Facebook Comments Box

Sunday, August 31, 2014

MWANAZUONI MKUBWA ALHABIB UMAR IBN HAFIDH AWASILI KENYA

Mwanazuoni Mkubwa duniani Alhabib Umar bin Salim bin Hafidh jana amewasili jijini Nairobi Kenya katika ziara ya mwaliko wa Sheikh Al-Amoudy ambapo atakuwa nchini humo kwa muda wa wiki moja.




Katika ziara hiyo Alhabib Umar atafungua Markaz ya Dar Al-Mudathir iliyoko Malindi ambapo ni tawi la chuo cha Dar al Mustafa kilichoko Yemen. Mbali na Nairobi na Malindi sehemu zingine atakazotembelea ni Eldoret,Mombasa na atafungua misikiti kadhaa.




Angalia ziara yake kamili Alhabib Umar hapo chini.

-SAT. 30th AUG. -NAIROBI
Arrival: 7PM
-SUN.31st AUG. -NAIROBI/MALINDI
Muslim Children's Home & Imtiaz Sunni MOsque in Nairobi:AM

Flight to Malindi:PM

-MON. 1st SEP. -MALINDI/MAMRUI/MALINDI
Ziyara of Ash-Sharif Sa'eed al-Beidh, Mamrui:AM
Opening of Dar al-Mudathir, branch of Dar al-Mustafa, Malindi:PM
Opening forum with scholars and public, Malindi: 4:15PM

-TUESDAY 2nd SEPT. - MALINDI/MOMBASA

Opening of Masjid Abu Bakr Siddiq at Kwachocha, Malindi: 11AM
Programme at Masjid Konzi, Mombasa: 6:45PM

-WED. 3rd SEPT. - MOMBASA

Opening of Masjid Nur, Kikambala: 11AM
Hawl of Imam al Haddad RA at Memon Villa Hall: 6:45PM
-THUR. 4th SEPT. -MACKINNON RD/MAKINDU
-FRI. 5th SEPT. -MAKINDU/ELDORET
Jumuah at Makindu: 12:30PM
Flight to Eldoret from Nairobi: PM
-SAT. 6th SEPT. -ELDORET/NAIROBI
Opening of Majma'ul Khayrat Insitute, Eldoret: AM


YANGA YATANGAZA KAMATI ZAKE

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wajumbe Wenza wa Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendelo ya Michezo), Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji, wanapenda
kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wanaYANGA,
wameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji ya YANGA zifuatazo:
 
1) KAMATI YA UFUNDI
 
Wajumbe:
1) Duduma, Nassoro
2) Lamlembe, Roger
3) Malulu, Pascal
4) Msolla, Peter
5) Zangira, Steve
 
2) KAMATI YA SOKA YA VIJANA NA WANAWAKE
Wajumbe:
1) Katwila, Shaban
2) Kabisa, Jessica (Advocate)
3) Mazwile, Isack
4) Mwita, George
5) Tembele, Ally Mayay
 
3) KAMATI YA MASHINDANO
Wajumbe:
1) Cheyo, Magembe
2) Didi, Ibrahim
3) Hussein, Ndama Risasi
4) Katabalo, Moses
5) Katunzi, Mudhamiri
6) Kihanga, Pascal
7) Kingo, Ray Shauri
8) Kleb, Abdallah Bin
9) Luhago, David
10) Lukumay, Samwel
11) Macha, Innocent
12) Maige, Jackson
13) Mahende, Mugaya
14) Makay, Sule
15) Malebo, Michael
16) Malume, Paul
17) Matata
18) Mbise, Anandumi Timothy
19) Mlangwa, David
20) Mogha, John
21) Mutaboyerwa, Joseph John
22) Ntimizi, Said
23) Nyambaya, Lameck
24) Nyika, Hussein
25) Nyumbamkaly,
26) Ramadhan, Fulgence
27) Rashid, Ahmed
28) Suleman, Majid
29) Tenga, Frank
30) Tindwa, Beda
31) Zakaria, Dr.
 
Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamatiza YANGA zilizotajwa hapo juu.
Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji Wajumbe Wenza wa
Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendelo ya Michezo) watakuwa
Wenyekiti Wenza wa Kamati zilizotajwa hapo juu.
Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa
katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa
watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka
kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze ketenda
kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA.
(YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO)
(BENO NJOVU)
KATIBU MKUU WA YANGA


SIMBA YAVUNA MAGOLI KWA KMKM

Beki wa Simba "baba ubaya" akipambana na mchezaji wa KMKM
SIMBA SC imewafunga mabingwa wa Zanzibar, KMKM mabao 5 - 0 katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara usiku huu uwanja wa Amaan,Zanzibar.

KMKM inayofundishwa na Ally Bushiri ‘Bush’ ambayo Jumatano wiki hii ilifungwa 2 - 0 na Yanga SC, leo iligeuzwa asusa na Wekundu wa Msimbazi.

Simba SC ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza mabao 4-0, yaliyotiwa kimiani na Hamis Tambwe mawili, Amir Kiembe na Shabaan Kisiga 'malone' moja kila mmoja.

Viongozi wa Simba wakiongozwa na Hans pope
Amri Kiemba ndiye aliyefungua karamu ya mabao ya Simba SC hii leo, dakika ya tatu ya mchezo baada ya kupewa pasi nzuri na kiungo Mrundi, Pierre Kwizera na kuwatoka wachezaji wawili wa KMKM kabla ya kufumua shuti kali lililogonga mwamba wa ndani wa lango.

Amisi Tambwe akafuatia dakika ya 14 baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa Salim Amour kufuatia yeye mwenyewe kupiga mkwaju wa penati, baada ya Kiungo Haroun Chanongo kuangushwa kwenye boksi.

Tambwe tena akafunga bao la tatu dakika ya 23 akimalizia krosi maridadi ya Ramadhan Singano 'Messi' kabla ya kisiga kufunga la nne dakika ya 37, kufuatia kazi nzuri ya Kiemba.

Mchezaji ambae yupo katika mgogoro na ambae hajajua hatma yake kama atacheza au hata cheza ligi Emmanuel Okwi akiwa katika benchi la simba akiangalia kama anaweza kupata namba katika kikosi hicho cha Simba.
Kipindi ha pili, kocha Mzambia, Patrick Phiri alibadilisha kikosi kizima akimuacha Nahodha Joseph Owino na dakika ya 60 Elias Maguri akahitimisha karamu ya mabao kwa bao safi la tano.

Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyetangaza juzi kurejea Simba SC kutoka kwa mahasimu wao Yanga SC usiku wa jana alikuwepo, lakini alibaki benchi muda wote wa mchezo.

Hamis Tambwe na Singano wakishangilia Goli
Viongozi wa Simba SC wakiongozwa Makamu wa
Rais, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ na Mwenyekiti
Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe, Kassim
Dewji, Musley Ruwey, Mohammed Nassor ‘Steven
Seagal’, Crescentius Magori, Said Tuliy na
wengineo walikuwepo kushuhudia mchezo huo.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa:
Ivo Mapunda/
Hussein Sharrif ‘Cassilas’ dk46/Peter Manyika
dk84, Miraj Adam/Abdi Banda dk46/Nassor
Mssoud ‘Cholo’dk84, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’/
William Lucian ‘Gallas’ dk46/Mohammed Hussein
‘Tshabalala’ dk84, Joram Mgeveke/Hassan Isihaka
dk46, Joseph Owino, Pierre Kwizera/Abdallah
Seseme dk46, Haroun Chanongo/Twaha Ibrahim
‘Messi’ dk46, Amri Kiemba/Ibrahim Hajibu dk46,
Amisi Tambwe/Elias Maguri dk46, Shaaban Kisiga
‘Malone’/Awadh Juma dk46 na Ramadhani Singano
‘Messi’/Uhuru Suleiman dk46.
KMKM; Salim Amour, Pandu Hajji, Faki Hamad/
Makame Hajji dk30, Juma Rashid/Nassor Ali dk30,
Halfan Khamisi/Mudrik Muhibu dk30, Moka
Shaaban, Ame Khamis, Abdi Kassim ‘Babbi’, Haji
Simba/Kassim Nemshi dk30, Maulid Ibrahim na
Khamis Ali.


WAZIRI MKUU AKIMBILIA AFRIKA YA KUSINI

Jeshi la Lesotho
Sawa Waziri mkuu nchini Lesotho Tom Thabane ameiambia BBC kwamba amelitoroka taifa hilo baada ya kupata vitisho vya maisha yake.

Akizungumza kutoka nchini Afrika kusini,Bwana Thabane amesema kuwa vitendo vya jeshi nchini humo vya kusitisha huduma za serikali na kusababisha mapinduzi.
 
Awali Ripoti kutoka mji mkuu wa maseru zilisema kuwa jeshi lilizingira makao makuu ya polisi na kuzuia matangazo ya radio pamoja na mtandao wa simu katika mji mkuu wa Maseru.

Uchaguzi uliozongwa na utata nchini humo miaka miwili iliopita ulisababisha kuundwa kwa serikali ya muungano isio dhabiti.
Licha ya mazungumzo ya kuleta amani mnamo mwezi Juni ,hali ya wasiwasi ilitanda huku majirani wa taifa hiilo wakionya dhidi ya
mbinu yoyote isio ya kikatiba.
 
Taifa hilo limezungukwa na Afrika kusini na hutegemea sana jirani yake kwa maslahi pamoja na nafasi za kazi.

Chanzo: BBC SWAHILI


Saturday, August 30, 2014

HII NDIO TIMU ANAYOENDA RADAMEL FALCAO

Mchezaji wa Monaco Radamel Falcao ameuthibitishia ulimwengu kuwa atajiunga na Madrid. Mchezaji huyo alituma ujumbe wa furaha katika akaunti yake ya tweeter na baadae kuufuta ujumbe huo ila tayari watu tulikuwa tumesha upiga picha.
 Wadadavuaji wengine wanasema huenda akaunti yake itakuwa imetekwa na maharamia wa mtandao maarufu kwa jina la kiingereza la "hackers "
Chini ni picha ya ujumbe huo.




RAIS KIKWETE ATEMBELEA SOKO LA MAZAO KIBAIGWA



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea soko la nafaka la kimataifa la Kibaigwa mkoani Dodoma katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo Agosti 28, 2014 , ambapo alijionea shehena kubwa sana ya mahindi iliyoletwa kutoka mashambani na kusafirishwa kila pembe ya nchi. Mwaka huu, kama ilivyokuwa mwaka jana, mavuno ya mahindi yamekuwa makubwa kiasi hata cha kupatikana kwa mavuno ya ziada yanayolemea maghala yaliyopo, ikiwa ni muendelezo wa mafanikio ya sera ya kilimo kwanza ambayo imekuwa ikileta matokeo mazuri kila mwaka. (picha hii na zote zinazofuata hapo chini ni kutoka Ikulu).














SALUM MWALIMU ACHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA CHADEMA

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Zanzibar Bi Maryam Ahmed Omar akimkabidhi fomu Salum Mwalim fomu ya kugombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho kundi la Zanzibar katika hafla fupi iliyofanyika ofisi kuu za CHADEMA kisiwani humo.

Mmoja wa wachama wa CHADEMA Zanzibar Bikwao Khamis akitia saini ya fomu ya udhamini wa Salum Mwalim (aliyesimama wa kwanza kushoto) anaegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho kundi la Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Jumbe Idrisa akitia saini ya fomu ya udhamini wa Salum Mwalim (aliyesimama wa kwanza kushoto) anaegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chjama hicho kundi la Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar

Salum Mwalim anayewania nafasi ya ujumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA kundi la Zanzibar akitia saini kitambu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi kuu za chama hicho Zanzibar kwa lengo la kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Mbunge wa CHADEMA viti Maalum wa CHADEMA Mwanamrisho Abama akimdhamini Mgombe Ujumbe wa Kamati Kuu wa Chama hicho Salum Mwalim katika ofisi za chama Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za CHADEMA Zanzibar.


MAJAMBAZI YABAKA NA KUPORA MILIONI 20

Watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wanadaiwa kumvamia mwalimu mmoja, wampora zaidi ya Sh. milioni 20 na kumbaka
mwalimu mwingine na kutokomea.

Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Nassa Ginery, wilayani Busega mkoani Simiyu.
Polisi mkoa wa Simiyu imethibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia juzi.
Akisimulia tukio, mwalimu aliyepatwa na mkasa huo, Samwel Mbochi alisema watu hao waliruka ukuta wa nyumba yake na kumvamia na kuanza kumshambulia mwilini na kudai awape pesa.
Alisema kuwa pesa hizo alikuwa ameziandaa kwa ajili ya kununua bidhaa kesho yake kwa kuwa amekuwa akijishughulisha na biashara
ya duka.

Alisema baada ya kuchukua pesa hizo, watu hao walimvamia mpangaji wake katika chumba kingine ambaye pia ni mwalimu na kumbaka kwa zamu kisha kutokomea kusikojulikana.
Afisa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani Simiyu, Evance Mwijage jana alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo. Mwijage alisema atawataja watu waliohusika kwenye tukio hilo
mara baada ya kupata taarifa rasmi kutoka polisi. 

CHANZO: NIPASHE


MAGAZETI YA LEO: JUMAMOSI TAREHE 30/08/2014





VIDEO: INSTAGRAM WAANZISHA HYPERLAPSE NA KAMERA YA KIPEKEE KWA MBWA

CHANZO: BBC SWAHILI

YANGA NA OKWI WAITWA NA TFF KWENYE KIKAO

Chini ni barua ambazo TFF wamewaandikia klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi kuwaita kwenye kikao cha kamati.



VIONGOZI WA SHURA YA MAIMAM WAMTEMBELEA DR SLAA

Viongozi wa Shura ya Maimam leo asubuhi wamemtembelea Dr. Slaa ofisini kwake iliyopo mtaa wa Ufipa Kinondoni. Lengo la ziara hiyo ni
kumweleza Dr. Slaa juu ya udhalilishaji wanaofanyiwa Masheikh 19 wanaotuhumiwa kwa kesi ya Ugaidi wakiwa chini ya vyombo vya
sheria.

Hivi karibuni imeripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari kuwa Mashekh hao wamekuwa wakidhalilishwa kijinsia na kuharibiwa sehemu za siri. Viongozi hao wamemwomba Dr. Slaa na Chama chake kuwaunga mkono katika kupaza sauti juu ya udhalilishaji huo na kumwomba ushirikiano katika maswala ya kisheria hasa ikizingatiwa kuwa CHADEMA ni wahanga wa matukio hayo ya udhalilishaji kwa vijana waliobambikwa kesi za ugaidi


Friday, August 29, 2014

UNANYASAJI MTANDAONI UMEMUUWA BETTY NDEJEMBI : TUPINGE UNYANYASAJI MITANDAONI

Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa watu wengine.Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: "kuuchukia ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli Kamwe asilani".

Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake binti huyo alinynyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo cha binti huyo, ukweli tu kwamba mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha flani.

Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu na
kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala
zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususan cha mtu maarufu.

Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni. Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki, wanaharamu na kila aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza. Kwa Twitter, matusi imekuwa ni njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye
'umaarufu' huko Twitter, na ukidadisi chanzo cha 'umaarufu' huo,
utaambiwa 'ah huyu ana matusi si mchezo!'

Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye
mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo. Marehemu aliitwa majina kadhaa ya
kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti. Kuna waliomwita Di Maria na wanajifahamu. Japo sijui chanzo cha 'ugomvi na aliogombana nao' (na ndio maana sikujihusisha nao kwani haukunihusu), kuna wanafiki wengi tu waliokuwa katika nafasi nzuri ya kuzima moto huo hasa kwa vile baadhi yao walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za 'ugomvi' husika.

La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni unafiki: baadhi ya watu walewale waliodiriki
kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa
wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake. Hii inanikumbusha
suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa, katika hali
ya utani japo wenye ukweli, kwamba 'wakati mwafaka kabisa wa
kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.

Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa
binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali Hata pasi uelewa wa taaluma ya saikolojia, tweets za aina hii zinaashiria tatizo, na laiti 'wenye upendo wa dhati' wangeingilia kati muda huo, huenda muda huu Betty asingekuwa marehemu.

Na hizo tweets mbili ambazo ni miongoni mwa za mwisho kabisa za
marehemu ni ushuhuda tosha wa jinsi alivyokuwa akisumbuliwa na
wanyanyasaji dhidi yake mtandaoni. Ndio pengine kilichomuua ni
maradhi ya kawaida ya kibinadamu lakini kila mwenye ubinadamu
hatoshindwa kuhusisha unyanyasaji huu na hali mbaya ya afya aliyokuwa nayo hadi anafariki.

Kuna watakaolaumu kuwa ninatumia kifo cha binti huyo kwa
'maslahi binafsi.' Hapana, sina maslahi yoyote binafsi hasa ikizingatiwa kuwa sikuwa nikifahamiana na marehemu. Hakuna anani-follow na mie sikuwa nam-follow. Labda maslahi pekee niliyonayo ni upinzani wangu mkali dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni. Vyovyote ilivyo, marehemu alikuwa burried kabla hajafariki na atakayetaka kukataa ukweli huo na akatae lakini utabaki kuwa ukweli usioweza kugeuka uongo. Na kwa hakika, kila
aliyeshiriki kumnyanyasa binti huyo atakuwa anasutwa na nafsi yake, hata kama atatafuta hifadhi kwenye 'huu sio wakati wa kulaumiana' au 'we failed you Betty.'

Mara nyingi nimekuwa nikiwalaumu watu wanaodai 'Instagram imekuwa mbaya' au Twitter imeharibika siku hizi' ambapo mara zote nimewakumbusha wahusika kuwa katika hii mitandao ya kijamii, ni muhimu kuwa makini katika nani wa kum-follow. Maana
yangu ni kwamba ukim-follow mtu mwenye matusi, utashuhudia matusi katika anachoandika. Ukim-follow mtu wa busara, utashuhudia busara. Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa tu la watu wenye busara na elimu zao lakini wepesi wa kuvutiwa na vitu vya 'kipuuzi' - umbeya, matusi, majungu, na upuuzi mwingine, na hawasiti kushea na wanaowa-follow. Ni hivi, mtu akitweet tusi, kisha ukali-retweet, utambue kuwa unalikuza (amplify) tusi hilo. Na kimsingi, kwa kiasi kikubwa, tuna-RT vitu tunavyoviunga mkono. Uki-RT tusi maana yake unaliunga mkono. Na ni wazi mwenye kujiheshimu, na kuheshimu 'watu wa maana' wanaom-follow hawezi
ku-RT upuuzi.

Tatizo kubwa sasa ni kwamba waweza kuamua kuwa-follow watu
unaodhani wana busara au akili za kutosha lakini ukaishia kusoma
vitu vya ajabu ajabu kwenye timeline yako kutokana na haya
'mahaba' ya ku-RT vitu vya kipuuzi. Binafsi, nadhani chanzo kikubwa cha mitandao ya kijamii kuwa 'sehemu za kukera, kuogopesha, kunyanyasana, nk' ni ile hali ya baadhi ya wenzetu kutokuwa na vitu muhimu vya kufanya katika maisha yao. Ni wazi kwamba ukiwa busy na maisha yako hutokuwa na muda wa kubughudhi wenzako.

Kingine kinachopelekea social media kuwa 'dunia uwanja wa fujo' ni ugonjwa mkubwa unawasumbua baadhi ya wenzetu: kusaka sifa
wasizostahili. Wanasema,. ashakum si matusi, 'lugha ya mpumbavu
ni matusi,' na ndo maana baadhi ya wenzetu wasio na cha maana cha kuongea katika hadhara hukimbili matusi, unyanyasaji, maneno
macha Nitamke bayana kuwa siandiki makala hii nikitegemea kuungwa mkono na wahusika wa unyanyasaji mtandaoni. Na kwa hakika kuna uwezekano mkubwa wa makala hii kuzua 'kampeni ya chuki' dhidi yangu kutokana na makala hii. Tatizo kubwa la wenzetu hawa ni kutotaka kuambiwa kuwa 'Hapana, hili ni kosa. Na kosa ni kosa, haliwezi kuwa sahihi.' Lakini pamoja na uwezekano wa 'kuwashiwa moto' kutokana na makala hii, wito wangu kwa kila mwenye busara na akili ni kuliangalia tukio hili la kusikitisha kama 'wake up call.' Tujifunze, tujisahihishe. Tuache kusherehesha vitu vya kipuuzi mtandaoni.

Ifike mahala, ukishindwa kumkemea mtu mwenye tabia mbaya mtandaoni basi chukua option rahisi ya kum-unfollow au ikibidi kum-block. Na ifike mahala kuwafahamisha watu wanaoendekeza utoto, majungu, umbeya, unyanyasaji na upuuzi mwingine kuwa kama hawana kitu cha maana cha kufany katika maisha yao basi isiwe sababu ya kuwasumbua wenzao wenye majukumu katika maisha yao. Tukemee maovu badala ya kutarajia yataondoka yenyewe tu. Tuomboleze kifo cha Betty kwa kusema 'NO' kwa cyberbullies (wanyanyasaji wa mtandaoni). Tufike sehemu tuache kuwasujudia wahuni wanaodhani matusi ni sehemu ya wimbo wa taifa. Tuwakwepe waendekeza majungu, wanyanyasaji, wataka sifa za kipuuzi, na watu wasiofaa katik maisha yetu. Wakati 'tunatafuta haki kwa marehemu Betty kutokana na unyama aliofanyiwa,' suala ambalo ni la kisheria, kilicho ndani ya uwezo wetu ni kukemea unyanyasaji mtandaoni (cyber bullying). Wakati hadi muda huu hatuwajui waliomfanyia marehemu unyama huo, takriban sote twawajua vema wanyanyasaji wa mtandaoni. Tuanze na hawa, kwani leo wamefanya kwa kwa marehemu Betty kesho itakuwa kwako.

Mwisho kabisa, ni muhimu kwetu sote kutambua kuwa tulitoka kwa
udongo na tutarudi kwa udongo. Kifo ni hatma ya kila mmoja wetu.Betty ametutoka lakini nasi twaelekea huko. Visa, chuki, kunyanyasana, na vitu vingine visivyopendeza japo ni kama sehemu
ya maisha yetu havipaswi kupewa nafasi katika maisha yetu haya ambayo hakuna mmoja wetu mwenye japo 'lue' ya lini yatafikia kikomo. TUPENDANE na TUHESHIMIANE.

Kwako marehemu Betty, hakuna tunaloweza kusema au kufanya sasa kurejesha uhai wako. Na hakuna neno sahihi la kuonyesha jinsi
gani kifo chako kimewagusa wengi. Kubwa tunaloweza kufanya ni kukuombea kwa Mwenyezi Mungu akupatie pumziko la milele na mwanga wa milele akuangazie upumzike kwa amani. Amina.

Chanzo: Vijimambo Blog


MAKUNDI YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE




BAADA YA KUWA NA MGOGORO NA YANGA OKWI RASMI SIMBA

NA BIN ZUBERY

STAILI ile ile waliyotumia Yanga SC kumpata mshambuliaji Emannuel Arnold Okwi ndiyo ambayo klabu yake ya zamani, Simba SC inatumia kumrejesha kundini Mganda huyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jioni hii mjini Dar es Salaam,
Okwi amesema kwamba amesaini Simba SC mkataba huru wa muda, baada ya Yanga SC kumpa barua ya kusitisha mkataba naye
jana pamoja na kumshitaki Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Okwi amesema ameamua kuomba kuichezea Simba SC kipindi hiki
ambacho ana matatizo na Yanga SC ili kulinda kipaji chake, kwa
kuwa hata FIFA haitaki mchezaji akae bila kucheza.“Sasa wakati Yanga wanaendelea na kesi yao, mimi ninaomba nichezee Simba SC ili kulinda kipaji changu. Nimewaandikia barua TFF na FIFA pia na nina matumaini usajili wangu utaidhinishwa, kwa sababu mimi si tatizo katika hili,”amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC,
Zacharia Hans Poppe amesema kwamba wamemsaini mchezaji huyo baada ya kupitia kwa kina suala lake na Yanga SC na kugundua haki ipo upande wa mchezaji.

“Baada ya kulipitia suala lake na Yanga kwa undani kabisa na vielelezo ambavyo mchezaji mwenyewe ametupatia, tumejiridhisha tuko sahihi kumsaini ili acheze mpira kunusuru kipaji chake kipindi
hiki ambacho ana matatizo na Yanga SC,”amesema Poppe.




MAGAZETI YA LEO: IJUMAA TAREHE 29/08/2014






Thursday, August 28, 2014

RAIS KIKWETE AZINDUA PROGRAMU YA UIMARISHAJI MIPAKA YA KIMATAIFA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka. (picha hii na zote zinazofuata ni kutoka Ikulu)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakitembelea eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakitembelea eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipata maelezo na kuangalia vifaa vya upimaji eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipongezana kwa furaha katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakichanganjya udongo na kujenga kwa pamoja alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakichanganjya udongo na kujenga kwa pamoja alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi na wananchi wa nchi zao wakisimama wakati nyimbo za Taifa za Burundi na Tanzania zikipigwa katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakijipatia chakula cha mchana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiagana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.





 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU