Facebook Comments Box

Thursday, September 13, 2012

MADAKTARI NAIROBI WAGOMA TENA

NAIROBI

Wagonjwa na watu wenye wagonjwa hospitalini nchini Kenya sasa hivi wako kwenye hofu kutokana na kutangazwa kuanza tena kwa mgomo wa Madaktari baada ya serikali kusema haitobadilisha chochote kwenye mishahara ya madaktari.
September 13 2012 Madaktari wote wa hospitali za Serikali Kenya wanatarajia kuanza kugoma kwa sababu serikali haijafanya kama wanavyotaka, yani kuongezewa mishahara.
Katika vichwa mbalimbali vya habari nchini Kenya Mtangazaji William Tuva wa Citizen Radio na Citizen Tv ameripoti pia kwamba baada ya vurugu kuendelea kati ya makabila ya Waorma na Wapokomo kwenye wilaya ya Tana River ambapo inaaminika zaidi ya watu 100 wamefariki dunia wakiwemo Polisi, Mbunge wa Galole ambae ni Naibu Waziri Godana amekamatwa na polisi na kupelekwa Mahakamani akidaiwa kuwa mmoja ya watu wanaohusika na uchochezi wa hizo vurugu, baadae aliachiwa kwa dhamana ya shilingi laki nne za Kenya.
Vurugu za sasa kwenye wilaya ya Tana River zimehusisha watoto pia kuuwawa kikatili na nyumba kuchomwa ambapo wataalamu wa mambo wanasema vurugu hizi zinahusika na siasa, yani kuna wanasiasa wanachochea kwa sababu uchaguzi mkuu unakaribia.
Kwenye sentensi nyingine William Tuva ameamplfy kuhusu mlipuko uliotokea Mogadishu Somalia kwenye hoteli aliyokuwemo rais mpya wa Somalia pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri lakini hao viongozi wote wamenusurika, waliopoteza maisha ni watu wengine saba.
Waziri huyo wa mambo ya nje alikwenda Somalia kumwakilisha Rais Mwai Kibaki kutoa pongezi kwa rais mpya wa Somalia

IANGALIE iPHONE 5 BAADA YA KUZINDULIWA



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU