Facebook Comments Box

Saturday, April 26, 2014

WILAYA MBILI KUUNDWA MKOA WA DAR ES SALAAM

Mkuu wa Mkoa wa DarEs Salaam
Said Mecky Sadick.
Wilaya mbili zinatarajiwa kuongezwa na kufanya idadi ya
wilaya kuwa tano katika jiji la Dar Es Salaam. Wilaya hizo
ni Kigamboni na Ubungo.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Said
Mecky Sadick wakati wa kuhitimisha kikao na baraza la
Mashauri jijini Dar Es Salaam siku ya Jumanne ambapo
wilaya ya Kigamboni itagawanywa na kuwa na majimbo
mawili ya Mbagala na Kigamboni.
“Mapendekezo hayo yatafikishwa kwenye serikali kuu na
uamuzi wake utatolewa mwezi ujao’, alisema Mkuu wa
Mkoa , ambaye alikuwa mwenyekiti wa baraza hilo,
lililokuwa likijadili pia muswada wa bajeti wa mwaka wa
fedha wa 2014/2015.
Wilaya hizo zitaungana na Manispaa za Kinondoni, Ilala na
Temeke za jijini Dar Es Salaam linalokadiriwa kuwa na
watu zaidi ya milioni 4.5 .


MKUTANO WA TAASISI YA DHI NUREYN WAANZA ARUSHA

Wajumbe kutoka sehemu mbalimbali duniani wamefika jijini Arusha kwa ajili ya mkutano mkubwa ulio andaliwa na taasisi ya Dhi Nureyn Tanzania yenye makao makuu mkoani Iringa.
Taasisi hiyo huji usisha na utoaji wa misaada na uendelezaji wa dini.
Sasa hivi taasisi hiyo inamiliki radio inayosikika mikoa ya nyanda za juu kusini.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU