Facebook Comments Box

Saturday, December 1, 2012

RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI YALIYOFANYIKA KITAIFA MKOANI LINDI LEO


Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu Mjini Lindi, huku wadau mbalimbali wa masuala ya mapambano ya ukimwi wakishiriki kwa kufanya maonyesho na kutoa elimu na maelezo mbalimbali yanayohusu mapambano ya ukimwi, Rais Pia ameshuhudia utiwaji saini wa msaada wa Dola za Kimarekani Milioni 308 kutoka mfuko wa Global Fund uliosainiwa kati ya Katibu katibu wa Ofisi ya rais Paniel Lyimo na Ramadhan Kijahkati Kabu Mkuu Wizara ya Fedha huku Mfuko wa Global Fund ukiwakilishwa na Christoph Benn Mkurugenzi wa mfuko huo. 
Christoph Benn Mkurugenzi wa mfuko Global Fund akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani iliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi.
Rais Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya wananchi wa mkoa wa Lindi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani iliyofanyika mjini Lindi leo . kutoka kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Mkurugenzi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi TACAIDS Fatuma Mrisho na kushoto ni mkuu wa mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila
Rais Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya wananchi wa mkoa wa Lindi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani iliyofanyika mjini Lindi leo . kutoka kulia ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Hussein Mwinyi, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Mkurugenzi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi TACAIDS,Fatuma Mrisho. 
Rais Jakaya Kikwete akishuhudia Utiwaji wa Saini wa msaada wa dola za Kimarekani milioni 308 kwa ajili ya mapambano ya Ukimwi nchini, mkataba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Paniel Lyimo kushoto na Ramadhan Kijah katikati, kulia ni Christoph Benn mkurugenzi wa Mfuko wa Global Fund, waliosimama nyuma kushoto ni Mkewa Rasi Mama Salma Kikwete, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi na kulia ni Ursula Muller Mjumbe wa bodi ya The Global Fund,
Rais Jakaya Kikwete akiongozana na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiingia kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi tayari kwa kushiriki katika maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani ambayo yamefanyika mkoani Lindi kitaifa.kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa TACAIDS Fatma Mrisho na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila
Rais Jakaya Kikwete akimuonyesha jambo Mkurugenzi wa tume ya kudhibiti Ukimwi Fatma Mrisho wakati alipotembelea mabanda mbalimbali katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani mjini Lindi leo.
Rais Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Bw.Rajab Mwenda afisa masoko wa Mpango wa damu Salama wakati alipotembelea katika banda hilo kwenye maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani mjini Lindi leo.
Baadhi ya viongozi wa Dini na waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika maadhimisho hayo wakifuatilia kwa karibu matukio yaliyokuwa yakiendelea katika maadhimisho hayo.
Waheshimiwa viongozi wa serikali na baadhi ya wabunge wakiwa katika maadhimisho hayo kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi.
Mwakilishi wa mfuko wa bima ya Afya ya Jamii mjini Lindi NHIF Bi. Fortunata Raymond wa tatu kutoka kulia akiongoza maandamano ya wafanyakazi wa mfuko huo katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani.
Kikundi cha matarumbeta kikiongoza maandamano hayo yaliyokuwa yakipita mbele ya Rais kwenye uwanja wa Ilulu leo mjini Lindi.
Kikundi cha kuigiza kutoka mfuko wa bima ya afya ya Jamiii NHIF kikiwapa ujumbe wananchi wqa mkoa wa Lindikuhusu maambukizi ya ukimwi
Kikundi cha ngoza za asili kutoka mkoani Lindi kkitumuiza katika maadhimisho hayo yaliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi


KILI STARS YASHINDA 7-0: ANGALIA PICHA HAPA

Kikosi cha Bara, Kilimanjaro Stars kilichofuzu kuingia Robo Fainali ya michuano ya CECAFA Tusker Challenge, baada ya kuilaza Burundi mabao 7-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Lugogo mjini Kampala, Uganda leo.

Ngassa baada ya kufunga la kwanza

Salum Abubakar akimiliki mpira mbele ya kiungo wa Somalia

Bocco akipiga kichwa mpira kwenye lango la Somalia

Kapombe akifanya kazi yake

Ngassa akimiliki  mpira mbele ya beki wa Somalia

Kipa wa Somalia akiokoa moja ya hatari langoni mwake

Kocha Poulsen

Wachezaji wa aStars Mwinyi Kazimoto kulia na Amir Maftah wakiwa na rafiki yao jukwaani

Amri Kiemba akimpongeza Ngassa kufunga 

John Bocco akimburuza Msomali

Bocco akifanya vitu, angalia miguu

Bocco anapongezwa na wenzake baada ya kufunga

Bocco anamuacha mtu

Amri Kiemba kulia

Bocco mawindoni

Yondan anaokoa
Mrisho na mpira wake baada ya kufunga mabao matano
    


KILI STARS YAIPA SOMALIA KIPIGO CHA MBWA MWIZI

Ngasa ang’ara
Mabao matano yaliyofungwa na mshambuliaji, Mrisho Ngassa na mawili kutoka kwa John Bocco. Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo ambao ulishuhudia, Tanzania Bara ikiizamisha, Somalia kwa mabao 7-0, kocha msaidizi wa timu hiyo, Slivester Marsh amesema wamefurahishwa na matokeo hayo japo wengi walikata tamaa ya kuona timu hiyo ikitinga hatua ya robo fainali. ” Ilikuwa ni mechi ngumu kwa upande wetu, tulionekana kama tusingefuzu kwa hatua ya robo fainali. Tunashukuru Mungu na tuna imani tunaweza kufanya vizuri zaidi” alisema, Marsh.
Ngassa, alitumia dakika 90 mchana wa leo kufunga bao lake la kwanza katika michuano, na kufunga mengine manne na kuwa kinara wa mabao katika michuano hiyo. Alifunga mara tano, uku mshambuliaji ‘ patna’ wake, Bocco, akifunga mabao mengine mawili na kufikisha mabao manne katika michuano inayoendelea ya Tusker Challenge Cup, uko, Uganda. Wawili hao, Ngassa na Bocco wamekuwa na wakati mzuri katika michuano hiyo na sasa wapo juu katika orodha ya wafungaji bora. Ngassa ana matano n ndiye anayeongoza, uku Bocco, akifuatia na mabao yake manne.
Katika mchezo wa leo, wachezaji, Edward Christopher, Athuman Idd ” Chuji” na Ramadhani Singano, walipata nafasi ya kucheza mchezo wao wa kwanza. Watatu hao waliingia kwa wakati tofauti katika kipindi cha pili, Edo, alimpokea, Bocco, kisha, Chuji akaingia mahali kwa Frank Domayo na Singano, mahali kwenye nafasi ya Salum Abubakary. Katika mchezo mwingine, timu ya Taifa ya Burundi, iliifunga, Sudan Kaskazini, bao 1-0, na kuwa vinara wa kundi kwa kufikisha pointi tisa, tatu juu ya zile za Stars.


MASHUJAA WASHINDWA KUZINDUA ALBAM YAO

Watu  mbalimbali wakiwa wamelizunguka jenereta Jana usiku.
  Mwanamuziki kutoka DRC-Congo,JB Mpiana akitumbuiza jukwaani mara baada ya kupanda mnamo majira ya saa tisa kasoro,baada ya hitilafu za umeme kwenye jenerata kurekebishwa.

SHOO YA UZINDUZI WA ALBAM YA PILI YA MASHUJAA BAND, ILIINGIA DOSARI NA KUTAKA KUSHINDWA KUFANYIKA  KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB USIKU HUU KUTOKANA NA KATIZO LA UMEME LA MARA KWA MARA LINALOSABABISHWA NA JENERETA LINALOTUMIWA KUTOA UMEME KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB,JIJINI DAR.

HALI HIYO IMEPELEKEA MMILIKI WA BENDI YA MASHUJAA,MAMA SAKINA KUPOTEZA FAHAMU NA KUKIMBIZWA HOSPITALI.

HADI SASA HAIJAFAHAMIKA KUWA HALI YAKE IKO VIPI KWANI HAKUNA TAARIFA ZOZOTE JUU YAKE.

MAFUNDI BADO WANAENDELEA NA MAREKEBISHO YA JENERETA HILO NA IWAPO LITAKAA SAWA,BASI NI MOJA KWA MOJA BENDI YA WENGE BCBG NDIO ITAPANDA JUKWAANI,CHINI YA MKONGWE JB MPIANA.

TUTAENDELEA KUJUZANA KADRI MAMBO YATAKAVYOKUWA YAKIENDELEA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB,KINONDONI JIJINI DAR ES SALAAM

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU