Facebook Comments Box

Saturday, October 13, 2012

MNYAMA AANZA KUSUASUA




DK: Mpira unamalizika hapa uwanja wa Mkwakwani kwa matokeo ya sare tasa.

DK 85: Simba  0 - 0 Coastal

DK 78: Atupele Green anakosa bao la wazi 

DK 75: Coastal wanafanya mabadiliko anaingia Danny lyanga anatoka Soud.

DK 68: Simba wanafanya mabadiliko anatoka Daniel Akuffoer anaingia Salim Kinje.

DK 65: Nsa Job anapewa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi ya pili ya njano.

DK 63: Nsa Job anapiga shuti kali linaokolewa kwa ustadi mkubwa na Juma Kaseja.

DK 60: Mwamuzi anawapa kadi za njano Nsa Job na Amir Maftah.

DK 55: Coastal wanakosa bao la wazi huku Simba wakifanya mabadiliko anatoka kinda Haruni Chanongo anaingia Uhuru Suleimani.

DK 47: Anaingia Lameck Dayton kuchukua nafasi ya Razack Khalfan aliyeumia.

DK 46: Kipindi cha pili kinaanza na ghafla Razack Khalfan anakaa chini akionekana kuwa na maumivu, machela zinambeba na kumtoa nje ya uwanja kwa jinsi inavyoonekana sidhani kama atarudi dimbani.

Mpira ni mapumziko hapa Mkwakwani Simba 0 - 0 Coastal.

DK 45: Coastal wanaendelea kuishika nafasi ya kiungo kwa sababu Selembe, Razack na Santo wanaelewana sana pia udhaifu wa Boban katika kukata unawapa wakati mgumu Kiemba na Kazimoto katika kuweza kumiliki dimba.

DK 40: Nsa Job anakosa bao la wazi bada ya kazi nzuri iliyofanywa na Selemani Kassim.

DK 35: Timu zote zinafanikiwa kufika kwenye lango la wapinzani lakini wanashindwa kuzitumia nafasi zao vizuri.

DK 30: Coastal 0 - Simba

DK 26: Simba wanapata kona yao ya kwanza lakini haizai matunda.

DK 25: Coastal wanaonekana kutawala sehemu ya kati ya kiungo inayochezwa na Jerry Santo na Razack Khalfan.

DK 20: Coastal 0 - 0 Simba

DK 15: Kichwa kizuri cha Felix Sunzu kinatoka nje.


DK 13: Haroun Chanongwa anapiga bonge la shuti linagonga mtambaa wa panya kipa wa Coastal Chove anashindwa kuzuia.


DK 10: Simba 0 - 0 Coastal


DK 9: Coastal wanafanya shambulizi la kushtukiza na mpira unatoka juu ya lango.


DK 1: Mpira unaanza hapa mkwakwani - Simba wamevaa jezi nyeupe na bukta nyekundu, Coastal wamevaa jezi nyekundu juu nyeupe chini.
endelea kufuatilia mtandao huuu tutakuletea picha zote za mchezo huu wa leo. 


PICHA YA JOE MAKINI YAVUJA

Picha ikimuonesha mwamba wa kaskazini a.k.a mweusi Joe makini akiwa na mrembo warda. picha hii imevuja. samahani lakini.....

KWA HERI KAMANDA LIBERATUS BALLOW

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza RPC Liberatus Ballow ameuwa usiku wa kuamkia leo na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi katika eneo la Kitangiri karibu na Hotel ya Tai Five majira ya kati ya saa saba hadi nane. Haya yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza Injinia Everest Ndikillo wakati akitoa taarifa za tukio la kuuawa kwa Kamanda Ballow. Tukio hilo ambalo limeacha simanzi kubwa kwa wakazi wa jiji la Mwanza pamoja na familia yake huku watu wa kijiuliza kuhusiana aliyehusika na mauuaji hayo ya kikatili. Taarifa ya Mkuu wa Mkoa zinasema kuwa Kamanda Ballow alikiuwa anatoka katika kikao cha harusi na ndugu yake aitwaye Sembeli Maleto kilichokuwa kinafanyika katika Hotel y a Florida na kish akumpelek amwanamke aitwaye Dorcas Moses Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Nyamagana maeneo ya barabara ya Kona ya Bwiru kwenda Kitangiri. Walipofika getini kwa Mama Dorcas mara waliwaona watu wawili wakiwa wamevaa makoti ya PolisiJamii, Mama Dorcas alimuuliza Kamanda Ballow kama anawafahamu Kamanda akasema kuwa hawa na watu wa ulinzi wa Jamii wako doria. Mara wale watu waliongezeka na kuwa sita wakaanza kama kuzozana wao kwa wao na ndipo Kamanda alipowauuliza kuna nini, Mmoja wao akajibu hakuna kitu na ikapelekea Kamanda kutaka kutoka nje ila wale watu watatu wakaizingira gari ya Kamanda Ballow aina ya Rav 4. Kamanda Ballow alipoona kama hali hewa inabadilika alichukua redio call ili aweze kuwa taarifu askari na ndipo wale jamaa walipompiga risasi kichwani nakupelekea kifo chake. Taratibu za mazishi ya Kijeshi bado zinaendelea na nyumbani kwa marehemu ambapo mwandishi wa blogu hii amefika na kukuta watu mbalimbali wakiwa katika hali ya majonzi sana. Mke wa Kamanda Ballow yuko Dar es Salaam na anatarajia kufika Mwanza. Mpaka sasa Polisi wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Dorcas kwa ajili ya Mahojiano huku uchunguzi mkali ukiendelea kuhusiana na kifo cha kamanda Liberetus Ballow.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU