Facebook Comments Box

Thursday, July 11, 2013

VIDEO: MWANAMKE AKIMPIGA MUME WAKE HADHARANI

.
.
Ni ngumu kumuona mwanaume akitokwa machozi kama hivi…. hii imetokana na mke wake kumpiga makofi hadharani kwenye mji wa Meru nchini Kenya ambapo Mwanamke huyo alikua anadai jamaa kamkana, japo anasisitiza kwamba ni mume wake na ndio baba wa watoto mapacha akiwemo mmoja alienae mgongoni, Mwanaume alikataa kabisa na kusema hata watoto sio wake.
Taarifa ambayo imerushwa na KTN Kenya, ni kwamba alichotaka Mwanamke ni Mwanaume huyo akubali tu kwamba ni mume wake na pia ndio baba watoto wa mapacha hao… lakini Mwanaume aliapa kabisa kwamba hausiki kwenye upande wowote, hicho ndio kilichompa hasira Mwanamke na kuanza kumpiga na baadae pia kusaidiwa kupiga na Mwanamke aliekua nae.
Kenya imekua kwenye mfululizo wa kesi za Wanawake kupiga waume zao nyumbani na hadharani pale wanapokosana ambapo February 2012 Umoja wa Wanaume Kenya ulitangaza kususia kula majumbani kwa wiki moja na kununua chakula hotelini mpaka Serikali itakapoingilia usawa wa Wanaume na kuhakikisha tabia ya Wanawake kupiga Waume zao inamalizwa.





MAWAIDHA: NAMNA YA KUSWALI NA SHEIKH RAMADHAAN KURIA BIN KAGUO




AKODI NDEGE YA KIFAHARI KWA MILIONI 162 KUMSAFIRISHA PAKA WAKE

Paka mwenye jina Marsik wa Urusi amesafirishwa na ndege binafsi ya Paramount Business Jets (PBJ), kutoka Urusi hadi Marekani kwa gharama ya dola laki moja ambazo ni sawa na shilingi milioni 162 za Tanzania.
Akisafiri kutoka Urusi hadi Marekani, Marsik anadaiwa kupata huduma ya nguvu kabla hajapanda na ndani ya ndege hiyo.
Vyeti vyake vya afya vinavyoonesha chanjo alizopata alivipata saa 24 kabla ya safari kuanza.
Tajiri huyo anadai kutumia kiasi chote hicho ili kuhakikisha kuwa paka wake anafika Marekani salama na kuepuka kunyanyasika ama kifo kwakuwa baadhi ya wanyama wanaosafiri kwa ndege za kawaida huwekwa kwenye sehemu ya mizigo hupoteza maisha.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU