Facebook Comments Box

Monday, February 25, 2013

TCRA YAIFUNGIA TV IMAAN

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imeifungia Televisheni pekee ya Kiislam ambayo inamilikiwa na Taasisi ya The Islamic Foundation ya Mjini Morogoro. Hiyo ndio Televisheni pekee ya Kisslam ambayo imekuwa ikimilikiwa na kuupasha habari umma wa Kiislam nchini Tanzania. 
Sababu za kuifungia Televishni hiyo bado hazijawekwa wazi. Televisheni hiyo imefungiwa tokea jumamosi.
Baadhi ya wananchi walioongea na Blog hii wamekuwa wakihisi labda ni katika mchakato wa kuendelea kuwashughulisha ili wasikae sawa katika malengo yao. Wenfgi wa wakazi wa Morogoro wamekuwa wakiitambua Taasisi ya The Islamic Foundation kama msaada mkubwa kwao na kwa jamii bila kujali hata rangi, kabila wala dini.
Kufungwa kwa Televisheni hii kumekuja huku serikali ya Morogoro ikiwa imekitambua kwa kuitunuku cheti maalumu Taasisi hiyo ya The Islamic Foundation kwa msaada wake mkubwa inaotoa kwa jamii. Wengi wamekuwa wakilaumu mamlaka hiyo ya mawasiliano kwa kitendo hicho tena kuifungia jumamosi wakati ofisi za kiserikali zikiwa zimefungwa.
Chini ni baadhi ya habari zilizowekwa na mmoja wa waandamizi waliokuwa wakishughulika na Televisheni hiyo ikitanabaisha kufungwa kwa Televisheni hiyo na kuwaomba Waislam Tanzania kuwa na Subra na kuongeza moambi katika ukuta wa mtandao wa jamii. Muhusika huyo anajulikana kwa jina la Ahmed Bawazir ambae jina lake limekuwa likisomeka hivyo kwa kiarabu

www.kitongoni.blogspot.com
 




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU