Facebook Comments Box

Monday, October 28, 2013

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA BAADA YA MECHI ZA LEO




KIBONZO: WATAFITI NA TANZANIA YETU




HIZI NDIO CHANELI ZINAZO PATIKANA KWENYE KING`AMUZI CHA AZAM MEDIA

Leo katika ukurasa wa Facebook wa Azam TV wameweka idadi na majina ya chaneli zinazopatikana kwenye king`amuzi chao. Chaneli zilizo orodheshwa zipo 45 ikiwa ni kinyume na tangazo lao linalo onesha zitakuwa chaneli kuanzia hamsini. Vilevile bado hawajaeleza kinaanza kupatikana lini na wapi na gharama zake za uwekaji na kwa mwezi. Ila katika maelezo hayo wameainisha chaneli za kulipia na za bure
Chaneli walizo weka ni hizo hapo chini:


FILAMU:
 

1.Sinema Zetu  2.MGM Movies  3.African Movie Channel  4.Zee Cinema  5.Star Gold

BURUDANI:
 

1.Azam 1  2.Azam 2  3.Fox Entertainment  4.FX  5.e.tv  6.ZOOM  7.Star Plus  8.Zing  9.Colours  10.Euro Channel

MICHEZO:

 

1.Setanta Africa  2.Kombat Sports  3.MCS Compact  4.MCS Extreme

MUZIKI:
 

1.MTV BASE  2.MTV India  3.Box TV

MAARIFA:
 

1.Nat Geo  2.Discovery Investigation  3.Discovery Science

MAISHA:
 

1.Fine Living  2.Outdoor  3.Landscape

HABARI:
 

1.BBC News  2.Al-Jazeera - English  3.Al-Jazeera - Arabic  4.ENCA  5.Times Now

WATOTO:
 

1.Kids Co  2.Nickelodeon  3.Al-Jazeera - Kids

CHANELI ZA BURE:
 

1.TBC  2.Clouds TV  3.ZBC  4.Channel 10  5.Mlimani TV  6.KBC  7.Citizen  8.K24  9.KTN
Tangazo la Azam Tv linalo onesha kuwa kutakuwa na Chaneli kuanzia hamsini

Picha ya maelezo ya facebook ya ukurasa wa Azam TV


PICHA: AJALI MBAYA KWENYE MPAKA WA SONGWE NA MBOZI: WATANO WAPOTEZA MAISHA


Basi la abiria aina ya coaster lenye namba za usajili  T378ADR likiobnekana muda mchache baada ya kupata ajali.
 Basi la abiria aina ya coaster lenye namba za usajili  T378ADR  likiwa limeharibika vibaya mara baada ya kupata ajali hiyo
Kiatu cha Abiria kikiwa kimebaki baada ya ajali hiyo 
 Wakazi mbalimbali wa mpakani mwa Mbozi na Songwe wakishuhudia Ajali hiyo 
 Hapa Basi la abiria aina ya coaster lenye namba za usajili  T378ADR baada ya kupata ajali 
 Baadhi ya watu wakiangalia kama kutakuwa na watu wamebakia katika ajali hiyo 
 Usukani wa Dereva ukiwa umetoka mara baada ya ajali hiyo 
 Basi la abiria aina ya coaster lenye namba za usajili  T378ADR  linavyo onekana kwa mbele 
 Hivi ndivyo Basi la abiria aina ya coaster lenye namba za usajili  T378ADR lilivyo haribika 
 Wananchi Mbalimbali wakiwa wanashuhudia ajali hiyo na kutoa msaada 
 Mmoja ya Majeruhi baada ya kufikishwa hospitali

CHANZO: MBEYA YETU BLOG

BABA AWACHOMA WATOTO MOTO BAADA YA KUZIDIWA NGUVU NA MAMA YAO



 Mtoto aliyefariki
Mtoto Matrida Michael mwenye umri wa miaka 9, mkazi wa Mtoni kwa Azizi Ally, wilayani Temeke jijini  Dar es Salaam, amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Oktoba 23, mwaka huu kufuatia majeraha ya moto aliyoyapata. 

Marehemu Matrida na watoto wenzake wawili, Tatu Mapunda (9) na Flora Mapunda (7), waliungua moto Oktoba 16, mwaka huu saa tano usiku wakiwa wamelala baada ya chumba chao kulipuliwa kwa petroli na mtu anayedaiwa kwa ni Brighton Mnamwa.

Inadaiwa kwamba chanzo cha Mnamwa kuamua kulipua watoto hao ni ugomvi baina yake na mkewe Janeth Lwena, waliyekuwa katika mzozo wa kumgombea mtoto wao wa miaka mitatu aitwaye Tulizo.

Watoto ambao wako hoi

Mama mdogo wa marehemu Mary Ivo ambaye alikuwepo msibani hapo, alisema kwamba dada yake yupo Muhimbili anawauguza majeruhi wawili waliobakia na kwamba wakati wa ugomvi wao, mke alimzidia nguvu mumewe.
Aidha aliendelea kueleza kwamba baada ya mke kumzidi nguvu, mume alizusha ugomvi mkubwa huku akitishia kumuua kwa panga, hata hivyo mke alimdhibiti.

‘Baadaye mume huyo inadaiwa kwa aliondoka hapo nyumbani na haikujulikana alikoenda, ndipo mke alienda chumba cha jirani na kumuomba Matrida abakie na watoto pale chumbani akatoe taarifa polisi lakini mtoto aliyekua akigombewa alienda naye kituoni,’ alisema mama mdogo.

Habari zinasema kwamba yule mume alienda kituo cha mafuta kununua petroli ili aweze kuwatekezeza wote, lakini hakujua kama mkewe pamoja na mtoto aliyekua akigombewa hawakuwepo.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba baada ya mume huyo kurudi, alimimina mafuta hayo katika chumba hicho kisha kukilipua wakati watoto hao watatu wakiwa katika usingizi na wananchi walipojitokeza walikuta chumba kikiteketea huku sauti ya watoto ikisikika wakiomba msaada.

Wananchi waliokuwepo kwenye eneo la tukio walisema kwamba walipatwa na uchungu hivyo walijitosa kuuzima moto ule na kuwaokoa watoto hao watatu huku wakiwa wameungua vibaya, waliwakimbiza Hospitali ya Temeke na kutokana na hali yao kuwa mbaya walipelekwa Muhimbili ambapo Matrida alifariki dunia.

Naye Michael Melkiori Kess, baba wa marehemu alisema kwamba amesikitishwa na kitendo hicho na amedai ni cha kinyama hivyo ameiomba dola kumsaka mtu huyo hatari kwani huko aliko kwa sasa bado anaweza kusababisha majanga megine.

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mtoni Sabasaba, Mwita Mang’ana alisema kwa kitendo hicho ni cha kinyama kwani amesababisha kujeruhi watoto wasiokua na hatia na amewataka wananchi kushirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha kuwa mtuhumiwa anapatikana .

Naye Kamanda wa Polisi mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba msako wa kumtafuta mtuhumiwa unaendelea sambamba na uchunguzi wa tukio.


NI JAMAL MALINZI




Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera, Jamal Malinzi amechaguliwa kuwa Rais Mpya wa shirikisho la soka nchini, TFF. 

Malinzi ameshinda uchaguzi huo wa leo uliokuwa ukifanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa NSSF, Water Front jijini Dar es Salaam kwa kupata asilimia 78 ya kura na kumbwaga mpinzani wake Athuman Nyamlani. 

Malinzi atachukua nafasi ya Leodegar Tenga aliyekuwa Rais wa TFF tangu mwaka 2005. Taarifa za kuchaguliwa kwa Malinzi kuwa rais mpya wa TFF, zimepokelewa kwa furaha na binti yake, mtangazaji wa Clouds FM, Loveness aka Diva aliyetweet: 

My dad is the new president TFF¦.. What a good news. Cant wait to get home and give him a big hug and a kiss. Gooooo Daddy” Diva (@DivaBos) October 27, 2013

Malinzi alishika nyadhifa mbalimbali Yanga zikiwemo seneta, mkurugenzi wa kuchaguliwa, kaimu katibu mtendaji na katibu mkuu. 

Amekuwa mwenyekiti wa mashindano ya mpira wa miguu mkoa wa Pwani (2009-2011) na mjumbe wa Baraza la Michezo la Mkoa wa Dar es Salaam (2009-2012). 

Toka 2011 hadi sasa ni mjumbe kwenye Kamati ya Utendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Misenyi, pia mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Kagera.


HOTUBA YA KWANZA YA JAMAL MALINZI BAADA YA KUSHINDA UCHAGUZI

 Hatimaye Tumechagua Mabadiliko,
 
Salamu kwa wanafamilia wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Salamu kwa wapenda michezo wa ndani na nje ya nchi yetu Tanzania.

Naanza kwa kumshukuru Mungu kwa hekima, busara, akili, vipaji na uwezo aliotujaalia kutuwezesha kutenda yote haya kwa amani na utulivu.

Shukrani za dhati zimwendee Bw. Leodegar Tenga, rais wa TFF 2005 - 2013 anayekabidhi madaraka kwa rais mpya wa TFF. Yeye na timu yake kwa hakika wanastahili pongezi kwa mengi mazuri waliyofanya.

Shukrani kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi 2013 kwa kunikubali, mimi Jamal E. Malinzi niwe Rais wa TFF kwa kipindi kijacho cha miaka minne.

Kweli dunia imekuwa kijiji, kwani kipindi cha masaa 72 baada ya kuzindua ilani yangu ya uchaguzi, nimepokea salamu, maoni na mapendekezo toka ndani na nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Burundi, Ivory Coast, Denmark na NewZealand.

Kupitia www.jamalmalinzi.com, twitter @jamalmalinzi, Jamii Forum, Facebook na mitandao mingine, naomba tuendelee kuwasiliana, kutoa maoni, kukosoa na kuchangia mijadala yenye tija na ufanisi ili Tanzania yote ipate neema ya mpira wa miguu.

Safari ni ndefu na wasafiri ni wengi kwenye vyombo vichache vya usafiri. Kwa wale ambao tayari wana ramani ya safari yetu, sote bila kujali tofauti zetu hasa wakati wa kuwania uongozi, tutoe mchango wake ili Tanzania isonge mbele katika ulimwengu wa soka.

Naam, kuna msemo wa Kiswahili unaosema 'kukata tamaa ukingali unaishi ni dhambi'. Naomba msemo huu na utuongoze kila tunapojikwaa tunanyuke na kuendelea na safari hadi tufike tulipopakusudia.

Historia imeshaanza kuandikwa, mwaka 2013 ni Tumechagua Malinzi, Tumechagua Mabadiliko na sasa tunasonga mbele.
 
Jamal E. Malinzi
Oktoba 27, 2013


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU