Facebook Comments Box

Wednesday, February 27, 2013

KIWANDA CHA NGUO CHA MAZAVA CHANUSURIKA KUUNGUA KWA MOTO


Picture
Suma na Asha wakiwa hoi baada ya kufikishwa wodi namba 3 hospitali ya mkoa wa Morogoro (picha: Dunstan Shekidele)
Imeripotiwa kuwa Kiwanda cha nguo cha Mazava kinachomilikiwa na wawekezaji kutonga  nje ya nchi, kilichopo Msamvu mkoani Morogoro kimepata hitilafu ya umeme majira ya saa nne wafanyakazi wakiwa ndani wakishona nguo.

Hali ya hewa iliyobadilika kutokana na moshi ndani ya jengo hilo imesababisha baadhi ya wafanyakazi wanaokadiriwa kuwa 30, kuanguka na wengine kupoteza fahamu  na hivyo kupelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Waandishi wa habari, Wafanyakazi wa shirika la umeme - TANESCO na Wafanyakazi wa zima-moto waliofika hapo kwa ajili ya kusaidia uokozi na kupata raarifa, walizuiwa kuingia ndani ya kiwanda hicho na wamiliki ambao ni raia wa China wakidai hakuna tukio lolote kubwa linalohitaji huduma ya uokozi hadi kuingia ndani.
Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele anasema kumbukumbu za matukio zinaonyesha kuwa  hili ni tukio la tatu.

Akiwahoji baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho, amefahamishwa kwamba hali hiyo huenda hali hiyo inatokana na hujuma za baadhi ya wafanyazi wanaolalamika kufanya kazi kwa saa 12 na kulipwa mashahara ya shilingi elfu 80/=.
Picture
(picha: Dunstan Shekidele)
Picture
Bi, Subira Juma Athumani [kushoto] akiwa na majeruhi wenzake. (picha: Dunstan Shekidele)



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU