Facebook Comments Box

Friday, June 5, 2015

BARCELONA NA JUVENTUS ZAWASILI KATIKA JIJI LA BERLIN TAYARI KWA FAINALI YA UEFA JUMAMOSI TAR 06-05-2015

 Mabasi ya timu hizo kama yanavyo onekana hapa:
Andrea Pirlo kama anavyo onekana hapo akishuka kwenye ndege:


175 WATHIBITIKA KUFARIKI KATIKA AJALI YA MOTO GHANA

Takriban watu 175 wamefariki mpaka sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.

Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na stima.

Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto huo, Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
 
Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.

Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena. Bwana Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu, Accra alipotembelea eneo la tukio.



AFISA MMOJA WA FIFA AKIRI KUPOKEA RUSHWA

Wizara ya Sheria ya Marekani imechapisha taarifa inayoelezea jinsi Afisa wa zamani wa FIFA Chuck Blazer alivyokiri kuwa yeye pamoja na wenzake walipokea rushwa ikiwa ni pamoja na kuichagua Afrika Kusini kuwa mwenyeji wa fainali ya kombe la dunia mwaka 2010.

Katika taarifa hiyo imeweka wazi mtandao wa malipo ya rushwa ulivyokuwa ukifanywa ndani ya shirikisho la soka duniani FIFA, taarifa zinazoegemea uchunguzi uliofanywa na shirika la kijasusi la Marekani FBI.

Taarifa hiyo ambayo inamwelezea Afisa huyo wa zamani wa Fifa kukiri kupokea rushwa sasa huenda ikaibua mengi kwenye kashfa ya rushwa inayoindamana shirikisho la FIFA.

Mmerakani huyo kwenye taarifa hiyo inadai alikuwa ni mmoja wa watu waliosuka mipango ya kupokea rushwa katika tukio jingine la fainali la kombe la dunia 1998.

Taarifa za Kukiri zipo katika maandishi wakati wa kesi yake mwaka 2013 ilipokuwa akisikilizwa katika mahakama ya Easten New York huko Marekani ambapo alikiri makosa kumi yaliyokuwa yanamkabili.

Blazer alikuwa afisa wa ngazi ya juu wa FIFA eneo la kanda ya Amerika Kaskazini na Kati na ukanda wa nchi Caribbean kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2011.

Marekani imefungua kesi ya rushwa inayowakabili maafisa wa FIFA jambo lililofanya Rais wa FIFA Sepp Blatter kuamua kutangaza kujiuzulu.

CHANZO: BBC

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU