Facebook Comments Box

Tuesday, July 23, 2013

PICHA ZA IKULU LEO RAIS KIKWETE AKIWA NA TONY BLAIR











SOMA WASIFU WA KOCHA MPYA WA BARCELONA

FC Barcelona imefikia makubaliano rasmi kumsaini Gerardo Martino kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, kwa mujibu wa mtandao rasmi wa FC Barcelona.
  
Kilichobakia kwenye makubaliano hayo ni kusaini mkataba baada pande zote mbili kukubalina kila kitu.

Ratiba rasmi ya kuwasili kwake Nou Camp, utiaji saini wa mkataba na kutambulishwa rasmi itatangazwa msaa kadha yajayo. 

Gerardo ambaye anajulikana kama ‘Tata’, alizaliwa jijini Rosario (Argentina) November 20, 1962. Ana uzoefu mkubwa wa soka la America ya Kusini, kwanza kama mchezaji na baada kama kocha, kazi yake ya mwisho ilikuwa kuiongoza klabu ya Newell's Old Boys, ambao alishinda nao ubingwa wa mwaka huu.

Gerardo Martino anakuwa kocha wa nne raia wa Argentina kuifundisha FC Barcelona baada ya Roque Olsen, Helenio Herrera na César Luis Menotti.

WASIFU WA KOCHA GERARDO MARTINO TATA

 
SOURSE:SHAFFIH DAUDA


VIDEO: MWANAMKE WA MIAKA HAMSINI AKISUKUMA MKOKOTENI ILI KUJIKIMU




OCD: MSIWAPE MAJAMBAZI DAWA ILI WASIKAMATWE WAPENI POLISI DAWA ILI WAWAKAMATE

Inaripotiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Polisi katika wilaya ya Mufindi, PCD Ambwene Manyasi amewataka waganga wa jadi kuacha mara moja kuwapatia majambazi dawa za kutokukamatwa na polisi, na badala yake waganga hao wawapatie askari polisi dawa za kuwaona na kuwakamata wahalifu.

Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.

OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:

"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutubu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."

Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.

OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.



KIBONZO: KIPANYA NA KODI MPYA YA SIMU

Picture: SIM Card Tax


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU