Facebook Comments Box

Saturday, November 29, 2014

HAYA NDIO MAAZIMIO YA BUNGE JUU YA ESCROW

MAAZIMIO YA BUNGE KUHUSU HOJA YA TAARIFA MAALUM YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU TAARIFA YA UKAGUZI 

MAALUM KUHUSIANA NA MIAMALA ILIYOFANYIKA KATIKA AKAUNTI YA ‘ESCROW’ YA TEGETA

PAMOJA NA UMILIKI WA KAMPUNI YA IPTL

_____________________________________

 

1.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuhusu Ukaguzi Maalum wa Malipo yaliyofanyika katika Akaunti ya Escrow ya Tegeta uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (‘CAG’) pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (‘TAKUKURU’) imeonesha kwamba kwamba Harbinder Singh Sethi, James Rugemalira (VIP), Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Waziri wa Nishati na Madini, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (‘TANESCO’) walihusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha kufanyika miamala haramu ya fedha za Akaunti ya Escrow ya Tegeta kwenda kwa makampuni ya Pan African Power Solutions Ltd. (‘PAP’), na VIP Engineering & Marketing (‘VIP’);

KWA KUWA, kwa sababu ya kuhusika kwa watu hao na miamala iliyofanyika kwenye Akaunti ya Escrow imeliingizia Taifa hasara ya mabilioni ya fedha za umma zinazotokana na kutokulipwa kwa kodi mbali mbali za Serikali na kushindwa kwa TANESCO kukokotoa upya kiwango cha malipo ya gharama za uwekezaji (‘capacity charges’) wa IPTL;

KWA KUWA, mabilioni ya fedha yaliyotolewa kwenye Akaunti ya Escrow yametumika kuwapa kile kinachoonekana kuwa ni rushwa baadhi ya viongozi na maafisa wa serikali kama vile Mawaziri, Majaji, Wabunge, Wenyeviti wa Kamati za Bunge, wakuu wa taasisi za umma, viongozi wa dini, mawakili wa kujitegemea na watu binafsi.

NA KWA KUWA, vitendo vilivyofanywa na watu hawa vinaashiria makosa mbali mbali ya jinai kama vile uzembe, wizi, ubadhirifu, kutakatisha fedha haramu, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa na kupokea mali ya wizi;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, TAKUKURU, Jeshi la Polisi na vyombo vingine husika vya ulinzi na usalama viwachukulie hatua stahiki za kisheria, kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, watu wote waliotajwa na Taarifa Maalum ya Kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusiana na miamala ya Akaunti ya Escrow, na watu wengine watakaogundulika kuhusika katika vitendo hivyo vya jinai kufuatia uchunguzi mbali mbali unaoendelea;

2.    KWA KUWA, vitendo vya kijinai wanavyhohusishwa navyo viongozi wa umma na maafisa wa ngazi za juu serikalini vinakiuka pia maadili ya viongozi wa umma na kuwanyima viongozi na maafisa hao uhalali wa kuendelea kushikilia nafasi za mamlaka katika uongozi wa umma;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO wawajibishwe, kwa kuishauri mamlaka yao ya uteuzi kutengua uteuzi wao;

3.    KWA KUWA, katika watu walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kashfa ya miamala ya Akaunti ya Escrow wapo pia viongozi wa Kamati za Kudumu za Bunge kama vile Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO;

NA KWA KUWA, Bunge na/au Kamati zake za Kudumu zina uwezo na mamlaka, kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, ya kuwawajibisha viongozi hawa wa Kamati kwa kuwavua nyadhifa zao;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Kamati husika za Kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka, na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge, kuwavua nyadhifa zao Wenyeviti tajwa wa Kamati husika za Kudumu za Bunge;

4.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba katika watu waliotajwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kashfa ya miamala ya Akaunti ya Escrow wapo pia Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania;

KWA KUWA, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (‘Katiba’) imeweka utaratibu mahsusi wa kushughulikia nidhamu ya Majaji;

KWA KUWA, utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji kwa mujibu wa Katiba unamtaka Rais kuunda Tume ya Uchunguzi ya Kijaji kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Majaji;

NA KWA KUWA, utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji kwa mujibu wa Katiba unamruhusu Rais kumsimamisha kazi Jaji au Majaji husika wakati uchunguzi wa tuhuma dhidi yake unaendelea;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aunde Tume ya Kijaji ya Uchunguzi kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania;

5.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba Stanbic Bank (Tanzania) Ltd. ilishiriki kupokea na kutakatisha fedha zilizotolewa kwa njia haramu kutoka katika Akaunti ya Escrow na kupelekwa katika akaunti zilizofunguliwa na PAP katika benki hiyo;

KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha kwamba akaunti za PAP  katika Stanbic Bank Tanzania Ltd. zimekwishafungwa baada ya fedha zote zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow kumalizika na Akaunti ya ya VIP katika Mkombozi Commercial Bank imebakiza kiasi fulani cha fedha;

NA KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati inaonesha kwamba kuna uwezekano fedha zilizotolewa kutoka kwenye akaunti za PAP na VIP zilipelekwa katika benki nyingine;

NA KWA KUWA, vitendo vya Stanbic Bank (Tanzania) Ltd., na benki nyingine kupokea na kutakatisha fedha zilizotolewa kwenye Akaunti ya Escrow ni vitendo vya jinai kwa mujibu wa Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, mamlaka husika za kifedha na za kiuchunguzi ziitaje Stanbic Bank (Tanzania) Ltd. na benki nyingine yoyote itakayogundulika, kufuatia uchunguzi wa mamlaka za kiuchunguzi, kujihusisha na utakatishaji wa fedha zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow, kuwa ni taasisi zenye shaka ya utakatishaji wa fedha haramu (institutions of money laundering concern);

6.    KWA KUWA, vitendo vya wizi, ubadhirifu wa mali ya umma, hujuma ya uchumi na ufisadi vimeongezeka, kushamiri na kushirikisha viongozi wa kisiasa na maafisa wa serikali pamoja na wafanya biashara wakubwa;

KWA KUWA, kwa mujibu wa sheria iliyoiunda, TAKUKURU inashughulikia vitendo vya aina zote za rushwa zikiwemo rushwa ndogo ndogo (petty corruption) na rushwa kubwa na ufisadi (grand corruption) na matumizi mabaya ya madaraka;

NA KWA KUWA, kwa sababu ya majukumu yake mapana kisheria, TAKUKURU inaelekea kuelemewa katika vita ya kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa letu kiuchumi, kijamii na kisiasa;

HIVYO BASI, BUNGE LINAAZIMIA KWAMBA, Serikali iandae na kuwasilisha Muswada wa marekebisho ya Sheria iliyoiunda TAKUKURU kwa lengo la kuanzisha taasisi mahsusi itakayoshughulikia, kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa;

7.    KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati imeonesha jinsi ambavyo TANESCO imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kulipa gharama za umeme unaozalishwa na IPTL na hivyo kuathiri hali ya kifedha ya Shirika hilo;

KWA KUWA, Taarifa Maalum ya Kamati inaonesha kwamba TANESCO itaendelea kulipa fedha nyingi kwa ajili ya gharama za umeme huo wa IPTL;

HIVYO BASI, Bunge linaazimia kwamba Serikali iangalie uwezekano wa kununua mitambo ya kufua umeme ya IPTL na kuimilikisha kwa TANESCO kwa lengo la kuokoa fedha za Shirika hilo.

8.    KWA KUWA, kwa miaka mingi mikataba mibovu ya kuzalisha umeme kati ya TANESCO na makampuni binafsi ya kufua umeme imeisababishia TANESCO hasara ya mabilioni ya fedha na hivyo kutishia uhai wake wa kifedha;

KWA KUWA, Bunge lilikwishaazimia kwamba serikali iwasilishe mikataba husika Bungeni au kwenye Kamati zake kwa lengo la kuliwezesha Bunge kutekeleza vyema wajibu wake wa kuisimamia na kuishauri serikali;

NA KWA KUWA, Serikali haijatekeleza Azimio hilo la Bunge hadi sasa;

HIVYO BASI, Bunge linaazimia kwamba Serikali itekeleze Azimio husika la Bunge mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile kabla ya kumalizika kwa Mkutano wa Bunge la Bajeti Serikali iwasilishe taarifa ya utekelezaji wa mapitio ya mikataba ya umeme.

Imewasilishwa leo hii tarehe 28 Novemba, 2014.

------------------------------------------------------

ZITTO ZUBERI KABWE (MB)

MWENYEKITI

KAMATI YA PAC



HELKOPTA YA MALI ASILI YAANGUKA UKONGA MOMBASA

Wananchi wakiangalia helkopta hiyo
Helicopter mali ya serikali wizara ya mali asili yaanguka maeneo ya moshi bar mombasa Dar na kuua wote walio kuwemo na kuangukia nyumba za wananchi.

Polisi wameshafika eneo la tukio
Wananchi wenye nyumba hizo bado haijajulikana kama wamekufa ama hawakuwemo. Rubani na capt wa ndege hiyo inasemekana walikuwa na uzoefu mdogo sana(masaa machache sana) kutoka chuo cha 44 cha huko south African.





Thursday, November 27, 2014

SHEIKH PONDA AACHIWA HURU


APPEAL YA SHEIKH PONDA IMESOMWA AMESHINDA HUKUMU YA KUMTIA HATIANI ILIYOTOLEWA NA MAHAKAMA YA KISUTU IMEFUTWA SHEIKH YUKO HURU SASA NA WANAKWENDA MOROGORO.
Maandamano kuelekea Mtambani kuwasikiliza viongozi wa kiislamu

JAJI AMEMTANGAZA SHEIKH KUWA NI ULAMAA MKUBWA WA DINI YA KIISLAMU.

BAADA YA KUFUTIWA KESI HIYO NA KUACHIWA HURU POLISI WALIMKAMATA TENA KWA KUWA KESI YA MOROGORO BADO HAIJAISHA.


 HAWAJAWEKA WAZI KAMA KESI HIYO INA DHAMANA AU HAINA.





Sunday, November 23, 2014

TAMKO LA HIZB UT-TAHRIR JUU YA YANAYOTOKEA KENYA

Kwa mara nyengine tena Waislamu nchini Kenya   wameshuhudia uvamizi wa polisi wa misikiti miinne Sakina Musa, Swafaa na Minaa Mjini Mombasa.

Kitendo hiki cha kinyama kilichopelekea
mauaji ya mwanafunzi mmoja huku vijana wapato mia mbili na hamsini kutiwa mbaroni, kilifanywa chini ya kisingizio cha kuwafurusha vijana wenye misimamo mikali. Harakati ya Hizb
ut-Tahrir Afrika Mashariki inalaani vikali kitendo hiki na twasema yafuatayo:-

Ukatili wa polisi wa Kenya umezidi sana hasa kwa Waislamu ; Huku kukiwa kuna magenge ya-nayotekeleza mauaji kama vile Baghdad boys na Mungiki ambayo wengi ya wafuasi wake ni wakristo hatujashuhudia hata kanisa moja likivamiwa na polisi kama inavyofanywa kwa Waislamu. Bali polisi katika kuendeleza maonevu kwa Waislamu, huwapachika majina radicalists na
extremists kuhalalisha unyama wao dhidi yao. Na hii ndio sura kamili ya polisi leo ndani ya nidhamu za kibepari namna
wanavyotumiwa katika kuwafanyia unyama Waislamu. Madai ya kuwa kuna Waislamu wabaya na Waislamu wazuri
‘radicalists and moderates ni njama tu kuwagawanya Waislamu.

Na hata kama kuna tofauti baina ya Waislamu kifikra na kimisimamo,basi waachiwe wenyewe Waislamu kwani Uislamu uliwawekea utaratibu maalum wa kutatua kasoro hizo. Hivyo haijakuwa halali kwa serikali kuendeleza mateso kwa Waislamu kwa kisingizio hicho. Tunakataa miito hii pamoja na vita
kupambana na ugaidi kwani vyote hivyo ni kuushambulia Uislamu na Waislamu.

Udhalilifu huu umetokamana kukosekanwa na waakilishi wa kikweli  wa mambo ya Waislamu. Hata wale baadhi ya wanasiasa wanaojitokeza ati kukashifu unyamu huo, wao hufanya hivyo kwa lengo tu la kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Ushahidi wa haya ni kuwa hao hao ndio huwadaa raia kuwa kushiriki kwao ndani ya nidhamu za kidemokrasia ndio njia ya kuzuia dhulma juu ya Waislamu. Na ukweli ni kuwa nidhamu za kidemokrasia ndio chanzo cha balaa zote zinazoshuhudiwa na watu wote Waislamu na wasokuwa waislamu.

Madhila haya leo ni sehemu tu ya miongoni mwa mengi yanayofanyiwa Waislamu kote dunia  na hayatokoma leo hadi pale Waislamu watapoweza kufanya kazi ya kubeba ulinganizi wa Kiislamu kwa lengo la kusimamisha utawala halisi wa Kiislamu Khilafah katika moja wapo ya nchi za Kiislamu.  Utawala huo ndio
utakaohifadhi kikweli Waislamu na Wasokuwa Waislamu na kuwakinga dhidi ya shari za maadui zao.

KUMB: 04 / 1436 AH   
25th Muharram 1436 AH
18/11/2014 CE
Shabani Mwalimu
Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari Hizb ut-Tahrir Afrika
Mashariki



RASMI: JAJA AONDOKA YANGA: NAFASI YAKE YAPEWA MBRAZILI MWINGINE

Kiungo mkabaji raia wa Brazil Emerson De Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili siku ya jumanne mchana jijini Dar es salaam kwa ajili ya majaribio katika klabu ya Young Africans na endapo atafuzu moja kwa moja atajiunga na mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara.

Emerson mwenye umri wa miaka 24 ambaye kwa sasa anachezea timu ya Bonsucesso FC iliyopo ligi daraja la pili nchini kwao Brazil, msimu uliopita alikuwa akicheza soka la kulipwa nchini Poland katika timu ya Piotrkow Trybunalski FC iliyopo Ligi Daraja la pili nchini humo.

Ujio wa Emerson kuja kufanya majaribio nchini unakuja kufuatia mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Brazil pia Geilson Santos "Jaja" kushindwa kurejea nchini baada ya kwenda kwao Brazil na kutoa taarifa kwamba hataweza kurejea tena nchini kutokana kukabiliwa na matatizo ya kifamilia.
Awali ilikua familia ya Jaja ije nchini katika kipindi cha mapumziko, lakini waliomba yeye Jaja ndio aende Brazil na mara baada ya kufika huko matatizo ya kifamilia aliyokutana nayo yamepelekea kushindwa kurejea nchini
 kuitumikia klabu yake na kuomba abakie kwao kwa ajili ya kutatua matatizo hayo.
Kuondoka kwa Jaja kunafanya klabu ya Young Africans kubakia na wachezaji wanne tu wa kimataifa ambao ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho hivyo endapo Emerson atafuzu  atakuwaa
 anakamilisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa.

Endapo Emerson atafuzu majaribo pamoja na vipimo atajiunga na kikosi cha kocha mbrazil Marcio Maximo katika nafasi ya kiungo mkabaji ikiwa ni sehemu ya kuboresha timu kuelekea kwenye michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya kimataifa.
Aidha kikosi cha Young African baada ya kuwa mapumzikoni kwa takribani wiki mbili, kinatarajiwa kuanza mazoezi siku ya jumatatu katika Uwanja wa shule ya sekondari Loyola kujiandaa na mchezo wa Nani Mtani Jembe
pamoja na mzunguko wa nane wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania bara.


Sunday, November 9, 2014

MWANAMUZIKI MKONGWE AMIGOLAS AFARIKI DUNIA

AMIGOLAS
Mwanamuziki mkongwe wa Bendi ya Africans Stars maarufu kama Twanga pepeta amefariki dunia katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Marehemu alipelekwa hapo akiwa nasumbuliwa na matatizo ya moyo.


PICHA YANGA ILIPO WAONESHA MGAMBO MATAA YA MJINI

Timu ya Young Africans Sports Club jana imewaonesha Mgambo JKT mataa ya mjini baada ya kuwachabanga mabao mawili kwa bila. Mabao ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva katika kipindi cha pili.
Kiungo mbrazili Coutinho akitafuta njia ya kumtoka beki wa mgambo

Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Mgambo JKT

Msuva akishangilia bao lake la pili




PICHA ZA BARABARA YA UKONGA MAZIZINI ILIYOTUMIA MILIONI 90 ILIVYO SASA



Hii ndiyo ile barabara ya Ukonga Mazizini- Moshi Bar ambayo inadaiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 90 kuikarabati kwa kiwango cha changarawe kwa umbali wa kilometa tatu. Picha hizi ni madimbwi ya mwanzo tu ya hizo kilometa tatu.



Meya Jerry Silaa wa Ilala ambaye ni Diwani wa Gongo la Mboto alipotembelea aliwaambia wananchi kuwa fedha za ujenzi huo ni kutoka mfuko wao. 
Picha zifuatazo ni za siku Meya Silaa alipotembelea ujenzi.



Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Ukonga Moshi Bar ya kilometa 3 kwa kiwango cha changarawe awamu ya kwanza, ikiwa ni utekelezaji wa miradi ya dharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinu uliotokea baada ya mvua kubwa kunyesha. Mradi huo unagharimu kiasi cha shilingi millioni 90. Pesa za ujenzi huo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Pia barabara hiyo itawekwa lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.



Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-Mazizini kulekea Moshi Bar



Mwonekano wa barabara hiyo


SHEREHE ZA JANDO BUTIAMA



Wanamwita "Dokta" wa kijiji cha Ryamisanga wilayani Butiama akiendelea na shughuli yake ya kumtahiri kijana kwa dakika 17 bila ganzi.



Baadhi ya vijana ambao wameshatahiriwa wakimtizama mwenzao ambaye anafanyiwa tohara



"Dokta" akijiandaa kuifanya kazi yake




Mashuhuda







Baadaye ni vinywaji



Msosi kama huu pia ulikuwepo



Picha, maelezo na Shomi Binda: HIVI NDIVYO TOHARA ZA KABILA LA KIKURYA ZINAVYOFANYIKA

WIMBO AMBAO LOKASSA YA MBONGO AMEMUIMBIA RAIS KIKWETE





Saturday, November 8, 2014

HATIMAYE SITTI MTEMVU AACHIA TAJI

Katika hali isiyotarajiwa mlimbwende alichukua taji la urembo la Tanzania mwanadada Sitti Mtemvu ameachia taji hilo. Katika barua ambayo amewaandikia wandaaji wa shindano hilo ameeleza jinsi anavyo andamwa na watu mbalimbali juu ya umri wake.

Barua aliyo andika ni hiyo hapo chini


Friday, November 7, 2014

WHATSAPP YAWAUMBUA WAONGO

Kuanzia juzi longo longo ya kwamba sikuupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kudai kuwa ujumbe haujafika utakuwa unaongopa mchana kweupe.

Huduma hiyo inapatikana kupitia Whatsapp katika simu zote za mkononi zenye uwezo wa kuitumia
Tick ya kijivu ina maana kuwa ujumbe umetumwa
Tick mbili za kijivu zina maana ujumbe umemfikia mlengwa
Tick mbili za blue zina maana kuwa mlengwa ameusoma ujumbe uliotumwa
Ukibonyeza na kushikilia ujumbe uliotuma inatokea maelezo ya kina ya ujumbe huo  (Pressing and holding an individual message shows the Message Info option) Ukibofya utaona muda kamili ambao ujumbe huo ulisomwa

Maoni kuhusu mabadiliko hayo yamepokelewa tofauti katika mitandao ya kijamii, wapo ambao hawajafurahishwa

Whatsapp haijatoa sababu za kufanya mabadiliko hayo ambayo yamewakera baadhi ya watumiaji.

Kuanzia juzi huduma hiyo inayomilikiwa na Facebook- itakuwa ikionesha tick mbili za rangi ya blue upande wa chini kulia katika kila ujumbe unaotuma kubainisha kuwa umesomwa.

Na ukibofya ujumbe wenyewe utaona muda kamili ambao.mlengwa alifungua na kuusoma ujumbe husika.


Thursday, November 6, 2014

RAIS AFANYA UTEUZI WA MAKATIBU WA KUU WA WIZARA

Rais Jakaya Kikwete amefanya uteuzi wa Makatibu Wakuu wa Wizara kwa kuteua Makatibu Wakuu wanne wapya na kuhamisha mmoja, uteuzi uliomuondoa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo.

Pallangyo sasa anakua Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, nafasi ambayo inatafsriwa kuwa adhabu, siku chache baada ya vyombo vya habari ikiwamo FikraPevu kuibua kashfa ya uhaba wa dawa katika hospitali kubwa za serikali. Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi na uhamisho wa Makatibu Tawala wa Mikoa.

Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya leo, Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi,
Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa walioteuliwa ni pamoja na Dkt. Donan Mmbando ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuchukua nafasi ya Pallangyo.

Katika uteuzi huo Dkt. Yohana Budeba anakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Mbogo Futakamba kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Dkt. Adelhelm James Meru ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Maliasili.

Kabla ya uteuzi wake, Dkt Mmbando alikuwa Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Budeba alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mifugo, Mhandisi Futakamba alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Dkt. Meru alikuwa Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje(EPZA).

Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Rais Kikwete amemhamisha Bibi Maimuna Tarishi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kwenda kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Adoh Steven Mapunda, Mkurugenzi Mtendaji, Manispaa ya Bukoba amepanda na kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Severine Kahitwa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita anakuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro na Dkt. Faisal Issa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro anahamishiwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
wa Mwanza. Wakati huo huo, Rais Kikwete amemteua Kanali (Mst) Joseph Simbakalia, Mkuu wa
Mkoa wa Mtwara, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa EPZA kuchukua nafasi ya Dkt. Meru.

Uteuzi huo unaanza leo na Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wataapishwa kesho, Alhamisi, Novemba 6, 2014, Ikulu, Dar es Salaam. Wakati huohuo, Rais Kikwete amefanya
uteuzi wa wakuu wapya wanne wa Mikoa, amewahamisha wengine sita na ameamua kuwa wengine watatu watapangiwa kazi nyingine. Mabadiliko hayo yanampumzisha

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Fabian Massawe na kuwahamisha wakuu wa mikoa ya Arusha Magessa Mulongo na Fatma Mwasa wa Tabora. Taarifa ya Balozi Sefue inawataja Wakuu
wapya wa Mikoa ni Bi. Halima Omari Dendego ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Dkt. Ibrahim Hamisi Msengi ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Bi. Amina Juma Masenza ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Bwana John
Vianney Mongella ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Taarifa inasema kuwa kabla ya uteuzi wake Bi. Dendego alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dkt. Msengi alikuwa Mkuu wa Wilaya
ya Moshi, Bi. Masenza alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela na Bwana Mongella alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha. Taarifa hiyo inasema kuwa Wakuu hao wapya wa Mikoa wataapishwa kesho,
Alhamisi, Novemba 6, 2014 saa saba mchana, Ikulu, Dar es Salaam.
Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ambao watapangiwa kazi nyingine ni Kanali (Mst) Fabian Massawe wa Kagera, Dkt. Christine Ishengoma wa Iringa na Kanali
Joseph Simbakalia wa Mtwara.

Wakuu wa Mikoa ambao wamehamishwavituo vya kazi ni Bwana  Magesa S. Mulongo ambaye anakwenda Mkoa wa Mwanza
kutoka Arusha, Dkt. Rehema Nchimbi ambaye anakwenda Mkoa wa Njombe kutoka Dodoma, Bwana Ludovick John Mwananzila
anakwenda Tabora kutoka Lindi, Kepteni (Mst) Anseri Msangi anayekwenda Mkoa wa Mara kutoka Njombe na Mhandisi Everist
Ndikilo ambaye anakwenda Arusha kutoka Mwanza.

Wengine waliohamishwa ni Luteni (Mst) Chiku A.S. Galawa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoka Tanga, Dkt.
Rajab Rutengwe ambaye anakwenda Mkoa wa Tanga kutoka Katavi, Bi Fatma Mwasa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kutoka Tabora na Bwana Magalula S. Magalula ambaye anahamishiwa Lindi kutoka Geita.

Taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,Morogoro, Pwani, Rukwa,
Shinyanga, Ruvuma, Singida na Simiyu watabakia kwenye vituo vyao vya sasa. Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi wa
Wakuu wapya wa Wilaya, kuhamisha baadhi yao na kutengua uteuzi wa baadhi. Taarifa kamili itatolewa na Waziri Mkuu baada ya
kuwa wamepangiwa vituo vya kazi.


Wednesday, November 5, 2014

REAL MADRID YAINGIA HATUA YA 16 KWA KUIFUNGA LIVERPOOL

Timu ya R.Madrid jana usiku ilipata ushindi kiduchu kwa kuichapa Liverpool ya England katika michuano ya kuitafuta Klabu Bingwa wa Ulaya. Wenyeji walipata bao la kuongoza na la ushindi katika dakika ya 27 ya mchezo kupitia kwa Kareem Benzema.
 Uwanja wa Santiago Bernabeu ulipofanyika mchezo huo kati ya wenyeji R.Madrid vs Liverpool.
 Kareem Benzemaa akishangilia bao lake lililoipa ushindi Real Madrid dhidi ya Liverpool.
Wachezaji wa Real Madrid wakimpongeza mfungaji wa bao pekee la mchezo huo, Kareem Benzemaa.
 Kareem Benzemaa katikati ya Kolo Habib Toure na Martin Skrtel.



Tuesday, November 4, 2014

MRISHO NGASSA NDIO MFUNGAJI BORA AFRIKA

Ngassa amemaliza kinara baada ya kufunga mabao sita na kufungana na Ndombe Mubele wa AS Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Haythem Jouini wa Esperance de Tunis ya Tunisia na El Hedi Belameiri wa ES Setif ya Algeria.

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Mrisho Ngassa amepata zali Afrika, baada ya kumaliza kinara wa mabao kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, licha ya klabu yake kuaga mashindano hayo katika mzunguko wa pili. Ngassa amemaliza kinara baada ya kufunga mabao sita na kufungana na Ndombe Mubele wa AS Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Haythem Jouini wa Esperance de Tunis ya Tunisia na El Hedi Belameiri wa ES Setif ya Algeria.

Ni baada ya Ligi ya Mabingwa Afrika kufikia tamati wikiendi iliyopita na ES Setif kutangazwa mabingwa wapya wakibebwa na bao la ugenini kutokana na matokeo ya sare bao 1-1 mchezo wa Algeria na sare mabao 2-2 mchezo uliochezwa Kinshasa.

Ngassa aliyafunga mabao hayo katika raundi ya kwanza walipocheza na Komorozine ya Comoro mchezo wa kwanza walishinda 7-0 na marudiano walitoka kifua mbele kwa mabao 5-2. 

Yanga ilitolewa kwenye mashindano na Al Ahly ya Misri kwa penalti 3-4. Lakini Ngassa hawezi kupewa zawadi yoyote kwavile wamefungana na kiutaratibu hata mchezaji akishinda tuzo hiyo CAF huwa haitoa zawadi.


HISTORIA FUPI YA MAREHEM JAFAR SIRAJ

Kabla ya kuwepo MuM alikuwa ni mhitimu wa Chuo cha Ualimu cha Kiislamu Ubungo Islamic Teacher's College ambako alihitimu mwaka 2004 na kisha akasomesha Msamala Muslim Songea na baadae Matangini Islamic Dar, akajiunga na
Chuo cha Waislamu Morogoro wakiwa ndio Batch ya mwanzo 2005. Baada ya kuhitimu alichaguliwa kuwa Mhadhiri Msaidizi na mwaka mmoja baadae alijiunga na Chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya Shahada ya Uzamili na kurejea MuM ambako amekuwa akifanya kazi mpaka mauti yalipomkuta.

Bro. Alianza kupata mtihani wa maradhi mwaka 2011 na 2012 au 13 aligundulika kuwa na Maji kwenye mapafu waislamu wakachukuwa  jukumu la kumpeleka India kwa matibabu akafanyiwa upasuaji na tatizo likapungua alirejea Alhamdulillaah ingawa alionekana wazi kuwa tayari amedhoofika, hakuwa Siraji yule handsome tuliyekuwa tukimjua.

Bro. Katika uhai wake ukiacha kwamba alikuwa superbright kitaaluma na kihoja na aliyekuwa na khofu ya dhati kwa Mola wake alikuwa role model, and very inspiring, fasaha na mtulivu sana asiye na papara katika mambo yake na huu ni sehemu ya urithi aliyotuachia.

Bro. Siraji alikuwa mtu huru na anayenyoosha maneno alipokuwa akisimamia haki, Kipindi cha mwangaza wa jamii Radio Iman na wasikizaji wake watashuhudia kwa hili na watasikitika sana kipindi hiki kumkosa huyu Akhy.

"Hao ni umma umekwishapita, wao wana malipo yao nanyi mna malipo yenu wala hamtoulizwa wao wamefanya nini (Bali mtaulizwa ninyi mmefanya nini) 2:141

Bro. Siraji ameacha mke na  watoto wawili wa kiume. Tunaamini wajibu wake kwa jamii ya waislamu na watanzania kwa jumla ameutekeleza kikamilifu na hivyo anastahiki akapumzike.

Sisi sote ni wa Allaah na kwake ndio Marejeo. Allaah amsamehe madhambi yake amrehemu na ampe makazi mazuuri peponi.


Sunday, November 2, 2014

MLIPUKO WA KITU KINACHODHANIWA KUWA BOMU WAUA MMOJA KISHAPU



Tarehe 01/11/2014 muda wa saa 07:45 hrs katika center ya Muhunze tarafa ya Kishapu na Wilaya ya Kishapu.

Gari no T. 848 AKA MITSHUBISH FUSSO likiendeshwa na Khalifa s/o Mussa 39, Muhangaza wa Ngara ambalo lilitoka tarehe 31/10/14 saa 04:00 hrs mjini Ngara kuja Mkoa wa Shinyanga wilaya ya Kishapu kupakia shehena ya mtama kwa mfanyabiashara alitwaye Donard s/o Nzugula (49) msukuma wa Muhunze.

Wakati gari hilo likiwa limeegeshwa dukani kwa mfanyabiashara huyo ili kusubiri kupakia mzigo huo dereva alishuka kununua sigara maduka ya jirani akamwacha utingo wake ndani ya gari peke yake ambaye anaitwa Juma s/o Rashid 21-23, mwangaza wa Ngara ambaye ni
familia ya mwenye gari.

Baada ya muda mfupi kama dakika 15 hivi dereva alisikia mshindo mkubwa na alipokwenda kwenye gari alimkuta utingo wake ametupwa nje ya gari na akiwa amefariki mwili wake ukiwa na majeraha tumboni,mkono wa kushoto kiganja kimekatika,mkuu wa kulia kwenye paja ambalo limechimbika hadi kwenye mfupa, shingoni upande wa kushoto kuna shimo kubwa lililosababishwa na kitu chenye ncha kali.

Pia mfanyabiashara Donard s/o Nzugala Mwalimu ambaye ameumia mkono wa kulia kwa kuchanwa chanwa na vipande vya chuma,amepelekwa hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi.

Wengine ni Maganga s/o Piusi (14 ), msukuma,mkulima wa Kishapu ambaye amejeruhiwa paja la kushoto, mgongoni na mkono wa kushoto.

Seni s/o Edward (25 ), msukuma mkulima wa Lubaga Kishapu amejeruhiwa bega la kushoto, majeruhi wote wametibiwa na kuruhusiwa.



SIMBA YAENDELEZA SARE: PHIRI ABAKIZA MECHI MOJA KUTIMULIWA


SIMBA SC imetoa sare ya sita mfululizo tangu kuanza kwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar, Uwanja wa Jamhuri, Morogoro jioni ya jana.

Hii inakuwa ni mechi ya 12 kwa Simba bila ushindi ukijumlisha na mechi sita za mwisho za msimu uliopita. Swala hili la kutoa suluhu limepelekea Simba kumpa kocha wa Phiri mechi tatu za mwisho na akihitajika kushinda mechi mbili. Jana wametoa suluhu mechi ya kwanza na zimebaki mbili, Hii ina maana akitoa suluhu yoyote au kufungwa ndio utakuwa mwisho wa Kocha huyo ambae ana historia ya kuja Simba na kufundisha mara kwa mara nusu msimu ikifika  msimu mwingine anaaga kuwa ana matatizo ya kifamilia na harudi tena.

Suluhu hiyo inawafanya Mtibwa wafikishe pointi 14 kileleni mwa ligi hiyo, wakati Simba SC imefikisha pointi 6 jana.Simba SC ilikwenda kupumzika ikiwa tayari inaongoza kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na beki wa kimataifa wa Uganda, Joseph Owino dakika ya 35 kwa kichwa akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Emmanuel Okwi.
 
Hali hiyo iliwafanya vinara wa hao wa Ligi Kuu wapate bao la kusawazisha dakika ya 58, mfungaji Mussa Hassan Mgosi aliyetumia makosa ya beki wa kulia, William Lucian ‘Gallas’ kuchanganyana na kipa wake, Manyika Jr.

VIKOSI VILIKUWA HIVI:
 
Mtibwa Sugar: Said Mohammed, Hassan Ramadhani, David Luhende, Andrew Vincent, Salim Mbonde, Shaaban Nditi, Mussa Ngosi, Mohamed Ibrahim, Ame Ally, Mussa Nampaka na Ally Shomary.

Simba SC: Peter Manyika, William Lucian ‘Gallas’, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Hassan Isihaka, Joseph Owino, Jonas Mkude, Ramadhani Singano ‘Messi’, Awadh Juma, Elias Maguri/Amisi Tambwe dk76, Said Ndemla na Emmanuel Okwi/Uhuru Suleiman dk75.


Saturday, November 1, 2014

PICHA YA LEO: KIONGOZI WA YANGA AKIKAGUA UDONGO WA UWANJA

Yanga leo inapambana na timu ya Kagera Sugar chini ni picha ya mmoja wa viongozi wa Yanga akifukia kitu katika uwanja wa kaitaba jana.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU