Facebook Comments Box

Wednesday, October 22, 2014

MSANII WA WANAUME FAMILY AFARIKI DUNIA TEMEKE HOSPITALI

Msanii Yesaya Ambilikile a.k.a YP aliye katikati ya Chege Chigunda kushoto na Mheshimiwa Temba kulia.

Hapa Yesaya Ambilikile anaonekana akiwa amesimama Kulia Kwa Stuko na Dogo Asley, na Waliokaa chini ni Said Fela a.k.a Mkubwa Fela(Meneja wa Kundi hilo) na Mheshimiwa Temba.


Aliyewahi kuwa msanii wa kundi la TMK Wanaume Family,Yesaya Ambilikile"YP"alifariki dunia usiku wa kuamkia jana(21-10-2014, Jumanne) katika hospitali ya Temeke baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kifua.

Utakapo taka kumtaja au kumkubuka YP ni lazima utamkumbuka au kumtaja Msanii Y-Dash kwakuwa wawili hao walikuwa Wanaume Famili kabla ya kutoka kwa madai kuwa hawapati maslahi yao wakiwa ndani ya kundi hilo na kuamua kuunda kundi lao ambalo lilijulikana kwa jina la majina yao ambalo ni 'YP NA Y-DASH'.

Kabla ya kuondoka Wanaume family YP anakumbukwa zaidi pale aliposhiriki vizuri kwenye Wimbo wa Chege Dar mpaka Moro,

Wasanii hawa walitoka baada ya msanii nguli wa Temeke Juma Kassim Kiroboto a.k.a JumaNature kujitoa ndani ya kundi hilo kwa madai kuwa kuna wasanii wengi ndani ya kundi hawapewi nafasi na hivyo hali hiyo inaweza kusababisha kuuwa vipaji vyao, ndipo akajitoa na kwenda kuunda Wanaume Halisi akiwa na Dolo. Na wakafanikiwa kurekodi wimbo wao wa Kwanza ujulikanao kama NDEGE TUNDUNI.


Akizungumza na mtandao huu Kiongozi wa kundi hilo Said Fela, amethibitisha kutokea kwa msiba huo. “Mpaka sasa hivi bado hatujaandaa ratiba, tunamsubiri kaka yake kwa sababu huyo mtu kafariki usiku hospitali. 

Kwahiyo ndugu zake wakishakuja ndiyo watasema tunazike vipi, kwa sababu alikuwa mkristo. Kwahiyo kwenye saa saba mchana ratiba itakuwa tayari,” alisema Fela.
 

“Tatizo alikuwa anaumwa kifua muda mrefu, lakini alishaanza kunywa dozi na juzi akazidiwa na tukampeleka hospitali. Jana ndo mwenyezi Mungu akamchukua. 

wazazi wake yaani Baba na Mama walifariki ila ndugu zake wapo keko, na kuna kibanda waliachiwa na wazazi wao, kwahiyo msiba utakuwa Keko.”


KURA YA MAONI YA KATIBA KUFANYIKA TAREHE 30 MACHI 2014



 Mwanasheria Mkuu wa Serikali JAJI FREDRICK WEREMA

Kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa itafanyika Machi 30 mwakani, Hayo yalisemwa jana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema ambaye hata hivyo alisema kwamba kabla ya kura hiyo, "lazima daftari la kudumu la wapigakura liboreshwe kwanza" ili kuwapa fursa wapigakura wapya ambao hawamo kwenye daftari hilo.


"Kuboreshwa kwa daftari la wapigakura ni lazima kwa sababu kuna watu wengi wamefikisha umri wa kupiga kura tangu tulipofanya uchaguzi mkuu na hawamo kwenye daftari hilo, kwa hiyo hatuwezi kuwanyima fursa ya kupiga kura kwa sababu ni haki yao kikatiba," alisema Jaji Werema na kuongeza.


"Lakini lazima tujue pia kwamba kuboreshwa kwa daftari hilo kunahitaji fedha, kwa hiyo kuboreshwa kwake kutategemea kama Serikali itatoa fedha kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ili kazi hiyo iweze kufanyika, tusipoboresha daftari tutasababisha kelele na malalamiko mengi".


Msimamo wa Jaji Werema ni sawa na ule wa Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva ambaye amesisitiza mara kadhaa kwamba tume yake haitoandaa uchaguzi wowote pasipo daftari la kudumu la wapigakura kuandikwa upya.


Jaji Werema alisema ikiwa Serikali itatoa fedha, uboreshaji wa daftari unaweza kukamilika ifikapo Februari 2015 na kwamba inatarajiwa Machi 30, mwakani kura ya maoni itapigwa kama kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa.


Alisema upigaji kura utatanguliwa na kampeni ambazo zitafanyika kwa siku 30 kuanzia mwanzoni mwa Machi ili kushawishi Katiba inayopendekezwa iungwe mkono au kinyume chake kwa makundi yanayoipinga.


Hadi sasa gharama za kusimamia kura ya maoni kwa ajili ya kupitisha Katiba Inayopendekezwa zimeendelea kuwa kitendawili.
Jana, Jaji Lubuva alisema asingeweza kuzizungumzia kwa kuwa yuko Dodoma kikazi na kuelekeza taarifa hizo zinaweza kupatikana kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Malaba.


Hata hivyo, alipotafutwa Malaba alisema anaweza kuzungumzia suala hilo katika mkutano na waandishi wa habari anaotarajia kuuitisha wiki hii.


SOMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 22 SEPTEMBA 2014 HAPA:




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU