Facebook Comments Box

Wednesday, September 26, 2012

TOVUTI ZA SIMBA NA YANGA ZAFUNGWA
















Katika hali ya kusikitisha na kushangaza zile tovuti za klabu kubwa za mpira hapa Tanzania za Yanga na Simba leo zimekuwa hazipo hewani. Watu mbalimbali ambao wamekuwa wakizitafuta kupata habari za klabu zao hizo kongwe. Wamekuwa wakikuta ujumbe unosema "This account has been suspended"
Baadhi ya wataalamu wa mambo ya mawasiliano wanasema hali hiyo itakuwa inatokana na kushindwa kulipia gharama za tovuti hizo kuwepo hewani. Tovuti ya yanga ni www.youngafricans.co.tz na ile ya watani wao wa jadi ni www.simba.co.tz
Juhudi bado zinafanyika kujua nini sababu ya tovuti hizo kutokuwepo hewani zote kwa pamoja kwa wakati mmoja. Ikumbukwe klabu hizi mbili ndio zinaongoza kwa kuingiza mapato na pia zina udhamini mnono.

OKWI KUIKOSA MECHI YA YANGA

Taarifa nilizozipata usiku huu kamati ya ligi iliyokutana leo imemfungia mshambuliaji wa Simba,Emmanuel Okwi michezo mitatu pamoja faini ya tsh 500,000 kutokana na kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo dhidi ya JKT RUVU kwa kosa la kumpiga kiwiko Kessy Mapande.
Kutokana na adhabu hiyo Emmanuel Okwi ataukosa mchezo dhidi ya Yanga. 

 HIVI NDIVYO ALIVYOPATA KADI NYEKUNDU






 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU