Facebook Comments Box

Friday, January 25, 2013

LULU KUENDELEA KUKAA MAHABUSU

Elizabeth Michael.

Kutokana leo kuwa siku ya sikukuu Dahamana ya Elizabeth Michael maarufu kama Lulu imepelekwa mbele mpaka jumatatu ya tarehe 28 January, 2013. Msanii huyo anahitaji Shilingi za kitanzania milioni 20 ili kupata dhamana hiyo. Binti huyo anashitakiwa kwa mauaji ya kuto kukusudia ya msanii mwenzake Steven Kanumba na amekuwa ndani tokea April 2012 mpaka leo.


HATIMAYE SERIKALI YAPUNGUZA MAKATO UWANJA WA TAIFA

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makala (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari, ofisini kwake katikati ya Jiji leo, kuhusu kupunguza makato ya mapato ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kukubali kulipa kodi za mishahara wa makocha wa timu ya taifa. Kulia ni Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah. 


Angetile Osiah: Katibu wa TFF akisaini hati ya makubaliano hayo.






Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kamati ya Ligi Kuu, Silas Mwakibinga akisaini hati ya makubaliano kuhusu matumizi ya Uwanja wa Taifa na mgawanyo wa mapato.source bin zubeiry


BREAKING NEWS: MABOMU YARINDIMA DUMILA SASA HIVI



Katika hali iliyodumu muda mrefu sana ya mapigano kati ya wakulima na wafugaji katika wilaya ya Kilosa imechukua hatua mpya. Sasa hivi kuna vurugu kubwa kati ya wakulima na wafugaji ambapo hadi gari la mkuu wa wilaya limechomwa moto. Muhabarishaji wetu kutoka eneo hilo anasema kuwa hali ilifikia hivyo baada ya mkuu wa wilaya kuhalalisha mashamba ya wakulima kuwa kijiji cha wafugaji. Mpaka sasa polisi wa kuzuia ghasia wapo eneo hilo wakipiga mabomu.

Hali ya usafiri imekuwa tete kutokana na ghasia hizo. Mahakama iliamua suala hilo lipelekwe kwenye utawala na mkuu wa wilaya siku ya jumatano kaamua Mabogile kiwe kijiji hali hiyo ndio iliyoleta vurugu zote. Mkuu wa wilaya alipopigiwa kutoa maelezo ya sakata hilo alioomba apigiwe simu jioni.


KIGOMA: KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAKATIZA MKATABA NA MKANDARASI

 
Kikao cha kamati ya ulinzi na usalama chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Mkoa Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya kimeridhia kusitishwa kwa Mkataba wa Mkandarasi M/S Kalyango Contructoins And Building Company Limited aliyekuwa akijenga daraja Nkwasi Wilayani Uvinza.

Mkandarasi Kalyango  Construction alikabidhiwa eneo la kazi Julai 5, 2012 na kutakiwa kukamilisha ujezi wa daraja la NKWASI   Okitoba 15, 2012, lakini pamoja na kuongezewa muda hadi Desemba 30, 2012 mkarandasi huyo alishindwa kukamilisha kazi hiyo.

Hadi anasimamishwa mkarandasi huyo alikuwa amelipwa zaidi ya milioni 25.7 ambazo ni kati ya shilingi milioni 97.4 alizostahili kulipwa kama angekamilisha ujenzi.

Baada ya taarifa ya mkuu wa mkoa safari  ikawa ni kuelekea eneo la ujenzi ambapo meneja wa wakala wa barabara mkoani Kigoma Narisi Choma ndiye aliyetoa taarifa kwa wafanyakazi wa  mkarandasi Kalyango kuwa hawatakiwi kuendelea na kazi.

Muda na  kwa nyakati tofauti wajumbe wa kamati ya  ulinzi na usalama, katika ziara zao, wamekuwa wakiwaonya wakandarasi wanaofanyakazi chini ya kiwango, kauli ambazo zinaungwa mkono na wakazi wa mwambao wa kusini mwa ziwa Tanganyika.




HUU NDIO USHAHIDI WA CHADEMA KUWA NAPE SIO MTOTO WA BRIGEDIA NNAUYE

Image and video hosting by TinyPic

Hoja ya Chadema ni kwamba kama Nape angekuwa mtoto halali wa Marehemu Brigedia Moses Nnauye basi lazima angetajwa kwenye tangazo hilo la kumbukumbu ya kifo cha mwanasiasa huyo maarufu. Je jina la Nape lilisahaulika kimakosa?Je hoja ya Chadema ina ukweli ndani yake?Labda Nape atajitahidi kutolea ufafanuzi tashwishwi hii.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU