Facebook Comments Box

Wednesday, July 31, 2013

BAADA YA KUTEMWA NA KLABU YAKE KASEJA AFANYA MAZUNGUMZO NA FC LUPOPO YA DRC

 

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, (Taifa Stars), Juma Kaseja Juma maarufu kama (Juma K. Juma) amesema kwamba amefanya mazungumzo na wakala wa klabu ya St. Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), lakini bado hajaingia Mkataba na klabu hiyo ya Lubumbashi.
 
  Kaseja amesema kwamba mtu aliyejitambulisha kwake kama wakala wa Lupopo alimfuata wakafanya mazungumzo na kufikia makubalino juu ya dau la usajili, mshahara na mambo mengine ya msingi.

Hata hivyo, kipa huyo namba moja Tanzania amesema kwamba baada ya mazungumzo hayo na maafikiano, wakala huyo amepeleka majibu Lupopo ambao wakiafiki ndipo masuala ya Mkataba yatafuatia.

“Nimezisikia hizo habari, kwamba mimi tayari ni mchezaji wa Lupopo, hapana, si kweli. Ni kwamba tumefanya mazungumzo tu na wakala wao na tumefikia makubaliano, nasubiri hadi nisaini Mkataba ndipo nitajihesabu tayari ni mchezaji wa Lupopo,”alisema Kaseja.

Pamoja na Simba SC kutomuongezea Mkataba Kaseja, ameendelea kuwa kipa chaguo la kwanza timu ya taifa mbele ya kocha Mdenmark, Kim Poulsen.
 
Iwapo Kaseja atafanikiwa kuingia Mkataba na Lupopo atakwenda kuwa mpinzani mkuu wa wachezaji wenzake wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea Tout Puissant Mazembe ya Lubumbashi.
 
Kaseja alicheza pamoja na Samatta na kiungo Mganda wa Mazembe, Patrick Ochan katika klabu ya Simba mwaka 2010 kabla ya 2011 wachezaji hao kuuzwa DRC.     
Source:Bin Zubeiry


MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA) IMEZINDUA KAMPENI YA KUHAMASISHA MATUMIZI MAZURI YA MAWASILIANO

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John S. Nkomo akizungumza mbele ya Wamiliki wa Blogs mbalimbali Tanzania na Waandishi wa habari katika Warsha ya kampeni ya kuzindua matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuhamasisha maendeleo.

ProfesaNkomo amesema kuwa kwa sasa kumekuwepo na ongezeko kubwa la matumizi ya intanet kwa Watanzania walio wengi toka watumiaji laki tatu miaka mitatu iliyopita hadi watumiaji milioni 7.6 kwa takwimu za hivi karibuni.

Amesema kuwa wengi wa watumiaji wa intanet matumizi yao ni katika kujifunza na kujielimisha pamoja na matumizi ya mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, BBM na Blogs zinazotoa habari mbalimbali kama vile habari za maendeleo, burudani na michezo.

Meneja uhusiano wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania Bw Innocent Mungi akiwakaribisha wadau mbalimbali wa habari na mitandao kuhusiana na uzinduzi wa kampeni hiyo.
Wadau wa mawasiliano ya kijamii, Blogs wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Mamlaka ya Mawasiliano katika uzinduzi wa matumizi mazuri ya mitandao kwa ajili ya kuhamasisha maendeleo ya Taifa kwa ujumla ambapo Mstari wa pili kulia mtu wa pili nyuma ni Muwakilishi wa kitongoni Blog Bw. Juma Kabange.
Wawakilishi wa TBC Bw. Elisha Elia na Bi. Daula Abdul
John Bukuku kutoka Full Shangwe Blog
Prof. John Nkomo akiwa na Mrisho Mpoto ambae ameimba wimbo maalum wa kampeni hiyo unaoitwa 'Delete Futa Kabisa' ukiashiria kufuta kabisa ujumbe mbaya utakaoupata katika simu yako au kwenye mtandao wako kabla hauja usambaza kwa wengine wengi.











JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhfKhIZuVa-nyuNh8KCKIUzrysQRxIceLLTs1qM7cj2O5-yWGphgpY2g1BzmFgFW1Cq4Y5O-J1D3xIk0ckg7VcUXIyEUb3S-qKf4YALtgq4O4gFXns4pRd5bLxckQtXczoDRxpotjUu9e8/s1600/TCRA_logo4.jpg

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
Taarifa kwa VYOMBO VYA HABARI

KAMPENI YA KUHAMASISHA MATUMIZI MAZURI YA MAWASILIANO

Siku za hivi karibuni, ongezeko la huduma za mawasiliano nchini limekuwa kwa kasi sana. Huduma za mawasiliano nchini katika kipindi kifupi zimekuwa sana na kuwafikia Watanzania wengi zaidi. Kutoka laini za simu za mkononi  milioni tatu tu mwaka 2000 hadi kufikia laini 28,000,000.  

Watanzania walio wengi hivi sasa wanafaidika kwa huduma za mawasiliano, yakiwemo mawasiliano ya simu za mikononi, utangazaji. Vile vile huduma za ziada kama kutuma na kupokea fedha kwa kutumia mitandao na simu za mkononi zimeongezeka maradufu. Wananchi wengi wanapata huduma za kibenki kwa kutumia simu zao, wanawasiliana kwa kutumia simu zao kupitia sauti, SMS na kadhalika.

Hali kadhalika kumekuwa na ongezeko la matumizi ya intaneti kwa watanzania walio wengi kutoka watumiaji laki tatu miaka mitatu iliyopita hadi watumiaji milioni 7.6 kwa takwimu za hivi karibuni. Wengi wa watumiaji wa intaneti matumizi yao ni katika kujifunza na kujielimisha pamoja na matumizi ya mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, BBM, LinkedIn na blog mbalimbali zinazotoa habari mbalimbali zikiwemo za kimaendeleo, burudani pamoja na michezo.

Matumizi haya ya intaneti yamewanufaisha watanzaia walio wengi kwani ni fursa murua ya kujifunza kupitia mitandao hiyo ya kijamii kwa kupata habari mpya, kujifunza na kuelimishana kuhusu shughuli za maendeleo na kuleta amani miongoni mwa watanzania.

Hata hivyo pamoja na maendeleo haya, kumekuwepo na baadhi ya watu wachache wanaotumia mawasiliano ya simu, mitandao ya kijamii, redio, TV na mawasiliano mengine kwa lengo la kuvuruga amani, kuchocheo vurugu, kuchonganisha watu, kusababisha ugomvi, kuwaumiza wengine kwa mambo yasiyo na ukweli, kupotosha jamii na hata kuvuruga maendeleo kwa ujumla.

Leo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inazindua kampeni ya kuelimisha umma kuhusu matumizi mazuri ya mawasiliano na inawatahadharisha wananchi kwamba kutumia mawasiliano vibaya kama ilivyoainishwa katika sheria ya Mawasiliano ya Kielectroniki na Posta (EPOCA) ya mwaka 2010 ni makosa. Katika kampeni hii, Mamlaka inakusudia kuwasihi wananchi kuhakikisha wanatumia mawasiliano vizuri ili kudumisha amani, mshikamano na upendo miongoni mwa watanzania.

Katika uzinduzi huu, Mamlaka imewaalika baadhi ya watumiaji mahiri wa mitandao ya kijamii ambao wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha watanzania walio wengi wanafaidika na mawasiliano. Miongoni mwao wako wamiliki wa blog mbalimbali, wasimamizi wa makundi mbalimbali katika mtandao wa FB na mengineyo. Nia ya Mamlaka ni kuomba ushirikiano kwao ili waweze kushiriki katika kampeni hii na kuwahamasisha mashabiki wao kutumia vizuri mitandao ya kijamii ili kunufaisha Taifa letu kwa matumizi mazuri.

Watumiaji wa simu za mkononi na wananchi wote wanashauriwa kuunga mkono juhudi zinazofanyika ili kufanikisha kampeni hii kwa ajili ya kudumisha na kuendeleza amani na usalama na kuharakisha maendeleo ya sekta ya Mawasiliano inaendelea kuchangia uchumi wa Taifa na kuiweka Tanzania katika mazingira mazuri zaidi kijamii, kiuchumi na kisiasa.


Imetolewa na:

 MKURUGENZI MKUU
Mamlaka ya mawasiliano TaNzania

31 Julai 2013












MATAWI YA YANGA YAUNGA MKONO UONGOZI KUIKATAA AZAM TV


Bakili Makele (kulia) akiongea na waandishi wa habari kwa niaba ya viongozi wa matawi, Moses Katabaro(katikati) na Lawrence Mwalusako (kushoto) 























Uongozi wa matawi wa klabu ya Yanga (wenyeviti na makatibu) leo umefanya kikao katika makao makuu ya klabu mtaa wa twiga/jangwani kisha kutoa tamko lao kwa waandishi wa habari kuhusiana na tamko la uongozi (kamati ya utendaji) kutokubali kuonyeshwa kwa michezo yake kwenye luninga.
Awali klabu ya Yanga juzi kupitia kamati ya utendaji ilifanya mkutano na waandishi wa habari juu ya mustakabali wa klabu kuhusiana na kutoridhishwa na kamati ya muda ya Ligi (TPL) kuingia makubaliano ya kurushwa matangazo ya televsheni kwenye michezo yake.
Akiongea na waandishi wa habari leo katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako alisema baada ya kukaa na viongozi wa matawi ya klabu ya Yanga jijni Dar es salaam kwa pamoja wamekubali na kuunga mkono hoja zilizowasilisha na viongozi juu ya haki ya matangazo.
Mmoja wa viongozi wa matawi Bakili Makele akiongea kwa niaba ya viongozi wa matawi, alisema TFF inaamua kukandamiza soka la Tanzania kwa kuviamulia maamuzi yake juu ya kuonyeshwa kwa michezo ya timu kwenye luninga.
Makele amesema taratibu za kuipa kampuni ya Azam TV tenda ya kuonyesha michezo ya Ligi Kuu haikua na usawa, kampuni hiyo bado haijaanza hata matangazo, haijulikani ofisi zake zilipo, uwezo wa kurusha matangazo haujulikani kwa watanzania lakini bado wamepewa nafasi hyo.
Kikubwa tunamuomba rais wa TFF Leodgar Tenga kulitazama suala hili kwa umakini, kwani mtazamo wetu viongozi wa kamati ya Ligi wametazama maslahi yao binafsi bila kuzingatia uwezo wa timu na maliasili watu (wapenzi,washabiki).
Huwezi kuipa mgawo sawa timu ya Yanga na timu nyingine ambazo katika mechi zao binafsi wanatapata washabiki 50 kwenye mchezo, wakati Yanga imeongoza kwa mapato katika msimu mzima wa Ligi Kuu ya Vodacom na wastani wa washabiki 8,000 kwa kila mchezo.
Mwisho Makele amesema wanauamini uongozi uliopo na wapo nao bega kwa bega, tunaomba jamii nzima itambue kuwa Yanga inapigania haki zake na hao wote wanaobeza msimamo wetu basi wajibu hoja kwa hoja na sio kuongea tu pasipo kujibu hoja. 

SOURSE:YANGA


KIBONZO: KUWAFUNDISHA WATOTO MAMBO YA DINI NI MUHIMU

www.kitongoni.blogspot.com



NASHEED: MAHER ZAIN - YA NABI SALAM ALAYKA (VOCAL ONLY)




MAWAIDHA: SHEIKH NAASOR BACHU - MAMBO YASIYOBATILISHA SWAUM




VIDEO: SAMSUNG S4 ACTIVE HAINGII MAJI WALA VUMBI





Tuesday, July 30, 2013

VIDEO: SHABIKI WA YANGA AKILIA BAADA YA KUTOSWA BSS




MAWAIDHA: SHEIKH YUSUF ABDI - MBONA HATUWI WACHAMUNGU?




TAMASHA LA SIMBA LAPELEKWA MBELE: TP MAZEMBE HAWATAKUJA KUSHIRIKI TAMASHA HILO

TAMASHA la kuazimisha siku ya Simba SC linaweza kusogezwa mbele kwa simu mbili, kupisha sikukuu ya Eid El Fitri hivyo kufanyika Agosti 10, badala ya Agosti 8, kama ilivyo kawaida yake.
Aidha, mpango wa Simba SC kucheza na mabingwa wa Afrika mara nne, Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeshindikana kutokana na timu hiyo ya Lubumbashi kutingwa na michuano ya Kombe la Shirikisho.
Kikosi cha simba kilichopita kikiwa na wachezaji wazuri kama Mrisho Ngassa, Juma Kaseja, Haruna Moshi na Mwinyi kazimoto


Na kwa sababu hiyo, timu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, Dar es Salaam sasa itacheza na SC Villa ya Uganda katika tamasha hilo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba ilitumai kucheza na Mazembe yenye wachezaji wake wa zamani wawili, Mbwana Samatta na Patrick Ochan ambao iliwauzua klabu hiyo miaka miwili iliyopita, lakini ratiba ya michuano ya CAF imeharibu mambo. 
Katika maendeleo mengine, wachezaji wa Simba SC waliokuwa na kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wanatarajiwa kujiunga na wenzao kambini, Bamba Beach, Kigamboni kuanzia leo jioni.
Wachezaji waliokuwa Stars ni viungo Amri Kiemba na Haroun Chanongo. Kiemba alicheza dakika zote 90 na kufunga la Stars ikilala 3-1 Uwanja wa Mandela, Namboole na kutolewa jumla ya mabao 4-1, baada ya awali kufungwa 1-0 Dar es Salaam wiki mbili zilizopita, wakati Chanongo aliingia uwanjani dakika ya 78 kumpokea John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC.

SOURSE: BIN ZUBEIRY

UJUMBE ALIOPEWA SHEIKH PONDA NA VIONGOZI WA UAMSHO ALIPOWATEMBELEA GEREZANI

Sheikh Ponda Issa Ponda
 
Na Bakari Mwakangwale, An-Nuur — VIONGOZI wa Jumuiyaya UAMSHO Zanzibar wamesema kwamba pamoja na kuzuiwa kwao Gerezani, hawana shaka kuwa ipo siku hakiitasimama na hatimaye kupatikana Taifa Uhuru la Zanzibari.

Kauli hiyo wameitoa mbele ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi zaKiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, muda mfupi baada ya kukutanana viongozi hao Ijumaa ya wiki iliyopita katika Gereza la Kiinuamiguu, lililopo Mtaa wa Kilimani Zanzibar.

Sheikh Ponda, alifika gerezani hapo akiwa katika muendelezo wa ziara zake anazofanya nchini na kuongea na Waislamu, baada ya kumalizika kwa kesi yake na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje.

Akiongea na Mwandishi wa habari hizi katika ofisi za Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Kinondoni, Jijini Dares Salaam, mapema wik ihii alisema alifanikiwa kuonana na viongozi wa UAMSHO na kuongea nao kwa muda wa dakika 45.

Alisema, Masheikh hao waliopo gerezani kwa muda wa miezi tisa sasa, wapo imara kiimani ambao walitumia fursa hiyo kumpa salamu kwa Wazanzibari huku naye akiwapa salamu kutoka kwa Waislamu wa Bara. “Hawana hofu pamoja na kushikili wa na Dola kwa muda wote huo, kwani wanachoamini wao kuwa wapo katika haki, na uimara wao unakuja kutokana na kuijua vizuri historia ya kupigania haki kuwa hata Mitume 
wa Mwenyezi Mungu, walipo tangaza haki, walipata misukosuko na kupigwa vita na watawala.” Alisema Shkh. Ponda, Akielezea hali za Viongozi hao wa UAMSHO.

Ponda, alisema kuwa Masheikh hao, MselemAli, Azan Khalid, Musa Juma pamoja nae Amir Farid Had, kwa kwa ujumla akiyatafakari maongezi yao anaona ni wazi kuwa msimamo wao ni kutorudi nyuma katika kupigania haki na zaidi alidai walimuambia hawana shaka kuwa ipo siku haki itasimama na batili itaondoka Visiwani humo. Alisema, Masheikh hao, walimtaka awafikishie ujumbe Wazanzibar katika mikutano yake kuwa wasiache kuzungumzia haki zao za msingi wanazodai kwani kwa kufanya hivyo ndiyo kuitendea haki Zanzibar.

“Katika fursa hii mliyoipata ya kuwahutubia Wazanzibar na hatimae Watanganyika, waambien imsimamo wetu bado ni uleule wa kutetea Taifa Uhuru la Zanzibari na bila shaka pia huo utakuwa ni Uhuru kwa Watanganyika pia,” alisema Sheikh Ponda, akimnukuu Amir Farid Had.

Sheikh Ponda alisema viongozi hao walimuagiza kutumia vema fursa ya mikutano yake Visiwani humo na hatimae Bara kwa kuinua hamasa za Waislamu huku wakimtaka kuwaelekeza kutumia vema mafunzo na misimamo waliyoitoa juu ya Taifa huru la Zanzibar.

“Darsa zetu bila shaka zimejenga imani na akida, vilevile zinatosha kuwa semina za kujitambua.

Lakini pia tulijenga hamasa kubwa na utayari wakutetea haki hadharani. Kama Waislamu hawatakiwi kurudi nyuma wasinyamaze hata kidogo”, alisema Sheikh Ponda, akidai kuwa huo ni ujumbe kutoka kwa Sheikh Mselem Ali.

Awali Sheikh Ponda, kwa upande wake aliwapa viongozi hao salamu na hisia za Waislamu wa Bara kufuatia ziara zake katika mikoa kadhaa ya Tanzania Bara zilizoandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu mara baada ya kutoka Gerezani.

“Waislamu wa Bara wanatambua msimamo wenu wa kupigania haki, pia wanaamini kukamatwa kwenu ni ukweli wa methali isemayo ‘kiza kinapozidi kuwa kinene ndivyo kupambazuka kunavyokaribia’ hivyo wako pamoja nanyi.” Alisema SheikhPonda, akirejea kauli yake mbele ya viongozi wa UAMSHO Gerezani.

Katika ziara yake hiyo Visiwani humo, Sheikh Ponda, pia alipata fursa ya kuwahutubia maelfu ya Wazanzibar katika mihadhara sita iliyoandaliwa na Jumuiya ya UAMSHO katika maeneo mbalimbali ya Unguja.

Akiwahutubia maelfu ya waumini waliohudhuria katika muhadhara uliofanyika Mkoa wa Mjini Maghribi Masjid Sahaba Daraja Bovu, Sheikh Ponda, aliwataka Waislamu wa Zanzibar kuchukua hadhari ya njama zinazopikwa kuvunja udugu wao kwa lengo la kuwagawa. Kwa mujibu wa Sheikh Ponda, alisema maelfu ya Waislamu waliokutana katika Msikiti wa harakati maarufu kwa jina la Msikiti wa Mbuyuni, walisema wanatafakari hatma ya viongozi wao wanaoshikiliwa na Dola kwa zaidi ya miezi tisa sasa.

“Msimamo kama huo ulitolewa tena katika mkusanyiko mkubwa uliofanyika siku iliyofuata (Ijumaa iliyopita) mara tu baada swala ya Ijumaa katika Msikiti wa kwa Mpendae kwa Kificho.

Kuonesha hisia zenu kama hivi bila shaka mnajenga nguvu kubwa ya pamoja na wakati utakapofika watawatoa tu viongozi wenu”. Alisema Sheikh Ponda, akiwahutubia waumini wa Nungwi.

Aidha Shkh Ponda, aliwataka waumini wa Nungwi kujiimarisha kwa miradi ya maendeleo kwa kutumia vizuri hazina kubwa ya ardhi waliyonayo ambayo imekuwa ikivamiwa kwa kasi kubwa na wawekezaji wa mahoteli ya kitalii, ambao kwa asilimia tisini wanaharibu utamaduni wa Mzanzibar.

Sheikh Ponda, alisema Jumuiya ya UAMSHO, inatarajia kufanya muhadhara mkubwa siku ya Ijumaa katika Msikiti wa Mbuyuni, lengo likiwa ni kufanyama jumuisho ya mihadhara iliyofanyika akiwa hukowiki iliyopita.

--
Rejea ya habari: An-Nuur no. 1081


Monday, July 29, 2013

NITAJIUZULU NIKIBAINIKA NAUZA MADAWA YA KULEVYA - IDD AZZAN

Picture: Idd AzzanIdd AzzanSiku chache baada ya jina lake kutajwa kwenye waraka unaodaiwa kuwa barua kutoka kwa mmoja wa Watanzania waliofungwa katika jela huko Hong Kong, Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan amezungumza na kusema kuwa yupo tayari kujiuzulu ubunge ikiwa itabainika anajihusisha biashara ya dawa za kulevya.

Idd Azzan amekaririwa katika habari iliyoandikwa na mwandishi Bakari Kimwanga, na kuchapoishwa kwenye gazeti la MTANZANIA jana akisema kuwa hatua ya kuhusishwa na biashara haramu ya dawa za kulevya ni kutotenda haki mbele ya jamii hasa wapiga kura wake na Taifa kwa ujumla. Akasema mtu aliyendika barua ya tuhuma dhidi yake amedhamiria kumshushia heshima na huenda ana jambo limejificha.

Alisema kutokana na hali hiyo, anashindwa kuchukua hatua yoyote ya kufanya zaidi ya kuliandikia barua Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi dhidi ya barua hiyo kuweza kubaini ukweli wa jambo hilo.

Ni kweli nimeiona hiyo barua katika mtandao, inayodaiwa imeandikwa na kijana ambaye amekamatwa Hong Kong nchini China. Lakini ninajiuliza kama kweli yeye ni raia mwema, katika hili kwa nini hakutaka kutaja jina lake kwenye barua hiyo?

Hata nilipoisoma nimebaini kuwa huyo mtu ametumika na huenda kabisa hayupo nje ya nchi, kwani 
katika maelezo yake anataja jina la Balozi Philip Marmo kuwa amemsaidia hali ya kuwa hivi karibuni Rais Kikwete alimteua Balozi mpya Abdulrahman Shimbo na Marmo kuwa Balozi wa Shirikisho la Ujerumani.

Kingine naona alijaribu kuandika uongo kuweza kuaminisha jamii, kwani hata hilo jila la balozi mwanzo limetajwa jina la Bernard na kukatwa kwa wino. Ninapenda kulieleza Taifa kuwa naomba vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa jambo hili na nikibainika ninauza dawa za kulevya nipo tayari kujiuzulu ubunge wangu.

Kubwa haki itendeke katika kufanya uchunguzi wa jambo hili, ila ni lazima jamii na Watanzania kwa ujumla tusikubali kwa makusudi watu waichafue nchi yetu kwa chuki na fitna tu.

Sijawahi kuuza dawa za kulevya na hata katika familia yangu hakuna mtu anayefanya biashara hiyo haramu. Kila mmoja anajua kuwa Idd nilikuwa Diwani wa Kata ya Magomeni, huku kazi yangu kubwa ikiwa ni biashara ya magari na daladala ambayo ninaendelea nayo hadi sasa mbali ya ubunge kama nilivyopewa heshima na wapiga kura wangu wa Kinondoni.
Alipoulizwa kuwa ni hatua gani ikibainika hakuna ukweli wa jambo hilo baada ya vyombo vya usalama kufanya uchunguzi, Azzan alisema: “Ni ngumu kusema hatua gani nitachukua ikibainika hakuna ukweli, lakini nataka kusema kama yule aliyeandika barua hii angetaja jina lake ni wazi baada ya uchunguzi ningeweza kuomba ushauri kwa mwanasheria wangu hatua za kuchukua, lakini kwa kuwa hakutaja jina ni ngumu kuweza kuamua.” 

Source: WAVUTI

DIAMOND ANUNUA MTAA DAR ES SALAAM

Na Shakoor Jongo
WAKATI Wema Isaac Sepetu akiongeza idadi ya magari kwa kununua mkoko wa maana, zilipendwa wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemziba mdomo baada ya kununua eneo kubwa ambalo ndani yake kuna nyumba tatu, jirani na anapoishi Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006, Ijumaa Wikienda lina maelezo kamili.

Eneo alilonunua Diamond katika Mtaa wa Kaprikoni-Kijitonyama jijini Dar.
Tukio hilo lilijiri hivi karibuni Mtaa wa Kaprikoni-Kijitonyama jijini Dar na kusababisha watu kupigwa na butwaa na kudai kuwa kweli ‘dogo’ ana jeuri ya fedha kwa kitendo hicho cha kununua karibia mtaa wote huo.
Diamond.
Akizungumza na gazeti, hili muda mfupi  baada ya kukamilisha kila kitu kuhusiana na ununuzi wa eneo hilo ambalo kwa mujibu wake anatarajia kujenga jengo lenye ghorofa nne na nyumba za kawaida tatu, Diamond alisema kuwa anajitahidi kuongeza idadi ya mijengo anayomiliki kwa kuwa ndicho kitu cha thamani kuliko magari.
Mkoko wa Wema.
“Najua (nyumba) zitanisaidia endapo muziki wangu utakosa soko. Mimi na mama yangu (Sanura Kassim ‘Sandra’) tuliishi kwa dhiki sana na sasa kwa kipindi hiki ambacho Mungu ananisaidia na kuniwezesha kupata fedha kwa wingi, siwezi kuishi maisha ya anasa ya kununua magari ya kifahari,” alisema.
 
Wema.
Katika hali iliyotafsiriwa kuwa ni kumtunishia msuli Wema, jamaa alitupia maneno: “Mimi siyo kama hao wanaokimbilia kununua magari ya kifahari ili mradi waonekane wako juu kifedha.
Eneo alilonunua Diamond anayemiliki nyumba zaidi ya tano Dar lipo mtaa wa nne kutoka anapoishi Wema.

KIBONZO: ANGALIA UKAGUZI WA WABONGO KWENYE VIWANJA VYA NDEGE VYA NJE

Picture



YANGA WAKATAA AZAM TV KUONESHA MECHI ZAO


mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji (katikati) akiongea na waanidishi wa habari, Makamu mwenyekiti Clement Sanga (kushoto) na mjumbe wa kamati ya utendaji Mark Anthony (kulia)

 
Uongozi wa klabu ya Yanga leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu ya urushwaji wa michezo yake ya Ligi Kuu katika kituo cha luninga cha Azam ambacho kimeingia makubaliano na kamati ya Ligi Kuu  kuonyeshwa michezo yote ya ligi kwa kipindi cha miaka miatatu (3).
 
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusuf Manji amesema uamuzi wa kamati ya ligi kuingia mkataba na kituo cha Azam Tv bila ya kuwashirikisha wahusika wenyewe ambao ni vilabu vishiriki haukuwa sawa.
 
Sisi kama klabu ya Yanga tulikaa kikao cha kamati ya utendaji na kuona taratibu za kupewa haki ya matangazo kwa kampuni ya Azam haikua sawa, sisi viongozi wa kalbu ya Yanga hatukushirikishwa katika mchakato huo hivyo tukaona ni vema tuje kwa vyombo vya habari tuulezee umma juu ya maazimio ya kamati ya utendaji.
 
Ifuatayo ni taarifa kamili kwa vyombo vya habari: 
 
YAH: URUSHWAJI KATIKA TELEVISHENI MICHEZO YA YANGA.

Hivi karibuni, Tanzania Football Federation (TFF)  iliunda Tanzania Premier League chini ya Bodi yampitoBodi ya TPL ambayo ni msimamizi mpaka hapo Bodi itakayokuwa imechaguliwa kidemokrasia. Bodi hii imeamua peke yake kuingia katika mkataba wa miaka 3 (mitatu) na kampuni inayoitwa Azam Television (ambayo ina  mapromota wale wale wanaomiliki Azam Football Club). Makubaliano ambayo Bodi ya TPL inatarajia kuingia na Azam Television, Kamati ya Utendaji ya YANGA inalipinga kwa nguvu zote katika misingi ifuatayo:

1. BODI YA TPL

1.1 Bodi iliyoko sasa hivi ni ya mpito ambayo ilitakiwa kutenguliwa na Bodi iliyochaguliwa kidemokrasia kwa kupitia uchaguzi wa tarehe  ……….. mwaka huu na haitakiwi kuingia katika mikataba a miaka mingi wakati inakaribia kuondoka katika ofisi.

1.2 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haikuchaguliwa kidemokrasia.

1.3 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haina mjumbe hata mmoja aliyeteuliwa kutoka YANGA.

2. UTARATIBU WA DUNIA NZIMA

2.1 Haijawahi kutokea katika ligi ya mpira wa miguu ya kisasa kulazimishwa kwa Klabu inayoshindana katika ligi kuachia haki zake za urushwaji wa michezo zichukuliwe na chombo cha habari cha Klabu ya upinzani. 

2.2 Mfumo (undertaking) ambao TPL inataka kuanzisha kwa njia ya kulazimisha mkataba kwa YANGA iachie  urushwaji wa michezo yake ya soka yarushwe na Azam TV unatishia sana uwepo wa msingi wa ushindani katika soka ya Tanzania.

2.3 Makubalianokati ya TPL na Azam Television kuhusu utaratibu wa malipo yanasemakwamba Klabu ya YANGA na Klabu zingine zitakazoshiriki katika Ligi Kuu ya Tanzania  watapata mgao sawa wa mapato ya urushwaji wa michezo hii, ambayo YANGA inapinga kwa sababu kama inavyofanyika duniani kote kwenye ligi zilizofanikiwa (angalau) kutofautisha mgawanyo wa mapato kati ya timu kufuatana na matokeo ya mwisho wa ligi.

2.4 Kamati ya Utendaji ya YANGA siyo tu haikubaliani na mgawanyo sawa wa mapato ambao hautofautishi kati ya timu ya kwanza katika ligi na timu ya mwisho katika ligi, lakini pia ukosefu wa viwango (premiums) vitakavyolipwa: 

2.4.1 Vilabu vya mpira vyenye ufuasi wa washabiki wengi; 

2.4.2 Vilabu vya mpira vinavyoendeshwa na Wanachama; 

2.4.3 Vilabu vya mpira visivyopata ruzuku kutoka Serikalini n.k.

3. MIGOGORO YA MASLAHI

3.1 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mpito ya TPL ni Mkurugenzi mwandamizi wa Makampuni ya Azam na  kwa hivyo mazungumzo ya siri kati ya Bodi ya TPL na Azam ni ya kutiliwa mashaka.

3.2 Makampuni ya Azam yana yanashindana kibiashara na makapuni mengi yakiwemo ya utengenezaji wa vinywaji baridi na imeonyesha huko awali inaweka “matakwa maalum” muhimu zaidi kuliko mprira  wa miguu, kama vile Azam F.C. hawashiriki katika Kombe la Tusker na kwa hiyo YANGA inakuwa na msimamo kwamba kwa Azam Television kupewa leseni ya kurusha matangazo ya mpira wa miguu inatishia biashara za washiriki wa sasa na wa baadaye wa YANGA.

3.3 Azam na YANGA wana uadui wa kimichezo. Kumbuka, wakati MRISHO NGASSA alipotaka kwenda YANGA, Azam F.C. walimkopesha kwa nguvu kwa Klabu ya Simba! Kwa hiyo YANGA itahatarika kwa matangazo yenye upendeleo kama Azam Television itarusha hewani michezo yake n.k.

4. KUTOKUWA NA UWAZI

4.1 Mkataba wa utangazaji wa miaka mingi unaotaka kuingiwa kati ya TPL na ambao badohaujarushwa Television ya Azam haukushindanishwa na vyombo vingi vya habari,  na vyombo ambayo wako tayari kwenye soka havikujulishwa kuhusu fursa hii au walizuiliwa kufikisha mapendekezo yao ya maombi ya haki za kurusha matangazo katika Ligi Kuu (Tanzania Premier League).

4.2 Ukosefu wa uwazi wa TPL unanonyesha kuwa MoU iliyokusudiwa kuwekewa saini na TPL haikufikishwa YANGA kwa ajili ya mapitio ya kisheria, licha ya YANGA kufanya ombi hilo kwaTPL.

5. MAZINGATIO YA KIBIASHARA 

5.1 Mamlaka ya kuamua mzozo wowote wa mkataba wa leseni ya utangazaji wa Ligi Kuu (Tanzania Premier Leagu) itakuwa ni Mahakama ya kisheria na siyo FIFA. TPL inasingizia  kwamba leseni ya matangazo ambayo inakusudia kufanya kuwa ni maagizo ya FIFA na kwa hiyo YANGA inapaswa kuukubali "lock, stock and barrel."

5.2 TPL inaelezea kimakosa makubaliano ya leseni ya urushaji  wa mchezo ya mpira inayotarajia kuingia na Television ya Azam kama "makubaliano ya udhamini" (“sponsorship agreement”) ambayo siyo sahihi, kwa sababu urushaji wa michezo ya mpira wa miguu ni biashara inayotokana na maslahi ya uhusiano na hivyo 
wahusika wote ni lazima wazingatie maslahi yao ya kifedha.

Kwa mfano, moja ya vyanzo muhimu vya mapato ya YANGA ni mapato ya kiingilio ya mlangoni yatokanayo na michezo ya mpira wa miguu ambayo urushwaji wa michezo hii itapunguza mapato haya. Kwa wastani michezo ya YANGA  Dar es Salaam huingiza makusanyo ya mlangoni shilingi milioni 50 kwa kila mchezo na hata kushuka kidogo kwa 25% katika mahudhurio ya mechi za YANGA zinafikia mara mbili ya mapendekezo ya mapato takribani Sh milioni 8.3 kwa mwezi kupokelewa na YANGA kutoka mradi wa kibiashara kati ya TPL na Azam Television. Kwa kuzingatia haya, kwamba hata siku za nyuma kama kulikutokea fursa ya kurusha mchuano wa mpira unapochezwa, wadau wote (Timu za mpira wa miguu, TFF na Mtangazaji)  walikuwa wanaafikiana kwanza kwa pamoja kuhusu mapato na mgawanyo wake.

Kamati ya Utendaji ya YANGA ina maoni kwamba makubaliano yoyote ya kibiashara yanayoihusu ni lazima iyalinde maslahi kifendha ya Klabu yake ambapo makubaliano ya TPL / Azam Television hayaangalii na kwa hiyo, Kamati ya Utendaji ya YANGA haitaki mchezo wake urushwe hewani na Azam Television.

Msisitizo wa TPL kuwa lazima Azam Television irushe hewani michezo ya YANGA linasikitisha. Kamati ya Utendaji ya YANGA haina tatizo na Vilabu vingine vya mpira wa miguu zikiruhusu michezo yao kurushwa na Azam Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mchezo wake wa Vodacom Premier League katika Azam Television.
......................
(YUSUF MANJI)
MWENYEKITI
YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB
29 JULAI, 2013


Sunday, July 28, 2013

VIDEO: TANZANIA SIO MALI YA CCM AU CHADEMA - MSIGWA (MB)




PICHA ZA MTANZANIA ALIEITWA KUFANYA MAJARIBIO CHELSEA AKIHOJIWA NA VOA

Picture
Davis Mosha "The Boss" akifanya mahojiano na kituo cha VOA jijini Washington DC, kulia ni mwanae Edgar Mosha mwanafunzi mwenye kipaji cha masomo na soka.
Picture
Edgar Davis Mosha mtoto wa mfanyabiashara tajiri na maarufu boss wa kampuni ya DELINA, Bwana Davis Mosha ahojiwa na VOA (Voice of America). Edgar na baba yake wametua kwa kishindo nchini Marekani wakitokea Uingereza ambapo Edgar amepeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kuitwa  kufanya majaribio na klabu ya Chelsea ya Uingereza. Swahili TV itakuletea Exclusive video karibuni.
Picture
Kutoka kushoto; Juliet , Sunday Shomary, Edgar Mosha, Davis Mosha "The Boss" na Chief wa VOA Idhaa ya Kiswahili Dkt. Hamza Mwamoyo.
Picture
Picture
Picture
Picture
Picture
Picture
Baada ya mahojiano na kituo cha VOA msafara wa The Boss ulielekea Sequoia kwa hafla fupi .
Picture
Edgar na Juliet wakiwa Sequoia water front.
Picha zote na maelezo ni kutoka SwahiliTv watembelee kwa mengi mengineyo katika SwahiliTv.blogspot.com


NAPE NNAUYE AKERWA NA KUSIKITISHWA NA HABARI YA GAZETI LA MTANZANIA

Nimestushwasana na stori ya gazeti la Mtanzania inayodai kuninukuu kuwa nimesema wazee waliopendekeza serikali tatu wanasubiri kufa!

Kwa kweli nimesikitishwa sana hata na jinsi maneno ndani yalivyopangiliwa kiasi kwamba inanipa tabu kuamini kama mhariri aliipitia hii stori ukiachilia mbali kama aliyetumwa kuja kuandika stori alikua ni "too junior".

Nawaheshimu sana wazee wangu hawa hata kama nikipishana nao kimawazo siwezi kufikia kutamka maneno makali kiasi hicho.

Nilichosema ni kuwa ukilinganisha vijana na wazee, vijana wanawajibu mkubwa wa kuamua kesho yao badala ya kudhani kuna mtu atawaamulia. Hivyo wanawajibu mkubwa kwani takwimu zinaonyesha asilimia 60% ya idadi ya watu nchini ni vijana! Sasa sijui kama kwa mwandishi na mhariri wake tafsiri ndio hiyo?!!!

Imenisikitisha sana!

Nape Moses Nnauye
The CCM Secretary for Ideology & Publicity



Saturday, July 27, 2013

ACHOMA NYUMBA MOTO KWA KUNYIMWA PENZI NA SHEMEJI

Polisi mjini Bomet, Kenya wanamtafuta mwanaume mmoja aliyetajwa kwa jina moja tu la Robert, mwenye umri wa makamo kwa tuhuma za kuchoma nyumba ya kaka yake moto na kukimbia, kwa hasira za kunyimwa ngono na mke wa kaka yake.

Kwa mujibu wa taarifa za Chifu wa Merigi, Richard Kiprono Lang’at, mtuhumiwa alitumia mwanya wa kaka yake anayetumikia kifungo gerezani, kumhadaa na kumtongoza shemeji yake.

“The woman’s husband is serving a life sentence in Naivasha Maximum Prison after he was found guilty of defilement,” “His brother has, however taken advantage of his absence to demand sex from the woman,”  alisema Lang’at.



KIBONZO: KIPANYA AKIFUKIA HELA ARDHINI

Picture


VIDEO: MAN CITY WAKIJIFUNZA JINSI YA KUJIANGUSHA UWANJANI




VIDEO: NSAJINGWA AKIELEZA KWANINI AMEONDOKA YANGA NA KUWA KOCHA




AZAM MEDIA YALIPA BILIONI 6.5 KUONESHA MECHI ZA LIGI KUU TANZANIA



Badhi ya viongozi wa TFF wakisaini mikataba na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam, Said Mohammed (wa kwanza kulia) leo kwenye Ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam.
Televisheni ya Azam inayojulikana kama Azam TV imeingia mkataba wa miaka mitatu wa kuonesha michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambapo mkataba huo umetajwa kuwa na thamani ya Tsh bilioni 6.5
Aidha Televisheni hiyo itakuwa na majukumu ya kuonesha mechi za moja kwa moja (LIVE) zisizopungua 60 za Ligi hiyo huku nyingine 180 zikiwa zimerekodiwa.


ANGALIA MISHAHARA MIPYA YA WAFANYAKAZI WA SERIKALI HAPA

Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimuudumia mgonjwa hospitalini hapo. Wafanyakazi wa sekta ya afya ni miongoni wa walio ongezewa mishahara na serikari katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14. Picha na Maktaba  


Dar. Serikali imetangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma itakayoanza kutumika mwezi huu, huku kima cha chini kikiongezwa kwa asilimia 41.18 kutoka Sh 170,000 hadi Sh240,000.
Vilevile, mishahara ya watumishi wengine wa umma imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41. Waraka namba moja kwa watumishi wa umma uliotolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi Julai 2 mwaka huu, unaeleza kuwa marekebisho hayo ya mishahara yatahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa.
Wengine watakaonufaika na marekebisho hayo ni watumishi walioshikizwa kwenye taasisi za umma na watumishi ambao watakuwa kwenye likizo inayoambatana na kuacha kazi, kustaafu kazi au kumaliza mikataba baada ya Julai mosi mwaka huu.
Waraka huo umeonyesha kuwa watumishi wa serikali ambao wanapata mishahara binafsi isiyo ndani ya viwango vya mishahara ya serikali hawatahusika na marekebisho hayo.
Mei 29 mwaka huu, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, aliliambia Bunge, kwamba Serikali imekamilisha majadiliano ya kuongeza kima cha chini cha mshahara katika sekta 12 binafsi, kitakachoanza kutumika rasmi Julai mosi.
Waziri Kabaka alitaja sekta hizo kuwa ni ya Ujenzi, Shule Binafsi, Nishati, Viwanda na Biashara, Hoteli na Huduma za Majumbani, Ulinzi Binafsi, Madini, Afya, Uvuvi na Huduma za Majini, Usafirishaji, Mawasiliano na Kilimo. Kwa mujibu wa Kabaka, mishahara imepanda kwa kiwango cha asilimia kati ya 21 na 65 huku Afya ikiongoza kwa kuongezwa ikifuatiwa na sekta ya hoteli na huduma za nyumbani yenye asilimia 55.
Mei mosi mwaka huu akiwa mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete, aliahidi unafuu wa maisha kwa wafanyakazi kwa kuangalia uwezekano pia wa kupunguza kodi kwenye mishahara, Lipa Kadiri Unavyopata (PAYE).
Kuhusu kuongeza mishahara, Rais Kikwete aliahidi wafanyakazi wote kwamba Serikali itaendelea kuiongeza kulingana na hali ya uchumi wa nchi. Waraka huo unaonyesha kuwa mishahara mipya kwa watumishi wa serikali kada ya masharti (operational service), ngazi ya mshahara na mshahara mpya kwenye mabano ni;

TGOS A
TGOS A 1. (Sh240,000), TGOS A 2. (Sh245,600), TGOS A 3. (Sh251,200), TGOS A 4. (Sh256,800), TGOS A 5. (Sh262,400), TGOS A 6. (Sh268,000), TGOS A 7.(Sh272,000), TGOS A 8(Sh279,000), TGOS A 9.(Sh284,800), TGOS A 10(Sh290,400), TGOS A 11(Sh296,000), TGOS A 12(Sh301,600), TGOS A 13(Sh 307,200), TGOS A 14(Sh312,800), TGOS A 15(Sh 318,400), TGOS A 16(Sh324,000), TGOS A 17(Sh329,600) na TGOS A 18(Sh335,200).
TGOS B
TGOS B 1. (Sh347,000), TGOS B 2. (Sh356,500) TGOS B 3 . (Sh366,000), TGOS B 4 . (Sh375,500), TGOS B 5. (Sh385,000), TGOS B 6. (Sh394,500), TGOS B 7. (Sh404,000), TGOS B 8. (Sh413,500), TGOS B 9. (Sh423,000), TGOS B 10. (Sh432,500), TGOS B 11 . (Sh442,000) na TGOS B 12. (Sh451,500).


TGOS A
TGOS A 1. (Sh240,000), TGOS A 2. (Sh245,600), TGOS A 3. (Sh251,200), TGOS A 4. (Sh256,800), TGOS A 5. (Sh262,400), TGOS A 6. (Sh268,000), TGOS A 7.(Sh272,000), TGOS A 8(Sh279,000), TGOS A 9.(Sh284,800), TGOS A 10(Sh290,400), TGOS A 11(Sh296,000), TGOS A 12(Sh301,600), TGOS A 13(Sh 307,200), TGOS A 14(Sh312,800), TGOS A 15(Sh 318,400), TGOS A 16(Sh324,000), TGOS A 17(Sh329,600) na TGOS A 18(Sh335,200).
TGOS B
TGOS B 1. (Sh347,000), TGOS B 2. (Sh356,500) TGOS B 3 . (Sh366,000), TGOS B 4 . (Sh375,500), TGOS B 5. (Sh385,000), TGOS B 6. (Sh394,500), TGOS B 7. (Sh404,000), TGOS B 8. (Sh413,500), TGOS B 9. (Sh423,000), TGOS B 10. (Sh432,500), TGOS B 11 . (Sh442,000) na TGOS B 12. (Sh451,500).
TGOS C
TGOS C 1 . (Sh471,000), TGOS C 2 . (Sh482,000), TGOS C 3 . (Sh493,000), TGOS C 4. (Sh504,000), TGOS C 5. (Sh515,000), TGOS C 6. (Sh526,000), TGOS C 7. (Sh537,000), TGOS C 8. (Sh548,000), TGOS C 9. (Sh559,000), TGOS C 10. (Sh570,000), TGOS C 11. (Sh581,000) na TGOS C 12. (Sh592,000).
Watumshi wa serikali wenye taaluma mbalimbali
TGS A
TGS A 1. (Sh249,000), TGS A 2. (Sh255,600), TGS A 3. (Sh262,200 ), TGS A 4. (Sh268,800 ), TGS A 5. (Sh275,400), TGS A 6. (Sh282,000), TGS A 7. (Sh288,600 ), na TGS A 8. (Sh295,200).
TGS B
TGS B 1. (Sh311,000), TGS B 2. (Sh319,500), TGS B 3. (Sh328,000), TGS B 4. (Sh336,500), TGS B 5. (Sh345,000), TGS B 6. (Sh353,500), TGS B 7. (Sh362,000), TGS B 8. (Sh370,000), TGS B 9. (Sh379,000) na TGS B 10. (Sh 387,500).
TGS C
TGS C 1. (Sh410,000), TGS C 2. (Sh420,000), TGS C 3. (Sh430,000), TGS C 4. (Sh440,000), TGS C 5. (Sh450,000), TGS C 6. (Sh460,000), TGS C 7. (Sh470,000) na TGS C 8. (Sh480,000). TGS C 9. (Sh490,000), TGS C 10. (Sh500,000), TGS C 11. (Sh510,000), TGS C 12. (Sh520,000).
TGS D
TGS D 1. (Sh567,000), TGS D 2. (Sh578,500), TGS D 3. (Sh590,000), TGS D 4. (Sh601,500), TGS D 5. (Sh613,000), TGS D 6. (Sh 624,500), TGS D 7. (Sh636,000), TGS D 8. (Sh647,500), TGS D 9. (Sh659,000), TGS D 10. (Sh 670,500), TGS D 11. (Sh 682,000),na TGS D 12. (Sh 693,500).
TGS E
TGS E 1. (Sh751,000), TGS E 2. (Sh766,500), TGS E 3. (Sh782,000), TGS E 4. (Sh797,500), TGS E 5. (Sh813,000), TGS E 6. (Sh828,500), TGS E 7. (Sh844,000), TGS E 8. (Sh859,500), TGS E 9. (Sh875,000), TGS E 10. (Sh890,500), TGS E 11. (Sh906,000), na TGS E 12. (Sh912,500).
TGS F
TGS F 1. (Sh1,003,000 ), TGS F 2. (Sh 1,022,400), TGS F 3. (Sh 1,044,800), TGS F 4. (Sh1,061,200), TGS F 5. (Sh 1,080,600), TGS F 6. (Sh1,100,000), TGS F 7. (Sh1,119,400), TGS F 8. (Sh 1,138,800), TGS F 9. (Sh 1,158,200), TGS F 10. (Sh1,177,600), na TGS F 11. (Sh 1,197,000) TGS F 12. (Sh 1,216,400).
TGS G
TGS G 1. (Sh 1,299,000), TGS G 2. (Sh 1,324,500), TGS G 3. (Sh 1,350,000), TGS G 4. (Sh 1,375,500), TGS G 5. (Sh 1,401,000), TGS G 6. (Sh 1,426,500), TGS G 7. (Sh 1,452,000), TGS G 8. (Sh 1, 477,500), TGS G 9. (Sh 1,503,000), TGS G 10. (Sh 1,528,500), TGS G 11. (Sh 1,554,000), na TGS G 12. (Sh 1,579,500).
TGS H
TGS H 1. (Sh 1,672,000), TGS H 2. (Sh 1,722,000), TGS H 3. (Sh 1,772,000), TGS H 4. (Sh 1,822,000), TGS H 5. (Sh 1,872,000), TGS H 6. (Sh 1,922,000), TGS H 7. (Sh 1,972,000), TGS H 8. (Sh 2,022,000), TGS H 9. (Sh2,072,000), TGS H 10. (Sh 2,122,000), TGS H 11. (Sh 2,172,000) na TGS H 12. (Sh 2,222,000).
TGS I
TGS I-1. (Sh2,317,000), TGS I-2.(Sh 2,413,000), TGS I-3. (Sh 2,509,000) na TGS I-4.(Sh 2,605,000).
TGHS I (Sh 2,800,000).
TGHS J
TGHS J (Sh 2,900,000
TGHS K
TGHS K (Sh 3,100,000)
TGHS L
TGHS L (Sh 3,400,000)
Watumishi wa Mahakama
TJS 1
TJS 1.1. (Sh 510,000), TJS 1.2. (Sh 535,000), TJS 1.3. (Sh 560,000), TJS 1.4. (Sh 585,000), TJS 1.5. (Sh 610,000), na TJS 1.6. (Sh 635,000) na TJS 1.7. (Sh 660,000).
TJS 2
TJS 2.1. (Sh 770,000), TJS 2.3. (Sh 805,000), TJS 2.3. (Sh 840,000), TJS 2.4. (Sh 875,000), TJS 2.5. (Sh 910,000), TJS 2.6. (Sh 945,000), na TJS 2.7. (Sh 980,000).
TJS 3
TJS 3.1. (Sh 1,075,000), TJS 3.2. (Sh 1,115,000), TJS 3.3. (Sh 1,155,000), TJS 3.4. (Sh 1,195,000), TJS 3.5. (Sh 1,235,000), TJS 3.6. (Sh 1,275,000), na TJS 3.7. (Sh 1,315,000).
TJS 4
TJS 4.1. (Sh1,420,000), TJS 4.2. (Sh 1,470,000), TJS 4.3. (Sh 1,520,000), TJS 4.4. (Sh 1,570,000), TJS 4.5. (Sh 1,620,000), TJS 4.6. (Sh 1,670,000), na TJS 4.7. (Sh 1,720,000).
TJS 5
TJS 5.1. (Sh 1,805,000), TJS 5.2. (Sh1,875,000), TJS 5.3. (Sh 1,945,000), TJS 5.4. (Sh 2,015,000), TJS 5.5. (Sh 2,085,000), na TJS 5.6. (Sh 2,155,000).
TJS 6
TJS 6.1. (Sh 2,250,000), TJS 6.2. (Sh 2,350,000), TJS 6.3. (Sh 2,450,000), TJS 6.4. (Sh 2,550,000), na TJS 6.5. (Sh 2,650,000).
TJS 7
TJS 7 (Sh 3,560,000)
TJS 8
TJS 8. (Sh 4,050,000)
TJS 9
TJS 9. (Sh 4,480,000)
TJS 10
TJS 10 (Sh 4,600,000)
Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
AGCS 1
AGCS 1.1. (Sh 360,000), AGCS 1.2. (Sh 380,000), AGCS 1.3. (Sh 400,000), AGCS 1.4. (Sh 420,000), AGCS 1.5. (Sh 440,000), AGCS 1.6. (Sh 460,000), AGCS 1.7 (Sh 480,000).
AGCS 2
AGCS 2.1.(Sh 510,000), AGCS 2.2.(Sh 534,700), AGCS 2.3.(Sh 559,000), AGCS 2.4.(Sh 584,100), AGCS 2.5.(Sh 608,800), AGCS 2.6.(Sh 633,500), AGCS 2.7.(Sh 658,200).
AGCS 3
AGCS 3.1.(Sh770,000), AGCS 3.2.(Sh 802,000), AGCS 3.3.(Sh 834,000), AGCS 3.4.(Sh 866,000), AGCS 3.5.(Sh 898,000), AGCS 3.6.(Sh 930,000), na AGCS 3.7.(Sh 962,000).
AGCS 4
AGCS 4.1.(Sh 1,075,000), AGCS 4.2.(Sh 1,113,000), AGCS 4.3.(Sh 1,151,000), AGCS 4.4.(Sh 1,189,000), AGCS 4.5.(Sh 1,227, 000), AGCS 4.6.(Sh 1,265,000), AGCS 4.7.(Sh 1,303,000).
AGCS 5
AGCS 5.1.(Sh 1,420,000), AGCS 5.2.(Sh 1,464,000), AGCS 5.3.(Sh 1,508,000), AGCS 5.4.(Sh 1,552,000), AGCS 5.5.(Sh 1,596,000), AGCS 5.6.(Sh 1640,000), AGCS 5.7.(Sh 1,684,000).
AGCS 6
AGCS 6.1.(Sh 1,805,000), AGCS 6.2.(Sh 1,867,000), AGCS 6.3.(Sh 1,929,000), AGCS 6.4.(Sh 1,991,000), AGCS 6.5.(Sh 2,053,000), na AGCS 6.6.(Sh 2,115,000).
AGCS 7
AGCS 7.1.(Sh 2,240,000), AGCS 7.2.(Sh 2,329,000), AGCS 7.3.(Sh 2,418,000), AGCS 7.4.(Sh 2,507,000), na AGCS 7.5.(Sh 2,596,000)
AGCS 8
AGCS 8(Sh 3,020,000)
AGCS 9
AGCS 9(Sh3,560,000)
AGCS 10
AGCS 10 (Sh 4,230,000)
AGCS 11
AGCS 11(Sh 4,485,000)
AGCS 12
AGCS 12 (Sh 5,000,000)
AGCS 13
AGCS 13(Sh 5,580,000)
Wafanyakazi wanaofanya utafiti wa kilimo na mifugo
TGRS A
TGRS A 1. (Sh 916,000), TGRS A 2. (Sh926,500), TGRS A 3. (Sh 937,000), TGRS A 4. (Sh 947,500), TGRS A 5. (Sh 958,000), TGRS A 6. (Sh 968,500), TGRS A 7. (Sh 979,000), na TGRS A 8. (Sh 989,500).
TGRS B
TGRS B 1. (Sh 1,060,000), TGRS B 2. (Sh 1,072,700), TGRS B 3. (Sh 1,085,400), TGRS B 4. (Sh 1,098,100), TGRS B 5. (Sh 1,110,800), TGRS B 6. (Sh 1,123,500), TGRS B 7. (Sh 1,136,200), na TGRS B 8. (Sh 1,148,900).
TGRS C
TGRS C 1. (Sh 1,252,000), TGRS C 2. (Sh 1,268,400), TGRS C 3. (Sh 1,284,800), TGRS C 4. (Sh 1,301,200), TGRS C 5. (Sh 1,317,600), TGRS C 6. (Sh 1,334,000),TGRS C 7. (Sh 1,350,400), na TGRS C 8. (Sh 1,366,800).
TGRS D
TGRS D 1. (Sh 1,473,000),TGRS D 2. (Sh 1,495,000), TGRS D 3. (Sh 1,517,000), TGRS D 4. (Sh 1,539,000), TGRS D 5. (Sh 1,561,000), TGRS D 6. (Sh 1,583,000), TGRS D 7. (Sh 1,605,000), na TGRS D 8. (Sh 1,627,000).
TGRS E
TGRS E 1. (Sh 1,736,000), TGRS E 2. (Sh 1,774,500), TGRS E 3. (Sh 1,813,000), TGRS E 4. (Sh 1,851,500), TGRS E 5. (Sh 1,890,000), TGRS E 6. (Sh 1,928,500), TGRS E 7. (Sh 1,967,000), na TGRS E 8. (Sh 2,005,500).
TGRS F
TGRS F 1. (Sh 1,114,000), TGRS F 2. (Sh 2,183,000), TGRS F 3. (Sh 2,252,000), na TGRS F 4. (Sh 2,321,000).
TGRS G
TGRS G 1. (Sh 2,440,000), TGRS G 2. (Sh 2,522,000), na TGRS G 3. (Sh 2,604,000).
TGRS H
TGRS H (Sh 2,950,000)
TGRS I
TGRS I (Sh 3,100,000)
Wafanyakazi Ofisi ya Bunge kada ya masharti (operational service)
PSOS A
PSOS A.1. (Sh 240,000), PSOS A.2. (Sh 245,600), PSOS A.3. (Sh 251,200), PSOS A.4. (Sh 256,800),PSOS A.5. (Sh 262,400), PSOS A.6. (Sh 268,000), PSOS A.7. (Sh 273,500), PSOS A.8. (Sh 279,200), PSOS A.9. (Sh 284,800), PSOS A.10. (Sh 290,400), PSOS A.11. (Sh 296,000), PSOS A.12. (Sh 301,600),PSOS A.13. (Sh 307,200), PSOS A.14. (Sh 312,800), PSOS A.15. (Sh 318,400), PSOS A.16. (Sh324,000), PSOS A.17. (Sh 329,600), na PSOS A.18. (Sh 335,200).
PSOS B
PSOS B.1. (Sh 347,000), PSOS B.2. (Sh 356,500), PSOS B.3. (Sh 366,000), PSOS B.4. (Sh 375,500),PSOS B.5. (Sh 385,000), PSOS B.6. (Sh 394,500), PSOS B.7. (Sh 404,000), PSOS B.8. (Sh 413,500), PSOS B.9. (Sh 423,000), PSOS B.10. (Sh 432,500), PSOS B.11. (Sh 442,000), na PSOS B.12. (Sh 451,500).
PSOS C
PSOS C.1. (Sh 471,000), PSOS C.2. (Sh 482,000),PSOS C.3. (Sh 493,000), PSOS C.4. (Sh 504,000), PSOS C.5. (Sh 515,000), PSOS C.6. (Sh 526,000), PSOS C.7. (Sh537,000), PSOS C.8. (Sh 548,000), PSOS C.9. (Sh 559,000), PSOS C.10. (Sh 570,000), PSOS C.11. (Sh 581,000), na PSOS C.12. (Sh 592,000).
Wafanyakazi wenye taaluma mbalimbali Ofisi za Bunge
PSS A
PSS A. 1. (Sh 249,000), PSS A. 2. (Sh 255,600), PSS A. 3. (Sh 262,200), PSS A. 4. (Sh 268,800), PSS A. 5. (Sh 275,400), PSS A. 6. (Sh 282,000), PSS A. 7. (Sh 288,600), na PSS A. 8. (Sh 295,200).
PSS B
PSS B. 1. (Sh 311,000), PSS B. 2. (Sh 319,500), PSS B. 3. (Sh 328,000), PSS B. 4. (Sh 336,500), PSS B. 5. (Sh 345,000), PSS B. 6. (Sh353,500), PSS B. 7. (Sh 362,000), PSS B. 8. (Sh 370,500), PSS B. 9. (Sh 379,000), na PSS B. 10. (Sh387,500).
PSS C
PSS C. 1. (Sh 410,000), PSS C. 2. (Sh 420,000), PSS C. 3. (Sh 430,000), PSS C. 4. (Sh 440,000), PSS C. 5. (Sh 450,000), PSS C. 6. (Sh 460,000), PSS C. 7. (Sh 470,000), PSS C. 8. (Sh 480,000), PSS C. 9. (Sh 490,000), PSS C. 10. (Sh 500,000), PSS C. 11. (Sh 510,000), na PSS C. 12. (Sh 520,000).
PSS D
PSS D. 1. (Sh 567,000),PSS D. 2.(Sh 578,500),PSS D. 3. (Sh 590,000),PSS D. 4. (Sh 601,500),PSS D. 5. (Sh 613,000),PSS D. 6. (Sh 624,000),PSS D. 7. (Sh 636,000),PSS D. 8. (Sh 647,500),PSS D. 9. (Sh 659,000),PSS D. 10. (Sh 670,500),PSS D. 11. (Sh 682,000), na PSS D. 12. (Sh 693,500).
PSS E
PSS E. 1. (Sh751,000),PSS E. 2. (Sh 766,500),PSS E. 3. (Sh 782,000),PSS E. 4. (Sh 797,500),PSS E. 5. (Sh 813,000),PSS E. 6. (Sh 828,500),PSS E. 7. (Sh 844,000),PSS E. 8. (Sh 858,500),PSS E. 9. (Sh 875,000),PSS E. 10. (Sh 890,500),PSS E. 11. (Sh 906,000),na PSS E. 12. (Sh 912,500).
PSS F
PSS F. 1. (Sh 1,003,000),PSS F. 2. (Sh 1,022,000),PSS F. 3. (Sh 1,041,800),PSS F. 4. (Sh 1,061,200),PSS F. 5. (Sh 1,080,600),PSS F. 6. (Sh 1,100,000),PSS F. 7. (Sh 1,119,400),PSS F. 8. (Sh 1,138,800),PSS F. 9. (Sh 1,158,200),PSS F. 10. (Sh 1,177,600),PSS F. 11. (Sh 1,197,000),na PSS F. 12. (Sh 1,216,400).
PSS G
PSS G. 1. (Sh 1,299,000),PSS G. 2. (Sh 1,324,500),PSS G. 3. (Sh 1,350,000),PSS G. 4. (Sh 1,375,500),PSS G. 5. (Sh 1,401,000),PSS G. 6. (Sh 1,426,500),PSS G. 7. (Sh 1,452,000),PSS G. 8. (Sh 1,477,500),PSS G. 9. (Sh 1,503,000),PSS G. 10. (Sh 1,528,500),PSS G. 11. (Sh 1,554,000),na PSS G. 12. (Sh 1,579,500).
PSS H
PSS H. 1. (Sh 1,672,000),PSS H. 2. (Sh 1,722,000),PSS H. 3. (Sh 1,772,000),PSS H. 4. (Sh 1,822,000),PSS H. 5. (Sh 1,872,000),PSS H. 6. (Sh 1,922,000),PSS H. 7. (Sh 1,972,000),PSS H. 8. (Sh 2,022,000),PSS H. 9. (Sh 2,072,000),PSS H. 10. (Sh 2,122,000),PSS H. 11. (Sh 2,172,000),na PSS H. 12. (Sh 2,222,000).
PSS I
PSS I. 1. (Sh 2,317,000),PSS I. 2. (Sh 2,413,000),PSS I. 3. (Sh 2,509,000),na PSS I. 4. (Sh 2,605,000).
PSS J
PSS J (Sh 2,800,000)
PSS K
PSS K (Sh 2,900,000)
PSS L
PSS L (Sh 3,100,000)
Wafanyakazi wa kada ya Wakaguzi katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (SAIS)
SAIS A
SAIS A.1. (Sh 249,000), SAIS A.2. (Sh 255,600), SAIS A.3. (Sh 262,200),SAIS A.4. (Sh 268,800), SAIS A.5. (Sh 275,400), SAIS A.6. (Sh 282,000), SAIS A.7. (Sh 288,600), na SAIS A.8. (Sh 295,200)
SAIS B
SAIS B.1. (Sh 311,000), SAIS B.2. (Sh 319,500), SAIS B.3. (Sh 328,000), SAIS B.4. (Sh 336,500), SAIS B.5. (Sh 345,000), SAIS B.6. (Sh 353,500), SAIS B.7. (Sh 362,000), SAIS B.8. (Sh 370,500), SAIS B.9. (Sh 379,000), na SAIS B.10. (Sh 387,500).
SAIS C
SAIS C.1. (Sh 410,000), SAIS C.2. (Sh 420,000), SAIS C.3. (Sh 430,000), SAIS C.4. (Sh 440,000), SAIS C.5. (Sh 450,000), SAIS C.6. (Sh 460,000), SAIS C.7. (Sh 470,000), SAIS C.8. (Sh 480,000), SAIS C.9. (Sh 490,000), na SAIS C.10. (Sh 500,000),SAIS C.1.1 (Sh510,000), na SAIS C.12. (Sh 520,000).
SAIS D
SAIS D.1. (Sh567,000), SAIS D.2. (Sh 578,500),SAIS D.3. (Sh 590,000),SAIS D.4. (Sh 601,500),SAIS D.5. (Sh 613,000),SAIS D.6. (Sh 624,500),SAIS D.7. (Sh 636,000),SAIS D.8. (Sh 647,500),SAIS D.9. (Sh 659,000),SAIS D.10. (Sh 670,500),SAIS D.11. (Sh 682,000),SAIS D.12. (Sh 693,500).
SAIS E
SAIS E.1. (Sh 751,000),SAIS E.2. (Sh 766,500),SAIS E.3. (Sh 782,000),SAIS E.4. (Sh 797,500),SAIS E.5. (Sh 813,000),SAIS E.6. (Sh 828,000),SAIS E.7. (Sh 844,000),SAIS E.8. (Sh 859,500),SAIS E.9. (Sh 875,000),SAIS E.10. (Sh 890,500),SAIS E.11. (Sh 906,000),na SAIS E.12. (Sh 912,500).
SAIS F
SAIS F.1. (Sh1,003,000),SAIS F.2. (Sh 1,022,400),SAIS F.3. (Sh 1,041,800),SAIS F.4. (Sh 1,061,200),SAIS F.5. (Sh 1,080,600),SAIS F.6. (Sh 1,100,000),SAIS F.7. (Sh 1,119,400),SAIS F.8. (Sh 1,188,800),SAIS F.9. (Sh 1,158,200),SAIS F.10. (Sh 1,177,600),SAIS F.11. (Sh 1,197,000), na SAIS F.12. (Sh 1,216,400).
SAIS G
SAIS G.1. (Sh1,299,000),SAIS G.2. (Sh 1,324,500),SAIS G.3. (Sh 1,350,000),SAIS G.4. (Sh 1,375,500),SAIS G.5. (Sh 1,401,000),SAIS G.6. (Sh 1,426,500),SAIS G.7. (Sh 1,452,000),SAIS G.8. (Sh 1,477,500),SAIS G.9. (Sh 1,503,000),SAIS G.10. (Sh 1,528,000),SAIS G.11. (Sh 1,554,000),na SAIS G.12. (Sh 1,579,000).
SAIS H
SAIS G.1. (Sh 1,672,000),SAIS G.2. (Sh 1,722,000),SAIS G.3. (Sh 1,772,000),SAIS G.4. (Sh 1,822,000),SAIS G.5. (Sh 1,872,000),SAIS G.6. (Sh 1,922,000),SAIS G.7. (Sh 1,972,000).

SOURSE: MWANANCHI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU