Facebook Comments Box

Sunday, January 6, 2013

MCHUNGAJI AMBILIKILE AOTA TENA DAWA MPYA

Mchungaji Mstaafu Ambilikile Mwaisapile wa KKKT Loliondo ameitaka serikali kukaa mkao wa tayari tayari maana anadai ameoteshwa dawa mpya ambayo atakapo itangaza na kuanza kutoa tiba itajaza watu wengi katika kijiji hicho cha Loliondo. Hakuwa tayari kuweka wazi ni dawa aina gani ambayo ameoteshwa sasa hivi na itatibu magonjwa gani. Pamoja na kumdadisi ili aeleze kama masharti ni yaleyale au yamebadilika Mchungaji Mwaisapile hakuwa tayari kuweka wazi mpaka muda utakapofika.
Hii inaonekana inaweza ikawa neema tena kwa wafanyabiashara ya usafiri wa mkoa wa Arusha na Manyara pamoja na wakazi wa kijiji hicho cha Loliondo maana kwa idadi kubwa inayoenda huko biashara huwa inakuwa kubwa sana.
Mchungaji Ambilikile aliteka vichwa vya habari vya vyombo mbalimbali kwa dawa ambayo aliota mara ya kwanza kwa kipindi hiki umaarufu wake na jina lake lilikuwa likitoweka katika midomo na vichwa vya watanzania tusubiri kuona kama atarudi tena kwenye chati kama zamani.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU