Facebook Comments Box

Wednesday, July 30, 2014

ALICHOAMUA KINGWENDU BAADA YA MKEWE KUBAKWA


Muigizaji wa filamu za Kiswahili, mchekeshaji Kingwendu yuko katika wakati mgumu baad aya mkewe kubakwa na jirani yake wakati akiwa amelewa pombe.

Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa alizipata habari hizo wakati ambapo yuko safarini na majirani walimueleza kilichotokea kuwa mkewe na jirani huyo aliyembaka mida ya saa tano usiku wote walikuwa wamelewa.

”Kama ulivyosikia hiyo habari, mimi nilikuwa sipo ndo nimerudi jana, nataka nianze kufuatilia sheria sema sasa hivi nimefiwa na dada yangu tunapeleka msiba kijijini na baada ya hapo ninapumzika kesho tu halafu ninasafiri Nairobi, nikirudi Nairobi tarehe tano kuanzia tarehe sita ndo naanza kufuatilia.” Amesema Kingwendu.

Mchekeshajihuyo ameumizwa na kitendo hicho na ameamua kufuata taratibu za kisheria ili haki itendeke.
“Kutokana na kitendo alichokifanya na mimi nimejisikia vibaya, inanibidi nimtafute huyu bwana nimpate ili nimpeleke mahakamani, mke wangu bado niko naye, sema huyu jamaa aliyefanya unyamaa huu yupo jirani.

Mke wangu alikuwa amelewa na jamaa naye  alikuwa amelewa. Mke wangu sijui alikuwa anatoka wapi saa tano usiku ndo akakutana na huyo jamaa, majirani ndio walivyoniambia hivyo, walinipigia simu wakati nipo Shinyanga huko.”

  Source: Bongo5


PICHA: MORO BEST YAPATA AJALI

Basi la Moro Best Mpwapwa kuja Dar limepata ajali na kuua watu 15 hapohapo.




Tuesday, July 29, 2014

TAMASHA LA IDD TABATA SHULE:MECHI WALIO OA NA AMBAO HAWAJAOA

Washindi watarajiwa walio oa wakipanga timu na mikakati.  Hawa ni kutoka misikiti yote ya tabata ya Ansari suna.
Kipa wa walio oa akipangua shuti lilokuwa likielekea langoni kwake.
Beki wa wasela Ustaadh Ramadhan Kabange akienda kuvaa tayari kwa mpambano.



Saturday, July 26, 2014

MAJINA 70 YA WALIOPATA AJIRA YA UHAMIAJI

MAJINA 70 YA WALIOPATA AJIRA
YA MKAGUZI MSAIDIZI WA
UHAMIAJI.

TANGAZO KUITWA KWENYE AJIRA
NAFASI YA MKAGUZI MSAIDIZI WA
UHAMIAJI (ASSISTANT INSPECTOR OF
IMMIGRATION)

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, anawatangazia wafuatao
waliofaulu usaili wa kujaza nafasi ya
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji
(Assistant Inspector of Immigration)
wanatakiwa kuripoti Makao Makuu ya
Idara ya Uhamiaji, Mtaa wa Loliondo
Kurasini, Dar es Salaam tarehe 29 Julai
2014, saa 2:00 asubuhi. Aidha,
wahusika wote wanaelekezwa kufika
kwa wakati wakiwa na vyeti halisi vya
masomo na vya kuzaliwa.
Na
1 Abel Md. Maganya
2.Absolum Stafford Bashigwa
3 Agnes P. Mlay
4 Ali Musa Abdallah
5 Angela Kagaruki
6 Antony J. Nyagilo
7 Asteria Kiyanga
8 Awadhi Issa
9 Aziza Kaku
10 Bakari M. Khamis
11 Baraka Estomihi
12 Beatrice K. John
13 Bernard K. Mwampashe
14 Binasra J. Sabri
15 Charles M. Swai
16 Cosmas J. Mbuguni
17 Dativa J. Ndyetabura
18 David Muna
19 Doroth Ngai
20 Dotto Tabu
21 Emmanuel Gelison
22 Ezekiel A. Kibona
23 Fahamu Saidi
24 Farida Sued
25 Felix Mkemwa
26 Forget N. Charles
27 Frida N.Masomhe
28Gabriel M. Kamugisha
29 Gath E. Nyansambo
30 Gerald Moses
31 Gideon Kihoko
32 Godson Mwanawima
33 Grace C. Nyarata
34 Hamza Sanga
35 Hassan A. Mziray
36 Ibrahim Ally
37 Idd Mgoi
38 Joachim Joseph
39 John G. Mgayambasa
40 Joseph Gregory
41 Kennedy John
42 Khamis Moh'd Khamis
43 Kombo M. Ame
44 Kwame Charles
45 Lawi E. Kumburu
46 Mabrouk H. Thabit
47 Mangunda A. Kaporo
48 Marco Zacharia
49 Maria Agapith
50 Mateso Msigala
51 Meshack Mwaisela
52 Michael John
53 Miriam Mwakamele
54 Mlalama Fortinatus Amlima
55 Mussa Hemedi
56 Mwita Mwikwabe
57 Neema R. Mrope
58 Nyangoma Martin
59 Oscar Philip
60 Pasaka Wilson
61Pastory Packshard Mkongwa
62 Reagan H. Kawa
63 Rose Nseka
64 Senga Ally
65 Silvia Ngasoma
66 Sixtus Stephano Burashahu
67 Steven L. Kweka
68 Wendy Y. Mwalukasa
69 Witness Lwambo
70 Zulu P. Charles
Aidha, ni muhimu kufahamu kuwa
uchaguzi wa walioitwa kwenye ajira
umezingatia yafuatayo:
• Vipaumbele vya Idara ya Uhamiaji;
• Kutoa nafasi kwa waombaji kutoka
Zanzibar;
• Ufaulu kuanzia alama 50 asilimia na
kuendelea;
• Jinsia
Wasailiwa ambao majina yao hayamo
kwenye orodha hii wafahamu kuwa
hawakufanikiwa.
Atakayesoma tangazo hili amjulishe na

mwenzake.
Tangazo hili limetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
4 Mtaa wa Ohio
11483 Dar es Salaam



Friday, July 25, 2014

TV IMAAN WAPATA LESENI YA KURUSHA MATANGAZO


Hatimae TCRA leo watoa leseni ya urushaji wa matangazo ya Tv kwa TV Imaan na kuwa television ya kwanza afrika mashariki na kati kurusha matangazo yake kwa lugha ya kiswahili.
Tunawatakia mafanikio mema na Allah awaongoze katika kuwatoa watu kwenye giza na kuwapeleka kwenye nuru.
Br Arif Nahad akitoa hutuba
     
Br Arif Nahad na Br Ally ajiraan wakibadilishana mawazo katika hafla ya utoaji wa leseni


Mwenyekiti wa The Islamic Foundation akihojiwa na Jaffar Mponda



Tuesday, July 22, 2014

VIDEO NA PICHA:MABAKI YA MIILI YA BINAADAMU ZAIDI YA 20 YAKAMATWA BUNJU

Hii ndio gari iliyokutwa na mabaki ya miili ya binaadamu ambayo hutumika na wanafunzi wa udaktari kwa mafunzo "cadaver". Miili hiyo ilikuwa inaenda kutupwa kwenye jalala la kawaida.
Haya ndio mabaki ya viungo hivyo
Ki kawaida mabaki ya miili ya binaadamu ambayo hutumiwa na wanafunzi wa udaktari kwa ajili ya upasuaji huchomwa na moto na kuisha yote. ila haya yalikuwa yanatumiwa na wanafunzi  wa udaktari wa IMTU yalipelekwa muhimbili kwa ajili ya kuchomwa ila inasemekana hawakuwa na hela ndio maana muhimbili wakashindwa kuchoma na mwenye gari akaamua kwenda kutupa kwenye jalala la

Hili tatizo linaletwa na serikali kukubali kuzipa ruhusa taasisi na vyuo ambavyo havijajitosheleza. Chuo hakina hospital yake ambayo inaweza kutumika kuwafundishia wanafunzi wake ila unakuta kimepewa ruhusa na kinafanya kazi.

Ushauri wetu serikali ikague upya vyuo vyote vya udaktari ambavyo havina sifa na havijitoshelezi wavifunge.


Monday, July 21, 2014

VYOMBO VYA HABARI VINAICHUKIA ARSENAL?

Na: HASSAN KABANGE
Kinacho shangaza ni jinsi vyombo vya habari na wapinzani wetu wanavyo ogopeshwa na kushitushwa na uwezo wa ghafla wa Arsenal wa kipato ulioweza kuwavutia wachezaji mahiri duniani. Wanazidi kuchanganyikiwa wanapoona tunaweza kusajili mchezaji yoyote mahiri ambae Prof. Wenger atamtaka.
Mwanzo wa wiki hii Micheal Owen ametabiri Arsenal hawataingia nne bora hata kama wamesajili wachezaji wazuri. Hii sio mara ya kwanza kwa mkongwe huyo kutoa haya maneno ni kila mwaka anasema hivyo na Arsenal wanamdhirishia kuwa ni mtabiri muongo. Sina hofu na msimu huu itakuwa hivyo hivyo.
Mr. Rodgers yeye ameanza kitu ambacho watoto wa mjini wanaita "beef" kwa kusema kuwa Sanchez hakutaka kuishi jiji la Liverpool ndio maana hakujiunga na timu yao. Hapo yeye anazungumzia mazingira ya kijiografia hayo ndio yaliyomfanya Sanchez asiende kwao. Hili linakubalika ila sio sababu kuu kama ambavyo Mr Rodgers anataka kutuaminisha. Timu ya Arsenal inaonekana kukamilika na kujitosheleza katika kila idara, Sanchez atakuwa aliangalia viungo waliopo Arsenal na Liverpool kwa uhakika kabisa hauwezi kulingana viungo wa Arsenal wanawazidi wa Liverpool sana. Kila mshambuliaji ni ndoto yake kucheza mbele ya viungo hawa hebu fikiria mshambuliaji ucheze mbele ya viungo kama  Ramsey, Ozil na Carzola.
Kingine Barcelona na Arsenal ni timu ambazo zina shabihiana kwenye aina ya uchezaji na vilevile ni timu ambazo zina viwanja vizuri na vikubwa ni timu zenye washabiki wengi na mwisho ni timu zenye vifaa vya kutosha kwa ajili ya mazoezi.
Kingine ambacho Mr Rodgers anashindwa kukielewa ni kuwa Fabregas atakuwa alikuwa akimzungumzia Prof. Wenger pale Barcelona na hilo ndilo lililomfanya Sanchez achague kuja Arsenal. Kitu pekee ambacho kitawafanya Liverpool kutushinda katika pirika za kugombea mchezaji ni Prof Wenger kuendelea kufananisha kipaji, umri na mshahara.
Kuna mtu anajiita “Special One” yeye mwenyewe juzi juzi aliuchekesha umma baada ya kusema Fabregas hakutaka kujiunga tena na Arsenal na kusema ilimchukua dakika 20 kumshawishi ajiunge Chelsea (Sijui huyu "special one" alikuwa amevuta nini). Maana huu ni uongo ulio tukuka! Bado akaendelea kwa kusema Wilshere ni mfano mbaya kwa vijana baada ya kuripotiwa akiwa anavuta sigara hadharani. Hapa ndio utaona huyu ni "special one" wa ujinga na ujinga huu anao peke yake, huwa anatumia lugha zisizo na staha mbele ya waandishi wa habari ikitokea kakosana na mtu. Ni yeye alie mtetea John Terry kwa kulala na mke wa mchezaji mwenzake ni huyo huyo alie mtetea Hazard kwa kumpiga mtoto mateke ana orodha kubwa ya mambo ya ajabu anayo yafanya ila hayaoni na tukifananisha na hili kosa la Wilshere ambalo ni moja. Japo Wilshere aliahidi mbele ya umma kuwa hatavuta na akarudia tena lakini asihukumiwe kama ameua.
Kuna wakati nashangaa watu wanao isema Arsenal na Prof. Wenger, Liverpool haijashinda kombe lolote kwa muda mrefu vyombo vyote vya habari vimefumbia macho hili. Lakini wakati Arsenal tukiwa hatuna kombe kila mechi watangazaji na vyombo vya habari vilikuwa vikirudia hili.Sasa Arsenal tumepata kikombe je, vyombo vya habari vitakuja na mada gani juu ya Arsenal?
Arsenal ni klabu kubwa na nzuri, Hatupo makini "perfect" lakini angalau tunafanya vitu katika umakini unao hitajika bila kuangalia vilabu vingine vinafanyaje na hilo ndilo lililotufanya tuingie kwenye mtafaruku na vyombo vya habari. Walitakiwa watupongeze lakini tumekuwa tukilaumiwa.
Najivunia kuwa mshabiki wa Arsenal na filosofa ya klabu. Kuna wakati klabu inaniumiza lakini angalau hizi "video game" imenifundisha jinsi ya kukaa nao vizuri maadui.
Na sasa napenda kuwaambia maadui kuwa sasa ndio tupo katika mstari na huu ni wakati wetu.
COYG!!!!!


Friday, July 18, 2014

MUFT MENK: SOLUTION TO OUR STATE OF WEAKNESS




LINAH AAGWA RASMI THT AKIELEKEA NFZ

Mkurugenzi wa Tanzania House Of Talent (THT) Ruge Mutahaba akifafanua jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wanahabari,wadau na wasanii wa filamu na muziki,katika hafla ya kumuaga msanii Linah Julai 16, 2014 kutoka kwao na kuelekea kampuni ya No Fake Zone (NFZ) ambao ndiyo
wanaanza kumsimamia msanii huyo pamoja na kazi zake.


Baadhi ya wasanii walipewa tuzo mbalimbali katika sherehe hizo ambao ni Mwasiti, Dito,Linah na Mtayarishaji kutoka katika nyumba hiyo ya sanaa Imma Ze Boy ambao wote hao walipata vyeti.

 Msanii Dito
 Imma Ze Boy
 Linnah
 Mwasity

Linah pia alizindua video yake mpya chini ya kampuni NFZ iitwayo OLe Themba.

Waalikwa wakiifuatilia video ya wimbo huo Ole Themba kwa karibu kabisa kama wanavyooekana pichani.


MKurugenzi wa Kampuni ya NO FAKE ZONE (NFZ), Abby akizungumza jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali.

 Ommy Dimpoz
 Mwana FA
 Steve Nyerere, Kalala Junior na Christian Bella wakiwa na furaha.
Recho


WAFADHILI KUREJESHA MSAADA UGANDA IKIWA.........

Wahisani wamesema wameridhika na kazi ya serikali mwaka 2012/13

Mapema mwaka huu wafadhili kadha walikata msaada wao wa bajeti kupinga sheria kali dhidi ya wapenzi wa jinsia moja iliyopitishwa Februari. Wiki jana serikali ilitoa andiko linalojaribu kubainisha sheria hio dhidi ya wapenzi wa jinsia moja. 

Mnao siku ya Jumanne, wafadhili hao walionyesha kuridhika na kazi ya serikali mnamo mwaka wa fedha 2012/13, baada ya uhakiki wa kila mwaka kuhusu matendo ya serikali. Uhakiki huo unakusudiwa kuwapa fursa wafadhili kuamua ikiwa au la waendelee kugharimia bajeti ya Uganda kwa mamilioni ya dola.

Kwa jumla kasoro ya 20% ya bajeti ya Uganda inategemea misaada ya wafadhili. Wafadhili hususan kutoka Ulaya ambao husaidia bejeti ya Uganda walisitisha msaada wao kufuatia ripoti za ufujaji wa pesa za serikali pamoja na kupitishwa kwa sheria ya kuharamisha mapenzi ya jinsia moja. Nchi hizo kiwawakilishwa na Denmark pamoja na beki ya dunia wanaonekana kushawishika kuendelea kusaidia Uganda baada ya kukutana na waziri mkuu Amama Mbabazi.
Nyingi ya pesa inazopata Uganda kama msaada hutumiwa katika miradi ya afya Katika taarifa yao ya pamoja, wahusika wote walitambua jukumu la Uganda katika kuweka amani na uthabiti katika kanda nzima na kuhimiza uhuru wa kujieleza pamoja na uwazi katika masala ya usimamizi wa pesa za msaada.

Wamejitolea kuendelea kufadhili Uganda kwa kima cha dola milioni arobaini katika siku zijazo. Marekani pamoja na nchi nyinginezo kutoka Ulaya zilisitisha msaada wa mamilioni ya dola baada ya Rais Museveni kutia saini sheria ya mapenzi ya jinsia moja mapema mwezi huu. Nchi hizo zinataka Uganda ifutilie mbali sheria hio kabla ya kuanza kuipa tena msaada. 

Wiki jana Waziri wa mambo ya nje wa Uganda alitoa taarifa kusema kuwa sheria hiyo ilitafsiriwa visivyo kwani lengo lake ni kuwalinda watoto bali sio kumbagua yeyote, wala haijulikani ikiwa tamko hilo ndilo lililoifanya wahisani kuanza tena kutoa msaada.


Wednesday, July 16, 2014

HABARI NJEMA KATIKA VITA DHIDI YA VVU

Virusi sugu vya HIV

Kuna uwezekano kuwa janga la ukimwi huenda likadhibitiwa ifikapo mwaka 2030, kulingana na ripoti iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi.

 Ripoti hiyo imesema kuwa idadi ya visa vya maambukizi mapya na vifo kutokana na HIV, vimeendelea kushuka. Hata hivyo, shirika hilo linataka juhudi zaidi za kimataifa kufanywa kwani za sasa hazitoshi Na shirika la misaada la Medecins Sans Frontieres limeonya kuwa watu wanaoishi na virusi hivyo hawapati dawa za kutosha.

Kwa mujibu wa shirika hilo watu milioni 35 wanaishi na virusi vya HIV. Ripoti hiyo ilionyesha visa vipya vya maambukizi milioni 2.1 vilitokea mwaka 2013. Idadi hii iko chini kwa asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka 2001. Vifo kutokana na HIV pia vimepungua kwa asilimia 5 katika miaka mitatu iliyopita. Kwa sasa watu milioni 1.5 hufariki kutokana na ugonjwa huo kila mwaka.

Afrika Kusini na Ethiopia zimepiga hatua katika kupunguza vifo vya wagonjwa wa HIV.
CHANZO: BBC


KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA INGIA HAPA

Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6 yaliyofanyika tarehe Mei 5 –
21, yametoka.
Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa
waliofanya mtihani kidato cha 6 wamefaulu. Wasichana waliofaulu
ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825
Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420 sawa na asilimia 12.54
Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa na asilimia 1.74.


SHULE 10 ZILIZOONGOZA
1. Igowole
2. Feza Boys
3. Kisimiri
4. Iwawa
5. Kibaha
6. Marian Girls
7. Nangwa
8. Uwata
9. Kibondo
10. Kawawa


SHULE 10 ZA MWISHO
1. Ben Bella
2. Fidel Castro
3. Tambaza
4. MuhezaHigh School
5. Mazizini
6. Mtwara Technical
7. Iyunga technical
8. Al- falaah Muslim
9. Kaliua
10. Osward Mang'ombe




Tuesday, July 15, 2014

ISRAEL YAANZA TENA KUISHAMBULIA GAZA

 Israel imeanza tena kushambulia Gaza ikidai kuwa Hamas inaishambulia licha ya mkataba wa kusitisha vita kufikiwa. Awali Israel ilikubali kusitisha vita kufuatia pendekezo la Misri kwa
pande zote mbili kusitisha vita Jumanne asubuhi. Hata hivyo, kundi la Hamas, ambalo linadhibiti Gaza, lilikataa makubaliano hayo na kusema ni kama kusalimu amri.

Maafisa wa Palestina wanasema kuwa watu 192 wameuawa katika mashambulizi ya angani yaliyofanywa na Israel siku nane zilizopita ili kukomesha wapiganaji wa Hamas kuusha makombora nchini Israel.

Raia wanne wa Israel wamejeruhiwa vibaya tangu mashambulizi hayo kuanza , lakini hakuna taarfa zozote za vifo.
Wizara ya usalama nchini Israel imesema kuwa roketi 50 zimerushwa ndani ya Israel tangu isitishe vita. Mashambulizi ya hivi punde yamepiga maeneo mawili katika ukanda
wa Gaza. Kundi la Hamas lilisema kuwa hawajapokea pendekezo lolote la kusitisha mashambulizi.

Aliongeza kwamba Hamas inahitaji masharti yake yote kukubaliwa kabla ya kukubali kusitisha vita.
Idara ya usalama nchini Israel imekubali mapendekezo hayo lakini ikasisitiza kuwa itaendelea kushambulia Gaza ikiwa Hamas watasitisha kusidhambulia kwa roketi.


IPTL WATAKA KAFULILA AWALIPE BILIONI 310

Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imemfungulia kesi Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ikimtaka aombe radhi na kulipa fidia ya Sh bilioni 310. Katika kesi hiyo ya madai, Kafulila anadaiwa kuidhalilisha kampuni hiyo, kutokana na kauli alizotoa dhidi yake (IPTL).
IPTL na walalamikaji wengine Pan Africa Power Solution (PAP) na Mkurugenzi wa PAP, Harbinger Seth wanamlalamikia Kafulila kuwatuhumu kuchukua fedha kinyume cha sheria katika akaunti ya
Escrow iliyopo Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Walalamikaji hao kupitia kwa Wakili wao, Augustine Kusalika wamefungua kesi hiyo, wakitaka Kafulila awalipe Sh bilioni 210 kama fidia ya kutoa kauli za udhalilishaji,  kuwasababishia hasara katika biashara na kuharibu mtazamo wa biashara zao. Aidha, wanaiomba Mahakama iamuru Kafulila, awaombe radhi, pia awalipe Sh bilioni 100 kama hasara ya jumla pamoja na usumbufu
walioupata, kutokana na kauli za udhalilishaji. Kwa mujibu wa hati ya madai,  iliyopatikana mwishoni mwa wiki, Juni mwaka huu Kafulila alitangaza kuwa IPTL na Seth, walijipatia fedha kutoka akaunti ya Escrow kinyume cha sheria na kumuita Seth ni 'Singasinga', jambo lililomdhalilisha na kumharibia muonekano wake na biashara yake.

Walalamikaji hao wanadai kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,  bila kuwa na haki, Kafulila alitoa taarifa hizo, kuwa IPTL inajihusisha na biashara zisizo halali na za uongo, jambo
lililosababisha jamii kuamini na kuwaharibia mtazamo wa kibiashara. Aidha, wanadai  Kafulila akiwa mbunge alipoteza kinga ya wabunge inayowalinda wakizungumza bungeni, kwa kuwa alitoa taarifa hizo nje ya shughuli za Bunge.

Walidai Kafulila anaendelea kutoka taarifa hizo,  licha ya kumpa taarifa kwa maneno na maandishi, wakimtaka kuacha kufanya hivyo, kwa kuwa anawaharibia biashara kitaifa na kimataifa.

Kwa mujibu wa hati ya madai, IPTL iliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa ajili ya kusambaza umeme kwenye shirika hilo, lakini kulitokea mgogoro kati ya IPTL, Kampuni ya VIP Engineering and Marketing na Tanesco, jambo lililosababisha wafike Mahakama Kuu. Kutokana na mgogoro huo, Mahakama iliamuru Sh bilioni 200 zilizokuwa kwenye akaunti ya Escrow, zisitolewe hadi kesi hiyo itakapokwisha na baada ya kesi kuisha, Mahakama iliamuru IPTL ichukue fedha hizo.

Walalamikaji hao wanadai licha ya Kafulila, kujua kuwepo kwa mgogoro huo, aliendelea kutoa tuhuma hizo, huku akijua kuwa IPTL imechukua fedha hizo kwa amri halali ya Mahakama. Wakili huyo alisema wateja wake, wanaiomba Mahakama iamuru Kafulila awalipe Sh bilioni 310 kama fidia, aombe radhi, alipe gharama za uendeshaji wa kesi hiyo na amri nyingine, ambazo
Mahakama itaona zinafaa.


PICHA NA VIDEO YA DUKA LINALO UNGUA MWANANYAMALA MUDA HUU





MUQAWAMA WATUMA NDEGE ISIYO NA RUBANI TEL AVIV

Brigedi ya Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imetangaza kuwa, wahandisi wake wamefanikiwa kutengeneza ndege isiyo ya rubani kwa jina la Ababil 1. Ripoti iliyotolewa na brigedia hiyo hii leo, imeeleza kuwa, ndege hiyo imefanikiwa kuruka juu ya jengo la idara ya Wizara ya Vita ya utawala haramu wa Kizayuni mjini Tel Aviv. 

Ripoti hiyo imeongeza kuwa, ndege hiyo isiyo na rubani ni moja kati ya ndege tatu zenye kazi tofauti zilizoundwa na wapiganaji wa muqawama wa Kipalestina. Aidha imezitaja ndege hizo kuwa ni pamoja na ndege ya kijasusi inayofanya kazi za kuchukua habari mbalimbali za adui, ndege ya kutekeleza hujuma na mashambulizi na ya tatu ni ndege inayosheheni mada za miripuko na kujiripua katika eneo maalumu la adui. Imeelezwa kuwa ndege hiyo iliruka mapema leo asubuhi katika shughuli zake za kiupelelezi ambapo iliweza kutuma ripoti muhimu, suala ambalo limeutia kiwewe utawala huo bandia. Kwengineko Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa, watu 173 wameuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala haramu wa Israel katika eneo la Ukanda wa Gaza huku wengine 1, 200 wakijeruhiwa. 

Idadi hiyo imeongezeka kufuatia watu saba kuuawa shahidi hii leo akiwemo mtoto mchanga huku kijana mwingine akiuawa katika shambulizi la anga katika eneo la Rafah.

Wakati huo huo Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Mahmoud Abbas ameutaka Umoja wa Mataifa kuwasaidia Wapalestina. Abbasi ametoa ombi hilo kupitia barua aliyoiwasilisha kwa mwakilishi wa Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Robert Serry akimtaka awasilishe ujumbe huo kwa Katibu Mkuu wa umoja huo. Abbasi amesema kuwa, serikali ya Palestina imekwishachukua maamuzi maalumu ambayo yatatangazwa hivi karibuni kuhusiana na mashambulizi ya utawala haramu wa Israel.


Sunday, July 13, 2014

MWENYEKITI WA CHADEMA KANDA YA KUSINI AJIUZURU

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Kanda ya  kusini  ambaye pia ni Mchungaji  wa Kanisa la Avangelisitic Assemblies of God Tanzania(EAGT),Joseph Matare amejiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na Kanisa lake hilo Kuagiza
Wachungaji wake ambao ni Viongozi wa  Vyama vya Siasa kuachana na Nafasi zao za Kisiasa. Joseph Matare akizungumza na Waandishi wa habari Mjini Songea amesema kuwa ameamua kujuzulu Nafasi yake ya Uongozi wa CHADEMA Kanda ya Kusini inayojumuisha Mikoa ya Lindi,Mtwara na Ruvuma kufuatia  Kanisa lake katika Mkutano wake wa Kanda kuagiza Wachungaji wake wote ambao ni Viongozi wa Kisiasa kuachia nafasi zao na badala yake wasimamie Kazi ya Mungu Katika Makanisa yao. ‘Kufuatia maagizo ya Mkutano huo wa Kanisa uliofanyika Njombe nimeamua kutii na  leo tarehe 10 Julai  2014 nimeamua kujiuzulu na Katibu wangu Mkuu Dr Wilbroad Slaa nilimjulisha tangu tarehe 04 Juni mwaka huu’ alisema  Matare katika taarifa yake ya kujiuzulu. 

Anafafanua kuwa muda  wa Viongozi wa Kanda ulikuwa ni wa muda na wa mpito hadi  uchaguzi wa Kanda utakapopita ambao ulipaswa kufanyika Juni 2014 na kwamba muda umeongezwa hivyo ameona aheshimu  maagizo yaliyomuweka madarakani. Hata hivyo Matare anasema kuwa anawatia moyo Makamanda wote wa CHADEMA  waliobaki kuendelea kupigania Nchi ili iondokane na uovu  unaotendeka sasa na kwamba Mungu atakuwa nao wale wote wanaotafuta haki kwa ajili ya Wananchi walio wengi.

Anasema  kuwa ameondoka bila kuwa na Ugomvi na Kiongozi yeyote wa CHADEMA   hivyo wataendelea kushirikiana kutafuta  haki akiwa Mwanachama wa Kawaida na Mchungaji. 

Matare ambaye ni Mchungaji wa Kanisa la EAGT  Mkuzo la Mjini Songea la Mkoani Ruvuma  amesema kuwa anatambua juhudi za Viongozi wa CHADEMA katika kupigania haki za Wananchi na
Wabunge wote wa CHADEMA katika kupigania haki na kwamba ipo siku Mungu atawalipa ujira wa kazi wanayofanya. Anasema kuwa Mungu anatambua kazi  nzito wanayofanya Viongozi wa CHADEMA ambayo amesema ni ya kutafuta Ukombozi kamili wa Nchi na itakuwa  ni uendawazimu kubeza kazi hiyo.


Saturday, July 12, 2014

AJALI ENEO LA UBUNGO MATAA MUDA HUU

Gari la mchanga lililokuwa likitokea maeneo ya kimara limemshinda dereva wakati wa kukata kona kutoka barabara ya Morogoro kuingia barabara ya Mandela hapa eneo la Ubungo. Hakuna mtu aliye fariki bali ni majeraha machache kwa dereva.




Friday, July 11, 2014

DIAMOND PLATNUMZ APOKELEWA KWA SHANGWE NA BASHASHA AKITOKEA MAREKANI

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya hapa Tanzania maarufu kama Bongo Fleva Naseeb Abdulmalik a.k.a Diamond Platnumz aliwasili jana tarehe 10/07/2014 akitokea Marekani alikokwenda kwa ajili ya kushiriki katika tuzo za BET ambazo hufanyika kila mwaka.

Diamond alikua katika kategori ya Best African Act ambayo ilichukuliwa na Davido kutoka Nigeria na yeye kuishia kupata cheti cha ushiriki ambapo kwake sio vibaya maana anaamini huo ni mwanzo mzuri kwake wa kuelekea katika mafanikio.


Baada ya kuwasili Diamond aliwashukuru wote waliofika kumpokea na kusema kuwa safari yake ilikuwa nzuri na amejifunza mambo mengi sana pia amekutana na watu wengi na tutarajie mengi mazuri katika muziki wetu.

Na kwa upande mwingine alitoa shukran za dhati kabisa kwa watanzania kuipokea vema video yake mpya ya mdogomdogo, ambayo inafanya vema kwenye vituo vya luninga hapa nchini kwa sasa.


Tuesday, July 8, 2014

BOMU LALIPUKA ARUSHA NA KUUWA NA KUJERUHI

Taarifa zilizotufikia za kusikitisha zinasema kwamba kumetokea mauwaji katika mgahawa wa Wama ulioko Gymkhana jijini Arusha (Pichani chini). Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamkia leo na kusababisha watu zaidi ya 8 kujeruhiwa vibaya, idadi ya waliopoteza maisha bado haijajulikana, majeruhi wote wamepelekwa katika hospitali ya Seliani jijini Arusha.




Thursday, July 3, 2014

MTOTO AFUNGIWA KWENYE BANDA LA MBUZI KWA MIAKA 10

Mwenyekiti wa Umoja wa Watu wenye Ulemavu Kenya, David Sankok akionyesha hali halisi ya maisha ya mtoto huyo kabla ya kuokolewa. Picha na Ndaya Mgoyo Juni 21 ilikuwa ni siku ya kawaida kwa Mama Nancy mkazi wa Narok nchini Kenya, lakini ilifichua siri nzito ya mtoto aliyefichwa kwa miaka kumi katika banda la mbuzi.Akiwa katika shughuli zake za nyumbani, mara akatokea mtoto mdogo wa jirani yake aitwaye Jane. 
     
Binti huyo akaanza kucheza na wenzake kwa dakika kadhaa na mara akaacha michezo na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani kwao.Wenzake wakamuuliza “mbona unakimbia wakati bado tunacheza”. Akajibu, “nakwenda kwenye banda la mifugo kumpa chakula Ben. Muda umekimbia na hakuna mtu nyumbani”.Kwa kauli hiyo, mwanamke huyo alitaka kujua iwapo Ben anaishi kwenye nyumba ya jirani yake kwani ni miaka 10 imepita tangu amtie machoni.“Ben yupo na anaishi kwenye banda la mifugo. Huwa anahudumiwa na mama, lakini kwa sasa mama hayupo na baba amekwenda kazini. Mimi nina jukumu la kumpa chakula,” alijibu Jane.

Mama huyo akapata shauku ya kumtembelea mtoto huyo kuona kinachoendelea kwa jirani zake, Lo! anachokiona haamini macho yake; Mtoto Ben amefungwa kwa kamba kwenye kigodoro chembamba akiwa hajiwezi kwa njaa. Hivyo ndivyo alivyoibuliwa mtoto Ben baada ya kukaa katika banda la mbuzi kwa muda wa miaka 10 bila majirani kufahamu. 

Ben, ambaye kwa sasa ana miaka   miaka 14 alizaliwa akiwa kiziwi, bubu   na ulemavu. Aibu ya kuzaa mtoto kama huyo ndiyo ilifanya wazazi wake wamfungie kwenye zizi la wanyama kwa muda wa miaka 10 na wakihakikisha  hakuna jirani wala ndugu wa karibu anayefahamu juu ya tukio hilo. Historia ya mtoto huyo Kwa mujibu wa baba mlezi Mr Jeremiah Mbusia,  ambaye ni askari katika Wizara ya Mali Asili, Narok Kenya, mtoto  huyo siyo wake wa
kuzaa bali alifika katika nyumba hiyo miaka 12 iliyopita akiwa na mama yake wakati huo mtoto huyo alikuwa na miaka minne.

 Alilelewa katika nyumba hiyo kwa miaka miwili na ndipo wazazi wake, yaani baba yake wa kambo na mama yake mzazi wakaamua kumuweka katika kibanda kidogo nje ya nyumba yao  na hutumiwa
kama zizi la mbuzi na kondoo. Maisha ndani ya  zizi Akiwa kwenye zizi mtoto huyo aliwekewa godoro ukutani na mkono wake mmoja ulifungwa kwa kamba ukutani. Ilikuwa ni vigumu kuvumilia harufu kali kutoka katika zizi hilo kwani kulikuwa na mchanganyiko wa kinyesi na mikojo ya binadamu na wanyama.

Wadogo zake Ben walisema kuwa wazazi wao huwa wanamsafisha mtoto huyo wakati wowote wanaotaka na kuwa anaweza kushinda na kinyesi au kulala nacho. “Ni mara chache kukuta akisafishwa   mara mbili kwa siku. Kwa kawaida husafishwa mara moja tu na wakati mwingine hasafishwi kabisa,” alisema mtoto huyo. 

Kwa nini ilikuwa rahisi kujulikana? Ugunduzi wa mtoto huyo ulitokana na ukweli kwamba mama yake aliamua kuondoka nyumbani na kuacha familia nzima kutokana na ugomvi na mume wake. Mama huyo alikuwa akifanya siri ya kulinda mtoto huyo asijulikane hapo nyumbani na alipoondoka watoto wenzake ndiyo walikuwa na jukumu la kumlisha mwezao. Kauli ya baba mlezi Kwa kujibu wa baba wa kambo, mama wa mtoto huyo alikuwa hamtaki mwanaye kwani aliamini kwamba kuishi naye ni kuongeza mikosi.

 Baada ya kuishi pamoja walijikuta wakiwa wamezaa watoto watatu na mama huyo aliona kuwa watoto hao ndio walikuwa muhimu katika maisha yake kuliko Ben, ambaye alimzaa na mwanaume mwingine kabla ya kuolewa katika ndoa rasmi. “Mama yake alikuwa hampendi na hata wazo la kumweka katika banda lilitoka kwake. Aliamini kuwa kukaa naye ndani kama watoto wa kawaida ilikuwa ni usumbufu na akitoa visingizio kwamba akikaa ndani anaweza kuvunja vitu na kuwa anaweza kushika vitu vya hatari kama vile moto,” alijitetea baba mlezi wa Ben. 

“Tulikosana na mama watoto kwa ugomvi wa kawaida tu katika familia, hiyo ilikuwa ni miezi minne iliyopita, ajabu ni kwamba amenikimbia na kuniachia familia akiwamo mtoto mlemavu.”

“Nashindwa kumlea vizuri kwa kuwa natakiwa kwenda katika mihangaiko yangu ndiyo maana wadogo zake walikuwa wakimhudumia wakati sipo.” Imefahamika kuwa mwanamke huyo amekimbilia kwao eneo la Rimuru, Kenya ambapo ni kwa wazazi wake na akiwaambia jamaa zake wa karibu kuwa hawezi kurudi katika nyumba ya mume wake kwani hawapatani. 

Kauli za majirani Majirani wanasema walikuwa wakifahamu kuwa nyumbani kwa jirani yao kuna mtoto mwenye ulemavu wa akili lakini hawakumwona kwa muda mrefu. 

“Tulikuwa tukifahamu kwamba kuna mtoto mlemavu wa akili lakini katika kipindi cha miaka 10 iliyopita hatukumwona. Tulidhani wamemhamishia sehemu nyingine. Ilikuwani vigumu kusikia sauti
kwa kuwa mtoto mwenyewe ni bubu na kiziwi,” alisema jirani mmoja. Kumuokoa Ben Baada ya majirani kupata taarifa za kuwepo kwa mtoto huyo, walimuita mwandishi wa habari mmoja ili kushuhudia hali halisi.

Mwandishi huyo alitoa taarifa polisi na pia kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Kenya, Dk David Ole Sankok na kwa pamoja walivamia katika nyumba hiyo iliyopo Fanaka Estate, Narok na kumwokoa mtoto huyo katika mateso.

 Baada ya kumtoa kwenye kibanda hicho waligundua kuwa hali ya mtoto huyo haikuwa nzuri kwani alikuwa amepooza upande mmoja wa kushoto kutokana na kulala kwa muda mrefu, viungo vyake vilikuwa vimejikunja kutokana na kukosa lishe kwa siku nyingi na nywele zake zilibadilika rangi kutokana na kutokaa kwenye mwanga wa jua kwa muda mrefu. “Alikuwa akitoa harufu kali, ilikuwa ni vigumu hata kumsogelea, lakini kwa kuwa tulikuwa tumedhamiria kumwokoa ilibidi tufanye hivyo,” akasema Dk Ole Sankok. “Tulimkuta katika mateso makubwa sana, eneo alilokuwa amelala lilikuwa na kunguni, chawa na viroboto wengi,” anasema.

Anaongeza kuwa wadudu hao walipokuwa wakimsogelea kinywani
alikuwa akiwatafuna na kuwameza kwani alikuwa na njaa muda wote.“Nilipoona hali hiyo nilijaribu kuondoa viroboto waliokuwa karibu na mdomo wake, kwa kuwa alikuwa amewazoea sana na aliona ni kama kitoweo chake alitoa sauti ya ukali kuashiria kwamba nisiwatoe, nilipojaribu kuwatoa kwa nguvu alitaka kuniuma kwa meno,” alisema daktari huyo. 

Wazazi wa kijana huyo walikuwa hawaaniki godoro nje kwani
hawakua na jingine la kumtandikia pia walihofia majirani huenda wangehoji. Huduma ya kwanza Baada ya kugunduliwa, Ben alipelekwa katika Hospitali ya Mji wa Narok kwa ajili ya matibabu. Alipewa huduma za haraka ikiwa ni pamoja na huduma za kurudisha afya mwilini kwa vyakula vya protini na vitamini.

 Vilevile alikuwa akianikwa juani mara kwa mara kwa lengo la kumrudishai vitamini. Kwa kuwa mgongo wa mtoto huyo ulianza kutoa vidonda alipewa matibabu ya vidonda. “Mtoto huyo alikuwa amepungua mwili kwa kiasi kikubwa  ilikuwa unaweza kumbeba kama mtoto mdogo. Hata   rangi yake ya ngozi ilibadilika,” alisema Dk Sankok, ambaye pia anaendesha kliniki binafsi katika mji wa Narok. “Licha ya kuwa na umri wa miaka 14 alikuwa na kilo 15 pekee,” aliongeza.

Sankok aliwahakikishia watu waliomzunguka mtoto huyo kwamba
atamfikisha katika kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa akili na viungo na atampa mazoezi ya kutosha kuhakikisha anarudi
katika hali ya kawaida.

“Unajua kuna wazazi ambao wana kawaida ya kuwaficha watoto
wao kwa sababu wana matatizo ya viungo ama   ya akili. Hilo siyo
jambo zuri hata kidogo, watoto kama hao ni binadamu wa kawaida
na wanatakiwa kulelewa kwa misingi yote ya kibinadamu,” anasema.

Anasema kama mzazi anaona hawezi kumhudumia mtoto kama
huyo ni bora amfikishe katika vituo vya kulea watu wa aina hiyo
kuliko kumficha ndani na kumpa mateso makubwa.
Chanzo: Mwananchi


AZAM WASAJILI MSHAMBULIAJI WA HAITI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Haiti, aliyecheza Kombe la Mabara mwaka jana nchini Brazil, Leonel Saint-Preux ametua Azam FC kwa ajili ya kujiunga nayo kwa msimu ujao.

Kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon amesema amekuwa na mchezaji huyo kwa siku mbili na atahitaji muda zaidi kumuona kabla ya kuamua kumsajili au la. Mshambuliaji huyo aliyezaliwa Machi 12, mwaka 1985 in Cap-Haitien mara ya mwisho alichezea klabu ya FELDA United F.C. ya Ligi Kuu ya Malaysia.

Preux alianzia Zenith ya kwao,ambako alikuwa mfungaji mzuri katika Ligi ya nchini humo. Saint-Preux alisaini Minnesota Thunder ya Daraja la Kwanza Marekani Aprili 15, mwaka 2009, kabla ya kuhamia Hanoi ya Vietnam.

Machi 2010 alisiani mkataba wa awali na Aztex, lakini akatemwa baada ya kufeli vipimo vya afya. Kimataifa Saint-Preux, alianzia kuchezea timu za vijana za Haiti wa umri tofauti. Alikuwemo kwenye kikosi cha Haiti kilichofuzu michezo ya Olimpiki mwaka 2008 mjini Beijing, akifunga bao la kukumbukwa kutoka umbali wa mita 40 timu yake ikishinda 2-1 dhidi ya Canada.

Alianza kuchezea timu ya wakubwa ya Hati mwaka 2007. Alifunga
bao lake la kwanza timu ya taifa ya Haiti Novemba 19, mwaka 2008 katika sare ya 1-1 Surinam. Haiti ilifungwa 10-0 na Hispania kwenye michuano.
Hii ndio mechi ambayo Haiti ilitandikwa goli 10 kwa 0 mshambuliaji huyu wa azam anaonekana akikabwa na beki ya Hispania ambayo imeonesha udhaifu mkubwa kwenye kombe la dunia linalo endelea Brazil hivi sasa. Katika mechi hiyo mshambuliaji huyu mpya wa azam hakuweza kumsaidia timu yake kabisa.
CHANZO: BIN ZUEIRY


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU