Facebook Comments Box

Saturday, June 1, 2013

MANJI: NGUVU YA YANGA SASA IMEELEKEZWA KWENYE UJENZI



Uongozi wa Yanga umesema umeelekeza nguvu zake katika kuanza ujenzi wa Uwanja wao wa kisasa kwenye eneo la Kaunda jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amesema wamekuwa wakiendelea na mchakato huo na mambo yatakapokamilika, kazi ya ujenzi itaanza.
“Usione tuko kimya, mchakato unaendelea nasi tunahitaji muda kwa ajili ya kujadili, kujipanga na baadaye kuanza.

“Kamati inayohusika na masuala hayo inaendelea tunakutana na wahusika na kujadili halafu tunaangalia nini kinaendelea na nini tuendelee nacho.


“Hivyo mnatakiwa kuvuta subira na baadaye mtaona mambo yanaendelea,” alisema Manji.

Tayari uongozi Yanga ulishateua kamati inayoshughulikia suala hilo iliyo chini ya Ridhwani Kikwete.

Lakini kampuni inayohusika na ujenzi wa uwanja huo kutoka China, ilishakabidhi ramani tatu kwa Yanga na wanatakiwa kuchagua moja ambayo itumike na ujenzi.


SOURSE: SALEH JEMBE


KAMA UNAMKUMBUKA KIBAKULI SASA HIVI YUPO HIVI

DSC00429Unamkubuka jamaa anaitwa Sadiki Mberwa maarufu kama Kibakuli, alikuwa staa kwenye maigizo ya Kaole kama mtoto mnoko wa Muhogo mchungu ambaye anajua kama baba yake ana nyumba nje lakini hamwambii mama yake mzazi. Mwisho wa siku na yeye anakuja kumtaka kimapenzi mama yake mdogo.

Kikubwa kilichokuwa kinamtamburisha Kibakuli ulikuwa ubonge wake, tofauti na sasa amekuwa mwembamba na amekuwa mtu mzima. Kibakuli alianza kuigiza kwenye miaka ya 1999 yupo darasa la sita wakati akiwa na Nyamayao ambaye alikuwa anaigiza kama dada yake. Hivi sasa Kibakuli ni soundman wa Landline Production na soon atarudi tena mbele ya camera. 
k
Kibakuli


YANGA NA SIMBA HATIHATI KUSHIRIKI KAGAME

Siku kadhaa baada ya Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati - CECAFA kuidhinisha michuano ya kombe la Kagame kuchezwa mjini Darfur -Sudan, serikali ya Tanzania imetoa tamko kuhusu timu za Simba na Yanga kwenda kushiriki michuano hiyo huko Sudan kwenye eneo ambalo limekuwa likiandamwa na vurugu kwa miaka kadhaa sasa.
 Kwa mujibu wa msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga ni kwamba serikali haidhani ni busara kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenda kwenye eneo hilo kushiriki Kagame Cup kutokana hali mbaya ya usalama iliyopo Darfur.
HIVI NDIVYO ALIVYOANDIKA KAMWAGA KWENYE UKURASA WAKE WA FACEBOOK.
 


NIPENI DILI WA MANGWEA




KIBONZO: NANI MJINGA?




TUMKUMBUKE NGWAIR KWA HUU WIMBO WAKE WA SHE GOT A GWAN




KIBONZO: ANGALIA HIKI KITUKO CHA BIBI HARUSI HUYU




FALCAO ATUA RASMI MONACO


KLABU ya Monaco usiku wa jana imethibitisha kumnasa mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao kutoka klabu ya Atletico Madrid.
Mabingwa hao wa Ligi Daraja la Kwanza Ufaransa, wamepania kuipindua Paris St Germain katika matawi ya juu ya Ligi Kuu Ufaransa.
New surroundings: Atletico Madrid's Radamel Falcao has joined Monaco
Monaco imesema katika tuvuti yake kwamba: "Monaco imefikia makubaiano na  Atletico Madrid na mchezani mwenyewe (Radamel Falcao) kwa uhamisho wa msimu  wa 2013-14.


KILIMANJARO: KITUO CHA MABASI CHA BOMA NG`OMBE CHAFUNGWA KWA MUDA

Kituo kikuu cha mabasi cha wilaya ya Hai kilichopo katika mji wa Boma Ng'ombe kimefungwa kwa muda  ili kupisha matengenezo makubwa ya kuweka lami.

Mkuu wa wilaya ya Hai, Novatus Makunga amewaeleza waandishi wa habari kwamba matengenezo hayo yanayokana na ahadi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010.

Ameeleza kuwa matengenezo hayo ya kipande cha urefu wa kilometa 0.85 utachukuwa siku 45 kwa gharama

 ya shilingi milioni 90.

Amefafanua kwamba matengenezo hayo yataunganisha barabara inayoingia kituoni hapo na ile ya Moshi hadi Arusha pamoja na kukiwekea lami.

Makunga ameeleza kuwa wakati kituo hicho kikiwa kimefungwa, hivi sasa kinatumika kituo cha muda katika eneo la Double Road. Ameeleza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2012/2013, Halmashauri ya wilaya ya Hai ilitengewa jumla ya shilingi 460,810,000 katika mfuko wa barabara.

Wilaya ya Hai ina barabara zenye urefu wa kilometa 466.2 ambapo kati ya hizo, kilomeya 32 ni barabara kuu, kilometa 42 ni za mkoa, kilometa 175.93 ni za wilaya na kilometa 150.27 ni za vijiji na barabara za Hai ni kilometa 66. Amesema kuwa barabara zinazopitika nyakati zote ni kilometa 235.53 ambazo ni sawa na asilimia 50.82.



PICHA YA RAIS MUGABE AKITAFAKARI KWA MAKINI KWENYE KIKAO

african leader sleeping addis ababa
HII ILIKUA NI MJINI ADISABABA MAY 26 MWAKA HUU KATIKA KIKAO CHA VIONGOZI WA AFRIKA



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU