Facebook Comments Box

Sunday, October 6, 2013

SIKILIZA WIMBO MPYA WA DIAMOND




YANGA YASOGEA KILELENI SASA BAADA YA KUITUNGUA MTIBWA SUGAR

IMEWEKWA OKTOBA 6, 2013 SAA 2:38 USIKU

Mshambuliaji wa Yanga SC, Mrisho Ngassa (wa pili kushoto) akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam jioni ya leo, 

Mshambuliaji wa Yanga SC, Didier Kavumbangu akimtoka beki wa Mtibwa Sugar, Salim Abdallah

Kavumbangu akitafuta maarifa ya kumtoka Salim Abdallah

Mrisho Ngassa alimpiga kanzu kipa wa Mtibwa, Hussein Sharrif 'Cassilas' lakini akapigiwa filimbi ya kuotea

Beki wa Mtibwa, Hassan Ramadhani akimdhibiti Mrisho Ngassa wa Yanga

Beki wa Yanga, David Luhende akiwatoka wachezaji wa Mtibwa, Ally Shomary na Salim Abdallah

Salim Abdallah wa Mtibwa akijiandaa kuondosha mpira kwenye hatari mbele ta Kavumbangu 

Beki wa Mtibwa Sugar, Dickson Daud akimiliki mpira mbele ya mshambuliaji wa Yanga SC, Didier Kavumbangu  

Kiungo wa Yanga SC, Nizar Khalfan akimtoka beki wa Mtibwa, Paul Ngalema

Kiungo mkongwe wa Mtibwa, Shaaban Nditi akipasua katikati ya wachezaji wa Yanga SC, Mbuyu Twite kulia na Didier Kavumbangu kushoto

Hata hivyo, Twite alimuangusha Nditi...

Shaaban Nditi akiwatoka Said Bahanuzi na Kavumbangu wa Yanga

Kikosi cha Yanga SC leo

Kikosi cha Mtibwa leo

Didier Kavumbangu akishangilia baada ya kufunga bao la pili 

Mpiga picha wa Azam TV, akirekodi kwa ajili ya matangazo ya Live ambayo kwa sasa yanarushwa kupitia TBC 

Kiungo wa Yanga SC, Athumani Iddi 'Chuji' akiwaongoza wenzake kuingia uwanjani tayari kwa mechi 

Pamoja na kuwa na maumivu ya jicho, kipa Deo Munishi 'Dida' alianzia benchi leo                 CHANZO BIN ZUBEIRY   


PICHA: MAZISHI YA DADA YAKE MBOWE


Umati mkubwa wa waombolezaji .katika mazishi ya dada wa Mwenyekiti wa Chadema,marehemu Grace Mbowe


Seehemu ya viongozi wa serikali na wa vyama vya siasa pamoja na wananchi waliojitokeza katika mazishi ya dada wa Mwenyekiti wa Chadema,marehemu Grace Mbowe


Watoto wa marehemu wakitoa heshima ya mwisho kwenye jeneza la mama yao
Grace Mbowe.



Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akiwa na viongozi wa dini pamoja na ndugu wengine
wakati wa mazishi ya dada yake marehemu Grace Mbowe.


Ndugu wa marehemu wakionekena wenye huzuni wakati wa mazishi ya ndugu yao Grace Mbowe.


Mbunge wajimbo la Moshi mjini Philemoni Ndesamburo akitoa pole kwa niaba ya Chadema taifa kwa mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge,William Lukuvi akitoa salamu za rambi rambi kwenye msiba wa dada wa kiongozi wa kambi rasmi ya upinzania Bungeni Freeman Mbowe.


Mbunge wa jimbo karatu Mchungaji Yohana Natse akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wabunge wa Chadema.




Wafanyakazi wenza na marehemu Grace Mbowe wakitoa salamu zao wakati wa mazishi hayo.


Watoto wa marehemu Grace Mbowe wakizungumza jambo wakati wa mazishi ya marehemu mama yao.


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya chama chake.


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma akimkabidhi rambi rambi toka CCM mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.


Baadhi ya viongozi wa vyama na serikali wakiwa katika mazishi ya marehemu Grace Mbowe.


Mwili wa marehemu ukipelekwa kaburini tayari kwa maziko.


Waombolezaji wakijiandaa na maziko


Watoto wa marehemu wakilia kwa uchungu.


Jeneza likishushwa kaburini


Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiteta jambo na mwanasheria Albert Msando wakati wa mazishi hayo.


Mbunge wa jimbo la Moshi mjini akiongea na mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Reginald Mengi.


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu dada yake,Grace Mbowe.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge,William Lukuvi akiweka shada la maua kwenye kaburi la dada wa Freeman Mbowe.

Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiweka shada la maua kwenye kaburi la dada wa Freeman Mbowe.
Mbunge wa jimbo la Moshi Mjini Philemon Ndesamburo akiteta jambo na mbunge wa zamani wa jimbo la Vunjo Aloyce Kimaro (kulia) wakati wa mazishi ya dada wa Freeman Mbowe


Mwenyekiti wa makampuni ya IPP akiteta jambo na mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga aliyekuwa mfanyakazi wa ITV kabla ya kupata wadhifa wa ukuu wa wilaya. Picha zote na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii

KIBONZO CHA LEO: VIGOGO WETU

Picture

TAARIFA: TATOA YASIMAMISHA KUSAFIRISHA MIZIGO NCHI NZIMA

PictureMsemaji wa TATOA nchini, Elias Lukumay
Chama cha wamiliki wa malori Tanzania (TATOA), leo Oktoba 5, 2013 kinatangaza kusimamisha kusafirisha mizigo nchi nzima kutokana na Wizara ya Ujenzi kuondoa nafuu ya kutolipa tozo ya uzito wa magari uliozidi asilimia tano (5% tolerance) ya uzito unaokubaliwa kisheria.

Tozo ya nafuu kwa uzito uliozidi asilimia tano (5% tolerance) ilitolewa na serikali mwaka 2006 baada ya kamati iliyoundwa na serikali pamoja na TATOA kubainisha kuwa mizani mingi nchini hazina uzani sawa, hali iliyopelekea kutofautiana kwa vipimo kwa mzigo mmoja.

Jambo la pili lililopelekea kuwekwa kwa tozo ya nafuu kwa mzigo uliozidi asilimia tano ya uzito ulikubaliwa ilikuwa ni ubovu wa barabara nchini pamoja na matuta (bumps) mengi ambayo yalikuwa yanapelekea mizigo kuyumba, wakati mizani hazifanyiwi uwianishi (calibration) wa mara kwa mara.

Sababu za Serikali kwamba tozo hili ya unafuu inapelekea uharibufu wa 

barabara na ongezeko la uzidishaji mizigo, hazina ukweli wowote, kwa kuwa tatizo la uzidishaji mizigo lilikuwa kubwa zaidi awali, kabla ya tozo ya unafuu haijawekwa, lakini pia TATOA, kama mdau mkubwa kwenye ujenzi wa barabara zetu katu hangependa kuona zinaharibika.

TATOA inaamini kuwa zoezi hili limefanywa kwa makusudi kuidhoofisha sekta, hasa kutokana na ukweli kwamba zoezi hili halikushirikisha wadau yaani TATOA, na pia juhudi za TATOA kufanya majadiliano na waziri husika zimepuuzwa.

Lakini zaidi ni kuwa ondoleo la tozo hili limekuja wakati ambapo serikali haijatekeleza malalamiko mengi kutoka kwa TATOA, hali ambayo inaonyesha dharau ya wazi kwa sekta ambayo ni ya pili kwa kuchangia pato la taifa.

Kwa muda mrefu sasa, TATOA imekuwa ikilalalamikia maswala ya ongezeko kubwa la bima, ukosefu wa sehemu za kupaki magari, tozo la barabara, uwepo wa geti moja tu kwenye mpaka wa Tunduma hali ambayo imepelekea msongamano na ucheleweshaji wa mizigo uliokithiri na sasa tozo ya asilimia tano (5% tolerance).
 
TATOA inaamini kwamba mambo haya yanazungumzika, na kusimamisha usafirishaji sio suluhisho la matatizo, lakini ukaidi wa wizara na waziri husika ndio vimepelekea hali hii.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU