Facebook Comments Box

Sunday, February 22, 2015

CHELSEA YATOKA SARE NA TIMU AMBAYO HUWA INAISUMBUA KATIKA LIGI BURNLEY

 Mshambuliaji wa Burnley akisawazisha bao na kufanya sare ya 1-1


Ivanovic akiifungia timu yake bao la kwanza katika mechi hiyo likiwa ni goli la 4 katika michezo 6 aliyocheza.
Mchezaji wa Chelsea Matic alipewa kadi nyekundu na kutolewa katika mchezaji huo baada ya kumsukuma mchezaji wa Burnley mpaka kumdondosha chini baada ya awali kumchezea rafu.
Wachezaji wa Burnley wakipongezana baada ya kufanikiwa kusawazisha wakiwa ugenini na kufanya mpambano huo kumalizika kwa kufungana 1-1.


ARSENAL YAICHAPA CRISTAL PALACE UGENINI

 Wachezaji wa Arsenal wakishangilia bao la kwanza lililofungwa katika dakika ya 8 na Sant Carzola
 Sant Carzola akishangilia baada ya kuipatia timu yake bao la kwanza likiwa ni bao lake la 7 katika msimu huu.
Straiker Force Giroud akiwatoka walinzi wa Cristal Palace na kufunga bao la pili na la ushindi kwa Arsenal lakini likiwa ni bao lake la 5 katika michezo saba aliyocheza.
Hapa Beki na kipa wa Cristal Palace wakiokoa michomo ya Monreal na Kosienly wa Arsenal


LEO NDIYO LEO FAINALI YA LIGI DARAJA LA KWANZA KATI YA MWADUI FC NA AFRICAN SPORTS YA TANGA NDANI YA AZAM COMPLEX CHAMAZI


Mwadui FC

African Sports

Fainali ya kumsaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), inatarajiwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika leo kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TTF imelazimika kuhamishia mchezo huo Chamazi.

Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.

Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia. Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Lakini pia katika uwanja huo wa Azam Cmplex kutakuwa na mpambano mwingine wa wenyeji Azam watakao cheza na Tanzania Prisons ambapo mchezo huo utaanza majira ya saa mbili kamili usiku.

Mjini Shinyanga wenyeji timu ya Stand United wataikaribisha Simba SC kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku wagonga nyundo wa jiji la Mbeya, timu ya Mbeya City wakicheza na timu ya Young Africans kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA

MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


WATAKA KUWA NA LADY JAY DEE COMMANDO, MAMAA SOME FOOD? ONA SIFA ZA MWANAUME AMTAKAE

 Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee hapa akiwa na aliyekuwa mumewe ambae wameachana Gardner G Habash ambae kwa sasa ni Mtangazaji wa kituo cha E-FM kilichopo Dar es Salaam.
Lady Jay Dee akiwa amesimama nyuma ya gari lake Range Rover.


Kama wewe ni Mwanaume mwenye ndoto za kuwa na Nyota huyu wa Muziki wa Tanzania angalia sifa alizo orodhesha katika mtandao wa Instagram huenda ukawa wewe.

Jide ambae ameachana na aliyekuwa mumewe kwa sasa yupo single na ameonekana kutaka kuwa na mtu mwingine ambae atakuwa na sifa ambazo amezitaja kuwa ni Anaejali na kujiheshimu, Mwenye roho ya upendo na huruma, Anaeweza kum take care financially, Asiechepuka hovyo, Asiwe tegemezi, Hata kama sio tajiri lakini asimtegemee yeye, Asiwe mlevi kupindukia wa kulala bar au kulala nje kwa "machangu" wa kinondoni au wa sehemu yoyote.

Lakini pia Jide amesema kuwa kwa sasa ana marafiki wengi lakini wengi wao ni wa kiume ambao walio wengi ni wa kutoka nje ya nchi na huwa anakutana nao kwenye mikusanyiko ya watu wengi na urafiki wao ni wa kubadilishana mawazo, kwenda dinner, na kualikana majumbani kufungua shampeni na kuchoma nyama. "Kama mmeniona nao huko We were just having fun", nothing serious alisisitiza Jide.

Amesema kwa sasa anae mpenzi wa miaka mingi sana ambae amekuwa akimpa karibia kila anachotaka kama vile, Amemjengea nyumba, amemnunulia viwanja, magari, anamlisha na kumvisha pia anamsomeshea ndugu zake, Amemfungulia Restaurant na ameahidi kumnunulia Beach House na Land Rover model ya 2015 ila hizo ni ahadi bado hajazitimiza.

Kila akitaka kwenda holiday anagharamia kila kitu, akitaka kwenda kwa Fans wa Paris analipa tena anmlipia ndege Business Class. "Sasahivi ameahidi kunilipia Trip ya Italy nikawaone kina Kayumba, Shopping na n.k tena hajawahi kunisaliti. JE WAMJUA HUYU MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI?, ANAITWA "MUZIKI".

Ila akasema maswali kuhusu mambo ya ndoa yake atayajibu siku nyingine ili aongelee maswala hayo tu hataki kuchanganya na mambo mengine maana yamesemwa mengi.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU