Facebook Comments Box

Thursday, February 28, 2013

HUYU NDIO MKURUGENZI MPYA WA BENKI YA NBC

NATIONAL BANK OF COMMERCE
PRESS RELEASE


The National Bank of Commerce (NBC) has today announced the appointment of Mizinga Melu as its new Managing Director, subject to regulatory approval. The appointment is with effect from 20th May 2013.

Mizinga is joining NBC from Standard Chartered Bank Zambia where until now she has been Managing Director since 2007. She takes over from Lawrence Mafuru, who left the bank in December, 2012.

Mizinga has previously served in senior roles at Standard Chartered, including as Global Head of Development Organisations in the United Kingdom where she was responsible for strategy development and implementation as well as Africa Regional Head of Financial Institutions in Kenya and South Africa where she led formulation of Standard Chartered’s FI business strategy in Africa. Prior, she served as Head of Treasury at Standard Chartered Bank Tanzania between 2000 and 2003.

Mizinga holds a Masters in Business Administration (MBA) from Henley Management College (UK) and is an Associate of the Chartered Institute of Bankers (A.C.I.B). She holds numerous other banking qualifications.

Commenting on the appointment, Barclays Africa Chief Executive Officer and Head of Africa Group Strategy, Kennedy Bungane said: “The appointment of Mizinga reiterates the importance of NBC to our ‘One Africa Strategy’ and we are excited that she is joining us at a time we are making steady progress towards our goal of becoming the go-to bank in Africa.”

Dr. Mussa Juma Assad, Chairman of NBC commented: “The board welcomes Mizinga to NBC and looks forward to working with her in maintaining the position of NBC as a leading bank in Tanzania.”

Commenting on her appointment, Mizinga said: “NBC has over the years proven to be an important financial services provider in Tanzania. I am privileged to have the opportunity to lead this great bank at this important moment and I am looking forward to working with every colleague in NBC as we continue on our journey of transforming the bank in the market.”

Mizinga will report directly to Kennedy Bungane, Barclays Africa Chief Executive Officer and will be a member of the Barclays Africa Executive Committee.


WAKILI: MAHAKAMA IMUONE PONDA HANA KESI YA KUJIBU



UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi ya Sh. milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imuone Ponda na wenzake wanakesi ya kujibu kwa sababu umeweza kujenga kesi yao.

Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya upande wa Jamhuri unaowakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na Inspekta wa Polisi,  Hamisi Said na upande wa utetezi unaowakilishwa na Juma Nassor na Njama kuwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo ya kuomba mahakama iwaone washitakiwa wanakesi ya kujibu au la.

Kweka ambaye alitumia dakika kumi tu kuwasilisha majumuisho alidai upande wa Jamhuri umeweza kujenga kesi yake kupitia mashahidi wake 16 na vielelezo 13 walivyovileta mahakamani ambapo waamini kisheria vitawafanya washitakiwa wapande kizimbani kujitetea.

Wakili wa utetezi Nassor Juma akiwasilisha majumuisho yake, aliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu na waachiliwe huru kwa sababu upande wa Jamhuri umeshindwa kujenga kesi yao.

Nassor alidai wanachokiona katika kesi hiyo ni kuwa kuna mgogoro wa ardhi ambao ulitakiwa ukatatuliwa kwanza na Mahakama ya Ardhi kwa mujibu wa kifungu cha 167 cha Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, “Sisi upande wa utetezi tunaiomba mahakama hii iwaachilie huru washitakiwa wote na iwaone hawana kesi ya kujibu kwas ababu kesi hii imefunguliwa kwa jazba na polisi na upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao utaweza kuishawishi Mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu,” alidai wakili Nassor.

Hakimu Nongwa aliarisha kesi hiyo hadi Machi 4 mwaka huu, ambapo atakuja kutoa uamuzi wa ama kuwaona washitakiwa wana kesi ya kujibu au la na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe rumande kwa sababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.



KUFELI KIDATO CHA NNE:LAWAMA ZINAPO MFIKIA NYERERE

Picture

UNAAMBIWA HII NDIO HOTELI NDEFU KULIKO ZOTE DUNIANI: ANGALIA NA MANDHARI YAKE

Hivi ndivyo jengo hoteli hiyo inavyo onekana

Hii ni sehemu ya kupumzika na kupata chakula kwenye hoteli hiyo



Hata hapa chakula kinalika






Hoteli hii imefunguliwa Dubai Tarehe 26 baada ya kupata hadhi ya Hoteli ndefu kuliko zote duniani kutoka kwa Guinness World Records ambao ni watunza kumbukumbu wa matukio wa dunia.
Hoteli hii ina mita 355 ambazo ni sawa na futi 1,099. Jengo refu kuliko yote duniani lina mita 828 ambazo ni sawa na mita 2,717

 

 

 

 

 



KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI ASKARI WAWAZUIA WANAHABARI


SAKATA la mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23), limeendelea kuchukua sura mpya baada ya wanahabari kunusurika kupigwa na askari polisi ambao walikuwa wakiwazuia kusogea katika chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo. Askari polisi hao wakiwa zaidi ya 10 walitumia nguvu za ziada katika kuwadhibiti wanahabari wa vyombo mbalimbali waliofika kusikiliza na kuripoti mwenendo wa kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji ya mwanahabari mwenzao, Mwangosi aliyeuwawa Septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi wakati wa polisi walipokuwa wakitumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) aliokuwa katika shughuli za ufunguzi wa matawi ya chama hicho. Hata hivyo moja kati ya mbinu waliyopata kuitumia leo wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani hapo ni kuwafukuza waandishi wa habari eneo hilo la mahakama na kumtoa mtuhumiwa huyo kwa kificho cha hali ya juu kwa kumweka katikati ya watuhumiwa wa makosa mingine zaidi ya 8 huku mtuhumiwa akijificha sura yake kukwepa kamera za waandishi na baadhi ya askari wakimkinga ili kukwepa kupigwa picha. Tukio hilo lilitokea muda wa saa 6.10 mchana wakati mtuhumiwa huyo askari alipokuwa akitolewa na watuhumiwa wengine kutoka chumba cha mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Iringa na kumpeleka katika chumba cha Mahakama ya wazi kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa tena. Hivyo katika hali ya kushangaza ni pale askari hao kuwataka wanahabari hao kusongea umbali wa meta 700 kutoka eneo la Mahakama hiyo wakati mtuhumiwa huyo akiingizwa katika chumba cha Mahakama ya wazi mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa, Gladys Barthy ili kesi hiyo iweze kutajwa kwa zaidi ya mara ya tano sasa bila upelelezi kukamilika. Uamuzi wa askari hao uliwashangaza hata baadhi ya wananchi waliofika kusikiliza kesi na kuwawekea dhamana ndugu zao na kulazimika kuungana na wanahabari kupinga uamuzi huo na kusababisha askari kuwafukuza pia wananchi hao na kuwataka waungane na wanahabari kuondoka eneo hilo la chumba cha mahakama. Hakimu mkazi mkoa wa mkoa wa Iringa mheshimiwa Barthy alisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi hao kuwazuia wanahabari si maagizo ya Mahakama na kuwa wanahabari hao walikuwa huru kuingia kusikiliza kesi hiyo na kuhabarisha umma kwani hakukiwa na siri wala hakuna maagizo ya mahakama ya kuwataka polisi kuwafukuza wanahabari mahakamani hapo. “Kwanza nawapa pore sana kwa misukosuko mlioipata ....ila mimi nilikuwa ndani ya mahakamani sikujua kinachoendelea huko nje ya mahakama ila nawahakikishieni kuwa kesi hii ilikuwa ikisikilizwa katika mahakama ya wazi na mlikuwa huru kusikiliza,” alisema hakimu huyo akiakimhoji mmoja kati ya viongozi wa polisi kuhusu polisi hao kunyanyasa wanahabari na kuwataka kutorudia kufanya hivyo tena. Mwendesha mashitaka wa serikali Blandina Manyanda aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo na kuwa upelelezi bado haujakamilika na mahakama hiyo kupanga tarehe 14 machi ambapo kesi hiyo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.

SOURCE: WAVUTI



BAADA YA KUJAZWA MAHELA MILOVAN AONDOKA BONGO


ALIYEKUWA kocha wa Simba Milovan Cirkovic ameondoka nchini jana alfajili na shirika la ndege ya Uturuki baada ya kufanikiwa kulipwa fedha zake dola 32 alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kocha huyo ambaye alikuja nchini mapema mwezi huu kwa ajili ya kudai fedha zake baada ya kudanganywa na uongozi wa Simba kuwa wanamtamlipa fedha zake bila mafanikio yoyote ndipo aliamua kuja kudai mwenyewe.

Hata hivyo baada ya kusota muda mrefu huku viongozi wakiwa wanampa ahadi kila siku hatimaye jana alfajiri alifanikiwa kuondoka baada ya kulipwa deni lake la Dola 32 kutoka kwa Malkia wa nyuki Rahma Al Kharoos ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na mfadhili wa klabu hiyo.

Kocha huyo ameondoka na rekodi ya ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0 dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
 
Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema kuwa uongozi wake haupaswi kulaumiwa kwa kusajili wachezaji wasio kuwa na uwezo bali anayetakiwa kulaumiwa ni aliyekuwa kocha wao Mserbia Milovan Cirkovic.

Rage alisema kuwa wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni pendekezo la kocha huyo ambaye alitimuliwa raundi ya kwanza baada ya timu kutofanya vizuri katika michezo yake ya mwisho.

Alisema awali waliwaleta wachezaji wawili kutoka Cameroon lakini kocha aliwakataa na kuwasajili wachezaji wake ambao aliwataka yeye.

Aliongeza kuwa haoni sababu ya wao kulaumiwa kwa sababu wao ni uongozi na sio wachezaji na kuongeza kuwa kama watu wanawalaumu wao wanacheza namba ngapi uwanjani.

Rage akiwa anatoa kauli hiyo tayari kocha Milovan kwa upande wake alikwisha sema kuwa katika wachezaji ambao alitaka wasajiliwe aliyesajiliwa ni Mrisho Ngassa pekee na wengine uongozi ulishindwa.

Msimu huu simba iliweza kusajili beki Lino Musombo, Kanu Mbiyavanga (Congo), Patrick Ochierg (Kenya) na Komabil Keita (Mali).

Lakini baadaye waliwaacha wachezaji watatu na kumbakiza mmoja Keita kwa madai ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri katika timu yao.


DOLA 337,000 ZATUMIKA KUNUNUA iPAD BUNGENI

 

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.


BUNGE nchini Uganda limetumia zaidi ya  dola 377,000 kununa kompyuta aina ya iPad kwa ajili ya wabunge wote .
Maofisa wa bunge hilo walisema kuwa mbali na kuwaweka wabunge hao karibu na  ulimwengu wa teknolojia, wanatarajia kuwasaidia kupunguza gharama za fedha zinazotokana na matumizi ya uchapishaji wa nyaraka mbalimbali.
Kamishna wa bunge hilo Elijah Okupa alisema kuwa kompyuta hizo ni bora na zinafaa kwa matumizi hivyo ni vyema zikatumiwa vizuri.
Alisema  iPad hizo zitakuwa ni mali ya wabunge lakini kama mtu atatumia kwa muda wa miaka mitano asitegemee itakuwa na ubora uleule wa kumwezesha mwingine atumie kwa miaka hiyo alisema Okupa
Kwa mujibu wa takwimu kutoka katika bunge hilo zilionyesha Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya dola 12 katika miaka miwili sasa kwa ajili ya mahitaji ya kama kompyuta, uchapishaji wa nyaraka, mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mawasiliano kuwa bora katika bunge.
Kwa mujibu wa mbunge kutoka mashariki, Medard Segona alisema kuwa kutokana na uwepo wa ipad hizo wanategemea kupunguza matumizi ya fedha zilizokuwa zikipotea hapo awali.
‘’Vifaa hivyo vitapunguza sana matumizi ya fedha kwa kuwa hapo awali wizara ya fedha ilikuwa ikichapisha zaidi ya nyaraka 400 kwa kila mbunge na maofisa wengine waliopo ndani ya bunge hilo’’alisema
Aliongeza kuwa komputa hizo ni muhimu kwa utendaji kazi hasa katika kipindi hicho cha kuendeleza matumizi ya teknolojia.
Hata hivyo taarifa zilisema kuwa wabunge hao bado hawana uelewa mzuri juu ya matumizi hayo licha ya kuwa kampuni imeahidi kutoa  mkataba wa mafunzo ambayo pia yatasaidia kupunguza gharama za matumizi.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU