Facebook Comments Box

Wednesday, January 2, 2013

HII NDIO SIKU AMBAYO SAJUKI ATAZIKWA

TAARIFA ULIYOKO MPAKA MUDA HUU NI KUWA MAZISHI YA JUMA KILOWOKO 'SAJUKI' YATAKUWA IJUMAA SAA TANO KWENYE MAKABURI YA KISUTU DAR ES SALAAM

HALI ILIVYO NYUMBANI KWA MAREHEMU SAJUKI

 Mke wa marehemu, Juma Kilowoko 'Sajuki', Wastara Juma, akiwa na simanzi nzito kwa kumpoteza mumewe.
 Baba mzazi  wa marehemu, Juma Kilowoko 'Sajuki' akiwasiliana na ndugu na jamaa msibani hapo.…
 Dada wa marehemu Sajuki akilia kwa uchungu.


Bibi wa marehemu Sajuki akiwasili msibani leo.
Pichani juu ni baadhi ya taswira za waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Juma Kilowoko 'Sajuki', Tabata- Bima jijini Dar es Salaam. Sajuki amefariki dunia leo alfajiri akiwa katika hospitali ya taifa Muhimbili ambapo alikuwa akitibiwa.


BREAKING NEWS: SAJUKI AFARIKI DUNIA

Msanii wa filamu nchini Juma Kilowoko maarufu kwa jina la Sajuki amefariki dunia leo alfajiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kwa mujibu waa katibu wa chama cha waongoza filamu wilaya ya ilala Juma Amir Sajuki alikuwa akisumbuliwa na upungufu wa damu.
Sajuki alipata maradhi ambayo yalisababisha aende kutibiwa India. Hivi karibuni akiwa jukwaani Arusha Sajuki alizidiwa na kushindwa kusalimia washabiki wake.
Hivi sasa ilikuwa ikifanyika mipango apelekwe India tena na milioni 28 zilikuwa zikitafutwa kwa safari hiyo.
Inna Lillah wa inna illah rajiuun.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU