Facebook Comments Box

Tuesday, May 28, 2013

KIBADEN AANZA KASI RASMI SIMBA LEO

IMEWEKWA MEI 28, 2013 SAA 4:00 ASUBUHI
Kocha mpya wa Simba SC, Alhaj Abdallah Athumani Seif 'King Kibaden' au Chifu Mputa kulia akiwa na Wasaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo 'Julio' (katikati) na Suleiman Abdallah Matola 'Veron' kushoto kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Dar es Salaam asubuhi ya leo wakati kabla ya kuanza usaili wa wachezaji waliojitokeza kuomba kusajiliwa katika timu hiyo. Kibaden ameanza rasmi kazi leo na atasaini mkataba kesho.


Wazee wa Kijiwe; Jamhuri kulia na Matola kushoto wakiwa nje ya Uwanja wakiangalia vijana waliojitokeza kuomba kusajiliwa Simba SC wakati wanacheza kuonyesha vipaji vyao


Mchezaji wa kiungo aliyewahi kuchezea timu ya taifa ya vijana chini ya Jamhuhi  Kihwelo, Samuel Ngassa naye amejitokeza kuomba nafasi Simba SC


Matola akimpa taarifa muhimu Kibadeni, anayeandika


Kibadeni kulia na Matola aliyeipa mgongo kamera ya BIN ZUBEIRY 


Tabasamu mwanana; Kibadeni akifurahia kazi mpya Simba SC


Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala kulia na Meneja wa timu za vijana za Simba SC, Patrick Rweyemamu kushoto


Mungu nisaidie Kibadeni anione; Mmoja wa vijana waliojitokeza kujaribu bahati zao Simba SC akisali kabla ya kuanza kwa usaili


Sala inaendelea


Anamalizia sala


Anafunga sala
SOURSE:BIN ZUBEIRY


MUIGIZAJI DR CHENI ALISHWA SUMU



Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.
Akiongea na bongo movies leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.
Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema.
Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo.


HUYU NDIO ALIOKAMATWA AKIUZA UUME WA BINAADAMU


Jeshi la polisi nchini malawi wanamshikilia kijana mmoja baada ya kumkuta akiuza sehemu ya siri ya mwanaume.
Kijana huyo mwenye miaka 24 alikamatwa baada ya wananchi kutoa ripoti kituo cha polisi kuwa kunamzee kalala relini huku akiwa anatokwa damu nyingi 
 Polisi walifika eneo la tukio na kumkuta mzee huyo akiwa hoi na kuamua kumkimbiza hosipitali.

Baada ya kufikishwa hosipitali, madaktari  gundua kuwa mzee huyo alikuwa amejeruhiwa kwa kukatwa sehemu zake za siri...

Madaktari hao walilipoti kwa maofisa hao wa polisi na ndipo msako mkali ulipo pita katika wilaya ya Lakeshore mjini Salima na polisi hao kufanikiwa kumtia mbaroni kijana huyo baada ya kumkuta  akiwa katika gesti bubu akijaribu kuuza uume huo kwa dola za kimarekani 360.
  Mtuhumiwa Samuel Banda
Polisi walisema mtuhumiwa Samuel Banda alikamatwa na kiungo hicho ambacho alikuwa amekifunga katika karatasi nyeupe.

Mtuhumiwa alikiri kuwa huwa anauza viungo mbalimbali vya binadamu kwa wafanya biashara maarufu nchini humo ambao wanaamini wakivipata viungo hivyo huwasaidia katika biashara zao na huwaongezea utajiri.
 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU