiwa na alama za damu kwenye mashati na magauni yao ya shule na wengine wakitoa taarifa kwamba ndugu zao au marafiki zao wamepoteza maisha kwa sababu hawaonekani.
Tukiwa katika chumba maalum kilichoandaliwa kwa ajiri ya kupokea majeruhi wa ajari hiyo, dakitari alimwambia nesi mmoja amtizame mwenzetu ambaye aliletwa akiwa hajitambui.Alikuwa amelazwa chini pembeni yangu. Baada ya nesi huyo kutekeleza agizo hilo kwa kutumia kipimo ambacho alimuwekea kifuani, nilishuhudia mama huyo nesi akimwaga chozi bila kujizuia. Kumbe huo ndiyo ulikuwa mwisho wa kijana mpole Yusuph Bahati amabaye tuliwai kuishi jirani maeneo ya Kashai. Wakati huo nimeshafahamu kwamba kilichotokea ni mlipuko wa bomu.

Jioni ya siku hiyo baada ya kutolewa kwenye chumba cha upasuaji ndani ya Hospitali ya Mkoa  Kagera, nilijikuta ndani ya wodi namba 4 ya hospitali hiyo pamoja na wanafunzi wengine wengi.Wodi mbili za hospitali hiyo ambazo ni wodi namba 4 na namba 5 zilipokea majeruhi wa ajali hiyo na wagonjwa waliokuwa humo kabla ya ajari wakahamishiwa vyumba vingine. Nakumbuka tulilazwa wanafunzi wawiliwawili kitanda kimoja kwa siku hiyo ya kwanza. Kupitia maongezi ya siku hiyo, nikafahamu kwamba wametutoka wenzetu wanne kutokana na ajari hiyo akiwemo Ibrahim Mebu ambaye alifariki papo hapo.Huyu pamoja na mwingine aliyeitwa Salehe Abdarah tulikuwa wote darasa la nne, wakati Yusuph Bahati na Emanuel Joseph wakiwa darasa la tano.

Kutokana na maelezo yaliyotolewa na baadhi ya wanafunzi ,bomu hilo liliokotwa jalalani na mwanafunzi mmoja ambaye hakufahamika  kwa jina, akamuuzia Ibrahimu Mebu shilingi ishirini, wote pasipokujua kama ni kitu cha hatari. Ibrahimu alikaa nalo kwa takribani siku saba akija nalo darasani na kurudi nalo nyumbani kabla halijaripuka.Kilichosababisha bomu hilo kuripuka ni baada ya kulifungua ikiwa ni katika hali ya michezo pasipo kujua ni kitu gani kitatokea.

Shukurani za dhati ziwaendee wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera na Bugando ya Mwanza kwa jinsi walivyojitoa usiku na mchana kuhudumia majeruhi na hasa wale waliokuwa na hali mbaya sana akiwemo Benedict Nshegize. Nawashukuru pia askari wa jeshi la ulinzi waliofika shuleni hapo kuwaonesha wanafunzi aina na maumbo tofauti ya vitu vya hatari kama hivyo ili wanafunzi wasivisogelee pindi wavionapo na ikibidi kutoa taarifa mahali panapotakiwa. Shukurani kwa mkuu wa mkoa aliyekuwepo kwa kipindi hicho Mzee Philip Mangula kwa ukaribu na msaada aliyoutoa, wazazi, walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Tumaini na shule za jirani.

Kama msimamizi wa gazeti tanzu hili la Semadat (Semadat Blog) na mwandishi wa kumbukumbu hii ,nikiwa pia  miongoni mwa waliokuwa majeruhi wa ajari hiyo, natoa shukurani za pekee kwa wazazi wangu, baba yangu mzazi Mzee Felix Kalokola ambaye kwa sasa ni marehemu, mama yangu mzazi Bi.Philotea Kalokola, Baba mkubwa Mzee Petro Buberwa na mjomba wangu maarufu kama  Dr.Lugenga, wa Hospitali ya Mkoa Kagera. Pia namkumbuka babu yangu marehemu Philadelph Kamanzi ambaye aliendesha baiskeli jioni ya siku hiyo, akiwa na huzuni kubwa kutoka Kijijini Kasharu na kufika mjini Bukoba usiku baada ya kupata taarifa ambazo ni tofauti kidogo kwamba bomu hilo limeangamiza wanafunzi wote wa shule ya msingi Tumaini.

Sina cha kuwalipa ndugu  na marafiki zangu mlionipa huduma kwa kipindi cha takribani miezi miwili nikiwa hospitalini hatimaye nikapona na kurudi shule, hata nikaweza tena kuungana na wanafunzi wenzangu kucheza mpira muda wa mapumziko.
Namshukuru Mungu na namuomba awasaidie wanafunzi wote Tanzania, Afrika na Ulimwengu mzima, hasa wa shule za awali na msingi kuepukana na majanga kama haya.

Miaka 7 mpaka 10 baada ya tukio hilo (Kidato cha nne na cha sita)



ANGALIA JINSI VIDEO YA WIMBO MPYA WA DIAMOND UTAKAVYOKUWA




YUSSUF HIMID ALIEFUKUZWA CCM ATOA MSIMAMO WAKE





Aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kiembe Samaki Mansour  Yusuf Himid akielezea msimamo wake baada ya kufukuzwa Uanachama CCM ambapo amesema haendi Mahakamani kupinga uamuzi wa Chama, katika ukumbi wa Salama hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar)
 
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 
 
Aliyekuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilisihi Jimbo la Kiembe Samaki (CCM) Mansour Yussuf Himid amesema licha ya kufukuzwa Uanachama katika chama hicho hatoenda Mahakamani kutetea nafasi hiyo kwani kufanya hivyo ni kukaribisha Malumbano ambayo hayana tija.
 
Amesema kwenda kupinga uamuzi huo Mahakamani ni kuhalalisha yeye kuwa Mwakilishi wa Mahakama badala ya Wananchi jambo ambalo hapendelei kutokea katika maisha yake.
Mansour ameyasema hayo leo katika Kongamano la Kamati ya Maridhiano lililofanyika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar.
 
Amesema amekuwa akiulizwa Maswali mengi na Watu tofauti kuhusu mustakabali wake kisiasa baada ya kufukuzwa uanachama na kuongeza kuwa hana Pesa za kuchezea kwenda kupinga uamuzi wa Chama cha Mapinduzi Mahakamani.
“Wenzangu wamenipima na wameniona sifai ni haki yao, siendi Mahakamani, sina pesa za kuchezea wala sitaki kuwa Mwakilishi wa Mahakama” Alisema Mansour
Mansour aliyejiunga CCM mwaka 1987 alienguliwa Uanachama siku za karibuni kutokana na Kamati kuu ya Chama CC kuridhika na madai ya kwenda kinyume na misimamo ya Chama pamoja na kushindwa kuitetea Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mansour ameongeza kuwa kwenda Mahakamani ni kukaribisha malumbano na kusisitiza kuwa Waungwana hawalumbani hivyo ameamua kukaa pembeni.
Amedai kwamba baada ya kufukuzwa uanachama CCM vyama tofauti nchini vimejitokeza kuzungumza naye ili ajiunge navyo na kudokeza kuwa bado hajaamua ni Chama gani ataenda hadi pale muda utakapofika kufanya hivyo
Mansour amesisitiza kuwa hata kama Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC itaitisha uchaguzi mdogo katika Jimbo la Kiembesamaki yeye hatogombea na kwamba anaweza kufanya hivyo ifikapo mwaka 2015.
 
Ametumia fursa hiyo pia kuwaomba Radhi wana Jimbo la Kiembe Samaki alilokuwa akiliongoza toka 2005 na kuwashukuru Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliomsaidia katika kupindi chake chote cha Uongozi.
 
Akigusia suala la Muungano Mansour amesema ataendelea na harakati zake kusimamia maslahi ya Zanzibar  ili kuona mchakato wa Katiba Mpya unakuja na Katiba yenye Muundo wa Muungano wa Haki na Usawa baina ya Tanganyika na Zanzibar.
Awali katika Kongamano hilo Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Mzee Hassan Nassor Moyo alimshukuru Rais Kikwete kwa ujasiri wa kuleta mchakato wa Katiba Mpya na kusisitiza kuwa Kamati yake itaendelea kudai Muungano wa usawa na haki.
 
Mzee Moyo amedai kuwa Kamati yake haihitaji kutambuliwa na Watu wengine na kwamba inatosha kujulikana na Wananchi ambao wanafahamu wajibu wa Kamati hiyo.
Itakumbukwa kwamba kabla ya Kongamano hilo Chama cha Mapinduzi kilitoa taarifa kwa Vyombo vya habari kuhusu kutoitambua Kamati hiyo inayoongozwa na Mzee Moyo akisaidiwa na Makamo wake Aboubakar Khamis Bakar.
 
Katika hatua nyingine Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye alikuwa pia Mwanachama wa Chama cha Mapinduzi Eddy Riyami alitangaza kujiengua na Chama hicho na kusema kwa sasa yupo huru bila Chama chochote.
Kabla ya Kongamano hilo Kamati hiyo pia iliwasilisha maoni yake kwa Tume ya Katiba mpya ambapo maoni yake yalijikita katika kuifanya Zanzibar kuwa na Mamlaka yake kamili ndani ya Mfumo wa Muungano


JESHI LA POLISI LATOA TAMKO KALI KWA WAPIGA PICHA ZA UTUPU


Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni limetoa kauri nzito kuhusu picha za udhalilishaji zilinazosambazwa na wasanii  na baadhi ya watu hapa nchini..

Akiongea katika mahojiano maarumu mkuu wa kituo cha Polisi Oysterbay “OCD” Mtafungwa alisema kuwa kimsingi kupiga picha za utupu ni kosa kisheria hivyo endapo muhusika akimatwa atashtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Mtafungwa aliendelea kufafanua na kusema kuwa "Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kusimamia sheria iliyowekwa na serikali hivyo huwa kuna namna ya kuwakamata wahusika hasa kama kumetokea malalamiko toka idara flani kuhusiana na matukio yoyote yanayopelekea uvunjifu wa amani au kupotosha maadili” Alisema Kamanda huyo kipenzi cha watu

Aidha Kamanda huyo aliendelea kufafanua “ Pia Jeshi la polisi linamamlaka ya kumkamata mharifu yeyote kwa muda wowote endapo kipindi hicho akikutwa anafanya uharifu ni pamoja na upigaji picha hizo chafu, Lakini kubwa tuhajitaji kumkata mtu na ushahidi ili iwe rahisi kumbana na kumfikisha mbele ya sheria” Alisema

Mtafungwa alimaliza kusema Pindi tupatapo taarifa kuhusuiana na picha hizo chafu “ Tutaendelea kufatilia kupita mitandao ya kijamii ili kuona hizo picha zikoje halafu kuwatolea taarifa hadharani kupita kwa msemaji wa Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni RPC Wambura ambae kisheria ndiye mwenye mamlaka ya kusema” 
na kumchukulia hatua kali mpigaji wa picha hizo.
Alisema Mtafungwa


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU