Facebook Comments Box

Wednesday, June 5, 2013

KOCHA WA YANGA AWASILI KWA AJILI YA KUINOA TIMU KWA AJILI YA MSIMU MPYA

Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Ernie Brandts (kulia) baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam usiku wa leo akitokea kwao Uholanzi kwa mapumziko mafupi baada ya kumaliza msimu, tayari kuanza maandalizi ya kikosi chake kwa msimu mpya. Aliyemlaki kushoto ni Meneja wa Yanga SC, Hafidh Saleh.

Anaondoka Airport 

Baada ya kutua, kitu cha kwanza aliwasha simu yake

Anafungua mlango wa gari lake apakie mizigo

Anafungua mlango wa nyuma apakie mizigo

Hahitaji msaada wa mtu, anapakia mwenyewe

Anafunga mlango baada ya kupakia

BIN ZUBEIRY anaondoka baada ya kumaliza kazi yake

Brandts naye anapanda gari lake

Anapiga stata...


Anaondoka Airport 


POLISI WATUMIA MBWA KUTAWANYA WATU LEADERS BAADA MUDA WA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KUISHA

Asakari Polisi wakitumia mbwa kutawanya maelefu ya watanzania waliotaka kuuaga mwili wa Mangwea baada ya muda uliopangwa kukamilika
ASKARI wa Jeshi la Polisi walilazimika kutumia Mbwa kuwatawanya mamia ya Watanzania waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu Albert Mangwea lakini wakashindwa baada zoezi hilo kukatishwa.
Mangewa alifariki Dunia nchini Afrika Kusini katika Jiji la Johannesburg Mei 28 mwaka huu na kusafirishwa kuja nchini jana jioni, mamia hao wa watanzania wameshindwa kuuaga mwili wa kipenzi chao baada muda ulioapngwa kukamilka huku wakibaki katika foleni ndefu.
Kitendo cha Kamati ya maandalizi kukatisha zoezi la kuuaga mwili wa marehemu kwa sababu ya muda uliopangwa kukamilika iliwashangaza mamia ya watu waliokuwa kwenye foleni ya kusubiri kupata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho mbele ya Jeneza la Mangwea.
Zoezi hilo liloanza saa 2:30 asubuhi imesitishwa saa 6:30 mchana kwa saa za Afrika Mashariki na Kati, na msafara ukiongozwa na Askari wa Jeshi la Polisi pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama waliokuwa katika Viwanja vya Leaders Club.
Barabarani Asakari wa Kikoso Cha Usalama Barabarani pia walijiapanga vizuri kuhakikisha kwamba msafara wa mwili wa marehemu unapita vizuri katika maeneo yaliokuwa yamepangwa kuelekea mjini Morogoro.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Mr Blue alifika katika viwanja hivyo akiwa amechelewa na kukosa muda wa kuuaga mwili wa Mangwea lakini alipokutana na mashabiki wa muziki wake aliweza kusimama na kuwapa pole.
Mwili wa Mangwea hivi sasa uko safarini kuelekea Mjini Morogoro ambapo utalala nyumbani kwa mama yake na kesho uwakazi wa Mji huo pia watapata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho

ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUKUTWA AKIMBAKA BINTI WA MIAKA KUMI

Mkazi mmoja wa Mwangata katika Manispaa ya Iringa amenusurika kuuwawa na wananchi baada ya kukutwa akimbaka binti wa miaka kumi.

Tukio hilo linaelezwa kutokea jana saa nane mchana, pale ambapo mazazi wa binti huyo alipomsikia mwanaye akilia kwa uchungu, na aliposogea kujua kulikoni, alimshuudia kijana huyo akiendelea na ubakaji jambo lililosababisha apige kelele kuomba msaada wa wananchi.


 
Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya ubakaji katika eneo hilo, mtuhumiwa huyo alijikuta akipokea hasira za wananchi kwa kupigwa na kunusurika kuchomwa moto baada ya baadhi ya wananchi wengine kushauri afikishwe polisi.

Mtuhumiwa huyo amefikishwa katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa akivuja damu kichwani.

PICHA ZA UWANGWAJI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA LEO VIWANJA VYA LEADERS



Umati wa watu wakiwa wamepanga mstari tayari kwa kwenda kuaga huku kikosi cha msalaba mwekundu na polisi kikiwa stand by just incase anything happens. Sasa naskia watu badala ya kwenda na kuaga wao wako busy wanapiga picha kha hizi teknolojia aiseee tutajutaaaa 
Baadhi ya ma super star wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga.
Jeneza likiandaliwa kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho


Diamond akiwa dada yake Queen Darlin


Diamond akimuaga Ngwair









MADIWANI WAPENDEKEZA JINA LA MKOA MPYA LIWE MBOZI, MAKAO MAKUU YAWE VWAWA

KIKAO cha dharura cha Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Mbeya kimependekeza jina la mkoa mpya wa Mbeya liwe ni Mkoa wa Mbozi badala ya mkoa wa Rungwe kama ilivyopendekezwa na wataalamu,wenye makao yake makuu wilayani Mbozi katika mji wa Vwawa. Wakizungumza katika kikao hicho Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya walisema kuwa azma ya kupendekeza kuwepo kwa mkoa mpya katika wilaya ya Mbozi umezingatia jiografia ya mkoa na fursa za kiuchumi zilizopo badala ya hamasa za siasa. ‘’Sisi ni madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya, hatuna maslahi yoyote ya kisiasa na wilaya ya Mbozi, tumezingatia fursa za kiuchumi na jiografia ya mkoa ambayo italeta tija na maslahi kwa Taifa,’’alisema Bw. Mashauri Mbembela Diwani wa kata ya Nsalaga. Awali katika mapendekezo hayo ambayo yaliwasilishwa na Ofisa Uchaguzi wa wilaya kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya Bi. Marietha Mlozi,Bw.Edward Mwaigombe alisoma taarifa ya mapendekezo ya jina la mkoa mpya kuwa ni Rungwe kama lilivyopendekezwa na wataalamu. Bw. Mwaigombe alisema kuwa, taarifa ya wataalamu imezingatia vigezo vya idadi ya watu, ukubwa wa eneo, huduma zilizopo na mawasiliano ambayo ni mapendekezo kutoka katika kamati za maendeleo za kata 14 za Ulenje, Lwanjilo, Ikukwa, Swaya, Mshewe, Igale, Iyunga Mapinduzi, Tembela, Bonde la Songwe, Utengule Usongwe, Ilungu, Ilembo na Inyala. Alisema kuwa kamati zilipendekeza mkoa wa Mbeya ugawanywe katika mikoa miwili ya Mbeya na Rungwe ambapo mkoa wa Mbeya wenye takwimu ya idadi ya watu 1,721,795 na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 41,544 umependekezwa kuundwa kwa wilaya za Chunya,Mbozi,Momba, ambapo makao yake makuu yanatarajiwa kuwa jiji la Mbeya. Bw. Mwaigombe alisema kuwa mkoa wa pili ambao una takwimu ya watu 985,915 na ukubwa wa eneo wa kilomita za mraba 22,073 unatarajiwa kuundwa na wilaya za Mbarali, Rungwe,Kyela na Ileje na makao yake makuu yanatarajia kuwa katika wilaya ya Rungwe. Aidha katika taarifa hiyo kwa madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, ilipendekezwa kuanzishwa kwa wilaya mpya kutokana na jiografia na kuzingatia mgawanyo mpya wa mkoa kati ya wilaya ya Mbeya na Halmashauri ya Jiji la Mbeya na kupendekezwa wilaya hizo zigawanywe katika wilaya tatu. Hata hivyo katika mapendekezo ya madiwani wa halmashauri hiyo walisema kuwa mji wa Mbalizi ujigawe kutoka katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya na ujitegemee kuwa wilaya kamili. Katika mapendekezo ya awali madiwani walipendekeza majina mawili ya mkoa wa Mbozi na Mkoa wa Songwe ambapo jina la mkoa wa Mbozi lilipitishwa na madiwani kwa kura 24 dhidi ya kura 3 ambapo baadaye majina mawili ya mkoa wa Rungwe na mkoa wa Mbozi nayo yalipigiwa kura na jina la mkoa wa Mbozi lilipita kwa kura 24 dhidi ya kura tatu za jina la mkoa wa Rungwe. Akizungumza katika kikao hicho Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya Bw. Mwalingo Kisemba alisema kuwa mchakato huo umekuja baada ya ushauri na mapendekezo ya kuugawa mkoa wa Mbeya ambao kwa sasa una jumla ya watu milioni 2.7 na ukubwa wa kilomita za mraba 63,617.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU