Facebook Comments Box

Tuesday, October 1, 2013

SABABU YA CHUJI KUWEKWA BENCHI NA BRANDIS YAWEKWA HADHARANI





Athumani Idd Chuji - Kiungo mpigaji wa pasi ndefu Yanga

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernest Brandts amewataka wachezaji wake wacheze pasi fupi zenye akili kwa sababu ndiyo ushindi wao na si ndefu kama wanapopoa maembe mtini na akaweka wazi kuwa, alimtumia kiungo wake mkongwe, Athuman Idd ‘Chuji’ kama mchezaji wa akiba kwa sababu hajafanya mazoezi na timu kwa muda mrefu.
Chuji aliingia kipindi cha pili katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting akitokea benchi kuchukua nafasi ya Frank Domayo na dakika chache baadaye Yanga ikapata bao la ushindi lililofungwa na Hamis Kiiza raia wa Uganda matokeo yakawa ya ushindi wa bao 1-0 mwishoni mwa wiki.
Kutokana na kitendo hicho mashabiki wa soka walihoji na kupiga kelele kulikoni kiungo huyo aachwe nje wakati ni msaada kwenye timu.
Brandts alisema: “Nataka timu icheze mpira kwa pasi fupi fupi na kwa umakini na si ndefu zisizo na mpango kwa sababu ndiyo zinatugharimu na hata mechi yetu na Ruvu kipindi cha kwanza hatukuwa vizuri.” 

Akimzungumzia Chuji, kocha huyo alisema: “Sikuweza kumtumia kipindi cha kwanza kwa sababu hakuwa na muda mzuri wa pamoja na wenzake katika mazoezi na alikuwa kwao, kulikuwa na matatizo ya kifamilia.
Hali hiyo ndiyo ilinifanya nisimpange kikosi cha kwanza na ndiyo maana nilimtumia kipindi cha pili.”
Chanzo:Mwanaspoti


HEBU MTAZAME MOYES KATIKA KIBONZO HIKI ANAFURAHISHA KWELIKWELI




EVERTON YAICHAPA NEWCASTLE UNITED MAWILI KWA BILA


Mshambuliaji Romelu Lukaku amefunga mabao mawili katika ushindi wa 3-2 wa Everton dhidi ya Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika Uwanja wa Goodison Park.
 
Lukaku alifunga mabao hayo katika dakika za tano na 37,wakati lingine lilifungwa na Barkley dakika ya 25 na mabao ya Newcastle United yalifungwa na Cabaye dakika ya 51 na Remy dakika ya 89.
 
Mshambuliaji huyo anamuonyesha kocha wa Chelsea, Mreno Jose Mourinho kwamba alikosea kumruhusu kuondoka majira ya joto. 
 
Kikosi cha Everton kilikuwa; Howard, Baines, Distin, Jagielka, Coleman, Mirallas/Deulofeu dk73, McCarthy, Barry, Osman/Stones dk90, Barkley/Naismith dk88 na Lukaku.
 
Newcastle United: Krul, Debuchy, Yanga-Mbiwa/Williamson dk45, Coloccini, Santon, Anita/Cisse dk69, Tiote, Sissoko, Gouffran, Remy na Ben Arfa/Cabaye dk45.
Main man: Romelu Lukaku scored two of Everton's goals to put Newcastle to the sword at Goodison Park
Romelu Lukaku ameifungia mabao mawili Everton ikiilaza Newcastle 3-2 Uwanja wa Goodison ParkOpening salvo: Lukaku needed just five minutes to score Everton's first as they eased to victory
Dakika tano zilitosha kwa Lukaku kufunga bao la kwanzaBright spark: Ross Barkley continued to showcase his potential with a calmly taken second goal for Everton
Barkley akishangilia baada ya kufunga
Open goal: A defensive mistake from Newcastle allowed Lukaku to slam the ball home from close range
Lukaku akifunga bao la kwanzaOpen goal: A defensive mistake from Newcastle allowed Lukaku to slam the ball home from close range
Lukaku akifunga bao lake la pili


CHEZEA MVUA ZA DAR WEWE? MREMBO APANDA MKOKOTENI MWENYEWE!!!


Kama anavyoonekana hapo juu katika picha mbili, mrembo huyu akionekana japo akiwa na woga lakini alikuwa hana jinsi baada ya mvua kunyesha Dar na hali kuwa kama inavyoonekana hapo, hali ilibadilika ghafla na maji kujaa barabarani na foleni za hapa na pale ndani ya Jiji hili hapo Jana Tarehe 30/09/2013.


MKENYA ALIYE DAIWA KUMTEKA DR ULIMBOKA ATOZWA FAINI TSH 1, 000


Mtuhumiwa wa kutoa ushahidi wa uongo wa kumteka aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha madaktari, Dk Steven Ulimboka, Joshua Muhindi akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana,mara baada ya kulipiwa faini ya Sh 1,000.
Dar es Salaam. 

Mkenya Joshua Muhindi aliachiwa huru baada ya kulipa faini ya Sh1,000 kwa kupatikana na hatia ya kuidanganya polisi kuwa alihusika kumteka na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimhukumu kifungo cha miezi sita jela au kulipa faini hiyo. Mulundi alilipiwa faini hiyo na Mwandishi wa Habari wa Redio Times, Chipangula Nandule.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka kusoma maelezo ya awali na mshtakiwa huyo kukiri alitoa taarifa ya uongo kwa polisi kuhusu tukio hilo.
Kabla ya hukumu hiyo, Mulundi aliomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hilo lilikuwa kosa lake la kwanza. Pia alijitetea kuwa Juni 27, 2012 akiwa Arusha alitekwa na kupelekwa Dar es Salaam ambako alikuwa hana mwenyeji wala hakuwahi kufika.
Alisema kutokana na kutekwa huko alichanginyikiwa hivyo kukubali chochote alichoambiwa afanye kwa kuwa aliyemteka alikuwa na silaha na alimwelekeza mambo ya kuzungumza.
“Mheshimiwa kwa ajili ya vitisho hivyo, nilikwenda Kawe katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko kwenye eneo la Tanganyika Packers, mbele ya Mchungaji Joseph Malwa Kiliba na kuungama kuwa ni miongoni mwa watu waliomtesa Dk Ulimboka katika Msitu wa Pande,” alisema Mulundi na kuongeza.
“Siwalaumu Serikali, upande wa mashtaka wala polisi kwa kitendo cha kuniweka gerezani kwa muda mrefu, najilaumu mimi mwenyewe.” Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Kweka aliiambia Mahakama kuwa hana kumbukumbu za uhalifu za mshtakiwa lakini aliomba apewe adhabu kali kutokana na mazingira ya tukio hilo.
Akitoa hukumu, Hakimu Katema alisema alifikia uamuzi huo kwa kuzingatia maombi ya mshtakiwa ya kupunguziwa adhabu.
CHANZO: MWANANCHI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU