Facebook Comments Box

Saturday, October 18, 2014

RENAMO YAPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI MSUMBIJI




Raia wa Msumbiji walipiga kura kumchagua rais mpya na vile vile wabunge. Chama cha Frelimo, ambacho kimeiongoza nchi hiyo tangu ilipojinyakulia uhuru mwaka 1975, kimeshindana na chama cha upinzani, Renamo.

Kulingana na matokeo chama tawala kimeshinda uchaguzi huo ingawa upinzani Renamo unasema haukubali matokeo hayo ya uchaguzi uliofanyika Jumatano. Ulikuwa uchaguzi wa Rais na wabunge.

Msemaji wa Renamo anasema kuwa uchaguzi huo ulikumbwa na visa vya udagngayifu huku wapiga kura wakitishwa.
 AFONSO DHLAKAMA

Kiongozi wa Renamo, Afonso Dhlakama, alijitokeza kutoka mafichoni mwezi uliopita, na kuamua kuwania urais, baada ya mapatano ya amani kati ya chama chake na serikali.

 FILIPE NYUSI

Mgombea wa chama kilicho madarakani ni Filipe Nyusi, aliyekuwa wakati mmoja waziri wa ulinzi.

Chanzo:Bbc


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU