Facebook Comments Box

Friday, July 5, 2013

MKE WA MANDELA AELEZEA HALI YA MUME WAKE


 

Johannesburg. Mke wa Nelson Mandela, Graca Machel kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuzungumzia hali ya kiafya ya mumewe kwamba kuna wakati anazidiwa lakini hajambo.

Graca alisema hayo jana kwenye sherehe za uzinduzi wa siku ya Utamaduni na Michezo ya Nelson Mandela iliyofanyika kwenye Kituo cha Kumbukumbu ya Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini.
Alieleza sababu za kuhudhuria sherehe hizo kwamba kubwa ni kuwashukuru kwa kuwa pamoja na kumwombea afya njema Mandela tangu alipolazwa hospitali Juni 8, mwaka huu.
Graca alisema pamoja na kwamba Mandela amelala akiugua hospitali, lakini ameendelea kutoa zawadi kwa wanajamii wote ya kuwaunganisha pamoja, ambayo ni michezo na utamaduni.
“Madiba kuna wakati hayuko vizuri. Wakati mwingine anakuwa na maumivu. Lakini hajambo,” alinukuliwa Graca akizungumza katika sherehe hizo.
Katika hatua nyingine mjini Pretoria, Rais Jacob Zuma juzi alisema kuwa hali ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela bado ni mbaya na hakuna mabadiliko.
Rais Zuma alisema hayo baada ya juzi (Jumatano) jioni kwenda hospitali kumjulia hali Mandela, ambapo alikuwa na msafara mkubwa.
Kiongozi huyo pia aliwaomba wananchi wa Afrika Kusini kutenga dakika 67 kwa ajili ya Siku ya Mandela ya Julai 18, ambayo ni siku yake ya kuzaliwa.
Alisema kauli mbiu ya siku hiyo ni “Chukua hatua; penda mabadiliko; fanya kila siku iwe siku ya Mandela kwa kujielekeza katika masuala ya chakula, makazi na elimu.
Wakati huohuo, kumekuwa na hali ya utulivu katika eneo la Hospitali ya Medi-Clinic aliyolazwa Mandela, tofauti na ilivyozoeleka kuwa na pilikapilika nyingi.
Kwa mujibu wa taarifa, watu wanaopita eneo hilo la hospitali wamekuwa wakionekana wakiwa na hali ya utulivu, huku wengine wakipiga picha kwenye kadi, maua, bendera, vipeperushi na mabango yaliyowekwa kandokando ya hospitali hiyo, yakiwa na ujumbe wa kumtakia nafuu ya kuumwa Madiba.
Wakati hali hiyo ikiendelea kutokea mjukuu wa Mandela, Mandla Mandela ameendelea kuikoroga familia hiyo, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari akidai kushangazwa na mahakama ilivyoharakisha kesi hiyo kuhusu mvutano wa sehemu ya kuzikwa Mandela na siyo miaka miwili iliyopita baada ya yeye kufukua makaburi.

SOURSE: MWANANCHI


MAGUFULI: NINA UTAMANI URAIS


.
Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya serikali. 

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ifikapo mwaka 2015. 

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge. 

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani. 

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba, Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita  kuendelea na wadhifa huo. 

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,” alisema Dk. Magufuli. 

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama wazee, ninaahidi kuwapa Sh.   3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema. 

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha uvumi huo. 

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa  ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania nafasi hiyo.
SOURSE: MWANANCHI


RYAN GIGGS AND PHIL NEVILLE JOIN MAN UTD COACHING STAFF


Picture
L-T: Neville, Giggs
via BBC Sports -- Manchester United have named Ryan Giggs as player-coach and Phil Neville as their new first-team coach.

Giggs, who will be 40 in November, and ex-United player Neville, 36, are the latest additions to new manager David Moyes's backroom team at Old Trafford.

"I'm delighted that Ryan has accepted the chance to become player-coach," said Moyes.

Giggs added: "It's no secret I've been taking my qualification. I see this as the first step in my future career."

Neville, 36, takes up the role vacated by Rene Meulensteen, who has now joined manager Guus Hiddink at Russian club Anzhi Makhachkala.

Giggs continued: "It's a great privilege to be appointed as player-coach. I hope I will be able to bring my experience to bear, having been both a player and part of the Manchester United family for so long.

"I'm really looking forward to working alongside David and the team."

Moyes, who was announced as Sir Alex Ferguson's successor in May, will conduct his first news conference as manager of United on Friday at 16:00 BST.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU