Facebook Comments Box

Friday, July 18, 2014

MUFT MENK: SOLUTION TO OUR STATE OF WEAKNESS




LINAH AAGWA RASMI THT AKIELEKEA NFZ

Mkurugenzi wa Tanzania House Of Talent (THT) Ruge Mutahaba akifafanua jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wanahabari,wadau na wasanii wa filamu na muziki,katika hafla ya kumuaga msanii Linah Julai 16, 2014 kutoka kwao na kuelekea kampuni ya No Fake Zone (NFZ) ambao ndiyo
wanaanza kumsimamia msanii huyo pamoja na kazi zake.


Baadhi ya wasanii walipewa tuzo mbalimbali katika sherehe hizo ambao ni Mwasiti, Dito,Linah na Mtayarishaji kutoka katika nyumba hiyo ya sanaa Imma Ze Boy ambao wote hao walipata vyeti.

 Msanii Dito
 Imma Ze Boy
 Linnah
 Mwasity

Linah pia alizindua video yake mpya chini ya kampuni NFZ iitwayo OLe Themba.

Waalikwa wakiifuatilia video ya wimbo huo Ole Themba kwa karibu kabisa kama wanavyooekana pichani.


MKurugenzi wa Kampuni ya NO FAKE ZONE (NFZ), Abby akizungumza jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali.

 Ommy Dimpoz
 Mwana FA
 Steve Nyerere, Kalala Junior na Christian Bella wakiwa na furaha.
Recho


WAFADHILI KUREJESHA MSAADA UGANDA IKIWA.........

Wahisani wamesema wameridhika na kazi ya serikali mwaka 2012/13

Mapema mwaka huu wafadhili kadha walikata msaada wao wa bajeti kupinga sheria kali dhidi ya wapenzi wa jinsia moja iliyopitishwa Februari. Wiki jana serikali ilitoa andiko linalojaribu kubainisha sheria hio dhidi ya wapenzi wa jinsia moja. 

Mnao siku ya Jumanne, wafadhili hao walionyesha kuridhika na kazi ya serikali mnamo mwaka wa fedha 2012/13, baada ya uhakiki wa kila mwaka kuhusu matendo ya serikali. Uhakiki huo unakusudiwa kuwapa fursa wafadhili kuamua ikiwa au la waendelee kugharimia bajeti ya Uganda kwa mamilioni ya dola.

Kwa jumla kasoro ya 20% ya bajeti ya Uganda inategemea misaada ya wafadhili. Wafadhili hususan kutoka Ulaya ambao husaidia bejeti ya Uganda walisitisha msaada wao kufuatia ripoti za ufujaji wa pesa za serikali pamoja na kupitishwa kwa sheria ya kuharamisha mapenzi ya jinsia moja. Nchi hizo kiwawakilishwa na Denmark pamoja na beki ya dunia wanaonekana kushawishika kuendelea kusaidia Uganda baada ya kukutana na waziri mkuu Amama Mbabazi.
Nyingi ya pesa inazopata Uganda kama msaada hutumiwa katika miradi ya afya Katika taarifa yao ya pamoja, wahusika wote walitambua jukumu la Uganda katika kuweka amani na uthabiti katika kanda nzima na kuhimiza uhuru wa kujieleza pamoja na uwazi katika masala ya usimamizi wa pesa za msaada.

Wamejitolea kuendelea kufadhili Uganda kwa kima cha dola milioni arobaini katika siku zijazo. Marekani pamoja na nchi nyinginezo kutoka Ulaya zilisitisha msaada wa mamilioni ya dola baada ya Rais Museveni kutia saini sheria ya mapenzi ya jinsia moja mapema mwezi huu. Nchi hizo zinataka Uganda ifutilie mbali sheria hio kabla ya kuanza kuipa tena msaada. 

Wiki jana Waziri wa mambo ya nje wa Uganda alitoa taarifa kusema kuwa sheria hiyo ilitafsiriwa visivyo kwani lengo lake ni kuwalinda watoto bali sio kumbagua yeyote, wala haijulikani ikiwa tamko hilo ndilo lililoifanya wahisani kuanza tena kutoa msaada.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU